Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
CCM inayo dira. Inayo dira kwa muda mrefu tu. Dira ambayo wamiandika hadi kwenye vitabu vyao na wanajitahidi kutekeleza. Dira ambayo wana CCM wameikumbatia na kuitetea kile kukicha. Kuwaambia kuwa CCM haina dira ni sawa na kumuambia dereva hana usukani, ni sawa na kumuambia nahodha kuwa meli haina dira wakati yuko katikati ya bahari.
tatizo ni kuwa hiyo dira wanaitumia kwenda wapi? Ndio maana wakati mwingine inasemwa CCM imepoteza mwelekeo; inayo dira lakini haifuati dira hiyo matokeo yake inaelekea kule ambako dira haielekezi. Kutokana na ugumu wa manahodha wake, CCM haitaki kurudia dira, inataka kueendelea kuelekea inakoelekea.
Lakini uweezekano mkubwa ni kuwa siyo hawana dira bali wameipoteza na hakuna mwenye utayari wa kukila hilo!
tatizo ni kuwa hiyo dira wanaitumia kwenda wapi? Ndio maana wakati mwingine inasemwa CCM imepoteza mwelekeo; inayo dira lakini haifuati dira hiyo matokeo yake inaelekea kule ambako dira haielekezi. Kutokana na ugumu wa manahodha wake, CCM haitaki kurudia dira, inataka kueendelea kuelekea inakoelekea.
Lakini uweezekano mkubwa ni kuwa siyo hawana dira bali wameipoteza na hakuna mwenye utayari wa kukila hilo!