Kila kukicha CCM wanazidi kushindwa kuongoza nchi. Kwa kweli fanya utafiti nchi ipo mahali pagumu sana. Kila mwaka malaki ya watanzania wanaingia soko la ajira lakini kazi hakuna na uchumi haukui kiasi cha kutosha kuwapa nafasi. Wengi wamekuwa wamachinga. Sasa wamachinga wanapotetea haki yao ya kufanya biashara Mbeya, mwanza nk unasema chadema ndio wamechochea. Wamnafunzi wanafanya vurugu kwa kukosa mikopo unasema chadema wanahusika. Huo ni udhaifu mkubwa wa kiuongozi. kama kuna matatizo yaangalie na uyatatue badala ya kuwasingizia chadema. Na basi kama chadema wanaweza kuwahamasisha wamachinga, wanafunzi na raia kwenda barabarani basi ni chama chenye nguvu kubwa kuliko hata serikali. Hivi wanataka kutuambia wanafunzi wa udsm ni mazezeta hadi washawishiwe wagome bila kuwa na tatizo eti tu kwa kushawishiwa?