Uchaguzi 2020 CCM imechokwa na Watanzania tuache utani kabisa

Major

JF-Expert Member
Dec 20, 2007
1,865
2,439
Kama siyo mbinu ya JPM Kupiga Marufuku mikutano ya kisiasa tangu Alipoingia Madarakani, sasa hivi tungekuwa tunaongea mengine kabisa, Nina Imani hata kitendo cha kuvunja katiba ya Nchi makusudi ni baada ya Kuona CCM ilivyozidiwa ktk Kampeni za Uraisi, 2015. Binafsi Mimi siyo mfuasi wa Chama chochote cha siasa, ila Mmi ni Mtanzania ninayependa sana Nchi yangu.

Lakini kutokana na Chama hiki kushinwa kabisa kuwa na mbinu za kuwaletea Maendeleo Watanzania, niseme tu ukweli, ninatamani hiki chama kipumzishwe na tukikabidhi kazi chama kingine chochote cha siasa labda tunaweza kuona tofauti. Kwa sababu kwa CCM iliyopo ambayo imeshachoka kabisa, hata tungewapa tena miaka 50, bado tutadidimia tu, hawana jipya tena.

Kwanza tu mjue, Viongozi wengi wanaotuongoza Kutoka CCM ni wazee na wengi ni wagonjwa. Ushahidi ni wakati wa Yule babu wa Loliondo alipoamua Kugawa dawa yake maarufu Kama Kikombe cha Babu. Tulishuhudia jinsi Viongozi wetu walivyomiminika kugombea kikombe. bahati mbaya kile kikombe kilikuwa ni Tiba feki, kwa hiyo Mkae mkijua wale watu bado wanaumwa tena kwa sasa maradhi ndiyo yamekomaa, Mtu yeyote anayeumwa Mara nyingi huwa na msongo wa mawazo na Mara nyingi huwa hutumia fikra na akili zake zote kufikiri juu ya hatma ya Maradhi yake, Kwa hiyo tusitegemee lolote jipya juu ya hawa watu, ila inatakiwa tuwasaidie kuwaambia Wapumzike Wameshatutumikia vya kutosha, sasa ni Muda wetu kuwatunza.

Sababu kubwa ya JPM Kuangusha uchumi wa Nchi ni kutumia nguvu na Raslimali nyingi sana kuhakikisha anavunja nguvu ya Upinzani, badala ya Kuongoza Nchi yeye akaamua kudeal na Wapinzani. Kumbe alitakiwa tu kupiga mahesabu ya kawaida na apate majibu ya ni kwanini ni vigumu sana kuua upinzani. Matokeo yake ilipokuja ripoti ya CAG ikaonekana Tsh, 1.5 Trilion hakuna na Matumizi yake hayajulikani. Raisi mwenyewe Hiyo ripoti ilimuumiza sana, kwa sababu ninavyomjua Mimi huyu JPM ni mtu mwaminifu sana. Nina Imani alipojaribu kuwauliza watu wake walimwambia kuwa Hii 1.5 trillion ndiyo gharama ya Kukilinda Chama.

Gharama ya kuilinda CCM kwa sasa ni kubwa kuliko bajeti ya wizara yoyote ktk Nchi hii, kwa sababu kila mtu anajua, CCM Haina jipya na Muda wake umepita, CCM ya Sasa Bila Polisi haiwezi kupata hata 15% ya kura halali ktk uwanja wa Haki wa Kidemokrasia, Kamanda Siro huu ndiyo Muda wake halali kabisa kutajirika pamoja na Maafisa wake wa ngazi za juu, Ingekuwa Mimi ndiyo Kamanda Siro sasa hivi ningekuwa tajiri Mkubwa katika matajiri wa nchi hii. Potelea mbali.

Ikiwa vyama vya siasa vimezuwiwa kufanya mikutano kwa miaka 5 kinyume kabisa cha Sheria ya Nchi yetu, na wakati huo huo CCM pekee ndiyo wanaruhusiwa kufanya mikutano na ikiwa Tv, Redio na magazeti karibu yote yanaiimbia CCM pambio na bado watu hawaelewi na hawataki kabisa kusikia CCM, ni Matokeo ya kwamba, Sikio limeshakufa, hata utie ubani kiasi gani lazima harufu itatoka tu.

Rai yangu, kwa Wahusika wote wa CCM, Nguvu Mnayoitumia kukilinda hiki Chama Cha Wazee ambacho kimeshakufa,Ni bora mkatumia fedha hizo kwa kuwekeza ktk miradi ya maendeleo kwa Mustakabali wa Uzee wenu.
 
Wakati dai la kuchokwa CCM (labda pengine unamaanisha kiongozi/viongozi wake) huko pengine ndio hovyo kabisa. Hakuna utaratibu mahususi wa kupata viongozi unaojulikana zaidi ya kuona kuna dalili na viashiria vya ukand au udini au Kuna Wenyeviti maalum na Viongozi maalum)

So bado tuna mwendo mrefu wa kufikia tunachokihitaji mpaka kukifukia.
 
Ccm ccm hiki ni chama cha mapinduzi na kinachofanyika sasa ni maana halisi ya mapinduzi, mwaka wa nne huu nasikilizia maendeleo kwenye karatasi
Bro,Unaambiwa kwa sasa hivi hakuna Kitu chenye Gharama kubwa Kama kuilinda CCM kiharamu ktk Nchi hii, Hata hiyo 1.5 trillion iliyopotea ni kwa ajili ya Ulinzi wa chama. Ndiyo maana JPM akiulizwa tu juu ya ile 1.5 huwa hana majibu ya kueleweka. Huwa anakasirikaga sana,
 
Mwalimu alishaweka wazi kuwa sisiemu sio wazazi wake.
Wacha kumtajataja Mama wa Taifa.
nakumbuka kwenye bunge LA katiba akina lissu waliambiwa eti wasitaje taje jina la baba wa taifa, acha watu wacharuke! sasa kwani kutajwa kwa jina la maria ni haramu tz? hii mbegu iliopandwa naona inamea, wanatajwa mitume sembuse RAIA😀
 
Chama cha mashetani ccm kimechokwa vibaya sana ,sasa Jiwe anahasira sana maana yeye alijua anapendwa sana na watanzania ,sasa kilichomwacha hoi ni Kule kushindwa uchaguzi vibaya sana ile 2015 ,

pamoja na kupindua matokeo lakini ilimuuma sana ,ili kulipiza kisasi Jiwe akaanza kuwakomoa wananchi ,Mara vunjia nyumba ,Mara vyeti feki ,Mara tumbua tumbua ,Mara fungia biashara ,hiyo yote ilikuwa ni visasi na hasira za kukataluwa na watanzania .
 
Kama siyo mbinu ya JPM Kupiga Marufuku mikutano ya kisiasa tangu Alipoingia Madarakani, sasa hivi tungekuwa tunaongea mengine kabisa, Nina Imani hata kitendo cha kuvunja katiba ya Nchi makusudi ni baada ya Kuona CCM ilivyozidiwa ktk Kampeni za Uraisi, 2015. Binafsi Mimi siyo mfuasi wa Chama chochote cha siasa, ila Mmi ni Mtanzania ninayependa sana Nchi yangu...

Mimi binafsi yangu na familia yangu wenye umri wa kupiga kura wote hatuipendi CCM kabisa!

Hii ni kweli and Im not joking!

Sijui wengine!
 
Kama siyo mbinu ya JPM Kupiga Marufuku mikutano ya kisiasa tangu Alipoingia Madarakani, sasa hivi tungekuwa tunaongea mengine kabisa, Nina Imani hata kitendo cha kuvunja katiba ya Nchi makusudi ni baada ya Kuona CCM ilivyozidiwa ktk Kampeni za Uraisi, 2015. Binafsi Mimi siyo mfuasi wa Chama chochote cha siasa, ila Mmi ni Mtanzania ninayependa sana Nchi yangu...
Mimi huwa nachanganyikiwaga hapo.ccm inawanachama chini ya 14m.watanzania tupo over 59m.yaani inakuwaje mtu mmoja from kikundi cha watu wachache,avuruge utaratibu tuliokubaliana kama taifa kwa faida ya kikundi chake harafu sisi tumekaa tu tunamuangalia,Je sisi ni watu kweli?
 
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom