Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,471
- 46,002
Wiki hizi mbili status yangu WhatsApp imejazwa na posti za jumbe za heri kwa wafanyakazi, ndugu jamaa na marafiki wakiwatakia heri watu wao wanaogombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM.
Wengine hata sio watu wa siasa kabisa.
Katika mitandao nimeona hadi viongozi wa vyama vya upinzani kama ACT wakiwatakia heri 'watu wao' wanaogembea uongozi ndani ya CCM
Nimeona wafanyabiashara, wasomi, wasiosoma, wanaharakati, wazee kwa vijana wengi na wengine waliotimuka kutoka vyama vya upinzani kama CHADEMA wakigombea nafasi za uongozi ndani ya CCM.
Kuna namna CCM imejifungamanisha na maisha ya raia wengi wa nchi hii, wa kada zote, wa rika zote, wa pande zote, wa dini zote, wa Simba na Yanga na wa kabila zote kama vile samaki na maji. Wanaogelea humo, wanapata oksijeni humo, wanapata chakula humo. Katika mazingira upinzani ni kama nchi kavu katika, hauyumukiniki kwa wala hata haufikiriki kwa wengi.
Kazi ipo.
Wengine hata sio watu wa siasa kabisa.
Katika mitandao nimeona hadi viongozi wa vyama vya upinzani kama ACT wakiwatakia heri 'watu wao' wanaogembea uongozi ndani ya CCM
Nimeona wafanyabiashara, wasomi, wasiosoma, wanaharakati, wazee kwa vijana wengi na wengine waliotimuka kutoka vyama vya upinzani kama CHADEMA wakigombea nafasi za uongozi ndani ya CCM.
Kuna namna CCM imejifungamanisha na maisha ya raia wengi wa nchi hii, wa kada zote, wa rika zote, wa pande zote, wa dini zote, wa Simba na Yanga na wa kabila zote kama vile samaki na maji. Wanaogelea humo, wanapata oksijeni humo, wanapata chakula humo. Katika mazingira upinzani ni kama nchi kavu katika, hauyumukiniki kwa wala hata haufikiriki kwa wengi.
Kazi ipo.