CCM hatuna hoja za kumjibu Tundu Lissu, tunakwamishwa na watendaji wa Serikali

Wanabodi,Kila binadamu ana mapungufu yake ambayo wewe mwenyewe huwezi kujiona bali wanaokuangalia ndio wenye majibu sahihi juu yako.

Watendaji wa serikali ndio wanaotuangusha chama cha mapinduzi sana,Hawa watendaji wengi hawana elimu ya siasa wao wanafikiria familia na kulinda mishahara yao tu.

Kosa la kwanza,Wakati wa hali tata na katikati ya mapambano,Wanaibuka na kukoleza kutajwa tajwa kwa Tundu Lisu na wananchi,Kukataza matangazo ya BBC,VOA na DW kulikofanywa na waziri Mwakyembe na TCRA kuna jenga chuki kwa wananchi kwa ccm bila sababu za msingi ,Inapelekea lissu kushangiliwa huko Kahama kwa kuwa anatembelea mapungufu ya watendaji kuwa wananchi hamtaona BBC wala DW au VOA.Kuwa kutoonekana BBC, DW na Voa ccm ndio wamefanya hilo na wananchi limewaingia na kushangilia

Kosa la pili,Television ya Taifa yaani TBC sijaelewa kwanini mtendaji wake bado yupo ofisi anatengeneza chuki kwa CCM kuwa wanaogopa hoja za upinzani na wanaficha maovu,Hili ni kosa kubwa sana kimkakati kwa chama ,Ni pyschology ya kawaida hata Nyumbani Baba anapojisifia yeye tu kuwa anawasaidia watoto,Watoto baadae wakigundua ukweli familia nyingi Mababa wanadharaulika sana,Yapasa awe na asilimia katika kuonyesha mambo sio kila siku upande wa ccm tu.Leo hii watu wanadharau television ya Taifa na kuita Tbc ccm, Kila kitu kwenye Tbc wananchi wanachukulia ni uwongo na propaganda, Kuna mambo yamefanyika kweli lakini kuonyesha upande mmoja watu wanasema ni picha za kuchorwa kweli?

Kosa la tatu, Matamko ya Jeshi la polisi hasa watendaji wa juu kwenye mambo ya siasa yanafanya watu kuamini chama cha CCM hakishindi kihalali maeneo mengine bali kwa kubebwa na polisi,Wakati kuna maeneo ccm inashinda kwa uhalali kabisa hata wapinzani wanakubali matokeo.

Ni rahisi sana kuzijibu hoja za Tundu Lissu kisomi majukwaani kama watendaji wa serikali wangetambua chama kinachotawala kinahitaji hoja zenye mashiko.

Hoja za Tundu Lissu sio nyingi sana ,Kama wakati ule hoja za Dkt Slaa zilikuwa zikijibiwa na Nape Nnauye kwa ustadi mkubwa na vijembe vya hapa na pale kwanini leo?

Mosi,Hoja ya uhuru wa habari na kuongea,Hapa TBC na ndugu Mwakyembe walipasa kuwa wajanja wanaonyesha sehemu za mikutano ya Tundu Lisu halafu wanapigilia nondo zao kwa kuonyesha taarifa za Magufuli kuziba mabonde,Bila hivyo watu wanatafuta habari za Tundu lisu kinguvu.

Pili,Hoja za Malalamiko za wafanyakazi , wafanyabiashara na wakulima hapa watendaji walipaswa kuonyesha kitu gani kimefanyika kisheria,Mapungufu walioyaona kwa miaka mitano,Na nini matarajio ,Bora kukili mapungufu na kuahidi kuboresha,Kutokuongelea hili Tundu Lisu anazidi kutembelea udhaifu huu.

Hoja ya upendeleo wa mkoa wa Geita hasa chato ni suala rahisi sana kulijibu ,lakini kitendo cha kuuliza chato ni wapi sio jibu ya hoja hii,Hapa watendaji walipaswa kueleza sababu za kwanini wameweka mbuga au uwanja chato na sababu zipo nyingi za kushawishi Raia wa Mwanza ,Mbeya au Dar es Salaam,Kujibu kirahisi kunazidi kumpa sifa Tundu Lisu.

Chama cha mapinduzi kisiwaonea haya hawa watendaji wa serikali wanaotafuta sifa huku wakiharibu sifa na upendo wa chama kwa wananchi.
Watendaji ndio wasimamizi wa hii miradi na utendaji wa serikali kila siku ndio wa kujibu hizi hoja sio kukimbilia kuzuia hoja na kuzidi kumpa umaarufu Tundu lisu mbele ya wananchi

Watendaji wa serikali huu ulikuwa ndio muda wa kwenda Tbc kufanya mdahalo na watu wa upinzani kwa kuelezea mmejenga shule, Hospital na mm jifunza kitu gani na kitu gani kimebaki kwa miaka mitano ijayo sio kuelezea mafanikio tu wakati kuna mambo dhahiri hayajakamilika kwenye shule au hospital

Mfano mzuri na ambao utadumu,Ni kitendo cha kuwaacha watu huru kumpokea Tundu Lissu airport ,Hakuna fujo wala ugomvi uliotokea watu walishangilia sana na kurudi makwao kulala ,ccm ilichukua sifa kubwa kwa hili kwa wananchi ,Mbinu kama hii ya hamsini kwa hamsini ndio ujanja wenyewe.

Muda huu ndio mtu kama Humprey polepole angeacha vitisho na majigambo bali angekuwa anaitisha mijadala na wanasiasa wa upinzani.

Muda huu ndio ilikuwa unamuita Nape Nnauye kwenye Mdahalo na Halima Mdee wanabishana kwa hoja.

Bila mdahalo wa hoja za pande mbili wananchi wanazidi kuaminishwa ugumu wa maisha umesababishwa na ccm wakati kiuhalisia watendaji ndio wameleta matatizo na chuki kwa wananchi

Wafuatao walipaswa kutenguliwa kwa muda ile kujenga imani na kujitenga nao na chama, ccm ieleze kuwa hawa ndio wamezima bbc, Voa na DW, Pia ieleze kuwa hawa ndio wanaeneza chuki kwa ccm, Yote wanayofanya ccm iwaambie wananchi kuwa ni hawa watendaji na sio chama kinakosea

Mkurugenzi wa Tbc
Mkurugenzi wa TCRA
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo au Msemaji wa serikali

Tukutane Octoba,
Nikupongeze kwa hoja zako zenye mizania na afya zenye kurejesha amani na imani ya wananchi.
 
Hata zisipojibiwa HAPATI KURA labda za humu kwenye mitandao ambazo hazifiki 100K.

Nyomi ya kumshangilia si hoja hata wachawi, wezi wakionekana mchana hujaza nyomi
 
Hizo hoja zote alitakiwa kuziuliza bungeni apewe majibu na serikali hakufanya hivyo

Hata siku moja hajawahi ukiza. Bungeni wakati alikuwa mbunge ndio maana wananchi tunamshangaa

Alijalia tu kuongelea MIGA MIGA badala ya kuuliza maswali yanayohusu wananchi! Anakumbuka shuka wakati kumekucha!!! Too late

Alikula mishahara na miposho ya bure hayo maswali angeuliza bungeni
Muombe Mungu akujalie akili angalau yakuweza kuchanganua Chua na mchele.
 
Mkuu nina mashaka na uwezo wako wa kufikiri mambo

Una uwezo mdogo sana wa kufikiri

Sio kila jambo wewe unageuza mipasho na ngonjera

Kama una miaka zaidi ya 18 na una mawazo mgando kama uliyoyaandika hakika kama Taifa kuna kitu kwenye mifumo yetu ya elimu haipo sawa

Inakuwaje mtu mzima na mashavu yako unatoa mipasho na ngonjera

Kama huna la kuandika nenda kunywa maji pumzika

You are certified idiot
Nimemkote kwa mwambia angalau amuombe Mungu aweze kuchanganua Chua na mchele.

Yaani ni mburura hata kutofautisha ya kilichoandikwa na anachoongea hajui.
 
Wanabodi,Kila binadamu ana mapungufu yake ambayo wewe mwenyewe huwezi kujiona bali wanaokuangalia ndio wenye majibu sahihi juu yako.

Watendaji wa serikali ndio wanaotuangusha chama cha mapinduzi sana,Hawa watendaji wengi hawana elimu ya siasa wao wanafikiria familia na kulinda mishahara yao tu.

Kosa la kwanza,Wakati wa hali tata na katikati ya mapambano,Wanaibuka na kukoleza kutajwa tajwa kwa Tundu Lisu na wananchi,Kukataza matangazo ya BBC,VOA na DW kulikofanywa na waziri Mwakyembe na TCRA kuna jenga chuki kwa wananchi kwa ccm bila sababu za msingi ,Inapelekea lissu kushangiliwa huko Kahama kwa kuwa anatembelea mapungufu ya watendaji kuwa wananchi hamtaona BBC wala DW au VOA.Kuwa kutoonekana BBC, DW na Voa ccm ndio wamefanya hilo na wananchi limewaingia na kushangilia

Kosa la pili,Television ya Taifa yaani TBC sijaelewa kwanini mtendaji wake bado yupo ofisi anatengeneza chuki kwa CCM kuwa wanaogopa hoja za upinzani na wanaficha maovu,Hili ni kosa kubwa sana kimkakati kwa chama ,Ni pyschology ya kawaida hata Nyumbani Baba anapojisifia yeye tu kuwa anawasaidia watoto,Watoto baadae wakigundua ukweli familia nyingi Mababa wanadharaulika sana,Yapasa awe na asilimia katika kuonyesha mambo sio kila siku upande wa ccm tu.Leo hii watu wanadharau television ya Taifa na kuita Tbc ccm, Kila kitu kwenye Tbc wananchi wanachukulia ni uwongo na propaganda, Kuna mambo yamefanyika kweli lakini kuonyesha upande mmoja watu wanasema ni picha za kuchorwa kweli?

Kosa la tatu, Matamko ya Jeshi la polisi hasa watendaji wa juu kwenye mambo ya siasa yanafanya watu kuamini chama cha CCM hakishindi kihalali maeneo mengine bali kwa kubebwa na polisi,Wakati kuna maeneo ccm inashinda kwa uhalali kabisa hata wapinzani wanakubali matokeo.

Ni rahisi sana kuzijibu hoja za Tundu Lissu kisomi majukwaani kama watendaji wa serikali wangetambua chama kinachotawala kinahitaji hoja zenye mashiko.

Hoja za Tundu Lissu sio nyingi sana ,Kama wakati ule hoja za Dkt Slaa zilikuwa zikijibiwa na Nape Nnauye kwa ustadi mkubwa na vijembe vya hapa na pale kwanini leo?

Mosi,Hoja ya uhuru wa habari na kuongea,Hapa TBC na ndugu Mwakyembe walipasa kuwa wajanja wanaonyesha sehemu za mikutano ya Tundu Lisu halafu wanapigilia nondo zao kwa kuonyesha taarifa za Magufuli kuziba mabonde,Bila hivyo watu wanatafuta habari za Tundu lisu kinguvu.

Pili,Hoja za Malalamiko za wafanyakazi , wafanyabiashara na wakulima hapa watendaji walipaswa kuonyesha kitu gani kimefanyika kisheria,Mapungufu walioyaona kwa miaka mitano,Na nini matarajio ,Bora kukili mapungufu na kuahidi kuboresha,Kutokuongelea hili Tundu Lisu anazidi kutembelea udhaifu huu.

Hoja ya upendeleo wa mkoa wa Geita hasa chato ni suala rahisi sana kulijibu ,lakini kitendo cha kuuliza chato ni wapi sio jibu ya hoja hii,Hapa watendaji walipaswa kueleza sababu za kwanini wameweka mbuga au uwanja chato na sababu zipo nyingi za kushawishi Raia wa Mwanza ,Mbeya au Dar es Salaam,Kujibu kirahisi kunazidi kumpa sifa Tundu Lisu.

Chama cha mapinduzi kisiwaonea haya hawa watendaji wa serikali wanaotafuta sifa huku wakiharibu sifa na upendo wa chama kwa wananchi.
Watendaji ndio wasimamizi wa hii miradi na utendaji wa serikali kila siku ndio wa kujibu hizi hoja sio kukimbilia kuzuia hoja na kuzidi kumpa umaarufu Tundu lisu mbele ya wananchi

Watendaji wa serikali huu ulikuwa ndio muda wa kwenda Tbc kufanya mdahalo na watu wa upinzani kwa kuelezea mmejenga shule, Hospital na mm jifunza kitu gani na kitu gani kimebaki kwa miaka mitano ijayo sio kuelezea mafanikio tu wakati kuna mambo dhahiri hayajakamilika kwenye shule au hospital

Mfano mzuri na ambao utadumu,Ni kitendo cha kuwaacha watu huru kumpokea Tundu Lissu airport ,Hakuna fujo wala ugomvi uliotokea watu walishangilia sana na kurudi makwao kulala ,ccm ilichukua sifa kubwa kwa hili kwa wananchi ,Mbinu kama hii ya hamsini kwa hamsini ndio ujanja wenyewe.

Muda huu ndio mtu kama Humprey polepole angeacha vitisho na majigambo bali angekuwa anaitisha mijadala na wanasiasa wa upinzani.

Muda huu ndio ilikuwa unamuita Nape Nnauye kwenye Mdahalo na Halima Mdee wanabishana kwa hoja.

Bila mdahalo wa hoja za pande mbili wananchi wanazidi kuaminishwa ugumu wa maisha umesababishwa na ccm wakati kiuhalisia watendaji ndio wameleta matatizo na chuki kwa wananchi

Wafuatao walipaswa kutenguliwa kwa muda ile kujenga imani na kujitenga nao na chama, ccm ieleze kuwa hawa ndio wamezima bbc, Voa na DW, Pia ieleze kuwa hawa ndio wanaeneza chuki kwa ccm, Yote wanayofanya ccm iwaambie wananchi kuwa ni hawa watendaji na sio chama kinakosea

Mkurugenzi wa Tbc
Mkurugenzi wa TCRA
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo au Msemaji wa serikali

Tukutane Octoba,
We jamaa unauelewa mkubwa sana wa propaganda.

Salute kwako mkuu. Tazama kipindi cha JK walivyoweza,kila mtu alipewa airtime yake lakini CCM kilifanya kwa ustadi mkubwa ku lainisha hoja za wapinzani.

Tukupe tu cheo cha uenezi taifa..

Serikali imefanya mengi mazuri,kwa hizo changamoto ni namna tu ya kuwaelekeza wananchi namna gani zinaenda kutatuliwa.

Sio huu upuuzi wa hao uliowataja. Wanamchafua sana Magufuli.
 
Mchuma janga hula na wa kwao....!

Baba akiwa mshamba hata watoto watakua washamba,,bandiko lako lote naona umemruka Magufuli wakati unajua kabisa huyo ndo master mind wa hayo yote.Mara nyingi tumeona akitoa kauli mbaya kwa wapinzani na za kibaguzi hadharani,amewahi pia kuwatisha wakurugenzi kuwa wasithubutu kutangaza ushindi kwa upinzani kwa kua yeye ndo anawalipa mshahara(sio serikali yaani yeye).

Mtu huyu mara kadhaa amekua na tabia ya kudhalilisha wanawake bila kusahau aliwahi kuwaambia watanzania hatuna uhuru huo na yeye ndiye ameminya uhuru wa habari,,anapenda kusifiwa ukimkosa utapewa kesi ya uhujumu uchumi au utaambiwa wewe sio raia.Mtu huyu aliwahi sema wasaliti dawa yao ni kuwaondoa masaa mawili baadae mpinzani wake kisiasa anapigwa risasi 16 na mengine mengi.Magufuli amezuia CAG asikague ofisi yake,ndege zake alizonunua(sio zetu maana hazikaguliwi),amevunja sheria na katiba yetu mara nyingi ikiwemo kujenga uwanja na kuweka mbuga za wanyama kijijini kwake pasipo kuidhinishwa na bunge.Mtu huyu aliwahi mpangia spika wa bunge eti awafukuze wapinzani bungeni ili yeye awashugulikie nje na ni kweli spika alitekeleza hilo agizo....

Ukweli huyu Mtu asafishiki hata mkijitahidi kumsafisha bila kificho ameonesha ana roho ya namna gani,kwa sasa tupo nchi yetu lakini kama tupo utumwani hatuna uhuru.
 
Kabisa na Ndo maana mpaka leo hakuna aliyejibu hoja za Lissu kiufupi hata wale wazee wanaombea CCM ianguke mikononi mwa huyu mtukufu ili wapumue.
Polepole unayemtaja hawezi kujibu hoja za lissu hata siku moja , Lissu size zake ni akina kinana, makamba nao mmeshawachafua kijinga jinga tu.


Mtavuna mlichopanda.


Siasa ni sayansi inahitaji ubunifu, utafiti, uchambuzi na strategies siyo ubabe na vitisho muda wote.
 
NOTED MKUU na nukuu ...''' Watendaji wa serikali huu ulikuwa ndio muda wa kwenda Tbc kufanya mdahalo na watu wa upinzani kwa kuelezea mmejenga shule, Hospital na mm jifunza kitu gani na kitu gani kimebaki kwa miaka mitano ijayo sio kuelezea mafanikio tu wakati kuna mambo dhahiri hayajakamilika kwenye shule au hospital ''''

hayo uliyozungumza hiyo ndiyo polarity law . hakuna mazuri yasiyo kuwa na mafinyufinyu , wakikubali ushauri huu , ccm wameshinda asubuhi na mapema .
 
Mtoa mada kamlinda sana magu kwenye Uzi wake...😂😂😂😂 Ni watendaji tu sio rais aliyeleteleza haya Ila Ni watendaji tu. Mmeelewa watendaji😂😂😂😂😂✌️✌️✌️✌️🔥
 
Mleta Mada, hujawajua watu vizuri, hao wanaoubania Upinzani Maksudi si kwamba wanaipenda CCM ya jiwe, bali ni wapinzani wa ndani wa mlevi madaraka jiwe bin CCM. bila maadui wa ndani, adui wa nje, yaani Upinzani hawawezi kitu.

Kama kweli wewe siyo CCM kindakindaki, na unapenda Mabadiliko, usiwaamshe yaache yaendelee kuvurunda, ili kumpa Lissu kick! kwani polepole hajui kuwa anafanya kosa la ki-Siasa bana?

Kambona walimwachia huru na ulinzi juu, akaishia njia tusioijua wengi! akili unayowapa ni ya kuumaliza upinzani kinyemela! acha! Moderator fanya ujanja team Lumumba YASISOME HAPA!
 
Mkuu nina mashaka na uwezo wako wa kufikiri mambo

Una uwezo mdogo sana wa kufikiri

Sio kila jambo wewe unageuza mipasho na ngonjera

Kama una miaka zaidi ya 18 na una mawazo mgando kama uliyoyaandika hakika kama Taifa kuna kitu kwenye mifumo yetu ya elimu haipo sawa

Inakuwaje mtu mzima na mashavu yako unatoa mipasho na ngonjera

Kama huna la kuandika nenda kunywa maji pumzika

You are certified idiot
Duh! Mkuu mbona unamwelekeza huyu jamaa kwa ukali namna hii? Inaonekana ana unazi wa kijinga?! Next time mpuuze tu nalo ni jibu pia
 
24 Reactions
Reply
Back
Top Bottom