Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
Nashindwa kuwaelewa CCM! Kabisa nashindwa.
* Yaliwawezesha kutwaa nchi kutoka kwa wakaloni.
* Yaliwalea.
* Yaliwawezesha kusambaza itikadi na sera zenu -- kwa mfano za ujamaa.
* Yaliwawezesha kupambana vyema na wapinzani baada ya vyama vingi kuanza.
* Yalikuwa yanawapatia ushindi wa kishindo.
CCM – inakuwa vipi leo hii maandamano yanakuwa hayafai, hayana tija, ni matumizi mabaya ya hela za walipa kodi, na kadhalika na kadhalika?
Siku hizi chuki yenu dhidi ya maandamano ni nini hasa? Tuelezeni bila ya kutafuna maneno!
Nawasilisha!
Hawa jamaa kweli wameishiwa, kumbuka juzi juzi tu 2006 walikuwa kila JK akitoka matembezini ng'ambo wanaenda kumpokea aiport na baada ya hapo kuandamana