Elections 2010 CCM ifungue kesi ya Kikatiba dhidi ya CHADEMA kuwalazimisha kutambua matokeo!

nikaona Dr Mahanga anasema DR Slaa ni Dikiteta namba 1 na Mpendazoe Namba 2 kwa kukaataa matokeo ya segerea............. mliofuatilia matokeo ya segerea nani dikiteta?
 
Kwa mtazamo wangu naona mgogoro uliopo hapa ni kati ya CHADEMA na NEC sasa,CCM wameingia vipi katika mgogoro huu
 
Sasa hapo amechangia nini?
Ikiwa ameona haijaenda shule basi na alete yake kama hawezi kaa kimya kuliko kusema haijaenda shule.

mkuu unasumbuka na Taso? Browse nyuma uone michango hewa anayochangia. Yeye ni kuchukua post za watu na kuongezea upuuzi kidogo! Wala usisumbuke nae,hachangii anakebei tu!
 
Naomba nieleweke kwa yafuatayo:
1.CHADEMA KUTOMTAMBUA RAIS KIKWETE
Kwa hili naona halijaeleweka sawia,kwanza hoja ya msingi ya CHADEMA siyo kutomtambua rais
Bali ni kutokubali matokeo yaliyomuweka rais huyo madarakani.Ikumbukwe kuwa hoja hii ililetwa siku ya tatu ya kutangaza matokeo ambapo mgombea urais Kupitia CHADEMA mh.Slaa aliitaka tume kusitisha utangazaji wa matokeo hayo,kama kweli NEC ingekuwa tume ya haki kwa vyama vyote ingekubali kupitia kwa makini hoja ya mh.Slaa Kabla ya kumtangaza mshindi wa urais.Hapo ndipo ugomvi wa kikatiba unapoibuka.Kwa katiba ya sasa Mshindi wa urais hawezi kutenguliwa baada ya kuapishwa.Swali ni je kwanini hoja ya Slaa ilipuuzwa ilhali vielelezo muhimu alikuwa navyo kabla?

2.KUTOKA NJE YA BUNGE
Hili vyombo vingi vya habari vimeandika kuwa CHADEMA imemsusa rais kwa tafsiri ya kuwa haimtambui.Mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA ambaye ndiye kiongozi mkuu wa upinzani mh.Freeman Mbowe amelitolea maelezo kuwa ni shinikizo la kuvunja tume ya sasa ya uchaguzi na kuundwa kwa tume mpya ambayo itakuwa inajiendesha kwa uhuru na kwa haki kwa chaguzi zijazo na katiba mpya,tume ya sasa chini ya Lewis Makame iliundwa kwa parliamentary act ya mwaka 1971 ambayo inafuata mfumo wa chama kimoja cha siasa ndo maana tumeyaona yaliyotokea kwenye uchaguzi wa oct 31

Najaribu ku think critically kwanini vyombo vya habari vime report kwajinsi hiyo hata baada ya maelezo kutolewa na CHADEMA mara kadhaa? My interpretation is kama CCM ina influence na vyombo vingi vya habari; Je then sikwamba ni rahisi kwa CCM kudeal na CHADEMA kuukataa uraisi uliopo kuliko agenda ya Tume huru na Katiba mpya? Why kwasababu agenda ya pili public inakuwa united na ile ya kwanza division ni obviousy kwani ni rahisi kwa agenda ya kwanza CCM kuja na spining ya violence na kuleta division au hata kuwa na sababu tosha yakutumia nguvu kuzima hii hoja! Ama kweli siasa ya hitaji uwe smart kweli kweli ama sivyo inakula kwako!

CHADEMA men you have to be smart and play intelligently in this; kwepeni kabisa hiyo mitego yakupelekwa kwenye hilo la kwanza na mconcetrate na agenda ya tume huru na katiba mpya ili mpate public support ambayo nihitaji la wazalendo wote.
 
hii itakuwa si mada ya kuhoji kutangazwa "kwake" itakuwa ni kesi ya kuwalazimisha chadema wamtambue Rais na kutambua matokeo ya uchaguzi. Katiba haikatazi kesi ya kulazimisha watu kumtambua Rais.. Katiba inakataza kuhoji kuchaguliwa kwa yule aliyetangazwa kuwa Rais. Kwa hiyo CCM ina uwezo na haki ya kufungua kesi.. naomba tuwasihi walete kesi hiyo..

kesi hiyo itafunguliwa chini ya sheria gani. Naona unataka kumchokoza katibu mkuu wa ccm
 
si ndo hapo. watu wanaropoka ropoka tu kuhusu katiba. naona ndo limekuwa neno mvuto kwa watu!!

Haropoki, anajua sana anachoandika maana yake ili rais atambuliwe na upinzani lazima kuwe na kesi mahakamani na wadaawa katika kesi watakuwa chadema. Ili ccm washinde itabidi watoe ushahidi ( amabao hawana ) kama rais alishinda kweli na ili kesi utupiliwe mbali lazima CHADEMA watatoa ushahidi ( amabao wanao ) kuwa rais hakupata kura ambazo nec wanasema.

Katika kufanya hivyo CHADEMA watapata jukwaa la uhakuka la kuchambua udhalimu wote uliofanyika kufuatia uchaguzi ( wenzetu wanaita washing the linen in public).

Ndio maana naona kama Mwanakijiji anamchokoza katibu mkuu wa ccm
 
Haropoki, anajua sana anachoandika maana yake ili rais atambuliwe na upinzani lazima kuwe na kesi mahakamani na wadaawa katika kesi watakuwa chadema. Ili ccm washinde itabidi watoe ushahidi ( amabao hawana ) kama rais alishinda kweli na ili kesi utupiliwe mbali lazima CHADEMA watatoa ushahidi ( amabao wanao ) kuwa rais hakupata kura ambazo nec wanasema.

Katika kufanya hivyo CHADEMA watapata jukwaa la uhakuka la kuchambua udhalimu wote uliofanyika kufuatia uchaguzi ( wenzetu wanaita washing the linen in public).

Ndio maana naona kama Mwanakijiji anamchokoza katibu mkuu wa ccm

iyo yote naelewa...swali ni simple - hiyo kesi itafunguliwa chini ya kifungu gani cha katiba?
 
CCM wanaendesha mapambano haya kisiasa zaidi na labda kisaikolojia. Wanajua kabisa kwamba kwenda mahakamani ni out. Hivyo wanachofanya ni kuwahamasisha wa-TZ kisiasa waone kwamba CHADEMA hawana maana. Na hapo ndipo ulipo mtihani mkubwa sana kwa CHADEMA. Ingekuwa mahakamani bila shaka wangefaidi sana. Lakini mahasimu wao wanawajengea wananchi fikra kwamba hawa hawana adabu kwa rais kinyume na "utamaduni wetu", hawajali wananchi waliowachagua, wanatishia amani na utulivu, wana kiburi - hawataki ushirikiano na wapinzani wenzao, wadini, wakabila, wamegawanyika (interviews za Zitto & Shibuda TBC), n.k. Na kwa kujua wa-TZ wengi walivyo "wavivu wa kufikiri" CCM wanaweza kufanikiwa! Hapo tena ya nini kwenda mahakamani? CHADEMA wajiandae kuipangua offensive hiyo kama wanataka kubaki kama chama mbadala-wasipoteze muda kujijenga kisheria/kikatiba pekee.
 
hii itakuwa si mada ya kuhoji kutangazwa "kwake" itakuwa ni kesi ya kuwalazimisha chadema wamtambue Rais na kutambua matokeo ya uchaguzi. Katiba haikatazi kesi ya kulazimisha watu kumtambua Rais.. Katiba inakataza kuhoji kuchaguliwa kwa yule aliyetangazwa kuwa Rais. Kwa hiyo CCM ina uwezo na haki ya kufungua kesi.. naomba tuwasihi walete kesi hiyo..

Hii hoja kama una simu ya Peter Kisumo mpelekee, yeye anapenda kesi dhidi ya vyama vya upinzani
 
Kitu kikubwa ambacho wote kimetupita kushoto ni kuwa HAKUNA KIFUNGU CHOCHOTE CHA SHERIA AU KATIBA AMBACHO KESI ITA-BASE,kwani kesi zinafunguliwa kwa kufuata sheria kwa hiyo kesi hiyo anayoitaka mtoa mada itatupiliwa mbali kwa kuwa haina vifungu vya sheria wala katibba inavyovisupport...
 
Nilikuwa nafikiria namna nyingine ya kutatua mgogoro uliopo sasa hivi kati ya CCM na CHADEMA kuhusu suala la matokeo ya Urais. Nimefikiria kuna kesi mbili ambazo nikiwasikiliza CCM na wale wenye kulaani kitendo cha "kutoka nje" kilichofanywa na CHADEMA wanaweza kuja nazo.


1. Kesi ya Kikatiba ya kuwalazimisha CHADEMA kumtambua Rais Kikwete kwa vile waliamua kutoka wakati Rais ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu na Mkuu wa serikali ya JMT alipokuwa anazungumza. Kwa vile kitendo kile kimeelezewa na Kapt. Chiligati kuwa kilikuwa kinavunja Katiba basi mantiki inataka wale wanaotetea Katiba wachukue hatua za kuitetea Katiba hiyo kwa kufungua kesi ya Kikatiba dhidi ya CHADEMA.

2. Kesi ya pili nayo ni ya Kikatiba vile vile nayo iwe ni ya kulazimisha CHADEMA WATAMBUE matokeo ya Uchaguzi wa Rais kwani kutokutambua matokeo ya kura za Urais yanatuleta kwenye tatizo la kwanza hapo juu. Kwa vile CCM na wengine wanaamini kuwa kura zilizopigwa na kutangazwa zilikuwa ni halali na hakuna mashaka yoyote basi jawabu pekee ni kuwalazimisha CHADEMA KUKUBALI matokeo hayo. Katiba inazuia kuhoji kutangazwa kwa Rais lakini HAKUZUII kutetea kutangazwa huko mahakamani! Hivyo, CCM na wanasheria wake wafikirie namna ya kuthibitisha au kuutetea ushindi mahakamani. Hapa napendekeza wao CCM waitishe kura zote za Urais kutoka majimbo yote ili kuonesha kiasi cha kura alizoshinda. Watakapofanya hivyo watafunga kelele zote za Chadema na kuwaridhisha Watanzania kuwa hakuna kura zilizochakachuliwa. Hapa itakuwa ni goli kama la Maradona au lile goli la elfu moja la Pele.

Kwa ufupi naamini CCM wanaweza kutoa mfano wa utawala wa sheria kwa kwenda mahakamani kufungua kesi hizo za Kikatiba.

CCM haina time kwa sasa na upuuzi huo. Rais ni Jakaya Mrisho Kikwete naye anatokea CCM.
 
hakuna "mgogoro uliopo sasa hivi kati ya CCM na CHADEMA"

get your subject right

UKO TANZANIA HII AU WAPI??? HATA WALIOKO MAREKANI WANAJUA KWETU iko issue. Hivi yule Chiligati alieongea na kutishia kupeleka motion bungeni ni wa chama gani??? au ni wa Chama cha Dovutwa??? if so una haki ya kuongea upupu wako hapa JF.

Mwanakijiji hawa jamaa hawawezi fanya hivyo maana hawana haki ya kufanya hivyo hata kama mwanya wa kisheria na kikatiba upo.
 
hii itakuwa si mada ya kuhoji kutangazwa "kwake" itakuwa ni kesi ya kuwalazimisha chadema wamtambue Rais na kutambua matokeo ya uchaguzi. Katiba haikatazi kesi ya kulazimisha watu kumtambua Rais.. Katiba inakataza kuhoji kuchaguliwa kwa yule aliyetangazwa kuwa Rais. Kwa hiyo CCM ina uwezo na haki ya kufungua kesi.. naomba tuwasihi walete kesi hiyo..

Katiba ina kataza kuhoji matokeo ya Uraisi ambayo yametangazwa na NEC Lakini sina uhakika kama kifungu hicho kina ruhusu kuhoji namna NEC ilivyofikia kuyatangaza hayo matokeo kama anavyosema ndugu yangu Rutashubanyuma hapo juu. Kama hivyo ndivyo nahisi ni kama kitendawili cha Yai na Kuku kipi kilianza, maana kama unazuiwa kuhoji matokeo ya Urais vipi uruhusiwe kuhoji mchakato ulopelekea kuyapata hayo matokeo yalompatia Mr JK Urais??? Mi nafikiri njia muafaka ni CDM ambao wao wanaamini kuwa walishinda kwa mujibu wa returns zao walizopata kwa mawakala wao kama kweli ni AUTHENTIC basi kama walivyofanya kwenye Operation Sangara, basi waufikishe ukweli huu kwa wananchi na kuwaonyesha ushahidi kamili wa nani alifanya nini na kwa wakati gani. Wananchi wa leo si wa jana au juzi, wana uwezo mkubwa wa kuelewa mambo naamini kwa kuanzia na uchaguzi ujao wa serikali za mitaa in 2 yrs time watatoa hukumu inayostahili kwa wote waliodhulumu kura za wananchi na itakapofika 2015 itakuwa ni climax ya hukumu hiyo
 
Kwanza nakupengeza sana MMK kwa hoja yako. Ni hoja nzuri sana ambayo inatakiwa kuangaliwa vizuri. Kwa upande wa CHADEMA ni turufu kwani wataweza kujitetea na kueleza kwanini hawamtambui na pia CCM itabidi waonyeshe nikwa jinsi gani huyu RAIS WAO ameshinda kihalali.

Pili ikitokea CCM wakafanya hivyo mlango mwingine wa Demokrasia utakuwa umefunguliwa Tz. Na nadhani itapelekea MAHAKAMA ZETU sasa zitoe haki ya kweli siyo ujanja ujanja.
 
Katiba ina kataza kuhoji matokeo ya Uraisi ambayo yametangazwa na NEC Lakini sina uhakika kama kifungu hicho kina ruhusu kuhoji namna NEC ilivyofikia kuyatangaza hayo matokeo kama anavyosema ndugu yangu Rutashubanyuma hapo juu. Kama hivyo ndivyo nahisi ni kama kitendawili cha Yai na Kuku kipi kilianza, maana kama unazuiwa kuhoji matokeo ya Urais vipi uruhusiwe kuhoji mchakato ulopelekea kuyapata hayo matokeo yalompatia Mr JK Urais??? Mi nafikiri njia muafaka ni CDM ambao wao wanaamini kuwa walishinda kwa mujibu wa returns zao walizopata kwa mawakala wao kama kweli ni AUTHENTIC basi kama walivyofanya kwenye Operation Sangara, basi waufikishe ukweli huu kwa wananchi na kuwaonyesha ushahidi kamili wa nani alifanya nini na kwa wakati gani. Wananchi wa leo si wa jana au juzi, wana uwezo mkubwa wa kuelewa mambo naamini kwa kuanzia na uchaguzi ujao wa serikali za mitaa in 2 yrs time watatoa hukumu inayostahili kwa wote waliodhulumu kura za wananchi na itakapofika 2015 itakuwa ni climax ya hukumu hiyo

Unachosema ni kweli kwa upande fulani. Alichojaribu kuibua huyu MMK ni kuwa kama Cpt. Chiligati aliona kuna kifungu kilivunjwa waende mahamani kufungua kesi ya kikatiba kuwalazimisha CDM.

Pia kama umefuatilia Police wamezuia CDM kufanya mikutano yoyote ya hadhara mpaka hapo khali itakapo tulia. Hali gani mbaya wao ndiyo wanajua. Labda mpaka wamtambue JK.
 
Back
Top Bottom