‘CCM ilikufa Nyerere alipong’atuka’ , Vincent Nyerere (CHADEMA)

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,573
MBUNGE wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA), amesema hakupoteza muda kufuatilia mkutano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwani chama hicho kilishakufa baada ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kung’atuka.

Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Nyerere alisema CCM kwa sasa ni kikundi, kwani wao kwa wao wamebaki na siasa za kinafiki ikiwamo kuingia madarakani kwa kutumia fedha.
Alisema rushwa iliyokithiri katika chaguzi za chama, siasa chafu na kutotimiza ahadi walizotoa kwa wananchi kumeifanya CCM kupoteza hadhi ya awali iliyokuwa nayo enzi za Mwalimu Nyerere.
Aidha, aliiponda hotuba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, na kusema kuwa wakulima wanataka vitendea kazi na si porojo zitolewazo kuhusiana na suala zima la kilimo.
“Sioni Waziri Mkuu alichoongea kwani wakulima wanataka vitendo ambavyo ni vitendea kazi, wewe unamwambia mkulima kwa sasa tuweke mkazo katika suala la kilimo wakati humpi vifaa, ili atimize lile linalotakiwa, inasaidia nini?” alihoji.
Nyerere alisema kuwa mkakati wa Kilimo Kwanza hauwezi kufanikiwa bila serikali kujipanga upya na kuwawezesha wakulima kuwa na vitendea kazi na elimu ya kutosha kufahamu suala zima la kilimo ili kiwe biashara kwao.
Akizungumzia suala la maendeleo katika jimbo lake, mbunge huyo alisema kuwa japo wanapokea fedha ndogo za maendeleo amejitahidi kuhakikisha anashirikiana na wananchi waliomchagua kuipatia maendeleo Musoma.
 
MBUNGE wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA), amesema hakupoteza muda kufuatilia mkutano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwani chama hicho kilishakufa baada ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kungatuka.

Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Nyerere alisema CCM kwa sasa ni kikundi, kwani wao kwa wao wamebaki na siasa za kinafiki ikiwamo kuingia madarakani kwa kutumia fedha.
Alisema rushwa iliyokithiri katika chaguzi za chama, siasa chafu na kutotimiza ahadi walizotoa kwa wananchi kumeifanya CCM kupoteza hadhi ya awali iliyokuwa nayo enzi za Mwalimu Nyerere.
Aidha, aliiponda hotuba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, na kusema kuwa wakulima wanataka vitendea kazi na si porojo zitolewazo kuhusiana na suala zima la kilimo.
Sioni Waziri Mkuu alichoongea kwani wakulima wanataka vitendo ambavyo ni vitendea kazi, wewe unamwambia mkulima kwa sasa tuweke mkazo katika suala la kilimo wakati humpi vifaa, ili atimize lile linalotakiwa, inasaidia nini? alihoji.
Nyerere alisema kuwa mkakati wa Kilimo Kwanza hauwezi kufanikiwa bila serikali kujipanga upya na kuwawezesha wakulima kuwa na vitendea kazi na elimu ya kutosha kufahamu suala zima la kilimo ili kiwe biashara kwao.
Akizungumzia suala la maendeleo katika jimbo lake, mbunge huyo alisema kuwa japo wanapokea fedha ndogo za maendeleo amejitahidi kuhakikisha anashirikiana na wananchi waliomchagua kuipatia maendeleo Musoma.

Ni haki yake ya kikatiba uhuru wa kujieleza.
 
Tunapoenda kuandika Historia mpya 2015 ama Kabla ya hapo lazima tujikumbushe Historia fupi ya Mfu> CCM< ili mfu huyu asibaki kwenye makumbusho yetu ya historia ya vyama vya siasa bali mfu huyu aingie kwenye kumbukumbu ya vyama mufilisi wa mali za UMMA ( kupitia makada wake rejea majina Mwembe Yanga Temeke)

Wanajf: Tunajua kuwa Chama kinaweza kuishi iwapo tu kitakuwa kinakua na Kitakufa iwapo kitakosa Uvumilivu wa mawazo. Chama ambacho kuwepo kwake kunategemea wanachama wake kuzaliana kwa ajili ya kuongeza tu kura; huku mtoto akirithi nafasi ya baba yake; hicho si chama cha siasa." CCM inakufa kwakuwa haitaki mawazo mbadala, imewafanya watanzania kuwa waoga,waongo, Taifa limekuwa na Hofu mpaka inatia shaka katika uelewa wa mwananchi mmoja mmoja, CCM kimekuwa chama cha watoto wa viongozi waliyowahi kuongoza chama hicho na serikali.

CCM Inaona inahati miliki ya Taifa hili, Ukiwa upinzani unaonekana kama umefanya kosa la jinai kuwa upinzani, ni maswali yanayotia shaka kwa ustawi wa demokrasia tunayoimba. Tujikumbushe utawala wa Ufaransa ulipoa anguka baada ya viongozi wa juu kuingilia vyombo vya haki kama, mahakama nk. Taifa la Ufaransa lilijikuta kwenye wakati mgumu pale ambapo wananchi wake walipochoka na ukiukwaji wa haki zao kwenye vyombo vilivyopewa dhamana kama vile Mahakama Nk. Hapa kwetu kwasasa tumeona wale wasiyonacho wakienda kudai haki zao hawazipata, tumeona jeshi la polisi linavyotumiwa na chama cha CCM kufanya siasa na kudidimiza siasa za upinzani( Rejea kauli ya mwenyekiti wa Taifa wa ccm Mhe. jakaya Kikwete pale Dodoma) Matukio mengi ya mauaji ya kisiasa yametokea kwa mfano, Arusha walipokuwa wanadai haki yao juu ya meya feki, Igunga kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge, Iringa Mwandishi wa habari alipokuwa anafanya kazi yake ya uandishi, Arumeru Mahariki, Morogoro na kugineko kwingi.... Hii yote ni dalili ya Mtawala kuyumba na Kutaka kutumia nguvu kubwa kuendelea kuwepo kitu ambacho hakiwezekani wala haitakaa itokee ccm lazima ikubali kifo hiki.

Mwalimu Nyerere alikuwa na mapungufu yake ila alilipenda Taifa na atabaki kuwa mfano kwa Wanasiasa wote wajao isipokuwa wale waliyopo ndani ya ccm wanaopingana na uandilifu na kutaka kujilimbikizia mali kwani kipindi hicho CCM masalia nayo itakuwa Haipo kabisa. Watu wengi wenye kasoro wamejiingiza na kukichafua chama hiki (CCM) Sasa kimekuwa kama kokoro ambalo wakati mwingine hubeba viumbe visivyohitajika, Tuna watu wa ajabu ambao hawafanani na ccm> hiyo ni kauli ya mwanzilishi wa chama hicho Hayati Nyerere< Nashangaa kuona kunawatu wanajiita wanaccm wakati muanzilishi wa chama alikwisha kikana chama hicho kwa rushwa iliyokithiri Mtu kama Vuvuzela Nepi huyu ni mpiga domu iliaweze kula na kuishi ila hana mapenzi mema na taifa hili.

CCM wanapaswa waelewe kuwa Dunia imebadiliks ns Taifa linahitaji mabadiliko kuliko viraka wanavyokimbilia, Tunahitaji Chadema kushika nchi kwasasa kwani ndiyo chama pekee ambacho umma umeonyehsa tumaini la maisha yao lazima tukubaliane na ukweli huu... na ccm ikae ikijua kuwa, Watu wenye siasa za misimamo mikali kuhusu mambo mbalimbali, wapo kila mahali duniani, na kushamiri kwao kunachochewa na kiu yao kubwa ya damu ya karne kadhaa zilizopita. Tanzania kunawatu walipoteza uhai wao kwaajili ya kulipigania Taifa hili( Tanganyika) watu walinyongwa waliteswa waliuwawa walidhalilishwa kwaajili ya Taifa hili. Wananchi kwasasa wanataka Uhuru wa Maendeleo ni lazima ccm ikubali kifo hiki kwa hiyari 2015 ama kabla ya hapo vyote vinawezekana...

Uongozi si kulazimisha wananchi cha kufanya na wasipofanya unatumia polisi au jeshi dhidi yao. vyovyote vile; kutumia mabavu dhidi ya wananchi wenye njaa wanalalamikia kuongezeka kwa umasikini ni tusi kwa jamii yoyote ya Kileo na hii ni kupalia kaa na moto ambalo hujui litaunguza nini( watu wanataka mabadiliko siyo viraka vya wizara)

Babu yangu mzaa Mama Mzee Zuberi Mfinanga ambaye alikuwa Mlao kipindi cha Tanu wilayani Mwanga aliwahi kuniambia, Ukitaka ufaidi ukweli chagua jambo moja la utetezi wa haki ila uwe mchapakazi kundi hili ni kundi la watu wa chache sana kulinganisha na liliekundi la wapiga kelele ambao wanagemea kundi la wapenda sifa..... Vijana ama wototo wavigogo waliyopo ccm ni wapenda sifa ni wapiga kelele ili wapate kuishi... Ushindani wao hauwzi kulisaidia Taifa zaidi ya kulididimiza kwa kutumia raslimali za wanyonge kufanya mambo ya kuwapendeza wao kifo cha ccm ni lazima siyo ombi. namnukuu mwalimu nyerere" VIJINCHI vidogo duniani ni kama vile mwanamke mzuri aliyevaa nguo fupi huvutia waovu na walio na roho za shetani" ccm siyo chama cha siasa tena ni kikundi cha watu chenye uroho na raslimali za umma kwaajili ya kukinufaisha kikundi hicho.

Ona hivi karibuni wameanza kuwalazimisha watumishi wa umma kuripoti kwenye vikao vyao wakasahau kuwa sasa si wakati wa chama kimoja kila mtumishi wa umma anachama chake na wengine hawana( huu ni uwendawazimu kuingilia mamlaka isyokuhusu ccm imejivua nguo kwakuweka viongozi wasiyokuwa na uwezo wa kupima mambo na nyakati zilizomo wanaendesha siasa kwakukariri)

CCM ijiandae kwa kifo cha kufutika kwenye medani ya siasa nchini na ikubali kweli kwa hiyari.... tuishie hapa...MSIOGOPE TUTASHINDA, WE HAVE THE POWER (M4C)
 
Tunapoenda kuandika Historia mpya 2015 ama Kabla ya hapo lazima tujikumbushe Historia fupi ya Mfu> CCM< ili mfu huyu asibaki kwenye makumbusho yetu ya historia ya vyama vya siasa bali mfu huyu aingie kwenye kumbukumbu ya vyama mufilisi wa mali za UMMA ( kupitia makada wake rejea majina Mwembe Yanga Temeke)

Wanajf: Tunajua kuwa Chama kinaweza kuishi iwapo tu kitakuwa kinakua na Kitakufa iwapo kitakosa Uvumilivu wa mawazo. Chama ambacho kuwepo kwake kunategemea wanachama wake kuzaliana kwa ajili ya kuongeza tu kura; huku mtoto akirithi nafasi ya baba yake; hicho si chama cha siasa." CCM inakufa kwakuwa haitaki mawazo mbadala, imewafanya watanzania kuwa waoga,waongo, Taifa limekuwa na Hofu mpaka inatia shaka katika uelewa wa mwananchi mmoja mmoja, CCM kimekuwa chama cha watoto wa viongozi waliyowahi kuongoza chama hicho na serikali.

CCM Inaona inahati miliki ya Taifa hili, Ukiwa upinzani unaonekana kama umefanya kosa la jinai kuwa upinzani, ni maswali yanayotia shaka kwa ustawi wa demokrasia tunayoimba. Tujikumbushe utawala wa Ufaransa ulipoa anguka baada ya viongozi wa juu kuingilia vyombo vya haki kama, mahakama nk. Taifa la Ufaransa lilijikuta kwenye wakati mgumu pale ambapo wananchi wake walipochoka na ukiukwaji wa haki zao kwenye vyombo vilivyopewa dhamana kama vile Mahakama Nk. Hapa kwetu kwasasa tumeona wale wasiyonacho wakienda kudai haki zao hawazipata, tumeona jeshi la polisi linavyotumiwa na chama cha CCM kufanya siasa na kudidimiza siasa za upinzani( Rejea kauli ya mwenyekiti wa Taifa wa ccm Mhe. jakaya Kikwete pale Dodoma) Matukio mengi ya mauaji ya kisiasa yametokea kwa mfano, Arusha walipokuwa wanadai haki yao juu ya meya feki, Igunga kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge, Iringa Mwandishi wa habari alipokuwa anafanya kazi yake ya uandishi, Arumeru Mahariki, Morogoro na kugineko kwingi.... Hii yote ni dalili ya Mtawala kuyumba na Kutaka kutumia nguvu kubwa kuendelea kuwepo kitu ambacho hakiwezekani wala haitakaa itokee ccm lazima ikubali kifo hiki.

Mwalimu Nyerere alikuwa na mapungufu yake ila alilipenda Taifa na atabaki kuwa mfano kwa Wanasiasa wote wajao isipokuwa wale waliyopo ndani ya ccm wanaopingana na uandilifu na kutaka kujilimbikizia mali kwani kipindi hicho CCM masalia nayo itakuwa Haipo kabisa. Watu wengi wenye kasoro wamejiingiza na kukichafua chama hiki (CCM) Sasa kimekuwa kama kokoro ambalo wakati mwingine hubeba viumbe visivyohitajika, Tuna watu wa ajabu ambao hawafanani na ccm> hiyo ni kauli ya mwanzilishi wa chama hicho Hayati Nyerere< Nashangaa kuona kunawatu wanajiita wanaccm wakati muanzilishi wa chama alikwisha kikana chama hicho kwa rushwa iliyokithiri Mtu kama Vuvuzela Nepi huyu ni mpiga domu iliaweze kula na kuishi ila hana mapenzi mema na taifa hili.

CCM wanapaswa waelewe kuwa Dunia imebadiliks ns Taifa linahitaji mabadiliko kuliko viraka wanavyokimbilia, Tunahitaji Chadema kushika nchi kwasasa kwani ndiyo chama pekee ambacho umma umeonyehsa tumaini la maisha yao lazima tukubaliane na ukweli huu... na ccm ikae ikijua kuwa, Watu wenye siasa za misimamo mikali kuhusu mambo mbalimbali, wapo kila mahali duniani, na kushamiri kwao kunachochewa na kiu yao kubwa ya damu ya karne kadhaa zilizopita. Tanzania kunawatu walipoteza uhai wao kwaajili ya kulipigania Taifa hili( Tanganyika) watu walinyongwa waliteswa waliuwawa walidhalilishwa kwaajili ya Taifa hili. Wananchi kwasasa wanataka Uhuru wa Maendeleo ni lazima ccm ikubali kifo hiki kwa hiyari 2015 ama kabla ya hapo vyote vinawezekana...

Uongozi si kulazimisha wananchi cha kufanya na wasipofanya unatumia polisi au jeshi dhidi yao. vyovyote vile; kutumia mabavu dhidi ya wananchi wenye njaa wanalalamikia kuongezeka kwa umasikini ni tusi kwa jamii yoyote ya Kileo na hii ni kupalia kaa na moto ambalo hujui litaunguza nini( watu wanataka mabadiliko siyo viraka vya wizara)

Babu yangu mzaa Mama Mzee Zuberi Mfinanga ambaye alikuwa Mlao kipindi cha Tanu wilayani Mwanga aliwahi kuniambia, Ukitaka ufaidi ukweli chagua jambo moja la utetezi wa haki ila uwe mchapakazi kundi hili ni kundi la watu wa chache sana kulinganisha na liliekundi la wapiga kelele ambao wanagemea kundi la wapenda sifa..... Vijana ama wototo wavigogo waliyopo ccm ni wapenda sifa ni wapiga kelele ili wapate kuishi... Ushindani wao hauwzi kulisaidia Taifa zaidi ya kulididimiza kwa kutumia raslimali za wanyonge kufanya mambo ya kuwapendeza wao kifo cha ccm ni lazima siyo ombi. namnukuu mwalimu nyerere" VIJINCHI vidogo duniani ni kama vile mwanamke mzuri aliyevaa nguo fupi huvutia waovu na walio na roho za shetani" ccm siyo chama cha siasa tena ni kikundi cha watu chenye uroho na raslimali za umma kwaajili ya kukinufaisha kikundi hicho.

Ona hivi karibuni wameanza kuwalazimisha watumishi wa umma kuripoti kwenye vikao vyao wakasahau kuwa sasa si wakati wa chama kimoja kila mtumishi wa umma anachama chake na wengine hawana( huu ni uwendawazimu kuingilia mamlaka isyokuhusu ccm imejivua nguo kwakuweka viongozi wasiyokuwa na uwezo wa kupima mambo na nyakati zilizomo wanaendesha siasa kwakukariri)

CCM ijiandae kwa kifo cha kufutika kwenye medani ya siasa nchini na ikubali kweli kwa hiyari.... tuishie hapa...MSIOGOPE TUTASHINDA, WE HAVE THE POWER (M4C)

Mkuu umenena ya kuneneka, akinyanyuka Mwalimu huko alipo atawahukumu wengi waliyobadili muelekeo wa chama hiki na kukiweka mikononi mwa waroho na walafi aliyokuwa akiwapinga wazi wazi bila kujali umaarufu wao. ila kwasasa wameamua kubadilishana vijiti, sisi watanzania tuamue hatma ya taifa letu.
 
Back
Top Bottom