CCM Ilala kuandaa makada wake kuanzia shule za awali

Idimi

JF-Expert Member
Mar 18, 2007
14,965
10,460
CCM Ilala kuandaa makada wake kuanzia shule za awali
2007-10-29 18:26:54
Na Mariam Mkumbaru, Ilala


Katika kujihakikishia kuwa hapo baadaye kinakuwa na wanachama imara zaidi na waliopikika kuwa makada wa kweli, Chama cha Mapinduzi, CCM wilayani Ilala kimeanzisha utaratibu wa kutoa mafunzo maalum kwa watoto wa shule ya awali kuhusiana na chama chake.

Akizungumza katika mkutano na viongozi wa chama hicho na wanachama wengine wa chama hicho katika Kata ya Kitunda, Mwenyekiti wa CCM wilayani humo Bw. Suleiman Kalanje, amesema watoto wakiandaliwa kuwa wanachama wa chama hicho tangu katika ngazi ya awali, baadaye itakuwa rahisi kuwa na makada wanaokipenda kweli chama hicho tofauti na sasa ambapo baadhi hujiegemeza katika chama chao kwa nia ya kutimiza malengo yao mbalimbali.

``Tuimarishe Jumuiya zetu kwa kujenga ofisi imara za matawi na kuanzisha shule za awali kwa ajili ya kuandaa wanachama wa kweli kwa siku za baadaye ambapo wakati huo sisi tutakuwa wazee ama hatupo duniani,`` akasema Bw. Kalanje.

Aidha, Bw. Kalanje akatoa wito kwa viongozi mbalimbali wa chama hicho wilayani Ilala kujiimarisha kwenye matawi yao na hatimaye kuwezesha chama hicho kuendelea kufanya kazi katika mazingira ambayo yatasaidia kuleta maendeleo ya chama hicho.

Aidha, akasema muda wa kuwekeana visasi kutokana na matokeo ya uchaguzi ndani ya chama hicho umekwisha na iliyobaki na kuendeleza umoja na mshikamano wa kuimarisha chama chao.

SOURCE: Alasiri

Nakumbuka kulikuwa na programu za namna hii tukiwa shule za msingi miaka kibao iliyopita, tukijulikana kama chipukizi. Sasa kama inaanzia chekechekea basi makada watakuwa kiboko!
 
Mtupori,

hii itakuwa kali kwelikweli, natumaini kuwa upinzani nao wataruhusiwa kwenda chekechea (oh pliz tell me it's not true) wakaandae wanachama!
 
Mtupori,

hii itakuwa kali kwelikweli, natumaini kuwa upinzani nao wataruhusiwa kwenda chekechea (oh pliz tell me it's not true) wakaandae wanachama!

Huenda nao wapinzani wakafanya hivyo, ingawa sina uhakika ni mpinzani gani mwenye mawazo ya namna hii. Lakini makada wa zamani wa sisiemu toka chipukizi enzi za shule za msingi walikuwa bomba sana, walipikwa wakaelewa sera, tofauti na leo ambapo pesa mbele, chama nyuma.
 
Je ni ruhusa kufanya shughuli zozote za kisiasa katika taasisi ya elimu ambazo ziko chini ya muongozo wa wizara ya elimu?
 
Huyo kiongozi ni mzushi,hivi haelewi kama kuna vyuo vya siasa vya CCM tanzania nzima,kwenda kuwasomesha watoto kasumba za CCM ni kuwaharibia maisha yao kielimu na kisaikolojia,ni bora angelisema wanatoa scholarship kwa wanaomaliza shule kwenda kusomea UCCM kwenye vyuo vyao,unajua kuna watu wengine wanaona CCM kama ndio dini yao,sasa hapo wanatafuta njia za kuwabatiza UCCM hao vichanga.
 
Huyo kiongozi ni mzushi,hivi haelewi kama kuna vyuo vya siasa vya CCM tanzania nzima,kwenda kuwasomesha watoto kasumba za CCM ni kuwaharibia maisha yao kielimu na kisaikolojia,ni bora angelisema wanatoa scholarship kwa wanaomaliza shule kwenda kusomea UCCM kwenye vyuo vyao,unajua kuna watu wengine wanaona CCM kama ndio dini yao,sasa hapo wanatafuta njia za kuwabatiza UCCM hao vichanga.

..hapa mwiba at least umepata uhai kidogo maana ilikuwa sio muda mrefu JF wangekuzimia hiyo life support yako
 
Huyo kiongozi ni mzushi,hivi haelewi kama kuna vyuo vya siasa vya CCM tanzania nzima,kwenda kuwasomesha watoto kasumba za CCM ni kuwaharibia maisha yao kielimu na kisaikolojia,ni bora angelisema wanatoa scholarship kwa wanaomaliza shule kwenda kusomea UCCM kwenye vyuo vyao,unajua kuna watu wengine wanaona CCM kama ndio dini yao,sasa hapo wanatafuta njia za kuwabatiza UCCM hao vichanga.

acha unafiki,

endelea na kampeni yako ya kusema kuwa report ya wizi wa BOT ni longolongo
 
Je ni ruhusa kufanya shughuli zozote za kisiasa katika taasisi ya elimu ambazo ziko chini ya muongozo wa wizara ya elimu?


Sheria za nchi haziruhusu kitendo hiki. Lakini kwa kuwa sirikali iko chini ya sisiemu wanafanya wanavyotaka. Nakumbuka nikiwa mkoani Iringa mwaka 1998, waziri wa elimu enzi hizo Juma A Kapuya alivalishwa skafu za sisi M wakati akizindua jengo la nyumba ya mwalimu wa sekondari. Nikabaki nashangaa tu. Sherehe zilikuwa za kisirikali, sasa iweje waziri wa wananchi wote anavalishwa skafu za chama chake?
 
Back
Top Bottom