Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Nimeangalia sana mwenendo wa CCM ya leo na viongozi ambao wana historia nzito sana katika CCM na Tanzania kwa ujumla, na kufikia muafaka kwamba safari ya CCM kwenda huko wanakojua wenyewe mwisho wake sio mzuri.
Tangu uongozi wa CCM ya sasa uingie madarakani umekorofishana na karibu viongozi wote ambao huko nyuma walikuwa ni watu wenye heshima zao kubwa sana ndani ya chama.
Nakumbuka hii ni kuanzia Kingunge, Nyalandu, Prof. Mwandosya, Makamba, Membe, na Kinana! Na hata wamekua wakimchokonoa sana Kikwete, wengine kudiriki kumkosea heshima kwa kauli kwamba hakuna alofanya kulinganisha na Magufuli - kauli ambazo tungetegemea zitoke kwa watu wa vyama vya upinzani.
Hivi katika uzito wa kisiasa wa mtu kama Kinana, Makamba, leo hii ungetarajia waitwe hadharani kuhojiwa na Kamati ya Nidhamu ya CCM? Na jambo moja kubwa, hivi hawa wazito wa zamani wa CCM wanakorofishana na CCM kama chama au kiongozi mmoja tu ambaye mkipishana kauli anataka ionekane ionekane umeikorofisha CCM yote?
Nyie CCM huko mnakokwenda, au kwa usahihi zaidi, huko mnakopelekwa mwisho wake sio mzuri. Mark my words.
Tangu uongozi wa CCM ya sasa uingie madarakani umekorofishana na karibu viongozi wote ambao huko nyuma walikuwa ni watu wenye heshima zao kubwa sana ndani ya chama.
Nakumbuka hii ni kuanzia Kingunge, Nyalandu, Prof. Mwandosya, Makamba, Membe, na Kinana! Na hata wamekua wakimchokonoa sana Kikwete, wengine kudiriki kumkosea heshima kwa kauli kwamba hakuna alofanya kulinganisha na Magufuli - kauli ambazo tungetegemea zitoke kwa watu wa vyama vya upinzani.
Hivi katika uzito wa kisiasa wa mtu kama Kinana, Makamba, leo hii ungetarajia waitwe hadharani kuhojiwa na Kamati ya Nidhamu ya CCM? Na jambo moja kubwa, hivi hawa wazito wa zamani wa CCM wanakorofishana na CCM kama chama au kiongozi mmoja tu ambaye mkipishana kauli anataka ionekane ionekane umeikorofisha CCM yote?
Nyie CCM huko mnakokwenda, au kwa usahihi zaidi, huko mnakopelekwa mwisho wake sio mzuri. Mark my words.