Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Dalili zote kutoka Dodoma zinaonesha kuwa hatimaye mgogoro wa kiuongozi uliokikumba chama cha mapinduzi kwa takribani mwaka mmoja sasa utamalizwa kwa kutafuta njia ya upatanisho kati ya makundi yake mawili ambayo yamekuwa katika barabara ya kugongana kufuatia shutma za nani ni mwadilifu na nani ni fisadi.
Vyanzo mbalimbali kutoka Dodoma vinadokeza kuwa ripoti ya mzee Mwinyi iliyoundwa kutafuta chanzo na kutoa mapendekezo ya kutatua mgogoro huo inaonesha kuwa kwa hali iliyopo sasa itakuwa vigumu mno kwa chama hicho kutimuana au kupeana adhabu ambazo zitakifanya kionekane dhaifu. Kikubwa ambacho kinaonekana kubadilisha kabisa mwelekeo wa mapendekezo hayo ni kuundwa kwa Chama cha Jamii ambacho kinasubiri usajili wa muda ili kiweze kuanza kazi zake. Kuanzishwa kwa CCJ (kama nitakavyoonesha katika makala yangu mojawapo wiki hii) kunawatatiza viongozi wakuu wa CCM kwani kuanzia tetesi za uwepo wake juhudi nyingi zimekuwa zikifanyika kujua hasa ni "vigogo" gani wako nyuma ya chama hicho. Kutokana na kutokuwa na ushahidi wa nani anahusika au nani hausiki adhabu ambazo zinaweza kutolewa katika kikao hicho zaidi ni "onyo" na "karipio" kali lakini adhabu za kusimamishwa uongozi au hata kufukuzwa kutoka katika chama zinaonekana kukataliwa na wengi kwani itaonekana kuwapa faida baadhi ya watu kwenye chama hicho.
Kambi hizo ambazo zimekuwa zikigongana hasa kwa kutumia vyombo vya habari na kwenye majukwaa ya kisiasa ikiwemo Bungeni zilizaliwa mara baada ya ripoti ya Kamati teule ya Bunge iliyochunguza kampuni ya Richmond kuja na mapendekezo makali ambayo yalichangia kuanguka kwa aibu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa pamoja na mawaziri wengine wawili kitu ambacho kilisababisha kuvunjika kwa baraza la mawaziri wa Serikali ya Rais Kikwete.
Tukio la kujiuzulu Lowassa liligawa Bunge, wana CCM na Watanzania katika kambi zilizotofautiana kama Lowassa na wenzake walionewa au walistahili kuwajibishwa kutokana na tukio hilo. Wale ambao walionekana kumtetea Lowassa na wenzake mara moja wakaanza kuhusishwa na "watetezi wa ufisadi" huku kambi iliyosifia ripoti ile ya Richmond kuanza kuonekana ni "Wapiganaji wa ufisadi" Kwa mwaka mzima dalili za kambi hizo kupatana zilionekana kutoweka hasa kile amabacho kimetajwa kuwa ni jaribio la kumvua uanachama Spika wa Jamhuri ya Muungano na mmoja wa kambi kufanyika.
Spika Sitta alisalimika kuchukuliwa hatua na chama chake baada ya pendekezo la kuundwa ka Kamati ya Mzee Mwinyi, Mzee Pius Msekwa na Mzee Kinana kuundwa ili kutafuta chanzo cha migogoro ndani ya chama hicho, kupendekeza namna ya kutatua migongano ndani ya wabunge na jinsi ya kupendekeza namna jinsi Bunge litaweza kufanya kazi zake bila kusababisha migogoro kama hii. Juhudi za chini kwa chini za kuzipatanisha kambi hizo mbili hadi hivi sasa zimeshindikana na chanzo chetu kimoja kimetudokeza kuwa wananchi wasishangae kuona ni kina Mwakyembe na wenzake ndio wanapewa lawama za namna fulani kwa kuharibu sifa za wanachama wengine kwa kuwaita "mafisadi".
Ni matokeo ya uchunguzi huu yanaonesha kuwa CCM wataamua kutafuta njia za kidiplomasia zaidi kumaliza mgogoro wao kama walivyofanya kwenye suala la Richmond na hasa namna ya kuhakikisha hatimaye Lowassa na Mwakyembe wanakumbatiana, Mengi na Rostam wanakunywa chai pamoja katika hali ya kuonesha hatimaye "umoja na mshikamano" umepatikana ndani ya chama
Vyanzo mbalimbali kutoka Dodoma vinadokeza kuwa ripoti ya mzee Mwinyi iliyoundwa kutafuta chanzo na kutoa mapendekezo ya kutatua mgogoro huo inaonesha kuwa kwa hali iliyopo sasa itakuwa vigumu mno kwa chama hicho kutimuana au kupeana adhabu ambazo zitakifanya kionekane dhaifu. Kikubwa ambacho kinaonekana kubadilisha kabisa mwelekeo wa mapendekezo hayo ni kuundwa kwa Chama cha Jamii ambacho kinasubiri usajili wa muda ili kiweze kuanza kazi zake. Kuanzishwa kwa CCJ (kama nitakavyoonesha katika makala yangu mojawapo wiki hii) kunawatatiza viongozi wakuu wa CCM kwani kuanzia tetesi za uwepo wake juhudi nyingi zimekuwa zikifanyika kujua hasa ni "vigogo" gani wako nyuma ya chama hicho. Kutokana na kutokuwa na ushahidi wa nani anahusika au nani hausiki adhabu ambazo zinaweza kutolewa katika kikao hicho zaidi ni "onyo" na "karipio" kali lakini adhabu za kusimamishwa uongozi au hata kufukuzwa kutoka katika chama zinaonekana kukataliwa na wengi kwani itaonekana kuwapa faida baadhi ya watu kwenye chama hicho.
Kambi hizo ambazo zimekuwa zikigongana hasa kwa kutumia vyombo vya habari na kwenye majukwaa ya kisiasa ikiwemo Bungeni zilizaliwa mara baada ya ripoti ya Kamati teule ya Bunge iliyochunguza kampuni ya Richmond kuja na mapendekezo makali ambayo yalichangia kuanguka kwa aibu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa pamoja na mawaziri wengine wawili kitu ambacho kilisababisha kuvunjika kwa baraza la mawaziri wa Serikali ya Rais Kikwete.
Tukio la kujiuzulu Lowassa liligawa Bunge, wana CCM na Watanzania katika kambi zilizotofautiana kama Lowassa na wenzake walionewa au walistahili kuwajibishwa kutokana na tukio hilo. Wale ambao walionekana kumtetea Lowassa na wenzake mara moja wakaanza kuhusishwa na "watetezi wa ufisadi" huku kambi iliyosifia ripoti ile ya Richmond kuanza kuonekana ni "Wapiganaji wa ufisadi" Kwa mwaka mzima dalili za kambi hizo kupatana zilionekana kutoweka hasa kile amabacho kimetajwa kuwa ni jaribio la kumvua uanachama Spika wa Jamhuri ya Muungano na mmoja wa kambi kufanyika.
Spika Sitta alisalimika kuchukuliwa hatua na chama chake baada ya pendekezo la kuundwa ka Kamati ya Mzee Mwinyi, Mzee Pius Msekwa na Mzee Kinana kuundwa ili kutafuta chanzo cha migogoro ndani ya chama hicho, kupendekeza namna ya kutatua migongano ndani ya wabunge na jinsi ya kupendekeza namna jinsi Bunge litaweza kufanya kazi zake bila kusababisha migogoro kama hii. Juhudi za chini kwa chini za kuzipatanisha kambi hizo mbili hadi hivi sasa zimeshindikana na chanzo chetu kimoja kimetudokeza kuwa wananchi wasishangae kuona ni kina Mwakyembe na wenzake ndio wanapewa lawama za namna fulani kwa kuharibu sifa za wanachama wengine kwa kuwaita "mafisadi".
Ni matokeo ya uchunguzi huu yanaonesha kuwa CCM wataamua kutafuta njia za kidiplomasia zaidi kumaliza mgogoro wao kama walivyofanya kwenye suala la Richmond na hasa namna ya kuhakikisha hatimaye Lowassa na Mwakyembe wanakumbatiana, Mengi na Rostam wanakunywa chai pamoja katika hali ya kuonesha hatimaye "umoja na mshikamano" umepatikana ndani ya chama