CCM mlindeni Mwenyekiti wenu na aibu ya Ndugai

MtuHabari

JF-Expert Member
Oct 16, 2020
321
1,019
Ni wazi kuwa sakata la uvunjifu wa katiba Bungeni linamkera sana Mheshimiwa Rais mama Samia ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM.

Tatizo ni kuwa kama Rais hapendi aonekane kuwa anaingilia mihimili mingine ya nchi kwa kutoa kauli, maana kauli ya Rais ni kama sheria.
Spika Ndugai analijua hilo na anatumia upole huo wa mama kuendelea kufanya ujinga unao aibisha Bunge, Chama chake na Rais pia.

Je, kwa nini Ndugai ambaye ni mjumbe wa Kamati kuu ya chama CCM haimuonyi kuwa ana mdhalilisha Rais? Au kwa vile ni mwanamke mnayemuona "mzuri na mweupe" kama alivyokuwa anamuona na kumuita Marehemu Rais Magufuli wakati akiwa Makamu wa Rais?

CCM ni wajibu wenu kumlinda mwenyekiti wenu dhidi ya Spika anayetumia kinga ya kibunge kumdhalilisha mwenyekiti wenu, waagizeni wabunge wenu wamshikishe adabu kwa tishio la kumn'goa kwa kura na atashika adabu.
 
Mwenyekiti na spika wanayajua madhara ya kuwaondoa akina Mdee na genge lake ndo maana itabaki kuwa kelele mpaka 2025. Hakuna kitakachofanyika.....over!!
 
Hii issue ya Ndugai na Covid 19 sio suala la kuku na yai nini kilianza.

Wakina Halima hawakupendekezwa na chama kuwa wabunge. Hivyo yote wayafanyayo yasiwe kwa Jina la chama Bali kwa majina yao.

Tume ya uchaguzi iliandikiwa ipeleke udhibitisho wa kupendekezwa kwao tume imekataa au umekaa kimya. Maana wanajua kujibu kwa wanakuwa victim wa kwanza.

Halima waliitwa kwenye vikao Hali vya chama walau waeleze ni kitu gani kiliwasibu. Wote wakikataa kwenda.

Chama kikaamua kuwafukuza uanachama.

Sasa kwa Nini wanapambana nao bungeni. Wabgekuwa bungeni kwa Jina la chama tofauti chadema isingekuwa na tatizo nao lakini bado wanaendelea kutumia nembo na jina la chama wakati wao sio wanachama.

Suala la Baraza halina mashiko kwani hawapo nje Bunge kwa lugha nyepesi wamekaidi mamlaka ya adhabu ya awali hivyo hakuna Baraza mpaka waanze kumtumikia adhabu yao ya awali.

Pili unategemea Baraza litende tofauti na adhabu ya awali Tena kwa kiburi walichoonesha na mahaba waliyonayo kwa Speaker.

Speaker alipewa official notice ya kuvuliwa kwao uanachama, tume nao walijulishwa na wamekaa kimya. Ni suala la Muda tu, anakuja DPP mwingine soon utaona
 
Acheni porojo itisheni kikao cha baraza kuu LA Chadema limalize hiyo kesi msijifiche kwa Ndugai
Ndugai anateseka sana akilini na moyoni. Anajua kuwa watu wanajua jinsi alivyoshiriki kwenye ushetani akishirikiana na marehemu na mahela. Alijifariji sana wakati wa utawala wa marehemu maana alikuwa anajua kuwa wameamua kuendesha nchi kwa kuegemea kwa ibilisi.

Sasa nguo yake ya uovu imeanguka, utawala mpya unataka kujitenga na ibilisi. Ataondokaje katika tope la uovu alimoishi siku zote? Ndiyo maana anajifanya anawaelekeza CHADEMA cha kufanya ili wakifanya hivyo, yeye Ndugai awaondoe Covid 19 kwa kisingizio kuwa CHADEMA sasa wamefuata taratibu, na hapo mwanzo hawakufuata.

Angalizo:
CHADEMA, NAWASHAURI, KAMWE WASIFANYE YALE ALIYOSHAURI NDUGAI. MWACHENI AENDELEE NDUGAI AENDELEE KUTEMBEA NA TOPE LA UOVU NA UCHAFU, HUKU NZI WAKIMWANDAMA KILA SEHEMU.
 
Ni wazi kuwa sakata la uvunjifu wa katiba Bungeni linamkera sana Mheshimiwa Rais mama Samia ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM....
Kama Ndugai an ongea mbele ya bunge la Ccm badala ya kuomba muongozo kujua spika ana pata wapi kanuni zinazo muongoza kuwalinda wabunge wasio na dhamana ya chama, wao wana mpigia makofi, hapo kuna bunge au kuna kikao cha kusifu na kuabudu?
 
Walituaminisha wamekimbia nchi na kwenda kulelewa na wanaume wa kizungu kama wakimbizi kwa sababu hapa nchini walikuwa wanatishiwa maisha na mwendazake....
Jikite kwenye mada Husika Mkuu!
 
Mama Samia anajua yote yaliyotokea maana alikua na JPM.

Suala la viti maalumu ni suala la watu kuzidiana kete ndani ya chama ya list ya wabunge wa vitu maalum. Kuna watu walishapeleka majina fake NEC tofauti na majina yaliyokuwa yametayarishwa na Bawacha Mdee akiwa mwenyekiti.

Bawacha walivyoshtuka ndio list halisi ikawekwa wazi na wakatangazwa. Kwa hiyo kuna mijitu humu inashadadia hii issue wakati hawajui nini hasa kilitokea na uhuni ambao ulilengwa kufanywa na baadhi ya uongozi wa chadema dhidi ya list halali. KImsingi mgogoro unatokana na baadhi ya majina kutokuwepo kwenye list (ambao kimsingi hawajafanya chochote kujenga na kupigania chama).

Tuwaache akina Mdee wajenge nchi bungeni, na uongozi chadema ujipange na kujisafisha ndani kwa ajili ya 2025.
 
Back
Top Bottom