CCM na Rais Magufuli wanatumia ajali ya moto Mororgoro kama mtaji wa kisiasa na wakiwatukuza wahalifu kama mashujaa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,023
18,563
Ukweli ndio huo, labda kwa mtu asiye na uwezo wa kufikiri ndio hataona kwamba CCM na Magufuli wanataumia ajali ya moto Morogoro kama mtaji wa kisiasa.

Hatukatai kwamba wakati wa hili janga na msiba, labda si vema kuanza kuhukumiana, kama alivyosema Rais Magufuli, japo haina maana baada ya msiba kusiwepo kabisa kuhukumiana. Lakini sasa Rais Magufuli mwenyewe na CCM si kwamba tu hawahukumu, bali wanaenda mbali zaidi kwa kutumia tukio hili kama mtaji wa kisiasa, kujiuza kwa wananchi kisiasa.

Hawa watu waliokufa wakiiba mafuta kwenye ajali wote tunajua ni wahalilifu, vibaka. Tunachoona sasa ni kwamba wamegeuzwa kuwa mashujaa wa namna fulani. Majushaa wa kuiba kwenye tukio la ajali?

Zaidi ya zawadi za maelfu ya pesa yakitangazwa live na vyombo vya habari, kuambiwa serikali itagharamia matibabu (yaani mimi mlipa kodi nigharamie matibabu ya vibaka wa mafuta) sasa tunaambiwa wajajengewa mnara wa kumbukumbu!

MImi kama mlipa kodi wa Tanzania, sitaki hela yangu ya kodi itolewe kama zawadi kwa mhalifu, wala imjengee mhalifu mnara wa kumbukumbu. Labda kwa huruma inaweza kugharamia mazishi, kwa kuwa mhalifu aliyekufa hawezi kujizika.

Hivi tangu lini mhalifu amekuwa akitukuzwa kiasi hicho? Tangu lini Tanzania limewkuwa taifa la kutukuza uhalifu? Hivi CCM wamekuwa desparate kujiuza hadi kufikia kiasi hiki? Au CCM na Raisi Magufuli wanaona kuwa wao ndio kisababishi cha hali mbaya ya mzunguko wa fedha nchini kiasi kuwafanya watu kufanya chochote kujipatia fedha kidogo?

Binafsi wala hata sikuona haja ya raisi Magufuli kuwatembelea hawa watu hospitali na kufanya matangazo mengi ya kutoa msaaada wa fedha huku akitaja kiasi wanachopewa. Na wala sioni haja ya kuwajengea mnara wa kumbukumbu. Na kama ikibidi kujenga huo mnara, basi tuandike maandishi "hapa wamezikwa watu waliokuwa wakiiba mafuta baada ya ajali ya lori. Tujifunze ili tukio kama hili lisije tokea tena.

Sikatai kutoa maneno ya pole kwa wafiwa, lakini jambo la ajabu ni kuona Magufuli na CCM yake wakienda mbali zaidi na kulifanya tukio hili kuwa mtaji wa kisiasa. Hili ni tukio la kihalifu, kwa kiyo serikali na Raisi Magufuli walipaswa watende kwa umakini wakijua hilo, sio kulitumia kujijengea umaarufu wa kisiasa. Hivi mmefikia kuwa desparate kiasi hicho katika kujaribu kufanywa mpendwe na wananchi? CCM kimekuwa chama kibaya cha kujitembeza?

Ajali nyingi sana zimetokea nchini na kuua watu wasio na hatia. Ni mara ngapi umesikia Raisi Magufuli akitembelea majeruhi wa ajali hizo na kuwapa maelefu ya fedha au kuwajengea mnara wa kumbukumbu au ajali hizo kufanywa tukio la kitaifa? Kwa nini hii ya wahalifu hawa ionwe tofauti - au kwa kuwa inakuja tukielekea uchaguzi Mkuu kukiwa na tetesi kwamba serikali ya Magufuli inazidi kuporomoka katika umaarufu na kuwa katika uchaguzi wa haki hataweza kushinda?

NB: Kwa tukio kama hili Raisi Magufuli alipaswa kufanya yafuatayo badala ya kulitumia tukio kisiasa

Raisi angetoa salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na kuwapa pole wafiwa. Angetamka kwamba serikali itagharamia mazishi ya waliokufa ikiwa hawatatambuliwa na ndugu zao, na kugharamia matibabu kwa majeruhi.

Na pia angekumbusha Watanzania kwa ujumla kwamba wajiepushe na kujichukulia mali pale ambapo ajali zinapotokea, iwe gari binafsi au ya mizigo, kwa kuwa kufanya hivyo sio tu sio ubinadamu bali pia ni kitendo cha uhalifu na wanaofanya hivyo wakikamatwa watachukuliwa hatua kali.

Basi, hiyo ingetosha kabisa. Hakuna kutembelea hospitali na kutangaza "nakugawia laki tano ukanunue juice", hakuna kutangaza kujenga mnara wa kumbukumbu, hakuna la zaidi. Kwa kuwa wengi waliopatwa na janga hili kimsingi ni wahalifu.

La sivyo tutarajie siku moja Raisi Magufuli akitembelea majambazi waliojeruhiwa na polisi kwa risasi wakiwa wamelazwa hospitali na kuwapa pole na zawadi za fedha, kwa kuwa anajali sana utu.
 
Acha u$3&&$ maiti haisemwi vibaya, wameshakufa we tulia,hata ukikataa kutoa hela tyr mwenye nch kashasema huwezi zuia we tulia kuwa mpole
Mjinga wewe unakosa pointi nenda shule zaidi uondoe ujinga. Ninasema CCM wasiwatukuze, sisemi wawaseme vibaya. Kwani Magufuli asingeenda hospitali na kujitutumua kutoa msaada wa fedha ingekuwa kuwasema vibaya? Na wangezikwa bila mnara wa kumbukumbu ni kuwasema vibaya?
 
Yaani ndiyo maana siwapendi wapinzani kwaajili ya akiliyao mbovu kama mtoa mada hivi wewe ni binaadamu wa kawaida kweli au hiyo CHADEMA yako ndiyo inakufundisha uwe na roho mbaya kiasi hicho halafu mnakuja kutuomba muongoze nchi watu wenye rohombaya kama yako wewe?

Maneno hayo kamwambie tundu lissu wenu huko siyo mnatuletea huku sisi tuko kwenye majonzi ya msiba huna huruma kabisa
 
Teh ...

Ila mzee sio wote waliokufa ni vibaka wengine wapita njia pia konda dereva na mama abiria

Ila wale wengine mimi walinihuzunisha kuacha kusaidia mtu amenasa wao wanaenda kuiba mafuta aisee
Nadhani kama waliacha kusaida mtu alienasa wakakimbilia kuiba mafuta basi walipata adhabu iliyowastahili. Hatuhitaji watu wa namna hiyo katika nchi hii tunayojenga uzalendo wa kweli.
 
Wewe mnara ujengwe usijengwe wewe inakuhusu nini, unampangia rais kazi ya kufanya asiende hospital,
Fanya yanayokuhusu kumpangia rais majukum unajisumbua
Mjinga wewe unakosa pointi nenda shule zaidi uondoe ujinga. Ninasema CCM wasiwatukuze, sisemi wawaseme vibaya. Kwani Magufuli asingeenda hospitali na kujitutumua kutoa msaada wa fedha ingekuwa kuwasema vibaya? Na wangezikwa bila mnara wa kumbukumbu ni kuwasema vibaya?
 
yaani ndiyo maana siwapendi wapinzani kwaajili ya akiliyao mbovu kama mtoa mada hii kwanza acha us***nge hivi wewe ni binaadamu wa kawaida kweli au hiyo chadema yako ndiyo inakufundisha uwe na roho mbaya kiasi hicho halafu mnakuja kutuomba muongoze nchi watu wenye rohombaya kama yako wewe? maneno hayo kamwambie tundu lissu wenu huko siyo mnatuletea huku sisi tuko kwenye majonzi ya msiba huna huruma kabisa ms****nzi wewe

Mtu kama wewe nadhani tukio hili lingetokea katika ujirani wako unaonyesa wazi wewe na mkeo mngekuwa wa kwanza kukimbilia eneo la tukio mkiwa na vidumu vya kuibia mafuta. Kwa hityo unaona CCM ni bora zaidi kuwashangilia wahalifu?

Yaani nyie mnaona mtu anaeomkosoa Magufuli ni mhalifu zaidi wa kutekwa na kuuwawa na "Wasiojulikana" kimya kimya na aliye nafuu na bora ni huyu kibaka wa mafuta kwenye ajali na ndie anapaswa kusikitikiwa? Mmeishiwa sana nyie watu.
 
Huwez kusema hvyo wakat sio wote wakioungua walikua wakiiba umeshaambiwa wengne walikua wapita njia, mama ntilie , waokoaji nk we kaz ya kuhukum muachie aliyewaumba.
Basi hao wanastahili pole zetu. Lakini katika waliokufa ni wangapi walikuwa wapita njia au waokoaji? Na wapi umesikia serikali ikitoa msisitizo kwamba ushujaa wanaotangaziwa waliokufa ni wale waliokuwa waokoaji na wapita njia?

Tena kwa hili ulilosema basi tukijenga mnara tuandike "Mnara huu ni kumbukumbu kwa waokoaji na wapita njia waliokufa kwa ajali ya moto, sio vibaka waliokuwa wakiiba mafuta"
 
Mtu kama wewe nadhani tukio hili lingetokea katika ujirani wako unaonyesa wazi wewe na mkeo mgekuwa wa kwanza kukimbilia eneo la tukio mkiwa na vidumu vya kuibia mafuta. Kwa hityo unaona CCM ni bora zaidi kuwashangilia wahalifu? Yaani nyie mnaona mtu anaeomkosoa Magufuli ni mhalifu zaidi wa kutekwa na kuuwawa na "Wasiojulikana" kimya kimya na aliye nafuu na bora ni huyu kibaka wa mafuta kwenye ajali ndie anapaswa kusikitikiwa? Mmeishiwa sana nyie watu.
Yaani kama CHADEMA wamekutuma uchafue hali ya hewa umeshindwa huna huruma hata kidogo hivi chadema huwa mnachamaana kweli? akikaa kimya mnaongea vibaya akisaidia pia mnaongea vibaya mnataka afanye nini kilakitu nyie mnaona kibaya hamna sera bora mjikalie kimya kuliko kuendelea kuropoka kama yule mpumbavu wenu lissu anaeropoka mhovyo huko aliko hamna huruma mbwa nyie
 
yaani kama chadema wamekutuma uchafue hali ya hewa umeshindwa huna huruma hata kidogo hivi chadema huwa mnachamaana kweli? akikaa kimya mnaongea vibaya akisaidia pia mnaongea vibaya mnataka afanye nini kilakitu nyie mnaona kibaya hamna sera bora mjikalie kimya kuliko kuendelea kuropoka kama yule mpumbavu wenu lissu anaeropoka mhovyo huko aliko hamna huruma mbwa nyie
Kwa masikitiko yako ni kwamba mie sio Chadema, wala CCM wala chama chochote. Nawachukulia wanasiasa wote kwa ujumla kuwa ni watu ambao inabidi kujifanya hawana uwezo wa kufikiri, kama unavyodhihirisha na post yako hii
 
Mjinga wewe unakosa pointi nenda shule zaidi uondoe ujinga. Ninasema CCM wasiwatukuze, sisemi wawaseme vibaya. Kwani Magufuli asingeenda hospitali na kujitutumua kutoa msaada wa fedha ingekuwa kuwasema vibaya? Na wangezikwa bila mnara wa kumbukumbu ni kuwasema vibaya?

Kama umenuna kujengewa Mnara hao Watu Waliofariki, Basi Mnara nitakuja Kuuchomeka Kwenye Matako yako. OVA
 
Kwa masikitiko yako ni kwamba mie sio Chadema, wala CCM wala chama chochote. Nawachukulia wanasiasa wote kwa ujumla kuwa ni watu ambao inabidi kujifanya hawana uwezo wa kufikiri, kama unavyodhihirisha na post yako hii
basi kama huna chama basi wewe ni kama mwanamke malaya anaye gawa hovyo kila sehemu ni bora ukae kimya kuliko kuongea mambo ambayo kwanza huna uhusiano nayo kama siyo wa chama chochote sasa unalilia nini kama unaf**rw
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom