Kalunguine
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 2,543
- 134
Hapa mwanza,kuna chuo cha makada wawili wa chama cha mapinduzi,mmoja anaitwa samson itozya makunja na mwenzake anaitwa festo magambo,hawa jamaa wana NGO yao ambayo kwa sababu ya njaa wameigeuza kuwa chuo cha madini kinaitwa CRDO,wanafanya matangazo katika mikoa yenye migodi ya madini na wilaya zake wakiwahamasiha vijana kujiunga katika kozin zao na kuwa watawatafutia ajira mogodini na matokeo yake ni vijana weng kuishia kutapeliwa,serikali dhaifu ya CCM imeshindwa kuliona hili,na makada wake wanaanzisha vyuo vya kuchakachua uchumi mdoggo na wa shida wa vijana wake,kama kuna yeyote hapa JF anajua mahali pa kufikisha habari hizi atusaidie maana hapa mwanza vijana wanalizwa na hivi sasa wanatangaza kozi ya utalii hali hata majengo ya kufanyia kozi zao hawana,istoshe leo hii wanaofanya mafunzo ya madini wamepelekwa kwenda kusomea shule ya msingi ya nyanza ambapo wanafunzi wa shule ya msingi wametolewa darasani na kurusiwa kwenda makwao kupisha wanachuo waliofanyiiwa mchezo wa kuigiza na bwana makunja,na issue hii pale shule ya msingi ya nyanza C NI KATI kati ya bwana makunja na MWALIMU mkuu wa shule,hii ni halali? je hii ni halali watoto wetu wa shule ya msingi kukatishwa masomo yao kwa sababu ya utapeli wa bwana makunja na mwalimu mkuu aliyehongwa vipesa na uongozi wa CRDO?