MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,194
Wandugu, nachukuaa fursa hii kuwafagilia CCM kwa hatua inazochukua ambazo zimeendana na utafiti wa kisayansi. Uamuzi uliochukuliwa White House, Dodoma ulikuwa mgumu hatahivyo wa lazima kuendana na kipindi tulichoko.
CDM wameropoka sana kuhusu UFISADI ndani ya chama, Uongozi wa Kamanda JK ukawa kimya ukipanga mikakati, hatimaye kikosi kazi cha wasomi waliobea katika masuala ya siasa wakiongozwa na Profesa ukipewa kazi ya kufanya utafiti kwa kuhusisha makundi mbalimbali ya wanachama na watanzania kwa ujumla.
Data zikakusanywa toka kwa wananchi wakiwemo wana CDM ndipo ripoti ikatoka pamoja na mapendekezo yakawasilishwa CC. Watz inabidi tuwape dole CCM kwa kutambua hali halisi na kuchukua hatua za kuunda kikosi kazi cha wasomi. CDM poleni sana, kwani CCM tatizo limetambuliwa, limefanyiwa kazi na sasa wananchi wamerudisha imani kwa CCM yao.
CDM utaendelea na kususia vikao vya madiwani, wakati CCM ikichanya mbuga; kaskazini - kusini na mashariki - magharibi.
CDM tafadhali tumieni nafasi ya CCM kuondoa magamba kama changamoto kubwa kwenu na muanze na sera mpya kama mkiwa na nia ya dhati kuiondoa CCM mtaa wa Magogoni, vinginevyo mtabaki kupambana na vijana wa Saidi Mwema barabarani.
CCM Oyee na Operesheni Ondoa Magamba; BRAVO kOMREDI MUKAMA
CDM wameropoka sana kuhusu UFISADI ndani ya chama, Uongozi wa Kamanda JK ukawa kimya ukipanga mikakati, hatimaye kikosi kazi cha wasomi waliobea katika masuala ya siasa wakiongozwa na Profesa ukipewa kazi ya kufanya utafiti kwa kuhusisha makundi mbalimbali ya wanachama na watanzania kwa ujumla.
Data zikakusanywa toka kwa wananchi wakiwemo wana CDM ndipo ripoti ikatoka pamoja na mapendekezo yakawasilishwa CC. Watz inabidi tuwape dole CCM kwa kutambua hali halisi na kuchukua hatua za kuunda kikosi kazi cha wasomi. CDM poleni sana, kwani CCM tatizo limetambuliwa, limefanyiwa kazi na sasa wananchi wamerudisha imani kwa CCM yao.
CDM utaendelea na kususia vikao vya madiwani, wakati CCM ikichanya mbuga; kaskazini - kusini na mashariki - magharibi.
CDM tafadhali tumieni nafasi ya CCM kuondoa magamba kama changamoto kubwa kwenu na muanze na sera mpya kama mkiwa na nia ya dhati kuiondoa CCM mtaa wa Magogoni, vinginevyo mtabaki kupambana na vijana wa Saidi Mwema barabarani.
CCM Oyee na Operesheni Ondoa Magamba; BRAVO kOMREDI MUKAMA