CCM haitadumu chaguzi mbili kukiwapo tume ya uchaguzi huru

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
CCM haitadumu chaguzi mbili kukiwapo tume ya uchaguzi huru. Hivyo ndivyo inavyoonekana kwa sababu haitaki kata kata kuwapo kwa tume ya aina hiyo. inashinda kwa sababu ya tume hii ya sasa inayochaguliwa na mwenyekiti wa CCM!
 
Na Msajili huru wa vyama pia. Kama vyombo hivyo huru vikiwekwa sasa hivi, CCM itapata shida sana kushinda October hii, ukweli huu hauna wasiwasi.
 
Hakuna cha chaguzi mbili; ukifanyika uchaguzi wowote huru CCM haiwezi kushinda. Tukumbuke ksema uchaguzi huru; Hakika CCM haiwezi kushinda.
Angalia sasa hivi sheria ya gharama za uchaguzi imeshaanza kutumika lakini CCM wanahonga waziwazi na takukuru inaangalia tu, kisingizio eti wabunge wanatimiza ahadi zao kwa wananchi!
Rais naye anaibuka eti takrima haiepukiki! sheria imesema takrima ni rushwa, mahakama ikasema takrima ni rushwa lakini rais anaipaka mafuta na hivyo rais akitoa takrima takukuru wataangalia tu. Hakika uchaguzi hauwezi kuwa huru.
Sheria imesema kwa jimbo gharama mwisho 40milioni; leo JK anachangisha 500 milioni kumng'oa Ndesamburo kwenye jimbo moja! Atazitumiaje? Ndiyo maana anaibuka na kusema takrima kwa wazee wa kichagga haiepukiki!
Mwenye macho haambiwi tazama.
 
Back
Top Bottom