Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa umekiacha Chama Cha Mapinduzi kikiwa na makovu makubwa yakiongozana na maumivu makali. Kimepigwa ngumi na mateke ya kutosha.
Tumepata taarifa toka sehemu mbalimbali za nchi kwamba UKAWA wamejinyakulia viti lukuki kulinganisha na matokea ya miaka mitano iliyopita. UKAWA kupitia mshirika wake mkuu, CHADEMA, wamefanikiwa kusimamisha wagombea maeneo mengi kuliko ambavyo CHADEMA ilifanya miaka mitano iliyopita. Tumeshuhudia wagombea wa CCM waliopita bila kupingwa wakipungua sana. Kwa hali inavyoendelea, CCM inasubiri anguko lingine kabla ya uchaguzi Mkuu nalo ni kukataliwa kwa Katiba Pendekezwa!
Hii inaonyesha kwamba upinzani hapa nchini umeimarika na unazidi kuimarika kadri tunavyosogelea uchaguzi mkuu wa mwaka kesho. Kama UKAWA wataendelea kuwa pamoja na kuacha uroho ambao tumekuwa tukiushuhudia miaka kadhaa iliyopita, basi mwakani hali ni ya hatari kwa CCM. Kila kukicha watu wanapata confidence kwamba kumbe CCM inaweza kutoka na kisitokee chochote kama ambavyo waliaminishwa hapo zamani.
Kwa hiyo CCM inabidi ijipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu kama inataka kubaki madarakani. Hali ya sasa ya makundi ndani ya CCM itaendelea kuitafuna hadi inaondoka madarakani na kuitafuna hata kama itakuwa upinzani na matokeo yake tunaweza kushuhudia chama kingine kikongwe hapa Afrika kikipotea kwenye ramani ya vyama kongwe kama ilivyotokea kwa KANU, UNIP, UPC, n.k
Katika hali kama hii ya tishio kubwa kutoka UKAWA, kwa sasa CCM watake wasitake wana turufu moja tu nayo ni Dr. John Pombe Magufuli. Inajulikana kwamba wahafidhina wengi ndani ya serikali wanaiogopa misimamo ya Dr. John Pombe Magufuli lakini kwa hili wataona ni afadhali zimwi likujualo na hivyo wakamsimamisha kuwaokoa. Wanaweza wakaamua Rais asiwe Mwenyekiti wa Chama ili kupunguza nguvu zake ndani ya chama.
Huyu ndiye compromising candidate ndani ya CCM na anauzika kwa Watanzania walio wengi.
Najua watu watakuja na hoja ya uuzaji nyumba za serikali. Waliuziwa watanzania.
Tumepata taarifa toka sehemu mbalimbali za nchi kwamba UKAWA wamejinyakulia viti lukuki kulinganisha na matokea ya miaka mitano iliyopita. UKAWA kupitia mshirika wake mkuu, CHADEMA, wamefanikiwa kusimamisha wagombea maeneo mengi kuliko ambavyo CHADEMA ilifanya miaka mitano iliyopita. Tumeshuhudia wagombea wa CCM waliopita bila kupingwa wakipungua sana. Kwa hali inavyoendelea, CCM inasubiri anguko lingine kabla ya uchaguzi Mkuu nalo ni kukataliwa kwa Katiba Pendekezwa!
Hii inaonyesha kwamba upinzani hapa nchini umeimarika na unazidi kuimarika kadri tunavyosogelea uchaguzi mkuu wa mwaka kesho. Kama UKAWA wataendelea kuwa pamoja na kuacha uroho ambao tumekuwa tukiushuhudia miaka kadhaa iliyopita, basi mwakani hali ni ya hatari kwa CCM. Kila kukicha watu wanapata confidence kwamba kumbe CCM inaweza kutoka na kisitokee chochote kama ambavyo waliaminishwa hapo zamani.
Kwa hiyo CCM inabidi ijipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu kama inataka kubaki madarakani. Hali ya sasa ya makundi ndani ya CCM itaendelea kuitafuna hadi inaondoka madarakani na kuitafuna hata kama itakuwa upinzani na matokeo yake tunaweza kushuhudia chama kingine kikongwe hapa Afrika kikipotea kwenye ramani ya vyama kongwe kama ilivyotokea kwa KANU, UNIP, UPC, n.k
Katika hali kama hii ya tishio kubwa kutoka UKAWA, kwa sasa CCM watake wasitake wana turufu moja tu nayo ni Dr. John Pombe Magufuli. Inajulikana kwamba wahafidhina wengi ndani ya serikali wanaiogopa misimamo ya Dr. John Pombe Magufuli lakini kwa hili wataona ni afadhali zimwi likujualo na hivyo wakamsimamisha kuwaokoa. Wanaweza wakaamua Rais asiwe Mwenyekiti wa Chama ili kupunguza nguvu zake ndani ya chama.
Huyu ndiye compromising candidate ndani ya CCM na anauzika kwa Watanzania walio wengi.
Najua watu watakuja na hoja ya uuzaji nyumba za serikali. Waliuziwa watanzania.