CCM haina Makubaliano na Wananchi!

SYLLOGIST!

JF-Expert Member
Dec 28, 2007
7,016
6,601
Hivi karibuni kumekuwa na matamshi kuhusu CCM na utamaduni wake waku wachagua viongozi wake kwa mihula miwili miwili. Katika kutafakari hayo nilikaa na kujiuliza CCM wana makubaliano na wanachama wake katika chaguzi mbali mbali za viongozi?

Makubaliano ya wanachama wa CCM na chama chao ndio ridhaa ya Wananchi wote?

Piga-Ua jibu nililolipata ni hivi 'CCM haina Makubaliano na Wananchi' ya moja kwa moja bali kupitia kwa wanachama wake na hivyo sio lazima, si lazima kuwachagua kwa muhula mwingine....nasema hivi kwa kuwa wanachama wake wengi waliokuwa na makubaliano na chama chao wameingia makubaliano au mikataba mibovu kwa kutuhadaa- endapo watachaguliwa muhula wa pili wataweza kubatilisha hayo makubaliano/mikataba mibovu?

Nawasilisha
 
Mkuu hata sikuelewi kabisa...
Nachofahamu mimi ni kwamba CCM haina makubaliano na wananchi isipokuwa wanachama wake. Ni hivyo hivyo ktk vyama vyote wala sii CCM pekee isipokuwa ni wewe mwananchi unayetakiwa kukubaliana na chama kimojawapo ktk upigaji kura wako..Chama kinatoa Ilani, sera na mwongozo wake ambao wewe mwananchi unautazama na kuuchunguza kabla hujaingiza kura yako.

Ni kweli kabisa kwamba CCM hawataweza kubadilisha kitu ktk mikataba..Leo hii dhabau kwa mara ya kwanza imefikia dollar 1035 kwa Ounce ongezeko kubwa sana ktk GDP yetu lakini mfuko wa Taifa unaambulia ukoko kutokana na mkataba mbaya..Mh. Zitto hawezi kubadilisha kitu zaidi ya kubadilisha vipengele fulani fulani ambavyo haviwezi kuathiri pato la mashirika kama Barricks, isipokuwa katika madini mengineyo kama Copper na kadhalika ambayo pato na mchango wake ni mdogo sana.

Njia pekee kwetu sisi Watanzania ni kutafuta mgombea Independent, kichaa mmoja kama Chavez ambaye anaweza kubadilisha kila kitu hata kama nchi yetu irudi ktk Ujamaa kwa miaka mitano ijayo. lakini sidhani kama Wadanganyika wanaweza kusimama nyuma ya kiongozi huyo kwa mwaka mmoja tu..Licha ya hivyo sioni chama wala kiongozi yeyote anayeweza kusimama nyuma ya Ujamaa kama itikadi inayoweza kuleta maendeleo.
Hivyo, swala la mikataba mibovu hilo tusahau!..kwani tumesha UZA nchi. Ukiuza kitu hata iwe nyanya sokoni sidhani kama unaweza kudai kurudishiwa ati makubaliano yalikuwa mabaya!
 
Mkuu hata sikuelewi kabisa...
Nachofahamu mimi ni kwamba CCM haina makubaliano na wananchi isipokuwa wanachama wake. Ni hivyo hivyo ktk vyama vyote wala sii CCM pekee isipokuwa ni wewe mwananchi unayetakiwa kukubaliana na chama kimojawapo ktk upigaji kura wako..Chama kinatoa Ilani, sera na mwongozo wake ambao wewe mwananchi unautazama na kuuchunguza kabla hujaingiza kura yako.

Mimi nimekuelewa. Unacho kifahamu na mie nakifahamu. Ahsante kwa kufafanua

Ni kweli kabisa kwamba CCM hawataweza kubadilisha kitu ktk mikataba..Leo hii dhabau kwa mara ya kwanza imefikia dollar 1035 kwa Ounce ongezeko kubwa sana ktk GDP yetu lakini mfuko wa Taifa unaambulia ukoko kutokana na mkataba mbaya..Mh. Zitto hawezi kubadilisha kitu zaidi ya kubadilisha vipengele fulani fulani ambavyo haviwezi kuathiri pato la mashirika kama Barricks, isipokuwa katika madini mengineyo kama Copper na kadhalika ambayo pato na mchango wake ni mdogo sana.

Hapa si rahisi nikubaliane na wewe-ninaelewa wapo wenye ari ya mabadiliko-nilichomaanisha hapo juu ni "Je wanachama wa CCM wanaweza batilisha mfumo mzima au 'mikataba' yake na wanachama ya kuwachagua viongozi wake kwa mihula miwili? Where is their choice?

Njia pekee kwetu sisi Watanzania ni kutafuta mgombea Independent, kichaa mmoja kama Chavez ambaye anaweza kubadilisha kila kitu hata kama nchi yetu irudi ktk Ujamaa kwa miaka mitano ijayo. lakini sidhani kama Wadanganyika wanaweza kusimama nyuma ya kiongozi huyo kwa mwaka mmoja tu....

Hata ikiwa ndani ya CCM iwe...alimradi isionekane kama ni usaliti wa mkataba huo. Ndio wanaweza kisimama nyuma ya kiongozi yeyote kwa mwaka mmoja tu!

Hivyo, swala la mikataba mibovu hilo tusahau!..kwani tumesha UZA nchi. Ukiuza kitu hata iwe nyanya sokoni sidhani kama unaweza kudai kurudishiwa ati makubaliano yalikuwa mabaya!

Swala la mikataba mibovu ndilo lilionileta kuuliza hapa-Mkataba mzima wa CCM na wanachama wake ni mkataba mbovu- ni mfumo uliopitwa na wakati na haileti changamoto ya demokrasia ya kweli!
Mkanadara, nchi haijauzwa bado...labda CCM;)


Ahsante Mkandara
 
“
CCM ina utaratibu wa kuachiana vipindi viwili. Ni utaratibu uliowekwa kwa maslahi ya chama katika mazingira ya siasa za leo. Lakini, hata kama watajiotokeza wanachama wengine....... Sidhani kama kuna mwanachama ambaye anaweza kupitishwa ..............

Utaratibu huu ni wa CCM peke yake-na sio makubaliano na wananchi wengi ambao sasa wamechoshwa nyoyo na bongo zao.

Waachiane wenyewe huko CCM na siyo kupeana nafasi za uongozi serikalini

hebu fikiria, baada ya papa anapewa kidagaa naye awe papa kwa mgongo wa kura ya mwananchi?
 
Hivi leo mkichagua chadema au cuf kuongoza tz bara hiyo itakuwa serikali au vichekechesho, hata kama ccm hatuitaki lazima kwanza kitokee chama kijijenge kiwe na ukubwa (grassroots support, popular support, na uwingi wa vigogo) kama wa ccm. Hapo tutapata alternative. Mlioko nje mnajua kuwa labour na conservative au republicans na demacrats ni vyama karibu vinavyolingana ukubwa, sio sawa na cmm na chadema au ccm na cuf huku bara.
 
CCM wanaleta fedhea tena kwenye siasa na Serikali ya Wananchi. Watu millioni nane kwa arobaini na saba.

Msije humu" wanaharakati" manake mtabadilisha hili kuwa nataka Kumhujumu Raisi wangu, niliyemchagua.

Mheshimiwa kuna watu, wanaodai kukutetea kwa kusambaza uovu wa Chama chako ambaye wewe ni Mwenyekiti. Hao wameshakupeleka ambako ulikuwa hutegemei Kufika(na mikutano ya faragha ambayo ni zima moto tu huku moshi bado ukifoka).
Usemi mtandaoni...." dude lishawaka"

Hauwezi okoa CCM. Chukua chako Mapema na uanzishe chama mbadala au ujiunge.
Utabakia kuwa Raisi wa wanyonge na sio genge la walumbanao. Bila hivyo na wewe utakuwa kwenye genge kama hilo huko baadae? Nani alijua maovu ya CCM kama sio wenyewe kulumbana? Isitoshe, watu wanaendelea na hujuma hizo na kwa uharaka .
 
Hivi leo mkichagua chadema au cuf kuongoza tz bara hiyo itakuwa serikali au vichekechesho, hata kama ccm hatuitaki lazima kwanza kitokee chama kijijenge kiwe na ukubwa (grassroots support, popular support, na uwingi wa vigogo) kama wa ccm. Hapo tutapata alternative. Mlioko nje mnajua kuwa labour na conservative au republicans na demacrats ni vyama karibu vinavyolingana ukubwa, sio sawa na cmm na chadema au ccm na cuf huku bara.
Hujui kitu Wewe, wanajua siri viongozi wako tuu, ledger ya CCM ina wanachama wasiozidi milioni 3 na wengi katiyao ni feki, yaani hawakiungi mkono, daftali la CHADEMA lina wanachama dedicated 7 million, bado useme CCM wako juu ? Juu kwa lipi?

Hivi unafikili juhudi za kubana Hata mikutano ya ndani ni bure? Wasilolijua ni kwamba wanachama wa chama kama CHADEMA ni wenye upeo, si rahisi kuongopewa na kurubuniwa simply kwa sababu zisizo mbele wala nyuma.

Ushahidi angalia wamenunuliwa wabunge na madiwani je CCM imeongeza wana chama kwa hilo au imepunguza? Jibu unalo wewe!
 
Hujui kitu Wewe, wanajua siri viongozi wako tuu, ledger ya CCM ina wanachama wasiozidi milioni 3 na wengi katiyao ni feki, yaani hawakiungi mkono, daftali la CHADEMA lina wanachama dedicated 7 million, bado useme CCM wako juu ? Juu kwa lipi?

Hivi unafikili juhudi za kubana Hata mikutano ya ndani ni bure? Wasilolijua ni kwamba wanachama wa chama kama CHADEMA ni wenye upeo, si rahisi kuongopewa na kurubuniwa simply kwa sababu zisizo mbele wala nyuma.

Ushahidi angalia wamenunuliwa wabunge na madiwani je CCM imeongeza wana chama kwa hilo au imepunguza? Jibu unalo wewe!
Hahaha ubaya au uzuri wa madai ya wanasiasa ni kwamba wapiga kura wote ni wao. Nakumbuka marehemu Mtikila alikuwa akisema ana wanachama milioni 45 Tanzania nzima, lakini hakushinda ubunge kule kwa Kolimba.
Watanzania ni hawa hawa, wakija ccm wanahudhuria mkutano, wakija CHADEMA wanahudhuria hao hao. Kusema chama fulani kinawanachama wengi, hili ni debatable. Mimi nina kadi za vyama vinne na labda naweza kupewa zingine sijuu. Unakuwa kwenye mazingira flani, unapewa kadi huwezi kukataa, kinacho count ni nani anashinda, siyo idadi ya wanachama. I hate kuona kura zibaibwa au anatangazwa mtu ambaye hamjamchagua, lakini haya ya idadi ya wanachama siyatetei.
 
Kwa habari za hivi majuzi kuwa CCM hawata omba/au kuongeza miaka ya utawala wa Raisi, ni la kupongezwa. Laiti pia wakikubali kushindwa kwa miaka mitano ijayo, litakuwa la kupongezwa.

Miaka 10 iliyopita CCM kama chama kilijizatiti. walakini...Maisha ya watu, yalikuwa wasiwasi na ya kuweweseka, rushwa kwenye mishipa ya uchumi, kuporomoka kwa utamadumi nakadhalika

wananchi waliomba na sala zikajibiwa, tunaona mabadiliko hata ya macho....flyover n.k Walakini CCM imebadilika? Je tunaweza ona haya?

..kwa nini wananchi wasichague chama kingine? Je tutaona CCM ile ile?
 
Hivi leo mkichagua chadema au cuf kuongoza tz bara hiyo itakuwa serikali au vichekechesho, hata kama ccm hatuitaki lazima kwanza kitokee chama kijijenge kiwe na ukubwa (grassroots support, popular support, na uwingi wa vigogo) kama wa ccm. Hapo tutapata alternative. Mlioko nje mnajua kuwa labour na conservative au republicans na demacrats ni vyama karibu vinavyolingana ukubwa, sio sawa na cmm na chadema au ccm na cuf huku bara.
Acha utopolo. Jiwe alikuwa na ukubwa gani kabla ya kuokota urais?
Samiah, Polepole na Bashiru wana maajabu gani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom