CCM inaponata na beat za CHADEMA

TAI DUME

JF-Expert Member
Feb 20, 2014
8,846
23,090
Subal kheri Watanzania. Ni ndefu kidogo kama mvivu wa kusoma omba samari kwa jirani yako.

Kwa wale wapenzi wa muziki hususani mziki wa kufoka foka wanaelewa maana ya kunata na beat. Kwa wasioelewa ni kile kitendo Cha rapper kuimba sambamba na mdundo bila kuuacha nyuma au kutangulia mbele.

Sasa Basi kwa miaka mitano ya JPM, CCM kwa kiasi kikubwa imekuwa ikitekeleza sera au matamanio ya CDM waliyokuwa wanayapigia kelele kwa muda mrefu. Inawezekana kwa kujua au kutokujua. Ni wazi kwa kipindi hiki nchi iliendeshwa kwa matakwa ya CHADEMA. CCM haikutekeleza sera take isipokuwa ya CHADEMA.

No wonder hata mkuu wa kaya aliwapiga ban wapinzani kufanya siasa ikiwa ni ujumbe kwamba mnataka Nini Tena wakati yote mliyokuwa mnayalilia tunayatekeleza kwa vitendo. Inawezekana pia hii ikawa ni sababu ya baadhi ya wapinzani kuunga mkono juhudi za mwenyekiti iwe kwa hiyari au kuhiyarishwa.

Nitazungumzia machache.

Mosi, CHADEMA walikuwa wanataka rais mkali asiyecheka cheka hovyo. CCM ikawapa JPM.

Pili, CHADEMA walikerwa Sana na viongozi wakuu kusafiri safiri nje. Wakafikia hatua ya kusema CCM inaweza kubinafsisha nchi huko ulaya kwa kusaini mikataba hovyo hovyo. Kilio kikasikika JPM akapiga ban safari za nje.

Tatu. CHADEMA walisema hatuwezi kukuza utalii nchini Kama hatutafufua shirika la ndege. Tena kipindi kile shirika lilikuwa Lina ndege moja tu mbovu Tena ya kukodi. JPM akasema hewala, wengi wape ila wachache wasikilizwe. Wakasikilizwa na kupewa kabisa, Mungu awape Nini Leo shirika Lina midege ya kutosha.

Nne, CHADEMA walipigia Sana kelele ufisadi uliopo TANESCO. Kwamba shirika linajiendesha kwa hasara na halitoi huduma stahiki. JPM akaangalia mikataba ilivo pale akaona dawa ni kutafuta chanzo Cha umeme Cha uhakika. Akaja na stigglers gouge. CDM are very lack yaani kila kitu wanasikilizwa.

Tano, CHADEMA walichafukwa mno na utendaji mbovu wa watendaji wa serikalini, kwamba wengi wamewekwa kwa kujuana na hawana vigezo. Yaani wenye vyeti feki au wasionavyo kabisa ndio walioshikilia Ofisi za umma. Again JPM akaanza nalo Hilo. Waliowakera CHADEMA wote wakafyekelewa mbali.

Sita, CHADEMA walilalamika Sana miradi ya serikali haionekani na pesa zinatolewa. Yaani walikuwa wanataka kuona matokeo ya matumizi ya pesa za serikali. Wakafika mbali kulalamika kwamba miundo mbinu Kama barabara, reli na majini ndio backbone ya uchumi. JPM bwana maikivu sana hachoki. Akasema Sasa mtaona matokeo ya fedha zenu. Reli hii hapa, mabarabara njia kumi hayo hapo, madaraja sijui flyovers hizo hapo. Asee Mimi niaingeweza.

CHADEMA hao hao walilalamika Sana kuhusu Ada zinazotozwa mashuleni na kupelekea watoto wa masikini kunyanyasika. Ni kweli hii pia ilikuwa kero. Kilio kikasikika tatizo likapatiwa dawa.

Saba. Akh yapo mengi Sana yanafika hata 50 mengine mtajazia wenyewe msinichishe.
HOJA YANGU NI IPI SASA??

1. Ni kwamba vyama vyenye mawazo mbadala vikiwa makini Kama chadema, CCM itajikuta inacheza ngoma za upinzani kwa kutaka au kutokutaka.

2. Upinzani ili uweze kuongoza nchi sio lazima ungie madarakani. Wakiwa smart wanaongoza nchi kwa remote control huku wao wakiwa wanaongeza familia majumbani kwao.

3. Watanzania tusiwe na wasiwasi, hizi sera nzuri nzuri za cdm, CCM inazichukulia kwa uzito na kwa uhakika zitatekelezwa miaka mitano ijayo. Tena mengine yameshaanza kutekelezwa, juzi tuu zimetoka ajira elfu 13 baada ya CHADEMA kulalamika walimu hawajaajiriwa kwa miaka mitano. CHADEMA are luck utafikiri yule mwana mpendwa aliyekuwa anasikilizwa Sana.
Point ya kufungia Uzi wangu.

Sasa hivi CHADEMA wanakuja na hoja za kutaka maendeleo ya watu, hata rungwe amefikia hatua kugawa ubwabwa ikiwa ni msisistizo huduma Sasa ziende moja kwa moja kwa watu. Binafsi naamini in case CHADEMA wasipochukua nchi, JPM ni msikivu na atayatekeleza hayo kwa vitendo. Wapinzani turelax hoja zetu zinatekelezwa kwa remote control watake wasitake.

Mwisho mwishoni.
Kura nitapiga ya ubunge na diwani tuu, ya rais sipigi kwani nipige nisipige fidodido atashinda tuu.
Wasalaam
 
Hao wasiojua hali halisi, matatizo na mahitaji sahihi wanasubiri mwingine awapangie watekeleze, bila shaka na ndiyo sababu hawawezi kutekeleza kwa viwango sahihi. Na bila shaka kwakutokujua umuhimu wa hayo wanayoyatekeleza, kwa kuwa si agenda zao muhimu, hawajui hata namna wala umuhimu wa kuweka sera endelevu.

Watu hawa kama hawana sifa za kuongoza nchi, kwa nini wang'ang'anie madarakani badala ya kuwaachia wenye maono na sera zao waongoze kuzitekeleza?

CCM KUNG'ANG'ANIA MADARAKA KWA KIGEZO CHA KUIBA NA KUTEKELEZA SERA ZA CHADEMA NDIO TAFSIRI HALISI YA 'UROHO WA MADARAKA. KUACHA WATU WENYE UWEZO ILI KUWAFICHA WASIONEKANE NI HUJUMA KWA MAENDELEO YA TAIFA, MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA, UNYANYASAJI NA MATUMIZI MABAYA YA RASLIMALI ZA TAIFA.
 
Kazi ya serikali ni kusikiliza kero za wananchi wawe binafsi au kupitia vyama vyao viwe cha siasa nk na kuzifanyia kazi

Mleta mada unashangaa nini?

Serikali yaweza chukua ilani za vyama vyote ikaweka mezani na kuzifanyia kazi
 
Kazi ya serikali ni kusikiliza kero za wananchi wawe kibinafsi au kupitia vyama vyao viwe cha siasa no na kuzifanyia kazi

Mleta mada unashangaa nini?


WENYE UFAHAMU NI WANAOTUNGA SERA KWA KUWA PROACTIVE. SIYO KUSUBIRI I WATU WAUMIE, WAPIGE KELELE ETI NDIPO ISEME INAONDOA KERO.

CCM KUWA SLUGGISHLY REACTIVE TENA BILA SUSTAINABLE TANGIBLE VISIONS, NDIYO INAWAFANYA WATU WAWACHUKIE KWA KUWA MMEDUMAZA MAENDELEO YA TAIFA NA HAMFAI KWA LOLOTE. NDIYO UELEWE KWAMBA KILA MWAKA MNASHINDWA UCHAGUZI NA KUTUMIA MABAVU KWA SABABU HATA WEWE UMETHIBITISHA KWAMBA MKO CHINI SANA YA KIWANGO.
 
WENYE UFAHAMU NI WANAOTUNGA SERA KWA KUWA PROACTIVE. SIYO KUSUBIRI I WATU WAUMIE, WAPIGE KELELE ETI NDIPO ISEME INAONDOA KERO.
utawala wa nchi ni bottom up sio Top down Pekee!!!

Kero zinatakiwa kutoka chini kwenda juu zitafutiwe ufumbuzi na ufumbuzi ushuke chini

Vyama cha siasa ni sehemu ya bottom kupeleka Keri juu kupitia ilani zao na Kellele zao ili zifanyiwe kazi na serikali

Mfano sasa hivi CCM kila mkutano wa chama cha siasa uwe Raisi,mbunge au diwani typo kuwasikiliza kuchukua Keri halisia tuzifanyie kazi awamu hii ya sita tunayoingia
 
utawala wa nchi ni bottom up sio Top down Pekee!!!

Kero zinatakiwa kutoka chini kwenda juu zitafutiwe ufumbuzi na ufumbuzi ushuke chini

Vyama cha siasa ni sehemu ya bottom kupeleka Keri juu kupitia ilani zao na Kellele zao ili zifanyiwe kazi na serikali

Mfano sasa hivi CCM kila mkutano wa chama cha siasa uwe Raisi,mbunge au diwani typo kuwasikiliza kuchukua Keri halisia tuzifanyie kazi awamu hii ya sita tunayoingia

You do not know what planning or policy development is. Wewe piga kelele mitandaoni. Siyo kosa kwamba hujui!. Unazidi kufunua utupu wa ccm.
 
Kazi ya serikali ni kusikiliza kero za wananchi wawe binafsi au kupitia vyama vyao viwe cha siasa nk na kuzifanyia kazi

Mleta mada unashangaa nini?
Serikali yaweza chukua ilani za vyama vyote ikaweka mezani na kuzifanyia kazi

Kuna mjumbe aliomba kuwezeshwa kupata japo 7000/- kwa siku. Msaidieni kufika kwa chakubanga mkaongeza ongezea nguvu kidogo naye angalau mkono ukaenda kinywani.
 
You do not know what planning or policy development is. Wewe piga kelele mitandaoni. Siyo kosa kwamba hujui!. Unazidi kufunua utupu wa ccm.
Any plan must originate at the bottom to be successful It must use bottom up approach not Top down!! Wananchi chini ndio waseme wanataka nini ndio upange

Chadema mfano hakiongelei wananchi wanataka nini kinaongelea hasa wanasiasa wa Chadema wanataka nini!!! Urasikia tunataka uhuru wa kuongea,uhuru wa vyombo vya habari,uhuru wa kufanya mikutano ya siasa,Bunge live,tume huru ambayo vyama vyote vitashirikishwa,Katiba mpya,serikali ya mseto na ujinga mwingine usiowakilisha
Shida halisia za wAnanchi Bali njaa za wanasiasa wa Chadema

Wananchi wao wanataka huduma bora za afya,maji safi,barabara,elimu bure kwa watoto wao nk

Mpango huanzia kwa wadau chini ambao ni wananchi sio vitu vya kutunga ofisi ya mipango
 
Subal kheri Watanzania. Ni ndefu kidogo kama mvivu wa kusoma omba samari kwa jirani yako.

Kwa wale wapenzi wa muziki hususani mziki wa kufoka foka wanaelewa maana ya kunata na beat. Kwa wasioelewa ni kile kitendo Cha rapper kuimba sambamba na mdundo bila kuuacha nyuma au kutangulia mbele....
Hakuna chama wala mgombea wakushindana na ccm. Kwa sababu vyama vingine vinaongojwa na KIKI za maigizo
 
Subah kheri Watanzania. Ni ndefu kidogo kama mvivu wa kusoma omba samari kwa jirani yako.

Kwa wale wapenzi wa muziki hususani mziki wa kufoka foka wanaelewa maana ya kunata na beat. Kwa wasioelewa ni kile kitendo Cha rapper kuimba sambamba na mdundo bila kuuacha nyuma au kutangulia mbele.

Sasa Basi kwa miaka mitano ya JPM, CCM kwa kiasi kikubwa imekuwa ikitekeleza sera au matamanio ya CDM waliyokuwa wanayapigia kelele kwa muda mrefu. Inawezekana kwa kujua au kutokujua. Ni wazi kwa kipindi hiki nchi iliendeshwa kwa matakwa ya CHADEMA. CCM haikutekeleza sera take isipokuwa ya CHADEMA.

No wonder hata mkuu wa kaya aliwapiga ban wapinzani kufanya siasa ikiwa ni ujumbe kwamba mnataka Nini Tena wakati yote mliyokuwa mnayalilia tunayatekeleza kwa vitendo. Inawezekana pia hii ikawa ni sababu ya baadhi ya wapinzani kuunga mkono juhudi za mwenyekiti iwe kwa hiyari au kuhiyarishwa.

Nitazungumzia machache.

Mosi, CHADEMA walikuwa wanataka rais mkali asiyecheka cheka hovyo. CCM ikawapa JPM.
Pili, CHADEMA walikerwa Sana na viongozi wakuu kusafiri safiri nje. Wakafikia hatua ya kusema CCM inaweza kubinafsisha nchi huko ulaya kwa kusaini mikataba hovyo hovyo. Kilio kikasikika JPM akapiga ban safari za nje.

Tatu. CHADEMA walisema hatuwezi kukuza utalii nchini Kama hatutafufua shirika la ndege. Tena kipindi kile shirika lilikuwa Lina ndege moja tu mbovu Tena ya kukodi. JPM akasema hewala, wengi wape ila wachache wasikilizwe. Wakasikilizwa na kupewa kabisa, Mungu awape Nini Leo shirika Lina midege ya kutosha.

Nne, CHADEMA walipigia Sana kelele ufisadi uliopo TANESCO. Kwamba shirika linajiendesha kwa hasara na halitoi huduma stahiki. JPM akaangalia mikataba ilivo pale akaona dawa ni kutafuta chanzo Cha umeme Cha uhakika. Akaja na stigglers gouge. CDM are very lack yaani kila kitu wanasikilizwa.

Tano, CHADEMA walichafukwa mno na utendaji mbovu wa watendaji wa serikalini, kwamba wengi wamewekwa kwa kujuana na hawana vigezo. Yaani wenye vyeti feki au wasionavyo kabisa ndio walioshikilia Ofisi za umma. Again JPM akaanza nalo Hilo. Waliowakera CHADEMA wote wakafyekelewa mbali.

Sita, CHADEMA walilalamika Sana miradi ya serikali haionekani na pesa zinatolewa. Yaani walikuwa wanataka kuona matokeo ya matumizi ya pesa za serikali. Wakafika mbali kulalamika kwamba miundo mbinu Kama barabara, reli na majini ndio backbone ya uchumi. JPM bwana maikivu sana hachoki. Akasema Sasa mtaona matokeo ya fedha zenu. Reli hii hapa, mabarabara njia kumi hayo hapo, madaraja sijui flyovers hizo hapo. Asee Mimi niaingeweza.

CHADEMA hao hao walilalamika Sana kuhusu Ada zinazotozwa mashuleni na kupelekea watoto wa masikini kunyanyasika. Ni kweli hii pia ilikuwa kero. Kilio kikasikika tatizo likapatiwa dawa.

Saba. Akh yapo mengi Sana yanafika hata 50 mengine mtajazia wenyewe msinichishe.
HOJA YANGU NI IPI SASA??

1. Ni kwamba vyama vyenye mawazo mbadala vikiwa makini Kama chadema, CCM itajikuta inacheza ngoma za upinzani kwa kutaka au kutokutaka.

2. Upinzani ili uweze kuongoza nchi sio lazima ungie madarakani. Wakiwa smart wanaongoza nchi kwa remote control huku wao wakiwa wanaongeza familia majumbani kwao.

3. Watanzania tusiwe na wasiwasi, hizi sera nzuri nzuri za cdm, CCM inazichukulia kwa uzito na kwa uhakika zitatekelezwa miaka mitano ijayo. Tena mengine yameshaanza kutekelezwa, juzi tuu zimetoka ajira elfu 13 baada ya CHADEMA kulalamika walimu hawajaajiriwa kwa miaka mitano. CHADEMA are luck utafikiri yule mwana mpendwa aliyekuwa anasikilizwa Sana.
Point ya kufungia Uzi wangu.

Sasa hivi CHADEMA wanakuja na hoja za kutaka maendeleo ya watu, hata rungwe amefikia hatua kugawa ubwabwa ikiwa ni msisistizo huduma Sasa ziende moja kwa moja kwa watu. Binafsi naamini in case CHADEMA wasipochukua nchi, JPM ni msikivu na atayatekeleza hayo kwa vitendo. Wapinzani turelax hoja zetu zinatekelezwa kwa remote control watake wasitake.

Mwisho mwishoni.
Kura nitapiga ya ubunge na diwani tuu, ya rais sipigi kwani nipige nisipige fidodido atashinda tuu.
Wasalaam
Jiwe anatandaza ukabila kwa kasi kubwa sana na huyu sasa ni hatari kwa nchi yetu mtu atakayechagua ccm au jiwe ni kukosa tu akili.
 
Any plan must originate at the bottom to be successful It must use bottom up approach not Top down!! Wananchi chini ndio waseme wanataka nini ndio upange

Chadema mfano hakiongelei wananchi wanataka nini kinaongelea hasa wanasiasa wa Chadema wanataka nini!!! Urasikia tunataka uhuru wa kuongea,uhuru wa vyombo vya habari,uhuru wa kufanya mikutano ya siasa,Bunge live,tume huru ambayo vyama vyote vitashirikishwa,Katiba mpya,serikali ya mseto na ujinga mwingine usiowakilisha
Shida halisia za wAnanchi Bali njaa za wanasiasa wa Chadema

Wananchi wao wanataka huduma bora za afya,maji safi,barabara,elimu bure kwa watoto wao nk

Mpango huanzia kwa wadau chini ambao ni wananchi sio vitu vya kutunga ofisi ya mipango

Ubishi wako ni wa kipumbavu. Kam ahujui hujui. Kwa nini ninyi mnapotengeneza sera msitengeneze kama wanazotengeneza CHaDEMA ? Tumia whatever the approach you want likini uje na kitu sahihi. Kama wote ccm na CHADEMA mko level moja, na mnatkiwa kuja na sera za taifa, kwa nini nyinyi hamna uwezo wa kuja na sera sahihi mnasubiri CHADEMa itengeneze ninyi mkopi? Ujinga!. Kwa heri.
 
Back
Top Bottom