Elice Elly
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 1,268
- 1,593
Tukitaka nchi hii iendelee tuondoe ubaguzi huu wa KIPUMBAVU unaopandikizwa na wanasiasa kwa kutumia vyombo vya dola. Kumbagua mtanzania mwenzio kwa sababu ya itikadi za kisiasa haina tofauti na ubaguzi wa rangi, au ubaguzi mwingine wowote ule. Ni UPUMBAVU kufikiri kuwa ukiwa CCM unakuwa binadamu zaidi kuliko mwenzio asiye CCM.
Tar.03/11/2019 Chama cha mapinduzi tawi la UDOM, kilitoa taarifa ya kuwakaribisha chuoni wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Taarifa hiyo ilibandikwa ktk mbao za matangazo (kwa ruhusa ya uongozi wa chuo), kwenye miti, kuta za mabweni, na maeneo mbalimbali ya chuo. Pia ilisambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Hakuna aliyehoji, aliyekemea, wala aliyesema CCM wanaingiza siasa vyuoni.
Siku chache baadae, Shirikisho la wanafunzi ambao ni wanachama wa CHADEMA chuoni hapo (CHASO UDOM) nao wakatoa tangazo kama lile la CCM la kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuoni. Walipoenda kwa Dean of students kuomba kibali cha kubandika tangazo hilo kwenye mbao za matangazo wakanyimwa, na kukaripiwa vikali.
Kwa ustaarabu hawakutaka kuchafua kuta za mabweni (kama wenzao walivyofanya), badala yake wakaamua kusambaza taarifa yao kupitia mitandao ya kijamii.
Mwenyekiti wa tawi hilo Bw.Henry Mang'era ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa 3 akatuma taarifa hiyo kwenye magroup mbalimbali ya whatsapp. Kesho yake akakamatwa na kupelekwa mahabusu kituo cha Polisi Chimwaga. Kosa lake ni kusambaza taarifa inayoleta taharuki na kushawishi wanafunzi kufanya siasa chuoni kinyume cha sheria.
Kwa muda wa wiki mbili sasa polisi wamemshikilia, wakimpiga bila kumpeleka mahakamani. Wamekataa kumpatia dhamana licha ya jamaa zake kuwaomba polisi kumpa dhamana au kumpandisha mahakamani ili akajibu mashtaka yanayomkabili.
Waliomtembelea kituoni juzi wanasema alikua anachechemea na kushindwa kusimama vizuri. Inadaiwa alipigwa na kupata majeraha sehemu za goti.
Polisi wanafanya haya wakijua kabisa ni kinyume cha sheria, kwa sababu mtuhumiwa hapaswi kukaa kituoni masaa 48 bila kupandishwa kizimbani. This is detention without trial, ambayo haina tofauti na waliyofanya makaburu kule SA. Mang'era apelekwe mahakani, kama kuna kosa mahakama itaamua.
#Justice4Mangera
Tar.03/11/2019 Chama cha mapinduzi tawi la UDOM, kilitoa taarifa ya kuwakaribisha chuoni wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Taarifa hiyo ilibandikwa ktk mbao za matangazo (kwa ruhusa ya uongozi wa chuo), kwenye miti, kuta za mabweni, na maeneo mbalimbali ya chuo. Pia ilisambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Hakuna aliyehoji, aliyekemea, wala aliyesema CCM wanaingiza siasa vyuoni.
Siku chache baadae, Shirikisho la wanafunzi ambao ni wanachama wa CHADEMA chuoni hapo (CHASO UDOM) nao wakatoa tangazo kama lile la CCM la kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuoni. Walipoenda kwa Dean of students kuomba kibali cha kubandika tangazo hilo kwenye mbao za matangazo wakanyimwa, na kukaripiwa vikali.
Kwa ustaarabu hawakutaka kuchafua kuta za mabweni (kama wenzao walivyofanya), badala yake wakaamua kusambaza taarifa yao kupitia mitandao ya kijamii.
Mwenyekiti wa tawi hilo Bw.Henry Mang'era ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa 3 akatuma taarifa hiyo kwenye magroup mbalimbali ya whatsapp. Kesho yake akakamatwa na kupelekwa mahabusu kituo cha Polisi Chimwaga. Kosa lake ni kusambaza taarifa inayoleta taharuki na kushawishi wanafunzi kufanya siasa chuoni kinyume cha sheria.
Kwa muda wa wiki mbili sasa polisi wamemshikilia, wakimpiga bila kumpeleka mahakamani. Wamekataa kumpatia dhamana licha ya jamaa zake kuwaomba polisi kumpa dhamana au kumpandisha mahakamani ili akajibu mashtaka yanayomkabili.
Waliomtembelea kituoni juzi wanasema alikua anachechemea na kushindwa kusimama vizuri. Inadaiwa alipigwa na kupata majeraha sehemu za goti.
Polisi wanafanya haya wakijua kabisa ni kinyume cha sheria, kwa sababu mtuhumiwa hapaswi kukaa kituoni masaa 48 bila kupandishwa kizimbani. This is detention without trial, ambayo haina tofauti na waliyofanya makaburu kule SA. Mang'era apelekwe mahakani, kama kuna kosa mahakama itaamua.
#Justice4Mangera