CCM ilivyomdhalilisha Marehemu Reginald Mengi

Ciprofloxacin.

JF-Expert Member
Apr 15, 2015
1,583
2,696
Hayati Reginald Mengi ktk uhai wake hakuwahi kujionyesha hadharani kuwa yeye alikuwa ni mwanachama wa chama gani cha siasa.

Bali alijikita ktk kusaidia watu wenye shida mbali mbali za kimaisha wakiwemo walemavu, yatima na wajane.

Hiyo ndo ilikuwa ibaada ya hayati Reginald Mengi, ibaada njema kuliko zote ni kusaidia yatima, wajane na maskini.

Hakupenda kujihusisha na siasa kwa namna yoyote ile, na wala jamii haikujua Kama ni mwanachama wa chama gani cha siasa,na yeye hakupenda kujulikana kabisa.

Mara baada ya kutwaliwa na Mungu wakaibuka CCM na kuanza kutoa kiki kwamba alikuwa ni mwanachama wa CCM, huku ni kumdhalilisha Marehemu, Kama yeye hakupenda kujionyesha kwa nini nyie mwonyeshe uanachama wake baada ya kifo chake?

CCM ni chama kilichojaa watu wenye inferiority complex isipokuwa Katibu mkuu Dr Bashiru Ally, huyu ni mtu wa aina yake, aliyezungukwa na na vipofu wa akili.

Na ndo maana hata wanachama wa CCM si watu wa kawaida, mnaanzaje kutafuta kiki kwa Marehemu? ili watu waone kuwa CCM ni chama kizuri sana?

Mnakoelekea mtasema hata Trump ni mwana CCM.
 
Hilo la Mengi kuwa mwana CCM siyo issue sana maana kwa nchi hii ambamo usalama wa mtu kimaisha na kiuchumi inategemes chama alichomo haishangazi Mengi kuwa na kadi ya CCM. Siku za mwanzo wakati mwili wa marehemu ukisubiriwa toka Dubai (WAZEE WA FURSA) walitaka kuubeba kama mali ya Chama, labda familia ilishituka na majoho ya kijani yakaanza kupungua akabaki bwana MWENDATARATIBU na shati lake la mboga mboga.
Kuhusu Trump hilo pigia msitari kabisa. Umesahau jinsi ambavyo chombo kimoja cha habari nchini kilivyoeleza Dunia kwamba Bwana Donald mtoto wa Trump anahusudu sana "Mutu ya Chattle hadi anatakamani kuiga style yake ya uongozi"???
 
Kwenye ugomvi wa marehemu na manji.
Manji alikuwa anatumia wabunge na mawaziri wajinga kumdhalilisha mengi

Kuna kaada wa ccm alimdhalilisha mengi kwa kusema mengi sio ccm ni mpinzani

Mzee akiongea na wanahabari alionyesha Kadi mbili za chama TANU and CCM
 
Trump (turufu) alikuwa jirani yake Nnauye Oysterbay Hill Road karibu na shule ya msingi. Wakati wa kampeni za Trump (turufu) kuna shati moja la kijani alikuwa anapenda sana kulivaa na kwa mshono linafanana sana na alilokuwa akivaa Kolimba.
 
Wewe ni muongo,tena muongo kwelikweli ,muongo wa kiwango cha lami.Mengi alipotuhumiwa kuwa siyo mwana CCM,alitoka na kadi yake toka enzi za TANU na akarushwa katka taarifa ya habari ITV saa mbili usiku ,kama alivyofanya siku anakama madai ya yeye kuwa na kale kagonwa cha nyumbani.Au unataka kusema mzee alikuwa mnafiki?
 
Hayati Reginald Mengi ktk uhai wake hakuwahi kujionyesha hadharani kuwa yeye alikuwa ni mwanachama wa chama gani cha siasa.

Bali alijikita ktk kusaidia watu wenye shida mbali mbali za kimaisha wakiwemo walemavu, yatima na wajane.

Hiyo ndo ilikuwa ibaada ya hayati Reginald Mengi, ibaada njema kuliko zote ni kusaidia yatima, wajane na maskini.

Hakupenda kujihusisha na siasa kwa namna yoyote ile, na wala jamii haikujua Kama ni mwanachama wa chama gani cha siasa,na yeye hakupenda kujulikana kabisa.

Mara baada ya kutwaliwa na Mungu wakaibuka CCM na kuanza kutoa kiki kwamba alikuwa ni mwanachama wa CCM, huku ni kumdhalilisha Marehemu, Kama yeye hakupenda kujionyesha kwa nini nyie mwonyeshe uanachama wake baada ya kifo chake?

CCM ni chama kilichojaa watu wenye inferiority complex isipokuwa Katibu mkuu Dr Bashiru Ally, huyu ni mtu wa aina yake, aliyezungukwa na na vipofu wa akili.

Na ndo maana hata wanachama wa CCM si watu wa kawaida, mnaanzaje kutafuta kiki kwa Marehemu? ili watu waone kuwa CCM ni chama kizuri sana?

Mnakoelekea mtasema hata Trump ni mwana CCM.
Wewe ndio ulikua hujui yeye ni chama gani ,ila ilikua wazi yeye ni ccm kitambo sana ,na mafanikio yake yametokana na serikali ya ccm,kama hutaki acha
 
wewe ni mu
Wewe ni muongo,tena muongo kwelikweli ,muongo wa kiwango cha lami.Mengi alipotuhumiwa kuwa siyo mwana CCM,alitoka na kadi yake toka enzi za TANU na akarushwa katka taarifa ya habari ITV saa mbili usiku ,kama alivyofanya siku anakama madai ya yeye kuwa na kale kagonwa cha nyumbani.Au unataka kusema mzee alikuwa mnafiki?
Alitoka na kadi ya CCM tangu enzi za Tanu!
 
MIMI ni mwanaCCM ninaetamani mno kutokee pigo moja takatifu la kuua ndege kumi kwa jiwe moja tu pigo la pale lile genge lote la ufipa lililopata mhemko na joto la uchaguzi na kuingia barabarani bila utaratibu na kusababisha Akwilina akauwawa bila makosa genge lile lote fasta lifungwe jela Segerea leo hii ili mtaani kutulie bariiidi bila kelele kelele, yule binti asie na hatia ananiuma kweli kama mwanangu wa kumzaa! si unaona hapa nimesema mwenyewe itikadi yangu ndo inatakiwa hivi!

ila naungana nawe mtoa mada kukemea tabia za kumsemea mtu kitu chochote ambacho yeye mwenyewe hakukisema! ni moja ya alama za watu maskini wa akili walio nyuma katika human civilization kusikia watu wakisemeana kwa kila kitu, baba akimsemea mkewe au watoto, ambayo mara nyingi ni tabia duni za kunyamazisha sauti za wengine zisisikike! mara nyingi kwenye mkutano wa hadhara kijijini utasikia mtu mzima bila kutumia akili akipayuka "tunakufa njaa" Mkuu! kisaikolojia sio sahihi kusema "tunakufa njaa", sahihi ni kusema mimi Mary "nakufa njaa" mkuu nisaidie, sababu matumbo ya wengine huyajui yana nini ndani yake kama ni uji, ugali dona au Azam Sembe, maharage, viazi, maboga, mihogo au magimbi etc!

kama yeye mwenyewe hakusema na hakutaka ajulikane alikuwa na maana yake ni vizuri aheshimiwe, we can not prove alikuwa mwanachama wetu!
 
Wewe ndio ulikua hujui yeye ni chama gani ,ila ilikua wazi yeye ni ccm kitambo sana ,na mafanikio yake yametokana na serikali ya ccm,kama hutaki acha
Kwa hiyo unatuambia kuwa ni ccm ndio wamemuua ili kujikusanyia sifa?
 
Hayati Reginald Mengi ktk uhai wake hakuwahi kujionyesha hadharani kuwa yeye alikuwa ni mwanachama wa chama gani cha siasa.

Bali alijikita ktk kusaidia watu wenye shida mbali mbali za kimaisha wakiwemo walemavu, yatima na wajane.

Hiyo ndo ilikuwa ibaada ya hayati Reginald Mengi, ibaada njema kuliko zote ni kusaidia yatima, wajane na maskini.

Hakupenda kujihusisha na siasa kwa namna yoyote ile, na wala jamii haikujua Kama ni mwanachama wa chama gani cha siasa,na yeye hakupenda kujulikana kabisa.

Mara baada ya kutwaliwa na Mungu wakaibuka CCM na kuanza kutoa kiki kwamba alikuwa ni mwanachama wa CCM, huku ni kumdhalilisha Marehemu, Kama yeye hakupenda kujionyesha kwa nini nyie mwonyeshe uanachama wake baada ya kifo chake?

CCM ni chama kilichojaa watu wenye inferiority complex isipokuwa Katibu mkuu Dr Bashiru Ally, huyu ni mtu wa aina yake, aliyezungukwa na na vipofu wa akili.

Na ndo maana hata wanachama wa CCM si watu wa kawaida, mnaanzaje kutafuta kiki kwa Marehemu? ili watu waone kuwa CCM ni chama kizuri sana?

Mnakoelekea mtasema hata Trump ni mwana CCM.
Waliwahi mzushia kuwa si mwanachama akaitisha press akonyesha kadi yake ya mwaka 1977, ccm ni watu wa ajabu sana
 
yaani uanachama wake ulianzia TANU na hata ilipozaliwa CCM akawa mwanachama wa CCM. Hayo aliyathibitisha mwenyewe kwa kadi zake ndani ya kifuatacho ITV,labda kama video na taarifa ya habari na ITV vilieditiwa.
 
Wewe ndio ulikua hujui yeye ni chama gani ,ila ilikua wazi yeye ni ccm kitambo sana ,na mafanikio yake yametokana na serikali ya ccm,kama hutaki acha
Mafanikio ya Marehemu Mengi ni juhudi zake binafsi wapi Serikali ya CCM ilimjengea kiwanda? soma kitabu chake jinsi alivyopingwa kujenga kiwanda cha bonite.
 
Wewe hukusoma andiko, imeandikwa " Acha wafu wakazike wafu wao" ccm kama wanagombea maiti waaacheni maana walioko hai wanatafakari juu ya makinikia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom