CCM Mwisho wake kuwepo kama chama tawala ni 2020

Naona upinzani safari hii watashinda uchaguzi kwa kupigiwa kura na wamarekani. Mimi nashangaa hivi wamarekani nyinyi mnawaona watu sana eeh? Pole sana wale hawanaga marafiki huwaga wazee wa masilahi basi. Mjitathimini
Ni wazee wa maslahi,Ina maana mi macho alienda kuwabebembeleza awape na kuwaongezea migodi ya uranium kule Namtumbo ili wasishinikize jamaa kutoka madarakani kutokana na kuonesha kubariki uchafu wote unaotendeka nchini kwa kukaa kimya bila hata kuwakemea wanaofanya hivo?.
Nilikuwa nawaza tu
 
Tatizo hata vyama vya upinzani vifurukute vipi haviwezi kuachiwa na washika dola kukua na hata kushinda. Mbona washika dola wenyewe washasema!

Na hii siyo mara ya kwanza kutamkwa, sio Tanzania pekee, ni hata katika nchi nyingine za Afrika.

Hata hivyo binadamu ni viumbe wanaoishi kwa kubadilika kifikra. Itachukua muda lakini CCM haiwezi kudumu milele kama wenyewe wanavyo tangaza.

Na kwamba hiyo haitakuwa maajabu ya dunia. Dunia imesha shuhudia mengi yakitokea, mengine hata hayakupata kufikiriwa.

Inapendeza kupata chama mbadala kutawala, lakini kwa mazingira yaliyopo ni vigumu. Na kwamba hakuna chama kitakachopewa hiyo lulu katika kisahani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio yy tu wanasiasa wetu wote ngoja nikupe mfano mwaka fulani nilikuwa Ikulu ya Zanzibar kwenye maongezi na Komandoo akaniuliza hv una fikiria Ukarume unaweza kurudi tna znz siku jibu kitu mwenyewe akasema ilo aliwezekani ila baada muda nasikia alitaka kujiongezea muda madarakani isiwe miaka 10 tna...

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Rubawa, Kamandoo hata mimi nilizungumza nae, ni kweli alipanga kujiongezea au kumuweka mtu wake naomba nimuhifadhi, CCM bara ikafanya mambo, Karume akasimamishwa na kwenye matokeo, kiukweli naomba nisiseme ila wote wanajua kilichotokea.
Komandoo aliadhibiwa kiaina kama Aboud Jumbe.
P
 
Ukiacha watu wachache ambao kwa sababu zake mwenyewe Mh Magufuli amekubari kuwapa madaraka makubwa kudhurumu kunyanyasa sie wote tunao jaribu kuonyesha mapungufu machache ili km Taifa twende Pamoja. Ila yupo Sawa kwenye mengi Nasimama Nae Mh Magufuli Pamoja Dhuruma zote juu yngu na baadhi unazijua vzuri...

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Rubawa, hayo unayoyasema mimi pia nayapitia, baada ya lile swali la Ikulu, kuna watu wanafanya mambo ya kiajabu ajubu as if wametumwa na yeye, kwasababu wanajua huwezi kupata access kuuliza, lakini through circumnavigating, nimeweza kubaini hao watu hawajatumwa na Magufuli, tena usikute hata Magufuli mwenyewe hajui nini watu wake wanawafanyia dhulma kubwa watu in his name!.

Kwenye wateule wake, unaweza kukuta sii kweli
Mh rais Magufuli amewapa wateule wake madaraka makubwa ya kudhurumu na kunyanyasa kwa kisingizio cha kutumwa na rais, hivyo wewe kudhani ni kweli wametumwa na rais Magufuli hivyo kudhania kuwa Mh rais Magufuli anajua dhuluma zote juu yako, kumbe in reality rais Magufuli hajamtuma yoyote kufanya dhulma zozote na hivyo hajui chochote kuwa huku chini kuna watu wana nyanyasika.

The best way kuujua ukweli ni kufanya cross checking kwa kutumia njia inayoitwa circumnavigating ikishindikana, then unatumia direct.

Kuna mambo mengi mabaya wanamhisi ni rais Magufuli, lakini ukweli sio yeye na wala hajui kitu.

Mfano kuna watu wanadhani lile tukio la zile pyu pyu pale Dodoma ni yeye, kumbe sio yeye wala hakujua kitu, ila...

Mambo mengine ni too sensitive tuyaache yapite ila yote yana mwisho haya.
Pole kwa yote.
P
 
Wewe ndiye unaota
Ndoto unazoota baada ya kunywa kvant ipo siku utaenda kumshika makalio mamako mkwe, ndugu hizo pombe zimekushinda ziache, ni hivyo tyu. La maaskofu wenu limekuchachia umerukia jengine.

In God we Trust
 
Huo ndiyo ukweli kuwa ccm inafikia kikomo mwezi October
Ni ajabu sana kuwa washabiki was CCM hamtaki kuamini hivyo lakini walio madarakani wameshaujua ukweli huo ndio maana wanataka kutumia ujio wa ugonjwa wa Corona kama excuse ya kuahirisha uchaguzi wa Octoba.
CCM wanajua wazi kuwa kiburi cha Magufuli kimewaponza sana na kuwaondolea trust ndani na nje ya nchi na akakosekana wa kumshauri.
Suala la Tumehuru wamegundua wapinzani hawatanii tena, na nchi wahisani wameshika bango. Jee wataponea wapi?View attachment 1395442

Sent using Jamii Forums mobile app

In God we Trust
 
Sijawah kusikia taarifa ya USA kuhusu democrasia ya China... Tumejirahisisha sana
Na US hajawahi kuwanunulia China vyandalua vya malaria au msaada wa ARV.
Unapokuwa masikini na unalelewa hata vitu vidogo vidogo lazima ukubali hata mipango yako ya maisha anayekulea ana ihakiki.
Ni kama mtoto wako nyumbani, waweza kumsimamia hata ratiba ya kuoga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Itawatawala milele nyinyi mazuzu msiyo na faida kwa taifa
Maneno haya ya Mwalimu Nyerere ni ushahidi wa CCM kutawala milele" Rais bora atatoka CCM". ni ukweli mchungu lakini lazima mkubali Hilo.

Kila nikifikiri ni kwa namna gani CCM itaondoka nakosa majibu ya kuniridhisha hivyo Imani na matumaini yangu ya CCM kutawala milele yakishika kasi.

Ukweli ,CCM haina mpinzani hata tukibeza ukweli huu utatuweka huru tukiweka matumaini ya CCM kutawala milele kuliko kutoka miaka ya karibuni

In God we Trust
 
Mawazo uliyo nayo wewe leo ndio mimi pia nilikuwa nayo kabla ya July,2017, Baada ya kupata kibarua cha kuwa National Sales Manager wa kampuni kubwa binafsi ya usambazaji bidha za matumizi mbali mbali ya nyumbani, ilinipa fursa ya kutembelea karibu Wilaya zote na hasa miji mikubwa na midogo karibu maeneo yote ya Tanzania.

Nimejifunza mengi katika mzunguuko huo ambao nakaribia miaka 3, hali hiyo imenibadilisha sana na nilivyokuwa nafikiri kabla kuhusu kukubalika kwa vyama hasa vyama vya upinzani kulinganisha na CCM, kwa ushuhuda wa matembezi ya kikazi nilibadilisha muono wangu. Hatuna mgombea wa kuitikisha CCM kwa nafasi ya Urais labda kwa ushabiki. Tuna kazi ngumu sana ya kufanya na tunahitaji kufanya kazi ya kutosha.
Nina wasi wasi kuwa hata wabunge wa majimbo wanaweza wakapungua sana. Sidhani hata kumtikisa Mkulu tutaweza labda afanye blanda kubwa ambayo itamwodolea imani wapiga kura.

KWA MFANO: Ukisema hana uwezo wa kujieleza vizuri au kuelezea masuala ya kitaifa na kimataifa vizuri, MAJIBU....walikuwepo waongeaji wazuri sisi walitusaidia nini, sisi tunataka kazi na tunataka matokeo tuu na sasa tunaona jaribu kutembea nchi nzima inajengwa leo hii.

Ukiwaeleza jamaa amebana sana upande wa siasa
MAJIBU.. sasa kazi yetu ya kulima siasa inatusaidia nini?
Walioko vijijini wanaona tufauti ndogo sana ya mapato kati ya siku za nyuma na kulinganisha na leo. Hasa ukitilia maanani mazao yao mengi ya kilimo wanayauzwa na wanapata pesa labda kwa mazao machache ya biashara.

Kuna mengi ningechangia humu, lakini kwa kifupi elimu ya demokrasia bado sana miji mingi midogo na vijijini. Ngoja wazoee umeme, maji, barabara, na hospitali mpya zilizojengwa nina hakika baada ya kuzoea, mahitaji yao yatakua na hapo ndipo wataanza kuigeukia CCM kwa kuhitaji mambo mengi Zaidi..

Na wenzetu CCM wameweka watu wao katika kila ngazi ya utawala kuanzia nyumba kumi.

UPINZANI BADO TUNA KAZI KUBWA YA KUFANYA. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Unajua kwamba katika kipindi cha miaka minne iliyopita hakuna siasa za upinzani zilizo fanyika nchini kote zaidi ya kesi za polisi na mahakama kwa wapinzani? Unajua kwamba viongozi wengi wa upinzani walidhoofishwa kisha kulazimika kuikubali CCM hadharani ikiwa ni mbinu ya kuipaisha CCM?
Kama wewe ni National Sales Manager basi naipa pole hiyo kampuni unayofanyia kazi, kwani kama umekosa uwezo wa kuligundua hili uwezo wako utakuwa chini mno.
Hivi unajua kwa nini vijijini Waalimu walitumika sana kuijengea sifa CCM? Ndio wanaoaminika na ndio kundi la wasomi walio karibu nao. Jee mahusiano ya walimu na serikali ya CCM awamu ya tano unayajua kwa sasa?
Watumishi wengine jee? Nenda kwa wafanyabiashara ambao wanafunga biashara zao kila siku utawaambia nini na Magufuli? Usidanganyike na sifa za usoni ni kwa vile wanao mchalenji wanakiona cha mtema kuni kimya kimya.
Tumehuru na wapinzani kupata majukwaa ya kusemea nyongo zao ndio utajua kuwa CCM maisha yake yamekamatiwa na Uzi mdogo sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Gerald Magembe, kwanza asante kwa mchango huu, kama kuna Chadema wenye akili na wamekusoma hapa, wata copy na kuwatumia viongozi wao

Hakuna kitu kigumu na kinachotumia fedha kama research, hapa umewafanyia Chadema research ya bure, wangepaswa wakulipe. Michango kama hii yenye ukweli mchungu ndio itawasaidia wapinzani wa kweli. Numbers don't lie, CCM ina wajumbe wa shina, wale wajumbe wa nyumba kumi, huko ndio grassroots level, baada ya wajumbe wa mashina, wana mashina ya wakereketwa karibu vijiwe vyote ni CCM, wanakuja matawi, wanakua vijiji, kata, wilaya, jimbo, mkoa. Ndani ya ofisi zote za CCM kuna Jumuiya zao tatu za wanawake, vijana na wazazi, wakati kwenye vyama vya upinzani kuna maeneo hakuna hata ofisi moja ya chama chochote cha upinzani wilaya nzima.

Nikawashauri Chadema as the main opposition party, they should invest on people, kwa kutumia modern ways of mass mobilization through mass communications. Fedha zilizotumika kununua yale mandinga makubwa ya M4C zingetosha kabisa kuanzisha redio yake, tv yake, gazeti lake na interactive online forum ili to reach the masses wa grassroot level, wao wameng'ang'ania siasa za kiharakati za mikutano ya siasa na maandamano.

Utamwambia nini mtu anayesomeshewa bure watoto wake, kapatiwa maji, barabara, hospitali na huduma muhimu za jamii?.

Kila ukiwaambia ukweli huu wa 2020 Chadema wanakarika na kutukana hovyo humu mitandaoni.

Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? - JamiiForums

Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?!. - JamiiForums

Ile 2015 Chadema ilikuwa ichukue nchi, ika bugi tuu step

Kuelekea 2015: CHADEMA Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...! - JamiiForums

Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ... - JamiiForums

P.
Mkuu Pascal nimefurahi sana kuona muono wangu tupo wengi hasa kwa yeyote ambae kutafiti kidogo. Kwa hali inavyo endelea tutaruhusu vyama vya upinzani kukosa nguvu kabisa kama hatuta weka nguvu ya kutosha kubalisha hii hali.

Kwa hiyo kila tuandikapo kuhusu kufa kwa CCM naomba ukweli huu mchungu tuwe tukiujuwa. Kutembelea wananchi vijijini na miji midogo utajifunza mengi sana. Asilimia karibu 80% ya Watanzania vijijini na Miji midogo wanaamini Magufulu ni mtuu wao. Kila kilicho fanya vizuri na Halimashauri, Mikoa, Vijiji utasikia Viongozi wanasema kazi ya Mkulu na wananchi imeanza kuwaingia kuwa kila kizuri nchi hii kinafanya na Mkulu pekee au maelekezo yake.

Viongozi wengine wote wanaonekana ni wasumbufu tuu, Upinzani tusi zembee kuna kazi kubwa ya kufanya na kwa hali ilivyo kama uchaguzi unafanyika leo tutasumbuka na matokeo kwa kuwa hatuto amini. MAENDELEO HAYANA CHAMA.
 
Sitaki kusema mengi kwanini kinaenda kufa ila hoja kubwa ni toka baba wa taifa afariki CCM kimekuwa kikitawala kwa ujanja ujanja na propaganda

Kikubwa zaidi hawamu ya 5 imekizika kwa kupuuza wananchi wanataka nini kiufupi ccm haifanyii kazi matakwa ya watanzania walio wengi ili swala linaenda kuwaondoa madarakani kimchezo mchezo.

Wale mliokwapua pesa za umma muanze kuzilejesha bila kusahau mliokuwa mnafanya maovu mjindae kweli kweli.

Naapa kwa jina la baba la mwana na roho mtakatifu ccm haitarudi madarakani kwa sababu ya ubishi na mtakuja kukumbuka maneno yangu mlikuwa na muda wa kujirekebisha ila kibri kibri mjiandae kisaikolojia.
Utabiri kutoka MAREKANI!!!
 
Hivi kuna mkakati gani unaoeleweka utakaoitoa CCM madarakani kwa huo muda unaosema? Watu Wa hivi huwa naamini wakati wanaandika haya walikuwa wamelewa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom