IsayaMwita
JF-Expert Member
- Mar 9, 2008
- 1,127
- 140
"Tuwafanye waamini, wasadiki na pia watuunge mkono 2010" Hii ndiyo kauli mbiu ya ccm kwa sasa, kujiuzuru kwa maziri ndani ya serikali ni danganya toto na kamchezo ka funika kombe mwanahalamu apite.
Ndugu zangu watanzania poleni sana na haya yote tunayoyaona kwa sasa yakitokea ndani ya taifa letu hili lenye wananchi maskini,mtaamini kuwa CCM ni ndiyo waliotufikisha hapo tulipo,sote tunajua kuwa chama hicho ndicho kinatoa mwongozo na serikali inatekeleza.
Kulindana ndani ya chama hicho si swala geni kila mtanzania anajua, ila la kushangaza hata haya tunayoyaona kwa macho yetu na kushuhudia kama ufisadi bado wanaziba masikio na kutupuuza, wahusika hawawajibishwi kwa maana ya kufikishwa mahakamani, kila likifunuliwa hili wanalifunika kwa jingine, hebu sisi watanzania ni wajinga kiasi hicho?
Leo wameanza kuwatuhumu jamaa zao kwa hili na lile, hii waifanya ili sisi tuamini kuwa sasa ccm wamechukizwa na ubadhirifu wa mali za umma lakini si hivyo, lao ni moja Matanzania ni majinga tu"chukua chako ikibainika utajiuzuru hakuna shida" hii ni hatari sana kwa taifa changa kama Tanzania.
Tanzania kweli tutafika? kweli tutaendelea kuona propaganda za ccm kuwadanganya wananchi kule vijijini kuwa wao ni watendaji wazuri na kuendelea kushinda kwa kishindo? haitawezekana kamwe, watanzania tupeleke ujumbe kule vijijini ili ndugu zetu waujue wizi wa ccm ndani ya Taifa letu, na ndipo mabadiliko yatapatikana.
Ndugu zangu watanzania poleni sana na haya yote tunayoyaona kwa sasa yakitokea ndani ya taifa letu hili lenye wananchi maskini,mtaamini kuwa CCM ni ndiyo waliotufikisha hapo tulipo,sote tunajua kuwa chama hicho ndicho kinatoa mwongozo na serikali inatekeleza.
Kulindana ndani ya chama hicho si swala geni kila mtanzania anajua, ila la kushangaza hata haya tunayoyaona kwa macho yetu na kushuhudia kama ufisadi bado wanaziba masikio na kutupuuza, wahusika hawawajibishwi kwa maana ya kufikishwa mahakamani, kila likifunuliwa hili wanalifunika kwa jingine, hebu sisi watanzania ni wajinga kiasi hicho?
Leo wameanza kuwatuhumu jamaa zao kwa hili na lile, hii waifanya ili sisi tuamini kuwa sasa ccm wamechukizwa na ubadhirifu wa mali za umma lakini si hivyo, lao ni moja Matanzania ni majinga tu"chukua chako ikibainika utajiuzuru hakuna shida" hii ni hatari sana kwa taifa changa kama Tanzania.
Tanzania kweli tutafika? kweli tutaendelea kuona propaganda za ccm kuwadanganya wananchi kule vijijini kuwa wao ni watendaji wazuri na kuendelea kushinda kwa kishindo? haitawezekana kamwe, watanzania tupeleke ujumbe kule vijijini ili ndugu zetu waujue wizi wa ccm ndani ya Taifa letu, na ndipo mabadiliko yatapatikana.