Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Lengo la kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini ni kusikia kauli za upande wa pili za ukosoaji ili serikali ijisahihishe na itekeleze wajibu wake inavyopaswa ili ipate Imani ya wananchi.
Tumeshuhudia katika utawala huu wa awamu ya 5 ya serikali ya CCM ikiweka "mizengwe" mingi ya shughuli za upinzani. Naamini katika utawala huu wa awamu ya 5 wapinzani wanafanya shughuli zao katika mazingira magumu sana kuliko katika awamu zilizopita za serikali za CCM za awamu ya 3 na 4
Wakati hali ya kuendesha siasa kwa vyama vya upinzani ikiwa ni ngumu sana, hali ni tofauti wa upande wa CCM ambako Mwenyekiti wake wa Taifa tumemshuhudia akizunguka nchi nzima akifanya shughuli za kukinadi chama chake cha CCM huku akitumia mwamvuli wa shughuli za kiserkali!
Hivi kama kweli Mwenyekiti wa Taifa wa CCM angekuwa anafanya shughuli za kiserkali katika ziara hizo tusingeshuhudia upokeaji wa madiwani "walionunuliwa" kutoka Chadema katika ziara hizo??
Kama kweli ziara hizo zingekuwa za kiserikali tusingeshuhudia ziara hizo zikiandaliwa na makada wa CCM huku wahudhiriaji wakiwa "wameandaliwa" kwa kuvalia sare zao za CCM!
Pia tumeshuhudia ziara hizo zikipata coverage kubwa sana ya vyombo vya habari vya Umma na vya binafsi.
Tumeshuhudia pia vyombo hivyo vya habari vikirusha matangazo hayo Live katika masaa ya kazi ambayo sisi wananchi tuliambiwa kuwa sababu kubwa ya kutorushwa matangazo Live ya Bunge ni kuwa wakati huo ni wakati wa kazi kwa hiyo wananchi hawapaswi kuangalia Bunge Live na badala yake wanatakiwa "wachape" kazi muda huo!
Tatizo kubwa wanalolifanya CCM ni kuanganisha shughuli za kiserikali na shughuli za Chama chao kwa wakati mmoja.
Hapo CCM ndipo wanapofanya kosa kubwa, kuruhusu wao wafanye siasa, na wapinzani wasifanye!
Kosa lingine kubwa ni kukataa kukosolewa na pale unapokosoa, ndipo unapomuongezea ulaji yule unayemkosoa!
Refer issue ya aliyekuwa DC wa Arumeru, baada tu ya kukosolewa kuwa "anagawa" rushwa kwa madiwani wa Chadema, bosi wake ndipo alipompa "ulaji" wa Mkuu wa Mkoa!
Refer pia RC wa Dar, licha ya maelfu ya watumlshi wa Umma kutimuliwa kazi kwa kufoji vyeti, lakini ilipofika kwa RC wa Dar, tulimsikia Bosi wake akitamka kuwa yeye hajali kama RC wake kafoji vyeti, ilimradi tu anamkamatia wauzaji wa madawa ya kulevya, huyo ndiye RC bora kabisa nchini!
Najua uwanja wa ushindani hapa nchini hauko sawa, na hilo suala wananchi wameshalibaini, na kawaida wananchi huwa "wanasympasize" na watu wanaokandamizwa.
November 26 kuna chaguzi ndogo za kuziba nafasi zilizo wazi za madiwani na hapo kwa kuwa kura ni ya siri, hapo ndipo wananchi watakapoonyesha "hasira" zao za kukataa uminywaji wa demokrasia, ukandamizwaji na utumiaji vibaya wa vyombo vya dola kwa nia ya kuvikandamiza vyama vya siasa vya upinzani.
CCM bila kutumia vyombo vya dola ni wepesi kuliko karatasi ya tissue!
Tumeshuhudia katika utawala huu wa awamu ya 5 ya serikali ya CCM ikiweka "mizengwe" mingi ya shughuli za upinzani. Naamini katika utawala huu wa awamu ya 5 wapinzani wanafanya shughuli zao katika mazingira magumu sana kuliko katika awamu zilizopita za serikali za CCM za awamu ya 3 na 4
Wakati hali ya kuendesha siasa kwa vyama vya upinzani ikiwa ni ngumu sana, hali ni tofauti wa upande wa CCM ambako Mwenyekiti wake wa Taifa tumemshuhudia akizunguka nchi nzima akifanya shughuli za kukinadi chama chake cha CCM huku akitumia mwamvuli wa shughuli za kiserkali!
Hivi kama kweli Mwenyekiti wa Taifa wa CCM angekuwa anafanya shughuli za kiserkali katika ziara hizo tusingeshuhudia upokeaji wa madiwani "walionunuliwa" kutoka Chadema katika ziara hizo??
Kama kweli ziara hizo zingekuwa za kiserikali tusingeshuhudia ziara hizo zikiandaliwa na makada wa CCM huku wahudhiriaji wakiwa "wameandaliwa" kwa kuvalia sare zao za CCM!
Pia tumeshuhudia ziara hizo zikipata coverage kubwa sana ya vyombo vya habari vya Umma na vya binafsi.
Tumeshuhudia pia vyombo hivyo vya habari vikirusha matangazo hayo Live katika masaa ya kazi ambayo sisi wananchi tuliambiwa kuwa sababu kubwa ya kutorushwa matangazo Live ya Bunge ni kuwa wakati huo ni wakati wa kazi kwa hiyo wananchi hawapaswi kuangalia Bunge Live na badala yake wanatakiwa "wachape" kazi muda huo!
Tatizo kubwa wanalolifanya CCM ni kuanganisha shughuli za kiserikali na shughuli za Chama chao kwa wakati mmoja.
Hapo CCM ndipo wanapofanya kosa kubwa, kuruhusu wao wafanye siasa, na wapinzani wasifanye!
Kosa lingine kubwa ni kukataa kukosolewa na pale unapokosoa, ndipo unapomuongezea ulaji yule unayemkosoa!
Refer issue ya aliyekuwa DC wa Arumeru, baada tu ya kukosolewa kuwa "anagawa" rushwa kwa madiwani wa Chadema, bosi wake ndipo alipompa "ulaji" wa Mkuu wa Mkoa!
Refer pia RC wa Dar, licha ya maelfu ya watumlshi wa Umma kutimuliwa kazi kwa kufoji vyeti, lakini ilipofika kwa RC wa Dar, tulimsikia Bosi wake akitamka kuwa yeye hajali kama RC wake kafoji vyeti, ilimradi tu anamkamatia wauzaji wa madawa ya kulevya, huyo ndiye RC bora kabisa nchini!
Najua uwanja wa ushindani hapa nchini hauko sawa, na hilo suala wananchi wameshalibaini, na kawaida wananchi huwa "wanasympasize" na watu wanaokandamizwa.
November 26 kuna chaguzi ndogo za kuziba nafasi zilizo wazi za madiwani na hapo kwa kuwa kura ni ya siri, hapo ndipo wananchi watakapoonyesha "hasira" zao za kukataa uminywaji wa demokrasia, ukandamizwaji na utumiaji vibaya wa vyombo vya dola kwa nia ya kuvikandamiza vyama vya siasa vya upinzani.
CCM bila kutumia vyombo vya dola ni wepesi kuliko karatasi ya tissue!