Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,758
Habari ndio hiyo. Hayo yamesemwa na Dk Slaa katika mkutano wao na waandishi wa habari kuhusiana na tukio zima la Nyololo lililopelekea kuuawa kikatili kwa mwandishi wa habari wa Channel Ten na Mwenyekiti wa wanahabari mkoani Iringa- marehemu Daudi Mwangosi. Kumbe kazi ya John Mnyika sasa imekuwa rahisi zaidi maana pilisi na chama tawala wanafanya kazi yao kwa ufanisi sana. Ufanisi wa kuvuta hisia za wananchi pale ambapo cdm wanakuwa katika shughuli zao za kichama sehemu mbalimbali nchini, na hasa kupitia huu mkondo wa sasa wa Vuguvugu la mabadiliko (M4C).
Asanteni ccm na polisi kwa kazi nzuri ya uenezi ila hatutaki tena mauaji maana kazi ya uenezi haihusiani na mauaji bali sera, uhamasishaji, na utoaji taarifa chanya kwa jamii. Asanteni kwa maana mnarahisiaha mchakato wa kuelekea 2015 ambapo kazi yenu tukuka tutaienzi pale cdm itakaposhika Dola.
Asanteni ccm na polisi kwa kazi nzuri ya uenezi ila hatutaki tena mauaji maana kazi ya uenezi haihusiani na mauaji bali sera, uhamasishaji, na utoaji taarifa chanya kwa jamii. Asanteni kwa maana mnarahisiaha mchakato wa kuelekea 2015 ambapo kazi yenu tukuka tutaienzi pale cdm itakaposhika Dola.