Elections 2010 CCM kupoteza Strategic Constituencies ...... Slaa amewakata uti wa Mgongo

KipimaPembe

JF-Expert Member
Aug 5, 2007
1,285
696
Angalia Majimbo yafuatayo na Umuhimu wake kimkakati;
  1. Ilemela na Nyamagana - Mji wa Mwanza ndo capital of western Tanzania ukitegemewa sana na wakazi wa Shinyanga, Kagera, Mara, Kigoma na Tabora kwa shughuli nyingi za kiuchumi. Si siri, wakazi wengi wa mikoa hiyo wana connections Mwanza unaoangaliwa vile vile kama kituo kikubwa cha Tanzania's Gold mining industry ambayo iko tainted sana na mikataba Mibovu. CCM Kupoteza Mwanza ni kupoteza kanda yote ya ziwa..... Tusubiri tutaona.
  2. Mbeya na Iringa Mjini - Mji wa Mbeya ndo Kitovu cha biashara katika southern highlands ambapo Mikoa ya Rukwa, Iringa na Ruvuma huutegemea sana mji huu. CCM kupoteza Mbeya na Iringa ina maana kuwa southern highlands is gone.
  3. Arusha - Ndo makao makuu ya biashara ya utaliii Tanzania na ni mji muhimu sana kanda ya kaskazini mikoa ya Kilimanjaro na Manyara. Kupoteza Arusha ina risk kubwa ya kuwa majimbo mengine zaidi katika maeneo hayo yatafuatia.
  4. Dar es Salaam - Kawe na Ubungo; Middle class ya Tanzania iko maeneo hayo. Viongozi wengi hukaa maeneo hayo au wana nyumba huko. Kuyapoteza majimbo haya kuna strategic significance kuonyesha jinsi viongozi walivyo mbali na wale wanaoishi nao. Out of touch!
Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Mbeya ni kati ya mikoa yenye wakazi wengi sana hapa Tanzania. CCM kupoteza majimbo yenye umuhimu wa kimkakati katika maeneo hayo ni big blow na inaonesha Slaa ana uwezo wa kuyalinda majimbo hayo yaliyoanguka. Pole CCM, inaonesha kuwa zile ndoto za kuwa CCM itatawala milele zinaanza kuyeyuka ghafla!
 
Weeeelllllll saiiiiiid mkuu! wamepoteza mvuto mijini sasa tuone kama kweli wao ni chama cha wakulima waende back to basics wakawahudumie wakulima vizuri maana nduio waliowapigia kura!!, na wakishindwa basi 2015 ndio itakuwa mwisho wa chama chenyewe maana kitafutika kabisa kutoka katika fikra za wananchi wa huko vijijini pia.

Kumbuka baada ya uchaguzi huu tutegemee defectors wengi tu kutoka CCM ambao watakua wamechoshwa na jinsi Mkwere, familia yake, na mafisadi wanavyoendesha chama tulichokianzisha waTanzania wote.

BTW hivi kama Mkwere akishinda baraza lake la mawaziri atawaweka akina nani????? akina RA, Mo na EL???, maana mawaziri wake wote wamechemsha tayari...
 
CCM mwaka huu wana kazi ya kuchakachua kufikisha iyo 80 percent
 
Chama chenyewe kimeishajifia wanalazimisha mambo ambayo hayawezekani na ukweli wanaujua ni kuwa wamebanwa kila mahali wanachofanya sasa hivi ni kuchelewesha matokeo ili waweze kubadilisha matokeo au kufanya uhuni wa kuiba kura
 
CCM mwaka huu wana kazi ya kuchakachua kufikisha iyo 80 percent

Kitu kizuri ni kuwa inafahamika kuwa hiyo 80 percent hawana uhakika wa kuifikisha which means kila mtu anajua kinachoendelea sasa hivi wanachakachua ili waweze kuifikisha wakati wanajua kuwa wameshindwa kwahiyo wanatumia kila mbinu
 
Siyo strategic constituencies tu bali center forward wakutegemewa kwa mipango mingi Masha na Mahanga wamepigwa chini.
 
Watutangazie matokeo ya uraisi kwenye maeneo hayo basi. Kwa nini wanayaficha? Mbona ubunge tayari?
 
Angalia Majimbo yafuatayo na Umuhimu wake kimkakati;
  1. Ilemela na Nyamagana - Mji wa Mwanza ndo capital of western Tanzania ukitegemewa sana na wakazi wa Shinyanga, Kagera, Mara, Kigoma na Tabora kwa shughuli nyingi za kiuchumi. Si siri, wakazi wengi wa mikoa hiyo wana connections Mwanza unaoangaliwa vile vile kama kituo kikubwa cha Tanzania's Gold mining industry ambayo iko tainted sana na mikataba Mibovu. CCM Kupoteza Mwanza ni kupoteza kanda yote ya ziwa..... Tusubiri tutaona.


  1. Mkuu nakuunga mkono kwa ulilo lisema safi sana.

    Je kwa kuongezea niki sema au kupendekeza hoja ya Majimbo lipitishwe katika KATIBA mpya ijayo?
 
Angalia Majimbo yafuatayo na Umuhimu wake kimkakati;
  1. Ilemela na Nyamagana - Mji wa Mwanza ndo capital of western Tanzania ukitegemewa sana na wakazi wa Shinyanga, Kagera, Mara, Kigoma na Tabora kwa shughuli nyingi za kiuchumi. Si siri, wakazi wengi wa mikoa hiyo wana connections Mwanza unaoangaliwa vile vile kama kituo kikubwa cha Tanzania's Gold mining industry ambayo iko tainted sana na mikataba Mibovu. CCM Kupoteza Mwanza ni kupoteza kanda yote ya ziwa..... Tusubiri tutaona.
  2. Mbeya na Iringa Mjini - Mji wa Mbeya ndo Kitovu cha biashara katika southern highlands ambapo Mikoa ya Rukwa, Iringa na Ruvuma huutegemea sana mji huu. CCM kupoteza Mbeya na Iringa ina maana kuwa southern highlands is gone.
  3. Arusha - Ndo makao makuu ya biashara ya utaliii Tanzania na ni mji muhimu sana kanda ya kaskazini mikoa ya Kilimanjaro na Manyara. Kupoteza Arusha ina risk kubwa ya kuwa majimbo mengine zaidi katika maeneo hayo yatafuatia.
  4. Dar es Salaam - Kawe na Ubungo; Middle class ya Tanzania iko maeneo hayo. Viongozi wengi hukaa maeneo hayo au wana nyumba huko. Kuyapoteza majimbo haya kuna strategic significance kuonyesha jinsi viongozi walivyo mbali na wale wanaoishi nao. Out of touch!
Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Mbeya ni kati ya mikoa yenye wakazi wengi sana hapa Tanzania. CCM kupoteza majimbo yenye umuhimu wa kimkakati katika maeneo hayo ni big blow na inaonesha Slaa ana uwezo wa kuyalinda majimbo hayo yaliyoanguka. Pole CCM, inaonesha kuwa zile ndoto za kuwa CCM itatawala milele zinaanza kuyeyuka ghafla!

Jamaa wewe unaakili sana. Ndiyo maana Dr. Slaa ndiye Rais wa Tanzania. Nakupa asante.
 
Uchambuzi wako ni mzuri na wa kisasa sana. Vitu kama hivi ndo CCM wanaviimiss, wamejaza washangiliaji tu.
 
Back
Top Bottom