Benny Haraba
JF-Expert Member
- Dec 7, 2012
- 8,387
- 6,355
Eti watu wasiojulikana,kumbe hawakutakiwa wajulikane,kwa kulewa majukumu waliyokuwa wamepewa, walifanya yao binafsi piaKabla ya vyama sisi sote ni watanzania.
Moja ya imani za CCM ni kuwa binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.
Tumefikaje huku kwenye kuuwana, kutekana, kutesana, kupotezana, kubambikiziana kesi na yote yenye ukakasi huu?
Ilikuwaje kina Sabaya wakatambulika kama vijana wazalendo pamoja na matendo yao maovu?
View attachment 1986970
Kundi la watu wasiojulikana ni halisi, lipo na rasmi limejipenyeza katika utawala wa nchi hii. Pole pole kalitambua kama parallel power na kuwa kwa sababu ya kundi hilo, CCM wala hamsikilizwi tena katika uendeshaji wa nchi.
Si kweli kuwa kundi hili linawatumia ninyi kama koti tu, la kufichia madhambi yao? Si kweli kuwa nyie mko kimya kwa sababu ya vipande 30 vya pesa linavyowapa baadhi yenu?
Hamuioni chuki inayomea nchini kwa sababu ya kundi hili? Nanyi mmeridhia kufungamanishwa pamoja na kundi la wauwaji hawa?
Kulifumbia macho kundi hili ni kukubali kuwa mshirika wa haramu zake.
View attachment 1986971
Kulifumbia macho kundi hili hakutawaacha salama siku zote.
Ushauri wa bure kwenu kama nchi hii mnaipenda, basi jitengeni na kundi hili.
Kufanya hivyo hadharani kutawapa uhalali wa kujivua madhambi yao.
Kila mmoja na akaubebe msalaba wake mwenyewe.