TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
SERIKALI imeondoa kwa muda zuio la kuuza mahindi na sembe nje ya nchi ili kutoa motisha kununua mahindi ya ziada kutoka kwa wakulima kutokana na mavuno kuwa mazuri ikiwa ni dalili za awali za mafanikio ya utekelezaji wa Kilimo Kwanza.
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda alisema zuio hilo limeondolewa kwa makampuni yanayojishughulisha na biashara ya mahindi na sembe.
Alikuwa akizindua mradi wa matrekta ya Kilimo Kwanza wa Shirika Uchumi la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), Lugalo jijini Dar es Salaam leo (Alhamisi Okt. 7, 2010).
Lakini, Waziri Mkuu alitoa angalizo kwamba wananchi watumie vizuri fursa hiyo na wahakikishe wanajiwekea akiba ya kutosheleza familia zao na wasiuze chakula chao chote.
Akikariri taarifa ya tathmini ya hali ya chakula na lishe ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika mwezi uliopita, alisema imethibitika kuwa kuna chakula tani 12.8 nchini zikiwemo tani milioni 7.7 za mazao ya nafaka na tani milioni 5.1 zisizo nafaka na hivyo kujitosheleza kwa asilimia 112 na kuna ziada ya tani milioni 1.4, alisema.
Kutokana na mafanikio yanayoanza kujitokeza katika uzalishaji wa nafaka nchini, Waziri Mkuu alisema, serikali imeagiza Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula kununua tani 200,000 za mahindi kutoka kwa wakulima waliozalisha ziada.
Hadi Oktoba 5, 2010, jumla ya tani 96,680 zilikuwa zimenunuliwa na hivyo kuwezesha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula kuwa na akiba ya mahindi tani 144,367. Ununuzi bado unaendelea, alisema.
Akielezea mafanikio utekelezaji wa Kilimo Kwanza, Waziri Mkuu alisema pia kwamba matumizi ya mbolea yameongezeka kwa asilimia 76 kutoka tani 241,753 mwaka 2004/05 hadi 302,000 mwaka 2009/10 na upatikanaji wa mbolea ya ruzuku kutoka tani 53,389 hadi 150,000.
Idadi ya wataalamu wa ugani katika vyuo vya kilimo imeongeeka kutoka 650 mwaka 2005/2006 hadi 3,500 mwaka 2009/10 na kufanya idadi ya wataalamu wa ugani wanaofundisha wakulima teknolojia za kilimo cha kisasa kufikia 4,439, alisema.
Alisema upatikanaji wa mbegu bora nao umeongezeka kwa asilimia 54 kutoka tani 10,477 mwaka 2005/06 hadi 16,148 mwaka 2009/10 na uzalishaji wa chakula kutoka tani milioni 9.66 mwaka 2005/06 hadi milioni 12.8 mwaka 2009/10, sawa na ongezeko la asilimia 33.
Haya ni baadhi tu ya mafanikio ya Kilimo Kwanza. Naamini baada ya uzinduzi wa mradi huu wa matrekta, mafanikio zaidi yatapatikana, alisema.
Azma ya Kilimo Kwanza ilizinduliwa na Rais Kikwete mwaka 2009, ikilenga mapinduzi katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi kuongeza uzalishaji, ufanisi na tija katika sekta hizo na hivyo kutekeleza nguzo ya MKUKUTA ya kupiga vita umasikini wa Watanzania walio wengi.
Katika uzinduzi huo wa mradi wa matrekta ya Kilimo Kwanza, Waziri Mkuu aliwasha trekta la aina ya Farmtrac, lililounganishwa na kiwanda cha SUMAJKT Mwenge baada ya kupata vifaa kutoka kampuni ya Escorts ya India, chini ya mradi maalum wa kuunganisha matrekta hayo.
Chini ya mradi huo, unaofuatia makubalianao ya mkopo kwa Serikali ya Tanzania kutoka India, yatapatikana matrekta 1,860 na matrekta madogo (power tillers) 400 pamoja na zana za kilimo kutoka kampuni ya Escorts ya India.
Matumizi ya matrekta kwa kilimo, ni sehemu ya nguzo ya Kilimo Kwanza inayosisitiza matumizi ya zana bora na kuondoa jembe la mkono.Uingizaji wa materkta nchini umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka nchini. Katika kipindi cha mwaka 2005/06 hadi mwaka 2009/10 jumla ya matrekta makubwa 2,364 na matrekta madogo 3,214 yaliingizwa nchini n kuuzwa na makampuni binafsi.
Katika kwama 2009/10 jumla ya matrekta 627 na matrekta madogo 2,219 yaliingizwa nchini kwa ajili ya kusambazwa kwa wakulima kupitia Halmashauri na Vyama vya Ushirika.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi; Balozi wa Tanzania nchini India, Injinia John Kijazi na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Kocheril Bhagirath na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange pia walikuwepo kwenye sherehe hiyo ya uzinduzi wa matrekta.
(mwisho)
Imetolewa na:
Ofisi ya Waziri Mkuu,
S.L.P. 3021,
DAR ES SALAAM
Alhamisi Okt. 7, 2010
CCM kilijengwa kwa jasho la Wakulima na Wafanyakazi, hivyo mafisadi hawana haki yeyote kuwanyang'anya waliotoka jasho na damu kukiunda CCM.
Kama wao walikuja huko baadaye na kukifadhili chama, ilikuwa si kwa ajili ya kulijenga Taifa au kukiimarisha Chama, bali ni kujiwekea mianya na njoa nyoofu ya kuweza kujitunishia mifuko yao kwa kutuhujumu kwa kutumia dola na upindishwaji wa Sheria na kanuni.
Walichokifanya ni kwa manufaa yao na si manufaa ya Watanzania na wanachama ambao ni Wakulima na Wafanyakazi.
Mafisadi na Ufisadi ni Wanyonyaji na wanaimarisha Unyonyaji, sawa na minyoo inayokaa tumboni mwa kiumbe na kujishibisha chakula cha kiumbe huyu, au kupe anayeng'angania ngozi na kufnyonza damu kama si kunguni anayejificha kwenye godoro naye akisubiri mwenye godoro alale ili ajishibishe!
Originally Posted by Rev. Kishoka
CCM kilijengwa kwa jasho la Wakulima na Wafanyakazi, hivyo mafisadi hawana haki yeyote kuwanyang'anya waliotoka jasho na damu kukiunda CCM.
Kama wao walikuja huko baadaye na kukifadhili chama, ilikuwa si kwa ajili ya kulijenga Taifa au kukiimarisha Chama, bali ni kujiwekea mianya na njoa nyoofu ya kuweza kujitunishia mifuko yao kwa kutuhujumu kwa kutumia dola na upindishwaji wa Sheria na kanuni.
Walichokifanya ni kwa manufaa yao na si manufaa ya Watanzania na wanachama ambao ni Wakulima na Wafanyakazi.
Mafisadi na Ufisadi ni Wanyonyaji na wanaimarisha Unyonyaji, sawa na minyoo inayokaa tumboni mwa kiumbe na kujishibisha chakula cha kiumbe huyu, au kupe anayeng'angania ngozi na kufnyonza damu kama si kunguni anayejificha kwenye godoro naye akisubiri mwenye godoro alale ili ajishibishe!
ccm hailekebishiki solution nikuipiga chini ijifunze!Ccm ni ya matajiri siku hizi ndo mana anayetoa kikubwa ndo anathaminika