KipimaPembe
JF-Expert Member
- Aug 5, 2007
- 1,285
- 696
Angalia Majimbo yafuatayo na Umuhimu wake kimkakati;
- Ilemela na Nyamagana - Mji wa Mwanza ndo capital of western Tanzania ukitegemewa sana na wakazi wa Shinyanga, Kagera, Mara, Kigoma na Tabora kwa shughuli nyingi za kiuchumi. Si siri, wakazi wengi wa mikoa hiyo wana connections Mwanza unaoangaliwa vile vile kama kituo kikubwa cha Tanzania's Gold mining industry ambayo iko tainted sana na mikataba Mibovu. CCM Kupoteza Mwanza ni kupoteza kanda yote ya ziwa..... Tusubiri tutaona.
- Mbeya na Iringa Mjini - Mji wa Mbeya ndo Kitovu cha biashara katika southern highlands ambapo Mikoa ya Rukwa, Iringa na Ruvuma huutegemea sana mji huu. CCM kupoteza Mbeya na Iringa ina maana kuwa southern highlands is gone.
- Arusha - Ndo makao makuu ya biashara ya utaliii Tanzania na ni mji muhimu sana kanda ya kaskazini mikoa ya Kilimanjaro na Manyara. Kupoteza Arusha ina risk kubwa ya kuwa majimbo mengine zaidi katika maeneo hayo yatafuatia.
- Dar es Salaam - Kawe na Ubungo; Middle class ya Tanzania iko maeneo hayo. Viongozi wengi hukaa maeneo hayo au wana nyumba huko. Kuyapoteza majimbo haya kuna strategic significance kuonyesha jinsi viongozi walivyo mbali na wale wanaoishi nao. Out of touch!