CCM imejidhalilisha, kumbe huwa inawapa Maspika kusimamia mhimili wa Bunge ili kuficha madhambi na makosa ya serikali yake

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Jana ndio kila picha limeungua hapa nchini. Maana kauli za mkuu wa nchi na mwenyekiti wa CCM zimefunua macho watanzania.

Kumbe mtu kuwa spika lazima uaminiwe na wanaCCM ili kulinda maslahi yao na ya chama chao kwa kuficha makosa yao na madhambi yao. Ila ukifanya kazi ya kusimamia serikali na kueleza makosa ya serikali inakuwa nongwa.

Hii ni dalili mbaya sana na kuonyesha kuwa kumbe bunge la JMT kujaza wanaCCM bungeni ni kwa ajilo ya kulinda ufisadi na maovu ya chama chao.
 
Back
Top Bottom