CCM kukata Majina, alichokisema Mh. Rais, demokrasia na hatma ya Tanzania

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1592837099723.png
Ijapokuwa demokrasia ndio mfumo wa siasa wenye ubore zaidi duniani hadi sasa ukilinganisha na mifumo mingine, hivyo kutufanya wengi wetu kuutetea mara kwa mara; kuna mambo kadhaa ya msingi tunapaswa kufahamu.

Demokrasia kamili na uhuru katika hatua yake ya juu kabisa, vinafanya kazi kwa ufanisi katika jamii yenye kiwango cha juu sana cha kujitambua, ustaarabu, kuweza kuchanganua mambo na kuamua kwa busara. Ikiwa jamii ina kiwango cha chini cha tabia tajwa hapo juu, kwa kadiri kiwango cha demokrasia na uhuru wa watu kinavyoongezeka, ndio hatari ya kutokea majanga inavyoongezeka na kinyume chake. Hili tutalifafanua zaidi baadae.

Kwa bahati mbaya ni kwamba Afrika bado tupo watu wengi sana/wapiga kura ambao uelewa wetu juu ya mambo na uwezo wetu wa kuchanganua vitu na kufanya maamuzi sahihi ni mdogo. Kwa mfano, % kubwa ya watanzania hatuelewi falsafa, itikadi, misingi na sera ya vyama achilia mbali kuzifuata. Jiulize mfano ukisema chama cha mrengo wa kushoto, mrengo wa kati kushoto, mrengo wa kulia ujamaa wa kidemokrasia na vitu kama hivyo, ni watanzania wangapi wanaelewa unasema nini?

Wapiga kura wengi Afrika amma hupiga kura bila kujua nini wanafanya, au baada ya kuchanganywa ‘Manipulations’ au kwa mihemko ‘emotions’au kwa ushabiki usiokuwa na sababu za kueleweka. Ili hili lieleweke vizuri, nitatoa mifano michache.

Moja, Ushawahi kuona bungeni kwa mfano, mtu anatoa hoja nzuri sana, lakini wajumbe wakiulizwa ‘Mnaikubali hiyo hoja’ wanasema ‘hapanaaaaaaaa’ lakini sio kwamba hawaitaki hoja, ni kwa sababu ya nani katoa hoja, kwa hiyo wajumbe wakishaona mtoa hoja washaikataa hoja tayari hawana haja hata ya kuielewa kwanza?

Mbili, Unajua tunaweza kwenda wote kwenye uchaguzi, wewe ni muadilifu na unahoja nzuri, mimi nikawa ni mjinga flani tu, ila nikasubiria masaa kadhaa kabla ya uchaguzi nikakuzushia kwamba wewe unauza meno ya tembo huku nimetumbua mimacho kweli kweli, na wapiga kura wakakukataa na kunikubali mimi, kisha baada ya uchaguzi (kukushinda), nikasema nilikuwa natania tu, sijawahi kuuona ukiuza meno?

Tatu, Unajua wapiga kura kwenye nchi za kiafrika wakipewa rushwa humchagua mtoa rushwa na kuacha watu wenye maono?

Nne, Unajua kwa mfano wewe ukipiga kampeni kwa kuongea mambo ya maana mwingine akawa anakatika, una uwezo wa kushindwa uchaguzi, na hata mzee wa mauno alishinda kimzaha hivyo hivyo? N.k

Kwa mantiki hiyo basi;

  • Kwa sababu ya uelewa wa waafrika tuliowengi, demokrasia peke yake haiwezi kutusaidia kuwa na nchi zenye ustawi na uongozi bora bali inahitajika mfumo wa ziada kujazia demokrasia ‘Complementary system’

  • Kwa kuwa wapiga kura wanaweza kupiga kura kwa kuvurugwa ‘Manipulation’ kura pekee hazituwezeshi kupata viongozi wa maana, Hivyo utaratibu uliowekwa na CCM kuchuja majina kwa kuzingatia vigezo vingine zaidi ya kupigiwa kura sio tu kwamba ni mzuri bali ni muhimu sana kwa ustawi wa Taifa na hatma ya nchi.

  • Hoja ya Rais Magufuli kwamba watu ambao tayari wana vyeo vya kutumikia wananchi kama wakuu wa mikoa ni bora wasigombee ubunge, inaegemea kwenye mantiki zaidi kwa kuangalia ‘motive’ na inatokana na ‘complementary system iliyotajwa hapo juu kwa ajili ya maslahi ya Taifa

  • Kwa kuwa tatizo la rushwa kwenye uchaguzi bado ni kubwa, kazi anayoifanya polepole kukemea rushwa na kuwatahadharisha watakaotoa rushwa kukatwa majina sio tu kwamba ni nzuri bali pia ni muhimu.
Kwa ujumla, mfumo huo wa kuwa na ‘control mechanism’ zaidi ya kura, haukinzani na demokrasia bali unajazia mapungufu ya demokrasia hivyo sio ‘Contradictory system’ kama baadhi ya wadau wanavyodhani bali ni ‘Complementary system’ na bila kufanya hivyo, tunaweza kukuta nchi nzima ina wabunge wa ajabu haijapata kutokea na kila mtu akabaki anashangaa ikiwemo wapiga kura wenyewe. Kwa hiyo wale wanaodhani mfumo huo ni kinyume na demokrasia, ni vizuri wakafahamu ‘dynamics’ hizi na kwa hili, tunaweza kusema CCM inachukua hatua zasahihi kabisa na zinazokubalika kitaam ku‘regulate’ hali ya mambo kwa maslahi ya taifa.
 
Ukishajua mambo haya yanayoathiri tabia za wapiga kura wa Afrika na mienendo ya wagombea utaelewa ni kwa nini hii 'complementary system' sio tu nzuri bali muhimu sana.

Vinginevyo ni sawa na kugawa bastola kwa kila mwanakijiji kwa hoja kwamba kila mtu ana uhuru, haki ya kumiliki mali na kujilinda. Licha ya kwamba hoja hizo ni za kweli; kwa jamii isiyokuwa na ustaarabu na kujitambua kwa hali ya juu itabuka balaa isiyo ya kawaida. Hiyo haitajalisha sheria zilizopo,kwani ikitokewa watu wengi wakiwa na matatizo, sheria pia haziwezi kusaidia sana.
 
mbunge gani mwenye akili ndani ya ccm wote wanaweka akili zao mfukoni wanatoa yale ya mfuko wa nyuma ndo wanatumia
Kwa bahati nzuri au mbaya, hao unaowaona hawana akili, ndio cream kwenye jamii yetu. Ndio maana tunasisitiza kwamba ni lazima kama jamii tuwekeze kwenye self development ili kutoka kwetu wakiibuka viongozi wawe na taswira bora zaidi. Kinyume chake tunatamani kuwa na watu ambao hawapo kwenye 'Sample'
 
Ukishajua mambo haya yanayoathiri tabia za wapiga kura wa Afrika na mienendo ya wagombea utaelewa ni kwa nini hii 'complementary system' sio tu nzuri bali muhimu sana.

Vinginevyo ni sawa na kugawa bastola kwa kila mwanakijiji kwa hoja kwamba kila mtu ana uhuru, haki ya kumiliki mali na kujilinda. Licha ya kwamba hoja hizo ni za kweli; kwa jamii isiyokuwa na ustaarabu na kujitambua kwa hali ya juu itabuka balaa isiyo ya kawaida. Hiyo haitajalisha sheria zilizopo,kwani ikitokewa watu wengi wakiwa na matatizo, sheria pia haziwezi kusaidia sana.
kwa hiyo mnahalalisha uporaji wa haki ya raia kuchagu mtu wamtakaye

kwa hiyo mtu msiyemtaka akiingia ikulu kwenu mnamwita si mstaarabu kweli tumefika hapo?

kwa hiyo jamii yetu haina watu watu wasio na uwezo mpaka tangu tumepata uhuru mpaka leo hofu hiii inatoka wapi?

ama kweli mmelewa sana madaraka je nyerere angekuwa na mawazo kama haya angeaacha nchi kwa wengine

yajayo yanatisha sana ngoja tusubiri:confused::confused::confused::confused::confused:
 
hatimaye tumepata rais aliyetabiriwa na nyerere. hakuna cha kuregulate wala ndugu yake na regulation hapa ni one man show
Wewe unadhani changamoto zilizotajwa kwenye mada ya msingi, zinaweza kutatuliwaje nje ya kutumia njia hiyo?
 
Kwa bahati nzuri au mbaya, hao unaowaona hawana akili, ndio cream kwenye jamii yetu. Ndio maana tunasisitiza kwamba ni lazima kama jamii tuwekeze kwenye self development ili kutoka kwetu wakiibuka viongozi wawe na taswira bora zaidi. Kinyume chake tunatamani kuwa na watu ambao hawapo kwenye 'Sample'
nani kakuambia hawapo watu wazuri bashiru ally alipokuwa pale udsm ni huyu wa ccm? something is wrong somewhere???????????
 
kwa hiyo mnahalalisha uporaji wa haki ya raia kuchagu mtu wamtakaye

kwa hiyo mtu msiyemtaka akiingia ikulu kwenu mnamwita si mstaarabu kweli tumefika hapo?

kwa hiyo jamii yetu haina watu watu wasio na uwezo mpaka tangu tumepata uhuru mpaka leo hofu hiii inatoka wapi?

ama kweli mmelewa sana madaraka je nyerere angekuwa na mawazo kama haya angeaacha nchi kwa wengine

yajayo yanatisha sana ngoja tusubiri:confused::confused::confused::confused::confused:
Umesoma mada yote kabla ya kuanza kuchangia? ni kama maswali yote unayouliza yalishajibiwa. Rudia tena kusoma utaona majibu.

Labda ni kurahisishie kwa kukuuliza shwali rahisi tu. Unaamini kwamba kuna watu wanachaguliwa kuwa wabunge kwa mfano na hawana sifa kabisa za uongozi?
 
nani kakuambia hawapo watu wazuri bashiru ally alipokuwa pale udsm ni huyu wa ccm? something is wrong somewhere???????????
Kwani kuna mtu kasema hawapo watu wazuri? tatizo unakimbilia kwenye conclusion kabla hata ya kuelewa kwanza na hiyo hukupelekea kutengeneza wrong conclusions.
 
Wewe unadhani changamoto zilizotajwa kwenye mada ya msingi, zinaweza kutatuliwaje nje ya kutumia njia hiyo?
hofu yenu ni nini hata msitake mawazo mapya na akili mpya mpaka mjitengenezee mfumo wa kuwa nyima watu fursa mkiamini hafau huyu.

issue siyo hafai issue ni kuwa hawezi kunikubali wakati nitapoamua kufanya yale ya hovyo kwa raia watakaopewa nafasi ni wale jamii ya ndiyo mzee waoga na wanafiki wale wasio na uwezo kusema umekosea

hao ndo wanatafutwa wengine wote kata majina
 
Umesoma mada yote kabla ya kuanza kuchangia? ni kama maswali yote unayouliza yalishajibiwa. Rudia tena kusoma utaona majibu.

Labda ni kurahisishie kwa kukuuliza shwali rahisi tu. Unaamini kwamba kuna watu wanachaguliwa kuwa wabunge kwa mfano na hawana sifa kabisa za uongozi?
mtu anakuwaje mfano wakati sifa hana mbona unanichekesha kwenu ccm hakuna sifa maalum ya mtu kuwa mbunge? hata taahira anaweza chukua formu au una maanisha nini

mmefikia hatua mbaya sana
 
Ijapokuwa demokrasia ndio mfumo wa siasa wenye ubore zaidi duniani hadi sasa ukilinganisha na mifumo mingine, hivyo kutufanya wengi wetu kuutetea mara kwa mara; kuna mambo kadhaa ya msingi tunapaswa kufahamu.

Demokrasia kamili na uhuru katika hatua yake ya juu kabisa, vinafanya kazi kwa ufanisi katika jamii yenye kiwango cha juu sana cha kujitambua, ustaarabu, kuweza kuchanganua mambo na kuamua kwa busara. Ikiwa jamii ina kiwango cha chini cha tabia tajwa hapo juu, kwa kadiri kiwango cha demokrasia na uhuru wa watu kinavyoongezeka, ndio hatari ya kutokea majanga inavyoongezeka na kinyume chake. Hili tutalifafanua zaidi baadae.

Kwa bahati mbaya ni kwamba Afrika bado tupo watu wengi sana/wapiga kura ambao uelewa wetu juu ya mambo na uwezo wetu wa kuchanganua vitu na kufanya maamuzi sahihi ni mdogo. Kwa mfano, % kubwa ya watanzania hatuelewi falsafa, itikadi, misingi na sera ya vyama achilia mbali kuzifuata. Jiulize mfano ukisema chama cha mrengo wa kushoto, mrengo wa kati kushoto, mrengo wa kulia ujamaa wa kidemokrasia na vitu kama hivyo, ni watanzania wangapi wanaelewa unasema nini?

Wapiga kura wengi Afrika amma hupiga kura bila kujua nini wanafanya, au baada ya kuchanganywa ‘Manipulations’ au kwa mihemko ‘emotions’au kwa ushabiki usiokuwa na sababu za kueleweka. Ili hili lieleweke vizuri, nitatoa mifano michache.

Moja, Ushawahi kuona bungeni kwa mfano, mtu anatoa hoja nzuri sana, lakini wajumbe wakiulizwa ‘Mnaikubali hiyo hoja’ wanasema ‘hapanaaaaaaaa’ lakini sio kwamba hawaitaki hoja, ni kwa sababu ya nani katoa hoja, kwa hiyo wajumbe wakishaona mtoa hoja washaikataa hoja tayari hawana haja hata ya kuielewa kwanza?

Mbili, Unajua tunaweza kwenda wote kwenye uchaguzi, wewe ni muadilifu na unahoja nzuri, mimi nikawa ni mjinga flani tu, ila nikasubiria masaa kadhaa kabla ya uchaguzi nikakuzushia kwamba wewe unauza meno ya tembo huku nimetumbua mimacho kweli kweli, na wapiga kura wakakukataa na kunikubali mimi, kisha baada ya uchaguzi (kukushinda), nikasema nilikuwa natania tu, sijawahi kuuona ukiuza meno?

Tatu, Unajua wapiga kura kwenye nchi za kiafrika wakipewa rushwa humchagua mtoa rushwa na kuacha watu wenye maono?

Nne, Unajua kwa mfano wewe ukipiga kampeni kwa kuongea mambo ya maana mwingine akawa anakatika, una uwezo wa kushindwa uchaguzi, na hata mzee wa mauno alishinda kimzaha hivyo hivyo? N.k

Kwa mantiki hiyo basi;

  • Kwa sababu ya uelewa wa waafrika tuliowengi, demokrasia peke yake haiwezi kutusaidia kuwa na nchi zenye ustawi na uongozi bora bali inahitajika mfumo wa ziada kujazia demokrasia ‘Complementary system’

  • Kwa kuwa wapiga kura wanaweza kupiga kura kwa kuvurugwa ‘Manipulation’ kura pekee hazituwezeshi kupata viongozi wa maana, Hivyo utaratibu uliowekwa na CCM kuchuja majina kwa kuzingatia vigezo vingine zaidi ya kupigiwa kura sio tu kwamba ni mzuri bali ni muhimu sana kwa ustawi wa Taifa na hatma ya nchi.

  • Hoja ya Rais Magufuli kwamba watu ambao tayari wana vyeo vya kutumikia wananchi kama wakuu wa mikoa ni bora wasigombee ubunge, inaegemea kwenye mantiki zaidi kwa kuangalia ‘motive’ na inatokana na ‘complementary system iliyotajwa hapo juu kwa ajili ya maslahi ya Taifa

  • Kwa kuwa tatizo la rushwa kwenye uchaguzi bado ni kubwa, kazi anayoifanya polepole kukemea rushwa na kuwatahadharisha watakaotoa rushwa kukatwa majina sio tu kwamba ni nzuri bali pia ni muhimu.
Kwa ujumla, mfumo huo wa kuwa na ‘control mechanism’ zaidi ya kura, haukinzani na demokrasia bali unajazia mapungufu ya demokrasia hivyo sio ‘Contradictory system’ kama baadhi ya wadau wanavyodhani bali ni ‘Complementary system’ na bila kufanya hivyo, tunaweza kukuta nchi nzima ina wabunge wa ajabu haijapata kutokea na kila mtu akabaki anashangaa ikiwemo wapiga kura wenyewe. Kwa hiyo wale wanaodhani mfumo huo ni kinyume na demokrasia, ni vizuri wakafahamu ‘dynamics’ hizi na kwa hili, tunaweza kusema CCM inachukua hatua zasahihi kabisa na zinazokubalika kitaam ku‘regulate’ hali ya mambo kwa maslahi ya taifa.
Hakuna kutetea kwa lolote ni kuminywa kwa Demokrasia ambapo ni mbaya zaidi kuliko ile Lumumba wanalia kwa mbowe. Haiwezekani ukataji wa majina ukaegemea na SIKU HIYO KAAMKAJE ina maana mtakua mnaombea siku ya ukataji wa jina la Kawe Alumni awe alipewa ili aamke salama ndo apate demokrasia yake. Nlidhan kwa vile ni wakongwe basi demokrasia ndo ingeshika kasi ili kila MTU apate haki yake. Kumbe mnasubiria mkuu KAAMKAJE ndo mpate haki.
 
Hebu acha kuonyesha UZWAZWA wako.

Kwa bahati nzuri au mbaya, hao unaowaona hawana akili, ndio cream kwenye jamii yetu. Ndio maana tunasisitiza kwamba ni lazima kama jamii tuwekeze kwenye self development ili kutoka kwetu wakiibuka viongozi wawe na taswira bora zaidi. Kinyume chake tunatamani kuwa na watu ambao hawapo kwenye 'Sample'
 
Tena ndo vizuri ili wabunge vilaza wapungue
mbunge gani mwenye akili ndani ya ccm wote wanaweka akili zao mfukoni wanatoa yale ya mfuko wa nyuma ndo wanatumia
mtu anakuwaje mfano wakati sifa hana mbona unanichekesha kwenu ccm hakuna sifa maalum ya mtu kuwa mbunge? hata taahira anaweza chukua formu au una maanisha nini

mmefikia hatua mbaya sana
Wewe unatumia haki yako ya kidemokrasia tu ila huna hoja. Wewe huyo huyo ndio unasema wabunge wa CCM hawana akili, wewe huyo huyo ndio unabisha kuwa hakuna uwezekano wa mtu asiye na sifa za uongozi kuwa mbunge, kwa hiyo kwa mujibu wa maelezo yako kutokuwa na akili ni sifa ya uongozi?

Anyway, hoja zako ni reflexion ya tatizo la msingi la aina ya wapiga kura wanaozungumziwa kwenye uzi mama.
 
Hakuna kutetea kwa lolote ni kuminywa kwa Demokrasia ambapo ni mbaya zaidi kuliko ile Lumumba wanalia kwa mbowe. Haiwezekani ukataji wa majina ukaegemea na SIKU HIYO KAAMKAJE ina maana mtakua mnaombea siku ya ukataji wa jina la Kawe Alumni awe alipewa ili aamke salama ndo apate demokrasia yake. Nlidhan kwa vile ni wakongwe basi demokrasia ndo ingeshika kasi ili kila MTU apate haki yake. Kumbe mnasubiria mkuu KAAMKAJE ndo mpate haki.
yaani hawa majamaa wamefikia pale alipotabiri nyerere kuwa mkimaliza wale mnaohisi si ndugu zenu kwenye mfano wa muungano baadaye mtahisi kumbe sisi si wamoja wengine hawafai ndo hii ya kukata majina.

mwanzoni walikuwa wanaungana dhidi ya cdm sasa wanahisi wamewamaliza cdm wamehamia ndani kilio hicho cha huko ndani haiwaachi salama mpaka watauana wenyewe na kuparanganyika.

ile nyumba ya kijani balaaa yake suburini inakuja kwa kasi kweli
 
Wewe unatumia haki yako ya kidemokrasia tu ila huna hoja. Wewe huyo huyo ndio unasema wabunge wa CCM hawana akili, wewe huyo huyo ndio unabisha kuwa hakuna uwezekano wa mtu asiye na sifa za uongozi kuwa mbunge, kwa hiyo kwa mujibu wa maelezo yako kutokuwa na akili ni sifa ya uongozi?

Anyway, hoja zako ni reflexion ya tatizo la msingi la aina ya wapiga kura wanaozungumziwa kwenye uzi mama.
jibu swali nilikuuliza mbunge wa mfano anakuwaje usiruke ruke
 
Back
Top Bottom