CCM itumie njia gani ili iweze kukubalika na kushinda chaguzi bila kusababisha uwezekano wa kutokea kwa madhara

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,427
1573469058243.png
Angalizo; mada hii inaweza kuwa ngumu kidogo, kama umechoka akili unaweza kuiacha kwanza mpaka akili yako ikiwa imetulia ndio usome.

Kwanza ni vizuri chama cha CCM kustuka kuwa adui au hatari kubwa inayokikabili sio upinzani (Tutafafanua mbeleni). CCM inakabiliwa na hatari kubwa mbili;

Kwanza, masuala kadhaa yanayolalamikiwa lakini pengine bado jamii inaona hayajashughulikiwa kikamilifu na pili ni changamoto ya ‘Diminishing marginal utility’. Tutafafanua kwa kuanza na hii hoja ya pili.

Iko hivi, hata kitu kiwe kizuri kiasi gani, watu wanatabia ya kukinai wanapopata kitu hicho hicho kwa muda mrefu. Kanuni hii mara nyingi inatumika kwenye uchumi ikifahamika kama ‘Diminishing marginal utility’. Kwa mfano ukila samaki muda mrefu; hutataka tena samaki, sio kwa sababu samaki ni kitu kibaya, bali kwa sababu umekula sana samaki na umekinai.

Kwa hiyo basi, hata kama CCM iko perfect kwa 100% (by assumption at least), inakabiliwa na changamoto tajwa hapo juu na hiyo si changamoto ya kupuuzwa kwa sababu katika mazingira ya mtu kukinai, huhitaji mbadala wowote tu hata kama ndimu. Nini cha kufanya tutaeleza baadae.

Kwa nini tunasema upinzani hauwezi kuwa ndio adui au hatari inayoikabili CCM? Moja ya nchi zenye vyama vya upinzani ambavyo vipo ‘disorganized’ & ‘unfocused’ ni vya kwetu (Hili lishazungumzwa mara nyingi).

Vile vile, nguvu za chama chochote cha siasa duniani ziko kwenye maeneo makuu matano, Fedha, rasilimali watu, Ushawishi, mabavu(japo hii haishauriwi kutumika) na uadilifu. Ukiangalia vyama vya upinzani Tanzania vina nguvu moja tu kati ya hizo wakati CCM wanazo tatu ila katika mazingira ya kushangaza kabisa, mwenye 3 anamuogopa mwenye 1. Sababu ni hizi


  • Inaonekana kuna vitu CCM wali/wanatakakiwa kufanya(nao kwenye nafsi zao wanaamini walipaswa kufanya) ila hawajafanya, hali hiyo inawasababisha kukosa amani ndani ya nafsi na hivyo kupoteza kujiamini kwenye kujenga ushawishi. Hii inajibu swali la msingi ambalo watu wamekuwa wanauliza mara kadhaa.Kwa upande mwingine baadhi baadhi ya wadau pia hawaridhishwi na hilo (hili linaelewa bila shaka)
  • Hoja ya kukinai tuliyoieleza huko juu ambapo mtu akikinai kitu (hata kama ni kizuri) hatakitaka tena, anaweza kuacha nyama akala ugali na chumvi, sio kwa sababu chumvi ni nzuri kuliko nyama bali kashachoka nyama. Na
  • Tabia ya mwanadamu ya kushabikia upande dhaifu pale inapotokea mashindano kati ya upande wenye nguvu. Kwa mfano, inapotokea timu moja ya huko kilosa inacheza na Yanga, timu ya kilosa ikishambulia obvisly watu watashangilia kuliko yanga ikishambulia, sio kwa sababu hiyo timu ni bora zaidi ya yanga bali kwa sababu ya unyonge. Any way, nani anakumbuka vita ya Marekani na Vietnam?
Nini cha Kufanya;

  • CCM kama chama ikae chini iangalie vitu vinavyolalamikiwa na kuvishungulikia. Vingi ukiviangalia vina faida kuliko hasara. Hii itasaidia kujenga kujiamini na kuboresha ushawishi kisiasa.
  • Iangalie uwezekano wa kubadilisha jina na baadhi ya vionjo; Hii itasaidia kutatua changamoto ya ‘Diminishing Marginal utility’ iliyoelezwa hapo juu.
  • Isaidie kupatikana kwa mazingira rafiki ya demokrasia kwa wote, hiyo itasaidia kuondoa malalamiko lakini hatari kadhaa ambazo ziko wazi sana.
  • Hata kama CCM ina uwezo wa kutumia nguvu ya mabavu; nguvu hii haishauriwi sana kuitumia kwenye siasa za kiraia kwa sababu kwa kadiri unavyoitumia kwenye siasa za kiraia; ndivyo unavyopoteza ushawishi na hiyo sio nzuri. Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya mwanadamu kuhurumia upande unaoonekana kuumizwa na kujikuta akijiunga na upande huo japo kihisia (Rejea mchezo wa mieleka)
  • Baadaya ya hapo kila kitu kitakuwa safi, CCM safi, wapinzani safi, siasa safi Tanzania safi.
 
Vyama vya siasa (Vya kiraia) havishauriwi kutumia nguvu ya mabavu "Coersion power" hata kama vinayo kwa sababu, kwa kadiri chama kinavyotumia nguvu hiyo ndivyo kinavyopoteza nguvu ya ushawishi "Convincing power" na nguvu ya ushawishi ni muhimu zaidi kwenye siasa za kiraia kuliko nguvu ya mabavu.
 
Wapinzani wameogopa kushindwa wameamua kujitoa
Kwa upande mwingine kama kuna kitu ambacho nafsini mwako unaamini ulipaswa kukifanya lakini kwa sababu yoyote ile hukukifanya, au unaamini hukupaswa kukifanya ila kwa sababu yoyote ukakifanya, matokeo yake hukupotezea amani ya nafsi, Ukipoteza amani ya namfsi unapoteza kujiamini, ukishapoteza kujiamini inakuwa uweze wako wa kushawishi hata kama ulikuwa ni mkubwa unashuka, na ukishindwa kushawishi ni nini kilichobbaki hapo?

Kwa hicho hiyo changamoto inakuja hivyo. Ndio maana pia inashauriwa kuwa ni muhimu kuwa mkweli na dhamira njema. Unakuwa huna cha kupoteza
 
Na wale ambao hawataelewa vizuri kanuni ya hapo juu, wakumbuke visa vya watu wanaosomesha wake halafu baadae wanawakimbia. Sio kwa lazima wanaokimbiwa wawe ni watu wabaya sana kuliko huko mkimbiliaji anakokimbilia, bali ni kwa sababu ya kanuni ya hapo juu, na hiyo iko hivyo tu kiasili.
 
Yaan Tz ukiwa upinzani ni kosa hata usemekitu na kinamanufaa na kinaletamaendeleo utapingwa tu Kwasababu ww ni mpinzani.Hakuna faida sasa ya vyama vingi kama hali ni hii.
 
Ni kwa nanuni hii hii ya 'diminishing marginal utility' vyama vikikaa kwa muda flani madarakani vinabadilisha majina. Kama kilikuwa kinaitwa 'chungwa', kinajiita 'embe'! na kubadili baadhi ya features
 
Na pia ndio maana inashauriwa kwamba kiongozi akishakaa madarakani muda fulani hata kama anapendwa kiasi gani atoke kwanza na kama ni kurudi arudi baadae. Rejea kesi ya Putin.
 
Mbinu wanazotumia sasahivi ndio zinafaa, na wakibadili mbinu tu wanatoka kwenye game.
 
Angalizo; mada hii inaweza kuwa ngumu kidogo, kama umechoka akili unaweza kuiacha kwanza mpaka akili yako ikiwa imetulia ndio usome.

Kwanza ni vizuri chama cha CCM kustuka kuwa adui au hatari kubwa inayokikabili sio upinzani (Tutafafanua mbeleni). CCM inakabiliwa na hatari kubwa mbili;

Kwanza, masuala kadhaa yanayolalamikiwa lakini pengine bado jamii inaona hayajashughulikiwa kikamilifu na pili ni changamoto ya ‘Diminishing marginal utility’. Tutafafanua kwa kuanza na hii hoja ya pili.

Iko hivi, hata kitu kiwe kizuri kiasi gani, watu wanatabia ya kukinai wanapopata kitu hicho hicho kwa muda mrefu. Kanuni hii mara nyingi inatumika kwenye uchumi ikifahamika kama ‘Diminishing marginal utility’. Kwa mfano ukila samaki muda mrefu; hutataka tena samaki, sio kwa sababu samaki ni kitu kibaya, bali kwa sababu umekula sana samaki na umekinai.

Kwa hiyo basi, hata kama CCM iko perfect kwa 100% (by assumption at least), inakabiliwa na changamoto tajwa hapo juu na hiyo si changamoto ya kupuuzwa kwa sababu katika mazingira ya mtu kukinai, huhitaji mbadala wowote tu hata kama ndimu. Nini cha kufanya tutaeleza baadae.

Kwa nini tunasema upinzani hauwezi kuwa ndio adui au hatari inayoikabili CCM? Moja ya nchi zenye vyama vya upinzani ambavyo vipo ‘disorganized’ & ‘unfocused’ ni vya kwetu (Hili lishazungumzwa mara nyingi).

Vile vile, nguvu za chama chochote cha siasa duniani ziko kwenye maeneo makuu matano, Fedha, rasilimali watu, Ushawishi, mabavu(japo hii haishauriwi kutumika) na uadilifu. Ukiangalia vyama vya upinzani Tanzania vina nguvu moja tu kati ya hizo wakati CCM wanazo tatu ila katika mazingira ya kushangaza kabisa, mwenye 3 anamuogopa mwenye 1. Sababu ni hizi


  • Inaonekana kuna vitu CCM wali/wanatakakiwa kufanya(nao kwenye nafsi zao wanaamini walipaswa kufanya) ila hawajafanya, hali hiyo inawasababisha kukosa amani ndani ya nafsi na hivyo kupoteza kujiamini kwenye kujenga ushawishi. Hii inajibu swali la msingi ambalo watu wamekuwa wanauliza mara kadhaa.Kwa upande mwingine baadhi baadhi ya wadau pia hawaridhishwi na hilo (hili linaelewa bila shaka)
  • Hoja ya kukinai tuliyoieleza huko juu ambapo mtu akikinai kitu (hata kama ni kizuri) hatakitaka tena, anaweza kuacha nyama akala ugali na chumvi, sio kwa sababu chumvi ni nzuri kuliko nyama bali kashachoka nyama. Na
  • Tabia ya mwanadamu ya kushabikia upande dhaifu pale inapotokea mashindano kati ya upande wenye nguvu. Kwa mfano, inapotokea timu moja ya huko kilosa inacheza na Yanga, timu ya kilosa ikishambulia obvisly watu watashangilia kuliko yanga ikishambulia, sio kwa sababu hiyo timu ni bora zaidi ya yanga bali kwa sababu ya unyonge. Any way, nani anakumbuka vita ya Marekani na Vietnam?
Nini cha Kufanya;

  • CCM kama chama ikae chini iangalie vitu vinavyolalamikiwa na kuvishungulikia. Vingi ukiviangalia vina faida kuliko hasara. Hii itasaidia kujenga kujiamini na kuboresha ushawishi kisiasa.
  • Iangalie uwezekano wa kubadilisha jina na baadhi ya vionjo; Hii itasaidia kutatua changamoto ya ‘Diminishing Marginal utility’ iliyoelezwa hapo juu.
  • Isaidie kupatikana kwa mazingira rafiki ya demokrasia kwa wote, hiyo itasaidia kuondoa malalamiko lakini hatari kadhaa ambazo ziko wazi sana.
  • Hata kama CCM ina uwezo wa kutumia nguvu ya mabavu; nguvu hii haishauriwi sana kuitumia kwenye siasa za kiraia kwa sababu kwa kadiri unavyoitumia kwenye siasa za kiraia; ndivyo unavyopoteza ushawishi na hiyo sio nzuri. Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya mwanadamu kuhurumia upande unaoonekana kuumizwa na kujikuta akijiunga na upande huo japo kihisia (Rejea mchezo wa mieleka)
  • Baadaya ya hapo kila kitu kitakuwa safi, CCM safi, wapinzani safi, siasa safi Tanzania safi.

Rahisi sana ...... kwanza upinzani sio uadui wala vita
Ccm waache kutumia police kwa mambo ya siasa
Ccm waache kuwazibiti wa pinzani kwa kuwanyima mikutano. Kipindi cha awamu ya nne vyama viliruhusiwa ikitokea tuhuma upande huu basi upande mwingine unajibu na hoja inakufa.
Lakini sasa upinzani wanaminywa hawapati haki hata kama ccm wapo sahihi lakini kwa kuwaminya wezao wanaonekana hawako sahihi.
Mwisho kuwe na tume huru
 
Vyama vya siasa (Vya kiraia) havishauriwi kutumia nguvu ya mabavu "Coersion power" hata kama vinayo kwa sababu, kwa kadiri chama kinavyotumia nguvu hiyo ndivyo kinavyopoteza nguvu ya ushawishi "Convincing power" na nguvu ya ushawishi ni muhimu zaidi kwenye siasa za kiraia kuliko nguvu ya mabavu.

Uzi wako umefanana kabisa na post yangu niliyoiweka jana, nitakutag uone nilichosema kuhusu kanuni ya wakati. Mpaka nimepata mashaka kuwa umechukua mawazo yangu na kuyawekea vionjo ili inoge zaidi. Nakubaliana na ww kwa asilimia miamoja kuwa kwa sasa ccm iko kwenye hali hiyo ya kukinaiwa, hata wafanye nini, iwe kibaya au kizuri watu hawawataki tu basi.
 
wangeshindana wapi wakati mmewakata karibu wote?? yani unatoa kadi nyekundu kwa wachezaji 9 unabakisha wawili uwanjani, nao wanatoka kukuacha ucheze pekeyako halafu unalalamika eti wameogopa kushindwa? kama ulijua watashindwa umewatoa wa kazi gani? waache wote uwashinde
Wapinzani wameogopa kushindwa wameamua kujitoa
 
Uzi wako umefanana kabisa na post yangu niliyoiweka jana, nitakutag uone nilichosema kuhusu kanuni ya wakati. Mpaka nimepata mashaka kuwa umechukua mawazo yangu na kuyawekea vionjo ili inoge zaidi. Nakubaliana na ww kwa asilimia miamoja kuwa kwa sasa ccm iko kwenye hali hiyo ya kukinaiwa, hata wafanye nini, iwe kibaya au kizuri watu hawawataki tu basi.
Hapana, sijauona mkuu, ila kama upo na una maudhui haya haya basi ni jambo jema. nadhani ni vizuri kukazia hoja kwa sababu nadhani ni hoja nzuri na muhimu.

Ningependa pia kuona hoja yako kwenye uzi huo.
 
Angalizo; mada hii inaweza kuwa ngumu kidogo, kama umechoka akili unaweza kuiacha kwanza mpaka akili yako ikiwa imetulia ndio usome.

Kwanza ni vizuri chama cha CCM kustuka kuwa adui au hatari kubwa inayokikabili sio upinzani (Tutafafanua mbeleni). CCM inakabiliwa na hatari kubwa mbili;

Kwanza, masuala kadhaa yanayolalamikiwa lakini pengine bado jamii inaona hayajashughulikiwa kikamilifu na pili ni changamoto ya ‘Diminishing marginal utility’. Tutafafanua kwa kuanza na hii hoja ya pili.

Iko hivi, hata kitu kiwe kizuri kiasi gani, watu wanatabia ya kukinai wanapopata kitu hicho hicho kwa muda mrefu. Kanuni hii mara nyingi inatumika kwenye uchumi ikifahamika kama ‘Diminishing marginal utility’. Kwa mfano ukila samaki muda mrefu; hutataka tena samaki, sio kwa sababu samaki ni kitu kibaya, bali kwa sababu umekula sana samaki na umekinai.

Kwa hiyo basi, hata kama CCM iko perfect kwa 100% (by assumption at least), inakabiliwa na changamoto tajwa hapo juu na hiyo si changamoto ya kupuuzwa kwa sababu katika mazingira ya mtu kukinai, huhitaji mbadala wowote tu hata kama ndimu. Nini cha kufanya tutaeleza baadae.

Kwa nini tunasema upinzani hauwezi kuwa ndio adui au hatari inayoikabili CCM? Moja ya nchi zenye vyama vya upinzani ambavyo vipo ‘disorganized’ & ‘unfocused’ ni vya kwetu (Hili lishazungumzwa mara nyingi).

Vile vile, nguvu za chama chochote cha siasa duniani ziko kwenye maeneo makuu matano, Fedha, rasilimali watu, Ushawishi, mabavu(japo hii haishauriwi kutumika) na uadilifu. Ukiangalia vyama vya upinzani Tanzania vina nguvu moja tu kati ya hizo wakati CCM wanazo tatu ila katika mazingira ya kushangaza kabisa, mwenye 3 anamuogopa mwenye 1. Sababu ni hizi


  • Inaonekana kuna vitu CCM wali/wanatakakiwa kufanya(nao kwenye nafsi zao wanaamini walipaswa kufanya) ila hawajafanya, hali hiyo inawasababisha kukosa amani ndani ya nafsi na hivyo kupoteza kujiamini kwenye kujenga ushawishi. Hii inajibu swali la msingi ambalo watu wamekuwa wanauliza mara kadhaa.Kwa upande mwingine baadhi baadhi ya wadau pia hawaridhishwi na hilo (hili linaelewa bila shaka)
  • Hoja ya kukinai tuliyoieleza huko juu ambapo mtu akikinai kitu (hata kama ni kizuri) hatakitaka tena, anaweza kuacha nyama akala ugali na chumvi, sio kwa sababu chumvi ni nzuri kuliko nyama bali kashachoka nyama. Na
  • Tabia ya mwanadamu ya kushabikia upande dhaifu pale inapotokea mashindano kati ya upande wenye nguvu. Kwa mfano, inapotokea timu moja ya huko kilosa inacheza na Yanga, timu ya kilosa ikishambulia obvisly watu watashangilia kuliko yanga ikishambulia, sio kwa sababu hiyo timu ni bora zaidi ya yanga bali kwa sababu ya unyonge. Any way, nani anakumbuka vita ya Marekani na Vietnam?
Nini cha Kufanya;

  • CCM kama chama ikae chini iangalie vitu vinavyolalamikiwa na kuvishungulikia. Vingi ukiviangalia vina faida kuliko hasara. Hii itasaidia kujenga kujiamini na kuboresha ushawishi kisiasa.
  • Iangalie uwezekano wa kubadilisha jina na baadhi ya vionjo; Hii itasaidia kutatua changamoto ya ‘Diminishing Marginal utility’ iliyoelezwa hapo juu.
  • Isaidie kupatikana kwa mazingira rafiki ya demokrasia kwa wote, hiyo itasaidia kuondoa malalamiko lakini hatari kadhaa ambazo ziko wazi sana.
  • Hata kama CCM ina uwezo wa kutumia nguvu ya mabavu; nguvu hii haishauriwi sana kuitumia kwenye siasa za kiraia kwa sababu kwa kadiri unavyoitumia kwenye siasa za kiraia; ndivyo unavyopoteza ushawishi na hiyo sio nzuri. Hii ni kwa mujibu wa kanuni ya mwanadamu kuhurumia upande unaoonekana kuumizwa na kujikuta akijiunga na upande huo japo kihisia (Rejea mchezo wa mieleka)
  • Baadaya ya hapo kila kitu kitakuwa safi, CCM safi, wapinzani safi, siasa safi Tanzania safi.
Mambo ya msingi yanayopuuzwa na hao watu ni:
Democracy
Katiba na sheria
Uwazi na ukweli
Haki za binadamu na utawala bora
Tume huru ya uchaguzi
Uhuru wa kujieleza
Na mengine kibao. Hili la kuchuja au kukinaiwa ni mambo ya lugha tu, hakuna msosi hapo.
 
Hapana, sijauona mkuu, ila kama upo na una maudhui haya haya basi ni jambo jema. nadhani ni vizuri kukazia hoja kwa sababu nadhani ni hoja nzuri na muhimu.

Ningependa pia kuona hoja yako kwenye uzi huo.

Nimekutag, na maelezo hayo nimeyaeleza mara kwa mara. Wakati wa uchaguzi nilisema, watu wanamshangilia Lowassa lakini Lowassa sio msafi, na hata kiutendaji Magufuli ni zaidi yake. Ila tatizo ni mahitaji ya kizazi kwamba watu wameichoka ccm. Nikasema wangalau wabadili, au wafanye kama kilichofanyika Kenya kufa kwa KANU na leo akina Uhuru Kenyatta wanaongoza Kenya.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom