CCM na Maigizo yake ya Kuwajali Wananchi

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
Mpaka sasa napata shida kuwaelewa hawa chama tawala. Rais wa nchi ni mwenyeketi wa chama. Waziri Mkuu ni mjumbe wa halmashauri kuu, kiongozi wa caucaus ya CCM bungeni, na ndiye msimamizi mkuu wa shughuli zote za serikali. Spika wa Bunge ni mjumbe wa halmashauri kuu ya chama, Mawaziri kibao ni viongozi katika kamati kuu ya chama km kina Mwigulu, Asha Rose, na wengineo. Kwa maneno mengine karibia viongozi wote wakuu wa serikali ndio hao hao viongozi wakuu wa chama tawala.

Sasa inakuwaje kinana na nape wajifanye wanaumizwa sana na matatizo ya wananchi na kushanaa shida zao na kubaki kulalamika km hao wananchi wakati wao ndio wana miundo mbinu yote ya kufanya mabdiliko ili kero za wananchi zipungue? Wanashindwa nini kwa mfano kuamua kwamba kuanzia leo posho posho zilizoeleweka mwisho? Kuanzia leo hakuna kiongozi wa CCM kutumia shangingi? Ni nini kinawazuia kufanya uamuzi imara wa kuabdilisha maisha ya watanzania kwa kuamua kubana matumizi kwa kupunguza kuishi maisha ya anasa huku wengine wanyonge wanaumia? Wanashindwa nini wakati miundo mbinu yote wanayo na uwezo wanao kwa sababu wao ndio wenye serikali?


Kwa nini waje kushangaa huku mitaani matatizo yetu kana kwamba ni mageni na hawakuwahi kuyasikia? Kwa nini wasikae chini waksema enough is enough. sasa tunataka kubadilisha maisha ya mtanzania wakakaa na wakachukua uamuzi bila kuhiatjai kuja mitaani kulia na kulalamika na wananchi wakati wao ndio baba na mama? Wanamlalamikia nani?


Ni lini CCM wataacha haya maigizo na kuhaingaikia shida za wananchi kwa dhati bila unafiki? Wapinzani walalamike na nyie mlalamike? Vipi? CCM tunataka vitendo sio maigizo! Kiongozi mkuu kabisa wa chama huhitaji kuzunguka mikoani kuwaita mawaziri wako ambao kimsingi ni wewe uliyewateua (kwa sababu katibu mkuu na mwenyekiti wa chama wanshirikiana kwa ukaribu kushauriana kuhusu nani ateuliwe) ni mizigo. Huku ni kuwahadaa wananchi. haiwezekanai baba unapita mitaani unamlalamikia mke wako.. oo sijui huyu mwananmke yuko hivi na hivi, oo sijui hafai, sasa si umuache si una maamuzi wewe ya kumuacha km umeshindwa kumrekebisha?

kwani hao mawaziri waliwekwa na vyama vya upinzani? Si mliwaweka nyie? Sini makada wenu? Sasa kwa nini km wanaharibu msiwatoe mnakuja kutulilia sisi wananchi? Vitambi vinazidi kuongezeka huku mnajidai mnawalilia wananchi? Inawezekanje wewe kuwa unaumizwa na matatizo ya wananchi huku kitambi kinazidi kuongezeka? kweli nape? Hulali ukiwaza namna ya kutatua kero za wananchi wakati huo huo likitambi linazidi kumea? Are you serious? C'mon let's be serious!
 
Mkuu uzuri ni kuwa wananchi washashutuka na haya maagizo.
 
kinana mnafiki mkubwa kwani hao mawaziri wanatoka nje ya ccm na aliyewateua ameziba masikio
 
Siku hizi wanajifanya kula kwa mama lishe.

Huko Nzega na Igunga Kinana na Nape walikunywa Gongo na wananchi.
 
Acha ushabiki wewe.hao ni watendaji wa chama wanaowajibika kwa wanachama wao. Ni lazima waende kuibua kero na kuzileta serikalini ili zishughulikiwe. Hawa sio wapanda chopa wanaokwenda kuwaonyesha wananchi jinsi wanavyojua kutumia.
Mpaka sasa napata shida kuwaelewa hawa chama tawala. Rais wa nchi ni mwenyeketi wa chama. Waziri Mkuu ni mjumbe wa halmashauri kuu, kiongozi wa caucaus ya CCM bungeni, na ndiye msimamizi mkuu wa shughuli zote za serikali. Spika wa Bunge ni mjumbe wa halmashauri kuu ya chama, Mawaziri kibao ni viongozi katika kamati kuu ya chama km kina Mwigulu, Asha Rose, na wengineo. Kwa maneno mengine karibia viongozi wote wakuu wa serikali ndio hao hao viongozi wakuu wa chama tawala.

Sasa inakuwaje kinana na nape wajifanye wanaumizwa sana na matatizo ya wananchi na kushanaa shida zao na kubaki kulalamika km hao wananchi wakati wao ndio wana miundo mbinu yote ya kufanya mabdiliko ili kero za wananchi zipungue? Wanashindwa nini kwa mfano kuamua kwamba kuanzia leo posho posho zilizoeleweka mwisho? Kuanzia leo hakuna kiongozi wa CCM kutumia shangingi? Ni nini kinawazuia kufanya uamuzi imara wa kuabdilisha maisha ya watanzania kwa kuamua kubana matumizi kwa kupunguza kuishi maisha ya anasa huku wengine wanyonge wanaumia? Wanashindwa nini wakati miundo mbinu yote wanayo na uwezo wanao kwa sababu wao ndio wenye serikali?


Kwa nini waje kushangaa huku mitaani matatizo yetu kana kwamba ni mageni na hawakuwahi kuyasikia? Kwa nini wasikae chini waksema enough is enough. sasa tunataka kubadilisha maisha ya mtanzania wakakaa na wakachukua uamuzi bila kuhiatjai kuja mitaani kulia na kulalamika na wananchi wakati wao ndio baba na mama? Wanamlalamikia nani?


Ni lini CCM wataacha haya maigizo na kuhaingaikia shida za wananchi kwa dhati bila unafiki? Wapinzani walalamike na nyie mlalamike? Vipi? CCM tunataka vitendo sio maigizo! Kiongozi mkuu kabisa wa chama huhitaji kuzunguka mikoani kuwaita mawaziri wako ambao kimsingi ni wewe uliyewateua (kwa sababu katibu mkuu na mwenyekiti wa chama wanshirikiana kwa ukaribu kushauriana kuhusu nani ateuliwe) ni mizigo. Huku ni kuwahadaa wananchi. haiwezekanai baba unapita mitaani unamlalamikia mke wako.. oo sijui huyu mwananmke yuko hivi na hivi, oo sijui hafai, sasa si umuache si una maamuzi wewe ya kumuacha km umeshindwa kumrekebisha?

kwani hao mawaziri waliwekwa na vyama vya upinzani? Si mliwaweka nyie? Sini makada wenu? Sasa kwa nini km wanaharibu msiwatoe mnakuja kutulilia sisi wananchi? Vitambi vinazidi kuongezeka huku mnajidai mnawalilia wananchi? Inawezekanje wewe kuwa unaumizwa na matatizo ya wananchi huku kitambi kinazidi kuongezeka? kweli nape? Hulali ukiwaza namna ya kutatua kero za wananchi wakati huo huo likitambi linazidi kumea? Are you serious? C'mon let's be serious!
 
mtu mmoja aliwahi kutoa angalizo kuwa mkiwarudisha madarakani basi mjue mtakwisha, Watanzania wengi hawakuelewa maana yake kama wasivyoweza kuelewa kuwa ni kweli tumeshakwisha.
Sasa haya maigizo ya kandambili ndio fungakazi nyingine, na wadanganyika tunavyopenda maigizo na usanii tutakoma!
 
Siku hizi wanajifanya kula kwa mama lishe.

Huko Nzega na Igunga Kinana na Nape walikunywa Gongo na wananchi.

Wanafiki wakubwa sana hawa. Pia hao wananchi wanaokubali kufanyiwa maigizo haya nao ni "wajinga"
ImageUploadedByJamiiForums1400673009.728408.jpg


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Acha ushabiki wewe.hao ni watendaji wa chama wanaowajibika kwa wanachama wao. Ni lazima waende kuibua kero na kuzileta serikalini ili zishughulikiwe. Hawa sio wapanda chopa wanaokwenda kuwaonyesha wananchi jinsi wanavyojua kutumia.
Kero zinaibuliwa kwa miaka 50 unafikiri hawazijui.
 
Acha ushabiki wewe.hao ni watendaji wa chama wanaowajibika kwa wanachama wao. Ni lazima waende kuibua kero na kuzileta serikalini ili zishughulikiwe. Hawa sio wapanda chopa wanaokwenda kuwaonyesha wananchi jinsi wanavyojua kutumia.

Haya ndiyo tunayoita maigizo! kazi ya hao wabunge wenu, madiwani wenu, wenyeviti wa vijiji, wakuu wa wilaya, mikoa ambao wote ni makada wenu wao wameshindwa kuibua hayo mpaka kinana akayaibue? Usanii mtupu! Kimsingi chama ndio serikali, sasa mnaipelekea serikali ipi? Ya chadema? Matatizo ya wananchi yako wazi wala hayahitaji kuibuliwa yanatakiwa kufanyiwa kazi, basi! Huku kujifanya kuibua matatizo ya wananchi ndio usanii wenyewe! Kwa hilo eneo halina mbunge wa kusemea au madiwani?
 
Halafu naona wamebuni uniform mpya. CCM huwa wanadahani wanachukiwa kwa sababu ya Uniform zao za kijani? Jamani hapana mnchakuiwa kwa sababu ya umaskini mliowaletea watanzania! Siku hizo naona Nape yeye kaamua kushona uniform zake za kijani kwa mtindo wa kombati za chadema. Kukopi na kupaste! Wanadhani kombati za chadema ndizo zinazowavuitia wananchi kuupenda upinzani? Hapana! Ni kwa sababu wapinzani wanazungumza lugha ya wananchi, wanawatetea! Sio kombati! Nape Bwana!
 
Ni dhambi kwa kiongozi kula kwa mama ntilie? Nyie vijana mmekariri maisha.
Hapana! Ni dhambi kwa kiongozi kuwakebehi wananchi. Unatoka kujifanya kula kwa mamalishe halafu unapanda shangingi unaenda kulala three star au four star hotel! Unafiki mkubwa!
 
Acha ushabiki wewe.hao ni watendaji wa chama wanaowajibika kwa wanachama wao. Ni lazima waende kuibua kero na kuzileta serikalini ili zishughulikiwe. Hawa sio wapanda chopa wanaokwenda kuwaonyesha wananchi jinsi wanavyojua kutumia.

Ha ha ha ha ha..
Kinana msanii sana...eti na yeye akawa kama wananchi..1. Akawa na manati anawinda ndege na watoto 2. Akawa anaendesha ringi na watoto 3. Akawa anaendesha baiskeli akiambatana na yule tumbotumbo anayetumia mkorogo

Ila waliumbuka na yale maV.10 yao kila mmoja na la kwake walivyonasa kwenye matope..ha ha ha...wananchi wakajua kumbe ni zuga tu..
 
"kwani hao mawaziri waliwekwa na vyama vya upinzani? Si mliwaweka nyie? Sini makada wenu? Sasa kwa nini km wanaharibu msiwatoe mnakuja kutulilia sisi wananchi? Vitambi vinazidi kuongezeka huku mnajidai mnawalilia wananchi? Inawezekanje wewe kuwa unaumizwa na matatizo ya wananchi huku kitambi kinazidi kuongezeka? kweli nape? Hulali ukiwaza namna ya kutatua kero za wananchi wakati huo huo likitambi linazidi kumea? Are you serious? C'mon let's be serious!"

Inatia moyo kuona kwamba kuna Wabongo kama wewe mnaoona madudu na kujitoa kuelimisha umma. Kwa kuongezea hapo ili kuthibitisha MAIGIZO ni kwamba hao hao ambao Kinana na Nape wanawalalamikia kuwa ni mizigo ndio hao hao wanaacha shughuli za Bunge na ofisi zao kuja kuwapokea katika majimbo yao!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mimi nimesema na nitasema tena na tena CCM ni mahayawani na mtu anayewaunga mkono ni hayawani. Hawa mahayawani have never been serious. Wanacheza na ujinga wa wabongo PERIOD. Hadi Wabongo walio wengi tutakapotoka katika boksi la ujinga ndipo haya ma-beast yataacha MAIGIZO. We Angalia tu hata the so called mchakato wa Katiba mpya - ni MAIGIZO kwa kwenda mbele.
 
Back
Top Bottom