Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,427
Kwanza ni vizuri chama cha CCM kustuka kuwa adui au hatari kubwa inayokikabili sio upinzani (Tutafafanua mbeleni). CCM inakabiliwa na hatari kubwa mbili;
Kwanza, masuala kadhaa yanayolalamikiwa lakini pengine bado jamii inaona hayajashughulikiwa kikamilifu na pili ni changamoto ya ‘Diminishing marginal utility’. Tutafafanua kwa kuanza na hii hoja ya pili.
Iko hivi, hata kitu kiwe kizuri kiasi gani, watu wanatabia ya kukinai wanapopata kitu hicho hicho kwa muda mrefu. Kanuni hii mara nyingi inatumika kwenye uchumi ikifahamika kama ‘Diminishing marginal utility’. Kwa mfano ukila samaki muda mrefu; hutataka tena samaki, sio kwa sababu samaki ni kitu kibaya, bali kwa sababu umekula sana samaki na umekinai.
Kwa hiyo basi, hata kama CCM iko perfect kwa 100% (by assumption at least), inakabiliwa na changamoto tajwa hapo juu na hiyo si changamoto ya kupuuzwa kwa sababu katika mazingira ya mtu kukinai, huhitaji mbadala wowote tu hata kama ndimu. Nini cha kufanya tutaeleza baadae.
Kwa nini tunasema upinzani hauwezi kuwa ndio adui au hatari inayoikabili CCM? Moja ya nchi zenye vyama vya upinzani ambavyo vipo ‘disorganized’ & ‘unfocused’ ni vya kwetu (Hili lishazungumzwa mara nyingi).
Vile vile, nguvu za chama chochote cha siasa duniani ziko kwenye maeneo makuu matano, Fedha, rasilimali watu, Ushawishi, mabavu(japo hii haishauriwi kutumika) na uadilifu. Ukiangalia vyama vya upinzani Tanzania vina nguvu moja tu kati ya hizo wakati CCM wanazo tatu ila katika mazingira ya kushangaza kabisa, mwenye 3 anamuogopa mwenye 1. Sababu ni hizi
- Inaonekana kuna vitu CCM wali/wanatakakiwa kufanya(nao kwenye nafsi zao wanaamini walipaswa kufanya) ila hawajafanya, hali hiyo inawasababisha kukosa amani ndani ya nafsi na hivyo kupoteza kujiamini kwenye kujenga ushawishi. Hii inajibu swali la msingi ambalo watu wamekuwa wanauliza mara kadhaa.Kwa upande mwingine baadhi baadhi ya wadau pia hawaridhishwi na hilo (hili linaelewa bila shaka)
- Hoja ya kukinai tuliyoieleza huko juu ambapo mtu akikinai kitu (hata kama ni kizuri) hatakitaka tena, anaweza kuacha nyama akala ugali na chumvi, sio kwa sababu chumvi ni nzuri kuliko nyama bali kashachoka nyama. Na
- Tabia ya mwanadamu ya kushabikia upande dhaifu pale inapotokea mashindano kati ya upande wenye nguvu. Kwa mfano, inapotokea timu moja ya huko kilosa inacheza na Yanga, timu ya kilosa ikishambulia obvisly watu watashangilia kuliko yanga ikishambulia, sio kwa sababu hiyo timu ni bora zaidi ya yanga bali kwa sababu ya unyonge. Any way, nani anakumbuka vita ya Marekani na Vietnam?
- CCM kama chama ikae chini iangalie vitu vinavyolalamikiwa na kuvishungulikia. Vingi ukiviangalia vina faida kuliko hasara. Hii itasaidia kujenga kujiamini na kuboresha ushawishi kisiasa.
- Iangalie uwezekano wa kubadilisha jina na baadhi ya vionjo; Hii itasaidia kutatua changamoto ya ‘Diminishing Marginal utility’ iliyoelezwa hapo juu.
- Isaidie kupatikana kwa mazingira rafiki ya demokrasia kwa wote, hiyo itasaidia kuondoa malalamiko lakini hatari kadhaa ambazo ziko wazi sana.
- Hata kama CCM ina uwezo wa kutumia nguvu ya mabavu; nguvu hii haishauriwi sana kuitumia kwenye siasa za kiraia kwa sababu kwa kadiri unavyoitumia kwenye siasa za kiraia; ndivyo unavyopoteza ushawishi na hiyo sio nzuri. Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya mwanadamu kuhurumia upande unaoonekana kuumizwa na kujikuta akijiunga na upande huo japo kihisia (Rejea mchezo wa mieleka)
- Baadaya ya hapo kila kitu kitakuwa safi, CCM safi, wapinzani safi, siasa safi Tanzania safi.