Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Hivi karibuni limezuka wimbi la kuwarubuni wapinzani hasa viongozi kujiunga na chama cha mapinduzi kwa njia mbalimbali zikiwemo pesa na ahadi,
sina haja ya kutaja matukio ambayo pengine na wewe unayashuhudia yakiendelea kutokea kwa baadhi ya madiwani wa upinzani kurubuniwa.
Sijui kwanini hii hali inatokea sasa au labda ni baada ya Chama cha Mapinduzi CCM kuona kinazidi kupoteza mvuto mbele ya wananchi
siku hadi siku au ni baada ya kuhisi filosofia yao ya kujivua gamba waliyoianzisha haijapokelewa kama walivyotarajia.
Najaribu kujiuliza hii demokrasia mpya ya kulazimisha a forced democracy imetoka wapi na inatupeleka wapi, na je hii demokrasia itakisaidia chama au ndiyo inakididimiza zaidi, je wapinzani wamejipanga vipi kukabiliana na wimbi hili ambalo linatishia uhai wa vyama vyao.
Je hao viongozi wenye tamaa hiyo naweza kuwaita waroho jamii iwafanye nini pindi wanapobainika kwa sababu wanakera wanaudhi na wanarudisha nyuma maendeleo chukulia mfano wa sakata la madiwani wa Arusha.
Na mwisho je ni halali kwa chama kutumia mbinu hii kuvutia wananchi? katiba inasemaje, vipi msajili wa vyama anaafiki maana sijasikia akikemea jambo hili. Nimeongelea CCM zaidi lakini sina maana kuwa vyama vya upinzani havirubuni wanaCCM kujiunga navyo kwa njia ya pesa. Naomba kuwasilisha.
sina haja ya kutaja matukio ambayo pengine na wewe unayashuhudia yakiendelea kutokea kwa baadhi ya madiwani wa upinzani kurubuniwa.
Sijui kwanini hii hali inatokea sasa au labda ni baada ya Chama cha Mapinduzi CCM kuona kinazidi kupoteza mvuto mbele ya wananchi
siku hadi siku au ni baada ya kuhisi filosofia yao ya kujivua gamba waliyoianzisha haijapokelewa kama walivyotarajia.
Najaribu kujiuliza hii demokrasia mpya ya kulazimisha a forced democracy imetoka wapi na inatupeleka wapi, na je hii demokrasia itakisaidia chama au ndiyo inakididimiza zaidi, je wapinzani wamejipanga vipi kukabiliana na wimbi hili ambalo linatishia uhai wa vyama vyao.
Je hao viongozi wenye tamaa hiyo naweza kuwaita waroho jamii iwafanye nini pindi wanapobainika kwa sababu wanakera wanaudhi na wanarudisha nyuma maendeleo chukulia mfano wa sakata la madiwani wa Arusha.
Na mwisho je ni halali kwa chama kutumia mbinu hii kuvutia wananchi? katiba inasemaje, vipi msajili wa vyama anaafiki maana sijasikia akikemea jambo hili. Nimeongelea CCM zaidi lakini sina maana kuwa vyama vya upinzani havirubuni wanaCCM kujiunga navyo kwa njia ya pesa. Naomba kuwasilisha.