CCM kutishia watumishi wa umma kisa hawajahudhuria mikutano yao si haki!

sasa mihimili ya bunge,serikali na mhakama ina kazi gani? Kama chama tawala kinakuwa na uwezo wa kumwajibisha kila mtu. Na kama mtumishi wa serikali akikataa kuwajibishwa na chama cha siasa sheria inambana vipi kikatiba?

Ulikwisha jiuliza ni kwanini mawazili wanaambatana na viongozi wa chama mikoani?
 
Na sisi watumishi wa umma ni mazuzu tu acha watuburuze wanavyotaka! Wakati wa kura ndo huwa tuko msitari wa mbele kuchakachua ili magamba waendelee! Shenzi zetu! Jamani tubadili mtazamo. Ila hiki chama kimeshikwa pabaya, kinatapatapa sana!! Jana nilimwona Joyce Masunga-Shangingi la ccm SHY miaka ile -alivyotoa maagizo kwa DC eti apeleke mapendekezo ya kuwatimua kazi meneja wa TANROADS mkoa na TANESCO mkoa. Kisa hawakwenda kwenye kikao cha CCM! NYAMB...F!

Mkuu yote ya nini hayo,Hapa jukwaani siku zote mmekuwa mnaituhumu CCM kwa ujumla ndio maana na wao sasa wanayafanyia kazi yale ambayo ninyi mnafikiri ama kudhani kwamba ni mojawapo ya udhaifu wa serikali ya JK.Siwezi kuthibitisha kwamba watendaji ni watovu wa nidhamu ila kilichoonekana ni kama vile walijisahau tu kukiwajibikia chama.Hoja kuu hapa ni kwa namna gani watendaji wa serikali wasivyokiwajibikia chama chao kilichopewa dhamana ya kuwaongoza wao na ambapo kunapotokea udhaifu ndani ya serikali lawama kinapewa chama na si mtumishi mmojax2.
 
Bado kina Nape wana ndoto za chama kushika hatamu!

Ngoja waendelee kuota Wamekwishapitwa na wakati.

Watashangaa tu siku watakapotakiwa kujibu kwa umma wa watanzania kwa kutumia madaraka yao vibaya
 
sasa mihimili ya bunge,serikali na mhakama ina kazi gani? Kama chama tawala kinakuwa na uwezo wa kumwajibisha kila mtu. Na kama mtumishi wa serikali akikataa kuwajibishwa na chama cha siasa sheria inambana vipi kikatiba?
Kwa kifupi mtumishi wa serikali anayekataa kutumikia serikali iliyoundwa na chama tawala inbidi atafute ajira yake mwenyewe.
jalafu kazi ni simple tu, kama mtumishi huyo anajisikia hawezi kutekeleza sera za chama tawala basi anajiuzulu.
Siyo lazima kuajiriwa na serikali iliyochaguliwa na wengi na wewe minority unakwamisha matakwa ya wengi.
 
Nimeona Katibu wa CCM mwanza akiwa na Nape wakilalamika kitendo cha Watendaji wa serekali ...Tanroads na Tanesco kwa kukataaa kwenda kwenye mikutano Yao Kujibu Hoja za Wananchi

....Katibu ameenda Mbali kutushia kuwafukuzisha kazi.

Nimeshangaa sana Kama tunao wanasiasa ambao huwajui katika utendaji wa Vyama vingi....watumishi wa umma Kama hawa hawawajibiki kwa Katibu wa CCM na sio busara kuwatumia kisiasa .....Watofauutishe role ya mawaziri ambao wao ndio wasimamizi wa kisiasa serekalini na hawa Watendaji.

...Ni halali Kabisa kwa waziri kuwajibika kwa chama na Kijibu Hoja ......Lakini ni uwehu Kabisa kuwaonea Watendaji wa umma...kuwatumia kwenye majukwaa ya kisiasa.

Iwapo hawa Watendaji walitajwa watahamishwa au kufukuzwa kazi itaweka predecence mbaya.....na tunaomba katiba mpya iweke msisitizo juu na kuwalinda Watendaji wa umma dhidi ya wanasiasa.
Kwa mantiki ya proposition yako naona ni ujuha zaidi kukilaumu chama tawala kwa kushindwa utekelezaji wa sera zinazoihusu TANESCO na TANROADS.
 
siyo lazima watendaji kwenda kuelezea kwani wananchi si wanaona wenyewe Nape ni mtu wa kujisahau sana
 
Ndugu wana JF na watanzania wote:

Naona hii tabia ya viongozi wa CCM wa ngazi mbali mbali kupanda jukwaani na kuamrisha au kuwatishia viongozi na watumishi wa serikali ni udhalilishaji mkubwa usioweza kuvumilika. Haiwezekani watanzania tukafanywa matahira kiasi hicho. Siku mtu anapopewa kazi anapewa terms of reference na anajua kuwa anawajibika kwa nani. Haiwezekani na haiingii akilini kuwajibika kwa bosi wako kazini na huku unawajibika kwa viongozi wa CCM.

Tukichekelea hili na kuwashangaa wanaoamrishwa leo, kesho itakuwa zamu yangu na yako. CCM imeshazidiwa sasa wanataka kuturudisha mwaka 1970
 
Hili jambo linatia kinyaa mkuu hata leo nimeona kupitia ITV M/kiti wa CCM mkoa wa Geita akimsimamisha afisa mipango wilaya kwenye mkutano wa CCM Katoro.
Wafanyakazi wa serikali wasipokuwa na msimamo kuna siku wataamriwa kuchagua au kuchangia CCM kwa kukatwa mishahara.
 
Mnyika alishamlima katibu mkuu kiongozi na katibu mkuu utumishi.kimya
kuna kelele za katiba mpya,wakati mazuri ya katiba hii mbovu tumeshindwa kuyaheshimu
 
Tukiendelea hivi, masharti ya kupandishwa daraja au hata kuajiriwa itakuwa kuwa mwanachama wa CCM, subirini muone.

Kazini kwangu nimeona wiki iliyopita wafanyakazi ambao ni makada wa CCM wameanzisha umoja wao na wanafanya vikao na kuhamasisha wafanyakazi wengine kujiunga na CCM kwa ahadi za kijinga eti watatoka kimaisha. Unafikiri matokeo yake ni nini kama mtu akisema yeye siyo mwana CCM?
 
Tukiendelea hivi, masharti ya kupandishwa daraja au hata kuajiriwa itakuwa kuwa mwanachama wa CCM, subirini muone.

Kazini kwangu nimeona wiki iliyopita wafanyakazi ambao ni makada wa CCM wameanzisha umoja wao na wanafanya vikao na kuhamasisha wafanyakazi wengine kujiunga na CCM kwa ahadi za kijinga eti watatoka kimaisha. Unafikiri matokeo yake ni nini kama mtu akisema yeye siyo mwana CCM?

Mkusanyiko unaoruhusiwa ni ule tu wa Chama Cha wÀfanyakazi,

Waripoti kwa myika hao wasambaratishwe hakuna chadema wala ccm sehemu ya serikali
 
Wanachokosa kujua Ccm ni kuwa unaweza kumpeleka punda mtoni lakini huwezi kulazimisha kunywa maji. Mi nasema kuhudhuria tutahudhuria kwa sasabu ya kuogopa kufukuzwa kazi... hii haina maana maana kuwa nina upenda na CCm, anzi niko tayari kutoa dokument zote za ofisini ikiwa Chadema watatihitaji... hii ni9 kwa vile siipendi Ccm.
 
Back
Top Bottom