CCM ina ubavu wa kumwondoa Rais madarakani kama ANC ya Afrika Kusini ilichomfanyia Zuma?

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Kamati kuu ya chama tawala nchini Afrika Kusini, cha African National Congress, ANC imeamua kumuondoa rais Jacob Zuma kama kiongozi wa taifa hilo. Amepewa masaa 48 ya kujiuzulu. Taarifa hii ni kulingana na chanzo kutoka uongozi wa juu wa ANC, kilipozungumza na shirika la habari la Reuters, mapema hii leo. Hatua hii inafuatia kikao kilichodumu kwa masaa 13, kilichohusisha viongozi wakuu wa chama hicho.
 
Ccm inO ubavu wa kuweka vibaraka Zanzibar.
Wanaweza kumuondo rais na makamu wa ccm Zanzibar
Na anaemuondoa ni mwenyekiti wake wa bara
Sababu ni vibaraka hawana chao, wakienda kinyume na matakwa wa walio waweka wataondolewa.
Lakini ccm bara kumuwajibisha mwenyekiti wao hawana ubavu hata akijitangaza ufalme ....watashangiria na kufanya maandamano ya kuunga mkono
 
Anaeongoza ccm ni M/Kiti bali siyo wanachama kama ilivyo ANC ya South Africa, kwa hiyo kuondolewa madarakani haiwezi kutokea hata kwa kujaribu. Pili hichi chama akiwemo M/Kiti wao wameekeza sana kwa TISS ambao wanaangalia maslahi ya mwenyekiti pamoja na chama kwa ujumla, uvccm ikiwa kinara kwa kutumiwa kufanikisha hayo
 
Salaamu!

Rais wa Afrika Kusini anavyopatikana ni sawa na Tz?
Je, sheria za vyama vya siasa Afrika Kusini na Tanzania ni sawa?
Je, tz rais akijiuzuru chama kinateua au tunarudi uchaguzi mkuu?
Je, kilichofanyika Znz mwaka 1984 ni nini?

Lazima watu wasome historia na mifumo ya kisheria ktkt nchi tofauti wakati wa kufananisha jambo
 
Kamati kuu ya chama tawala nchini Afrika Kusini, cha African National Congress, ANC imeamua kumuondoa rais Jacob Zuma kama kiongozi wa taifa hilo. Amepewa masaa 48 ya kujiuzulu. Taarifa hii ni kulingana na chanzo kutoka uongozi wa juu wa ANC, kilipozungumza na shirika la habari la Reuters, mapema hii leo. Hatua hii inafuatia kikao kilichodumu kwa masaa 13, kilichohusisha viongozi wakuu wa chama hicho.
Zidumu fikra za mwenyekiti
 
Kamati kuu ya chama tawala nchini Afrika Kusini, cha African National Congress, ANC imeamua kumuondoa rais Jacob Zuma kama kiongozi wa taifa hilo. Amepewa masaa 48 ya kujiuzulu. Taarifa hii ni kulingana na chanzo kutoka uongozi wa juu wa ANC, kilipozungumza na shirika la habari la Reuters, mapema hii leo. Hatua hii inafuatia kikao kilichodumu kwa masaa 13, kilichohusisha viongozi wakuu wa chama hicho.
Kwa CCM ni alinacha!!!
 
Kamati kuu ya chama tawala nchini Afrika Kusini, cha African National Congress, ANC imeamua kumuondoa rais Jacob Zuma kama kiongozi wa taifa hilo. Amepewa masaa 48 ya kujiuzulu. Taarifa hii ni kulingana na chanzo kutoka uongozi wa juu wa ANC, kilipozungumza na shirika la habari la Reuters, mapema hii leo. Hatua hii inafuatia kikao kilichodumu kwa masaa 13, kilichohusisha viongozi wakuu wa chama hicho.
CCM haina ubavu huo, bali rais ndo mwenye ubavu dhidi ya CCM
 
Back
Top Bottom