CCM Kuwasingizia Chadema kwa matatizo ya nchi ni Udhaifu Mkubwa

Status
Not open for further replies.

ibange

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
1,543
550
Kila kukicha CCM wanazidi kushindwa kuongoza nchi. Kwa kweli fanya utafiti nchi ipo mahali pagumu sana. Kila mwaka malaki ya watanzania wanaingia soko la ajira lakini kazi hakuna na uchumi haukui kiasi cha kutosha kuwapa nafasi. Wengi wamekuwa wamachinga. Sasa wamachinga wanapotetea haki yao ya kufanya biashara Mbeya, mwanza nk unasema chadema ndio wamechochea. Wamnafunzi wanafanya vurugu kwa kukosa mikopo unasema chadema wanahusika. Huo ni udhaifu mkubwa wa kiuongozi. kama kuna matatizo yaangalie na uyatatue badala ya kuwasingizia chadema. Na basi kama chadema wanaweza kuwahamasisha wamachinga, wanafunzi na raia kwenda barabarani basi ni chama chenye nguvu kubwa kuliko hata serikali. Hivi wanataka kutuambia wanafunzi wa udsm ni mazezeta hadi washawishiwe wagome bila kuwa na tatizo eti tu kwa kushawishiwa?
 
tatizo serikali ya ccm haipendi kufanyia kazi ukweli. sasa wameanza kutoa lawama kama vyama vya upinzani, eti CDM wanafanya serikali ikose usingizi! shame up on them...!
 
kiukweli tuna bahati mbaya watanzania kwani tumekaa miaka 6 hatuna rais tunaongozwa na lisanamu la rais hakuna mtu pale ikulu ni sanamu tuu linavalishwa suti kila kukicha na ccmchoo inaongozwa na majambazi yote yanashinda kuiba mali za UMMA na kibaya zaidi kwa sasa ccmchoo kimeamua na kuwaua wananchi.kwa risasi,sumu,visu na madawa ya kulevya wanamtumia mdogo wake na rost tam kuyaleta nchini.hii nchi ni shamba la bibi.
 
Kila kukicha ccm wanawaza wafanye nini juu ya chadema badala ya kuleta maendeleo kwa wananchi.
Polisi badala ya kulinda usalama wa wananchi wanafanya kazi ya siasa.
 
Hata mimi wananishangaza sana ccm wanaacha kutatua matatizo wanamtafuta mchawi wanalala sasa kama ni cdm wawajibishwe basi
 
Udhaifu ni pale ambapo unakuwa ni uongo.UKWELI CDM wanaratibu vurugu ktk nchi yetu.Viongozi wake waliapa kuwa nchi haitatawalika coz watz waliwanyima kura 2010.Baada ya uchaguzi mkuu kauli hiyo inatekelezwa kwa vitendo e.g maandamano kila kukicha, vurugu mikoani na vyuoni, hujuma hata serikalini,kumdharau Rais aliechaguliwa kidemokrasia bungeni,kuwadharau ma-RC mfano mbowe kumdhihaki RC wa Arusha,kumpiga na kumvua DC Igunga,vurugu na kauli za wavuta bangi ndan ya bunge n.k haya ni PREMISES ya CDM wanaratibu vurugu hapa nchin lengo likiwa NCHI ISITAWALIKE.Lakini itatawalika na wahaini ikibidi mtatiwa ndani.
 
Udhaifu ni pale ambapo unakuwa ni uongo.UKWELI CDM wanaratibu vurugu ktk nchi yetu.Viongozi wake waliapa kuwa nchi haitatawalika coz watz waliwanyima kura 2010.Baada ya uchaguzi mkuu kauli hiyo inatekelezwa kwa vitendo e.g maandamano kila kukicha, vurugu mikoani na vyuoni, hujuma hata serikalini,kumdharau Rais aliechaguliwa kidemokrasia bungeni,kuwadharau ma-RC mfano mbowe kumdhihaki RC wa Arusha,kumpiga na kumvua DC Igunga,vurugu na kauli za wavuta bangi ndan ya bunge n.k haya ni PREMISES ya CDM wanaratibu vurugu hapa nchin lengo likiwa NCHI ISITAWALIKE.Lakini itatawalika na wahaini ikibidi mtatiwa ndani.

hayo unayoyasema yanatokana na ombwe/vacuum katika uendeshaji nchi mkuu. Tulia na uchukue nafasi ya mtu neutral utabaini unayoyasema yanasukumwa na mapenzi kwa upande mmoja wa aina moja ya mtazamo wa kuendesha mambo. Kama alivyosema mtoa thread tukiwa na majibu ya juu juu kama haya ya jibu kuwa ni CHADEMA kuhusu matatizo ya taifa hili daima hatutakuwa sahihi katika kupata utatuzi wa matatizo ya msingi ya nchi hii. Na kuwaambia wananchi kuwa matatizo yao ni CHADEMA ni tusi kubwa likimaanisha wao hawana akili za kuchanganua mambo. Mie wa kwanza kuchukia kwa vile sina chama.
 
CCM nchi imewashinda!!! Kwa sasa inataka iwajulishe umma kwamba CDM ndio inakwamisha maendeleo ya nchi, kwamba ni chama cha watu wenye vurugu. Wanajisahau kwamba wanaiongezea umaarufu.

CCM hawana pakutokea tena. Wanaficha madhambi yao kwa kutumia Dola!!!. Tatizo lingine hiyo dola imejaa watoto wa mashangazi, wajomba, mashemeji etc, hakuna sheria yoyote inayofuatwa. Ni amri tu..........
 
Kila kukicha ccm wanawaza wafanye nini juu ya chadema badala ya kuleta maendeleo kwa wananchi.
Polisi badala ya kulinda usalama wa wananchi wanafanya kazi ya siasa.

Ni-compare na machafuko yanayojitokeza mara kwa mara na kauli yako then na-declare kwa kusema naunga mkono hoja Mheshimiwa
 
Well it just shows how scared they are all becoming. Magamba are no nonsense people and with tempers as hot as an erupting volcano, they know whats heading their way and thats why they are trying to shift blame. Isn't it too pathetic of how the whole thing is set up?
 
Ni muda kidogo sasa kupitia vyombo mbalimbali vya habari tumeona au kusikia kile kinachoelezwa kuwa ni fedha zinazotumiwa na CCM ili kuvizoofisha vyama vya upinzani. Hii sio demokrasia hata kidogo. Nchi yoyote inayotaka maendeleo inahitaji kuwepo wapinzani imara kwani huisaidia serikali kwa kutoa changamoto mbalimbali ambazo endapo serikali husika itazitumia husaidia kuleta maendeleo kwa haraka zaidi. Haya yanayo endelea ni ishara tosha kwamba CCM sasa hawana tena uwezo wa kuongoza tena au kwa maneno mengine viatu walivyo vaa ni vikubwa kuliko miguu yao hivyo nchi inahitaji chama m'badala.

Wataalamu wa mambo wameweza kuhusisha harakati hizi na mipango ya serikali ya CCM kujaribu kuwasahaulisha wananchi juu ya tuhuma alizozitoa Mh Zito Kabwe juu ya fedha zilizofichwa Uswisi na sakata la Uozo wa mipango ya serikali juu ya Gesi ya mtwara. CCM watanzania shida yetu ni maendeleo tu. Liongozeni taifa kwa kuweka misingi imara ya uchumi na kuwasaidiwa wananchi waweze kuwa na maisha bora zaidi kwani hicho ndicho tunachokitaka.​
 
kiukweli tuna bahati mbaya watanzania kwani tumekaa miaka 6 hatuna rais tunaongozwa na lisanamu la rais hakuna mtu pale ikulu ni sanamu tuu linavalishwa suti kila kukicha na ccmchoo inaongozwa na majambazi yote yanashinda kuiba mali za UMMA na kibaya zaidi kwa sasa ccmchoo kimeamua na kuwaua wananchi.kwa risasi,sumu,visu na madawa ya kulevya wanamtumia mdogo wake na rost tam kuyaleta nchini.hii nchi ni shamba la bibi.
mbona tunashinda kila siku
 
Well it just shows how scared they are all becoming. Magamba are no nonsense people and with tempers as hot as an erupting volcano, they know whats heading their way and thats why they are trying to shift blame. Isn't it too pathetic of how the whole thing is set up?
hapo hujaeleweka iweke kwa kiswahili mkuu au mwombe TAYADI akusaidie
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom