CCM hoi wilaya ya Nyasa

chishango

JF-Expert Member
Feb 20, 2009
852
350
Kutokana na vuguvugu linaloendelea huko wilayani Nyasa imemlazimu Mbunge wa jimbo hilo ndg. John Komba kukimbia vikao vya bunge na kurudi jimbo wiki iliyopita. Hadi mchana huu wagombea 3 wa vitongoji wa CHADEMA katika kijiji cha Kihagara wamepita bila kupingwa katika kijiji na kitongoji alichozaliwa mbunge cha Lituhi CCM haikuwa na mgombea hali iliyomlazimu mbunge kwenda haraka kununua mtu wa kitongoji kingine ili ajaze fomu.

Ppingamizi limeshaandaliwakatika kijiji cha Ukuli kata ya Kingerikiti mgombea wa CHADEMA uenyekiti wa kijiji hana mpinzani yaani amepita bila kupingwa baada ya CCM kukosa mgombea katika kijiji cha Dar pori, CCM pia haina mgombea.

Nitaendelea kuwajuza maana hadi jioni ndio tutapata taswira ya jumla kwa sababu kuna baadhi ya kata bado taarifa zake hazijapokelewa.


UPDATE
Kitongoji cha Mkalole Kijiji cha Namgombo Kata ya Kilosa ccm wamekosa mgombea
 
Nyasa ipi pengine kunanyasa nyingine kule marangu ila siyo hii tuijuayo.
 
ccm sasa wanashirikiana na wasimamizi wa uchaguzi kutengeneza vituo feki vya kuandikisha wapiga kura. Huko Igoma mwanza vituo 9 vimebainika kutokuwapo kwenye orodha ya halmashauri.
 
Kutokana na vuguvugu linaloendelea huko wilayani Nyasa imemlazimu Mbunge wa jimbo hilo ndg. John Komba kukimbia vikao vya bunge na kurudi jimbo wiki iliyopita. Hadi mchana huu wagombea 3 wa vitongoji wa CHADEMA katika kijiji cha Kihagara wamepita bila kupingwa katika kijiji na kitongoji alichozaliwa mbunge cha Lituhi CCM haikuwa na mgombea hali iliyomlazimu mbunge kwenda haraka kununua mtu wa kitongoji kingine ili ajaze fomu.

Ppingamizi limeshaandaliwakatika kijiji cha Ukuli kata ya Kingerikiti mgombea wa CHADEMA uenyekiti wa kijiji hana mpinzani yaani amepita bila kupingwa baada ya CCM kukosa mgombea katika kijiji cha Dar pori, CCM pia haina mgombea.

Nitaendelea kuwajuza maana hadi jioni ndio tutapata taswira ya jumla kwa sababu kuna baadhi ya kata bado taarifa zake hazijapokelewa.

Ina leta raha. Noli wahi kusema kam Komba atathunutu kuchukua fomu nitatoa gari gangu bure kipindi chote cha kampeni kuwasaidia wapoinzani komba arudi porini akakae na wenzake. Hana adabu huyu muimba kwaya
 
Mwisho wa uongo ni aibu, mods akikisheni mnaondoa huu uongo uliodhahiri kabisa kwani katika wilaya tajwa hapo juu CCM imesimamisha viongozi wote katika ngazi zote na huo ni uzushi uliodhahiri kabisa!

Hivi vijana wa Bavicha mnadanganya kwa faida gani? Mnadanganya ili mpate nini? Mwisho wa huo uongo ni nini?

Ni bora kuandika ukweli ingawa unauma kuliko kuandika uzushi ambao unalaaniwa na Mungu hapa duniani na ahera pia!
 
Mwisho wa uongo ni aibu, mods akikisheni mnaondoa huu uongo uliodhahiri kabisa kwani katika wilaya tajwa hapo juu CCM imesimamisha viongozi wote katika ngazi zote na huo ni uzushi uliodhahiri kabisa!

Hivi vijana wa Bavicha mnadanganya kwa faida gani? Mnadanganya ili mpate nini? Mwisho wa huo uongo ni nini?

Ni bora kuandika ukweli ingawa unauma kuliko kuandika uzushi ambao unalaaniwa na Mungu hapa duniani na ahera pia!


Sasa kama unaona mleta mada ni mzushi tunaomba wewe utupe ukweli wa majina ya wanaogombea maeneo hayo tajwa.Nakama sio kweli inakuumiza nini kiasi ya kuomba msaada kwa mods?
 
Mwisho wa uongo ni aibu, mods akikisheni mnaondoa huu uongo uliodhahiri kabisa kwani katika wilaya tajwa hapo juu CCM imesimamisha viongozi wote katika ngazi zote na huo ni uzushi uliodhahiri kabisa!

Hivi vijana wa Bavicha mnadanganya kwa faida gani? Mnadanganya ili mpate nini? Mwisho wa huo uongo ni nini?

Ni bora kuandika ukweli ingawa unauma kuliko kuandika uzushi ambao unalaaniwa na Mungu hapa duniani na ahera pia!


Tupe unachokijua wewe sasa!
 
hongera mkuu kwa taarifa nzuri na zenye uhakika ambazo kimsingi sina shaka nazo 100 % kwani kijiji cha ukuli wamepakana na kijiji cha kingerikiti ambacho kwa miaka 5 mwenyekiti wake ni chadema bila shaka nao wameamua kuwaiga majirani zao kwa kumchagua mwenyekiti wa chadema.

Pia kuhusu kata ya kihagara huko nako sina wasiwasi na maelezo yako kwani diwani wa kata hiyo ni wa chadema na diwani huyo inaonekana amedhamiria kufanya kazi usiku na mchana ili kupata wenyeviti wa vijiji na vitongoji wa chadema ili kujitengenezea mazingira mazuri mwakani. Lakini kwenye kata hiyo hiyo kijiji cha songambele kitongoji cha yungu tangu uchaguzi wa mwaka ya 1999 ccm hawajawahi kuchukua kitongoji hicho , miaka hiyo yote mwenyekiti wa kitongiji wa chadema bwana kamoha nyirenda amekuwa akipita bila kupingwa kila mwaka wa uchaguzi ila safari ameamua kuacha kugombea mwenyekiti wa kitongoji na sasa anagombea mwenyekiti wa kijiji kwa tiketi ya chadema bila shaka atapita.

Kwa upande wa Lituhi maelezo yako yanaweza kuwa kweli kwa sababu pale nyumbani kwake lituhi hawampendi captain ndio maana walimchomea nyumba yake moto. hawampendi kwa sababu wananchi wengi wa Lituhi wanamlalamikia mbunge huyo kwa kuwajengea ukumbi wa mziki ambapo kila weekend wanafunzi huburudika hapo na wanadai hicho ndicho chanzo cha uasherati kwa watoto wao kwani siku ya jumatatu watoto hawaendi shule wanakuwa wamechoka na kucheza mziki siku ya jumapili. Walimu wa shule ya sekondari ya lituhi wamelalamika sana suala ukumbi huo kwamba unachangia kushuka kwa taaluma katika kata hiyo lakini mwisho wa siku wanaishia kuhamishwa. hivyo sina shaka na maelezo yako kuhusu Lituhi
 
Mwisho wa uongo ni aibu, mods akikisheni mnaondoa huu uongo uliodhahiri kabisa kwani katika wilaya tajwa hapo juu CCM imesimamisha viongozi wote katika ngazi zote na huo ni uzushi uliodhahiri kabisa!

Hivi vijana wa Bavicha mnadanganya kwa faida gani? Mnadanganya ili mpate nini? Mwisho wa huo uongo ni nini?

Ni bora kuandika ukweli ingawa unauma kuliko kuandika uzushi ambao unalaaniwa na Mungu hapa duniani na ahera pia!

Taarifa za hivi punde CCM imekosa mgombea Kitongoji cha Mkalole Kijiji cha Nangombo kata ya Kilosa
 
huyu mdudu tunaendelea kumumong'onyoa polepole mpaka 2015 itabaki kugawana mavazi tu no compromise
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom