Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,175
- 25,446
Sijui ndiyo sanaa za kisiasa au vipi.Kuna wakati hata werevu tunaachwa njia panda. CCM kama chama tawala, kupitia wasemaji wa chama au viongozi watokao humo, wamekuwa wakitoa kauli mbalimbali za 'kisanii' sana. CCM hujenga taswira ya kuwachukia Wazanzibari lakini kuupenda Muungano. Ajabu kabisa!
Kuanzia kwenye Bunge la Katiba, Wajumbe watokanao na CCM wamekuwa wakitoa matusi,kashfa,kejeli na kauli za kibaguzi dhidi ya Wazanzibari. Hali ilipozidi uwezo,UKAWA wakatoka nje ya Bunge lla Katiba. Chanzo kilikuwa hicho cha 'kuwachukia' Wazanzibari. Hata kwenye Bunge la Bajeti mambo kama hayo yamejitokeza.Rejea kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kauli ya leo ya Mbunge Ali Kessy wa Nkasi.
Ni CCM hao hao wanaoutaka mfumo wa Muungano uliopo ubaki.Wanajenga hoja kuwa ni mfumo huu uliopo tu ndio utaoulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Hapa wanadai kuupenda Muungano. Inawezekana mimi sielewi sanaa ya CCM. Lakini nahisi jambo.Kuna kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Hakuna mambo yaelewekayo katika jambo hili. Labda nieleweshwe na wajuzi wa jambo hili hasa watokao ndani ya CCM.
Kuanzia kwenye Bunge la Katiba, Wajumbe watokanao na CCM wamekuwa wakitoa matusi,kashfa,kejeli na kauli za kibaguzi dhidi ya Wazanzibari. Hali ilipozidi uwezo,UKAWA wakatoka nje ya Bunge lla Katiba. Chanzo kilikuwa hicho cha 'kuwachukia' Wazanzibari. Hata kwenye Bunge la Bajeti mambo kama hayo yamejitokeza.Rejea kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kauli ya leo ya Mbunge Ali Kessy wa Nkasi.
Ni CCM hao hao wanaoutaka mfumo wa Muungano uliopo ubaki.Wanajenga hoja kuwa ni mfumo huu uliopo tu ndio utaoulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Hapa wanadai kuupenda Muungano. Inawezekana mimi sielewi sanaa ya CCM. Lakini nahisi jambo.Kuna kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Hakuna mambo yaelewekayo katika jambo hili. Labda nieleweshwe na wajuzi wa jambo hili hasa watokao ndani ya CCM.