mkute
Member
- Jan 12, 2011
- 80
- 12
Katika uchaguzi uliopita jimbo la igunga mkoani Tabora,tulishuhudia ushindani mkali toka mwanzo wa kampeni mpaka siku matokeo yanatangazwa ambapo aliekuwa mgombea wa ccm alitangazwa mshindi kwa mujibu wa tume ya uchaguzi.
Kikubwa tulichokiona ni jinsi chama kilichokuwa kinatetea kuendelea kulishikilia jimbo hilo mara baada ya aliekuwa mbunge wa jimbo hilo fisadi Rostam kujiuzulu kwa kisingizio cha kuachana na siasa uchwara za ccm.Kwanza tukashuhudia jopo zima la viongozi wa serikali ya ccm wakihamia Igunga,pili viongozi wote waandamizi wa ccm mpaka wastaafu walifika Igunga kuinusuru ccm,tatu vyombo vya dola viliahidi kutoiangusha ccm,nne tumeshuhudia gharama kubwa sana iliyotumika takribani shilingi bilioni mbili za kitanzania,na tano kutumika kwa baadhi ya taasisi za dini [BAKWATA] ktk kampeni hizo kuisaidia ccm ili iweze kushinda.
Pamoja na nguvu zote hizo kutumika matokeo walioyapata ni mshangao mkubwa ukilinganisha na nguvu waliotumia,maana ninavyojua mimi kadri mtaji unapotumika mkubwazaidi, huzaa faida kubwa zaidi, lkn sivyo ilivyokuwa ccm walitumia nguvu kubwa wakapata kura kidogo.
Swali langu kwao kama jimbo dogo tu nguvu zote hapo, je 2015 nchi nzima itakuwaje watagawanyika vipi ili kuidhibiti chadema inayokuja kwa kasi kama mbogo aliejeruhiwa ikizidi kudhihirisha jinsi nguvu ya umma inavyofanya kazi. Ni nani watampeleka Mwanza,Arusha,Mbeya,Shinyanga,Kilimanjaro,Iringa,Mara,Bukoba,Kigoma.....?ili awasaidie kupiga kampeni kama ilivyokuwa Igunga?
Kikubwa tulichokiona ni jinsi chama kilichokuwa kinatetea kuendelea kulishikilia jimbo hilo mara baada ya aliekuwa mbunge wa jimbo hilo fisadi Rostam kujiuzulu kwa kisingizio cha kuachana na siasa uchwara za ccm.Kwanza tukashuhudia jopo zima la viongozi wa serikali ya ccm wakihamia Igunga,pili viongozi wote waandamizi wa ccm mpaka wastaafu walifika Igunga kuinusuru ccm,tatu vyombo vya dola viliahidi kutoiangusha ccm,nne tumeshuhudia gharama kubwa sana iliyotumika takribani shilingi bilioni mbili za kitanzania,na tano kutumika kwa baadhi ya taasisi za dini [BAKWATA] ktk kampeni hizo kuisaidia ccm ili iweze kushinda.
Pamoja na nguvu zote hizo kutumika matokeo walioyapata ni mshangao mkubwa ukilinganisha na nguvu waliotumia,maana ninavyojua mimi kadri mtaji unapotumika mkubwazaidi, huzaa faida kubwa zaidi, lkn sivyo ilivyokuwa ccm walitumia nguvu kubwa wakapata kura kidogo.
Swali langu kwao kama jimbo dogo tu nguvu zote hapo, je 2015 nchi nzima itakuwaje watagawanyika vipi ili kuidhibiti chadema inayokuja kwa kasi kama mbogo aliejeruhiwa ikizidi kudhihirisha jinsi nguvu ya umma inavyofanya kazi. Ni nani watampeleka Mwanza,Arusha,Mbeya,Shinyanga,Kilimanjaro,Iringa,Mara,Bukoba,Kigoma.....?ili awasaidie kupiga kampeni kama ilivyokuwa Igunga?