dosama
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 912
- 957
Source Tanzania Daima
BAADA ya suala la uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini kupigwa danadana, sasa Waislamu wametaka suala hilo liingizwe kwenye Katiba mpya.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiliweka suala la uanzishwaji wa mahakama hiyo katika ilani yake ya uchaguzi mwaka 2005/2010 na kuahidi kushughulikia.
Hata hivyo, suala hilo halikushughulikiwa na katika ilani yake ya mwaka 2010 hakikuliweka suala hilo.
Mwaka jana akizungumza katika Baraza la Iddi mjini Dodoma, Rais Kikwete alinukiwa akisema serikali haitaanzisha mahakama hiyo na badala yake Waislamu wenyewe ndio waianzishe.
Hoja hiyo ilipingwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu na kutoa kauli kuwa watatumia maandamano ya usiku na mchana, kushinikiza kuanzishwa kwa mahakama hiyo.
Akizungumza katika mahafali ya nne ya wahitimu wa Kiislamu katika Chuo cha Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda, alisema hatua hiyo imefikiwa baada ya jumuiya na taasisi za Kiislamu nchini kukaa na kukubaliana jambo hilo liingizwe katika katiba ili liweze kufanikiwa.
Kutokana na hali hiyo, aliwahamasisha Waislamu nchini kujitokeza kwa wingi katika Tume ya Katiba inayoongozwa na Jaji mstaafu, Joseph Warioba na kutoa maoni yao kuhusu jambo hilo, ili hatimaye liweze kuingizwa katika Katiba mpya.
Nchi yetu imo katika mchakato wa mabadiliko ya Katiba mpya. Katiba ni dira na ngome inayolinda haki na kuweka misingi ya maendeleo kwa wananchi. Tukio hili ni kubwa, ambapo kila jamii hupigania haki zake za msingi kuzingatiwa.
Katiba iliyopo ambayo Waislamu hawakushiriki, imechangia kwa kiasi kikubwa kuwaathiri kiimani, kisiasa, kiuchumi na kijamii. Kwa maana hiyo mchakato huu ni fursa muhimu kwa Waislamu kuhakikisha haki zao za msingi zinaingizwa ndani ya Katiba mpya, alisema.
Alisema katika jambo hilo wanataka katiba isajili mahakama hiyo, mashauri ya ndoa, talaka, watoto, vifo, mirathi, wosia, wakfu na biashara yasikilizwe na kadhi na bila kutafutwa ridhaa ya mtu au warithi pamoja na mahakama hiyo kuwapa msaada wa nguvu za dola.
Alisema kwa kuwa suala hilo limechukua muda mrefu ni vema sasa utekelezwaji wake uwekwe kwa mujibu wa katiba.
Wakati umefika kwa Waislamu kupigania na kwenda kutoa maoni katika tume ya katiba, ili tuweze kupata Mahakama ya Kadhi. Waislamu wamekuwa wakipuuzwa katika masuala mbalimbali kutokana na kutowekwa katika katiba lakini sasa umefika wakati wa kupeleka maoni na si kuendelea kulalamika, alisema.
Aidha, Sheikh Ponda alisema jumuiya hiyo ambayo ni jukwaa la Waislamu la kuratibu mchakato wa Katiba nchini, masuala mengine ambayo Waislamu wanayapigania yaonekane kwenye katiba mpya, ni kuingizwa katika katiba mpya siku ya Ijumaa kutambulikuwa kuwa ni siku ya ibada ambayo itawasaidia Waislamu kupata fursa ya kwenda kuabudu kwa uhuru zaidi.
Pia tunataka katiba itambue uwepo wa Mwenyezi Mungu, itoe uhuru wa kuabudu, kwani katiba iliyopo haijatoa uhuru huo na ndiyo maana Waislamu wanazuiliwa ibada pamoja na kuvaa hijabu vyuoni, majeshini na asasi za serikali.
Alisema kuwa pia wanataka katiba itoe usawa katika elimu kwa maana ya katiba kutamka uwakilishi sawa kwa Wakristo na Waislamu katika Baraza la Mitihani la Taifa.
Kabla na baada ya uhuru chombo hiki kimeendelea kutawaliwa na Wakristo na kusababisha upendeleo mkubwa katika uteuzi na usahihishaji wa mitihani, kuwe na uteuzi wa maofisa elimu wakuu wa shule, alisema.
Aidha, alisema wanataka sheria ya ugaidi ifutwe, kuwapo kwa uwakilishi wa dini bungeni, pamoja na baraza la madiwani na mawaziri kuwa na uwakilishi wa dini.
Pia tunataka katiba iruhusu vyama vya siasa vya kidini, Waislamu na Wakristo wapokezane urais, serikali ya Tanganyika irejeshwe, kuwapo kwa muungano wa serikali tatu, urais wa muungano uwe wa awamu pamoja na kuwapo kwa serikali ya majimbo, alisema.
Sheikh Ponda kuwa masuala mengine wanayotaka kuwamo katika Katiba mpya ni mgombea binafsi, matokeo ya urais kupingwa mahakamani, rais kutounda tume ya uchaguzi, adhabu ya kifo iwekwe ndani ya katiba, misamaha ya kodi na mikataba ya kanisa na serikali ifutwe na kikosi cha kupambana na rushwa kuundwa upya na kuingizwa kwenye katiba.
Concern;
Jamani sijafafanuliwa vzr juu ya haya.
Sheria ya ugaisi ifutwe kuna nini nyuma yake?
Haki ya kusoma hivi hawa watu mmekatazwa na nani kusoma? Mponda elimu yako ni darasa la ngapi na kwa nini?
Utawala wa kupikezana kwa manufaa ya nani?
Uhuru wa kuabudu nani kawanyima?
Sheria ya biashara kwa ...... sijaelewa kivp
BAADA ya suala la uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini kupigwa danadana, sasa Waislamu wametaka suala hilo liingizwe kwenye Katiba mpya.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiliweka suala la uanzishwaji wa mahakama hiyo katika ilani yake ya uchaguzi mwaka 2005/2010 na kuahidi kushughulikia.
Hata hivyo, suala hilo halikushughulikiwa na katika ilani yake ya mwaka 2010 hakikuliweka suala hilo.
Mwaka jana akizungumza katika Baraza la Iddi mjini Dodoma, Rais Kikwete alinukiwa akisema serikali haitaanzisha mahakama hiyo na badala yake Waislamu wenyewe ndio waianzishe.
Hoja hiyo ilipingwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu na kutoa kauli kuwa watatumia maandamano ya usiku na mchana, kushinikiza kuanzishwa kwa mahakama hiyo.
Akizungumza katika mahafali ya nne ya wahitimu wa Kiislamu katika Chuo cha Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda, alisema hatua hiyo imefikiwa baada ya jumuiya na taasisi za Kiislamu nchini kukaa na kukubaliana jambo hilo liingizwe katika katiba ili liweze kufanikiwa.
Kutokana na hali hiyo, aliwahamasisha Waislamu nchini kujitokeza kwa wingi katika Tume ya Katiba inayoongozwa na Jaji mstaafu, Joseph Warioba na kutoa maoni yao kuhusu jambo hilo, ili hatimaye liweze kuingizwa katika Katiba mpya.
Nchi yetu imo katika mchakato wa mabadiliko ya Katiba mpya. Katiba ni dira na ngome inayolinda haki na kuweka misingi ya maendeleo kwa wananchi. Tukio hili ni kubwa, ambapo kila jamii hupigania haki zake za msingi kuzingatiwa.
Katiba iliyopo ambayo Waislamu hawakushiriki, imechangia kwa kiasi kikubwa kuwaathiri kiimani, kisiasa, kiuchumi na kijamii. Kwa maana hiyo mchakato huu ni fursa muhimu kwa Waislamu kuhakikisha haki zao za msingi zinaingizwa ndani ya Katiba mpya, alisema.
Alisema katika jambo hilo wanataka katiba isajili mahakama hiyo, mashauri ya ndoa, talaka, watoto, vifo, mirathi, wosia, wakfu na biashara yasikilizwe na kadhi na bila kutafutwa ridhaa ya mtu au warithi pamoja na mahakama hiyo kuwapa msaada wa nguvu za dola.
Alisema kwa kuwa suala hilo limechukua muda mrefu ni vema sasa utekelezwaji wake uwekwe kwa mujibu wa katiba.
Wakati umefika kwa Waislamu kupigania na kwenda kutoa maoni katika tume ya katiba, ili tuweze kupata Mahakama ya Kadhi. Waislamu wamekuwa wakipuuzwa katika masuala mbalimbali kutokana na kutowekwa katika katiba lakini sasa umefika wakati wa kupeleka maoni na si kuendelea kulalamika, alisema.
Aidha, Sheikh Ponda alisema jumuiya hiyo ambayo ni jukwaa la Waislamu la kuratibu mchakato wa Katiba nchini, masuala mengine ambayo Waislamu wanayapigania yaonekane kwenye katiba mpya, ni kuingizwa katika katiba mpya siku ya Ijumaa kutambulikuwa kuwa ni siku ya ibada ambayo itawasaidia Waislamu kupata fursa ya kwenda kuabudu kwa uhuru zaidi.
Pia tunataka katiba itambue uwepo wa Mwenyezi Mungu, itoe uhuru wa kuabudu, kwani katiba iliyopo haijatoa uhuru huo na ndiyo maana Waislamu wanazuiliwa ibada pamoja na kuvaa hijabu vyuoni, majeshini na asasi za serikali.
Alisema kuwa pia wanataka katiba itoe usawa katika elimu kwa maana ya katiba kutamka uwakilishi sawa kwa Wakristo na Waislamu katika Baraza la Mitihani la Taifa.
Kabla na baada ya uhuru chombo hiki kimeendelea kutawaliwa na Wakristo na kusababisha upendeleo mkubwa katika uteuzi na usahihishaji wa mitihani, kuwe na uteuzi wa maofisa elimu wakuu wa shule, alisema.
Aidha, alisema wanataka sheria ya ugaidi ifutwe, kuwapo kwa uwakilishi wa dini bungeni, pamoja na baraza la madiwani na mawaziri kuwa na uwakilishi wa dini.
Pia tunataka katiba iruhusu vyama vya siasa vya kidini, Waislamu na Wakristo wapokezane urais, serikali ya Tanganyika irejeshwe, kuwapo kwa muungano wa serikali tatu, urais wa muungano uwe wa awamu pamoja na kuwapo kwa serikali ya majimbo, alisema.
Sheikh Ponda kuwa masuala mengine wanayotaka kuwamo katika Katiba mpya ni mgombea binafsi, matokeo ya urais kupingwa mahakamani, rais kutounda tume ya uchaguzi, adhabu ya kifo iwekwe ndani ya katiba, misamaha ya kodi na mikataba ya kanisa na serikali ifutwe na kikosi cha kupambana na rushwa kuundwa upya na kuingizwa kwenye katiba.
Concern;
Jamani sijafafanuliwa vzr juu ya haya.
Sheria ya ugaisi ifutwe kuna nini nyuma yake?
Haki ya kusoma hivi hawa watu mmekatazwa na nani kusoma? Mponda elimu yako ni darasa la ngapi na kwa nini?
Utawala wa kupikezana kwa manufaa ya nani?
Uhuru wa kuabudu nani kawanyima?
Sheria ya biashara kwa ...... sijaelewa kivp