CCM Haina Mafanikio ya kuwaonyesha Watanzania Waielewe!

Elly B

JF-Expert Member
Jan 11, 2011
1,194
906
Ndugu zangu,

Mjumbe mmoja wa Baraza la Wazee la CCM Taifa amependekeza kikaoni Dodoma kuwa dawa kuu ya wapinzani ni kuwaonesha wananchi mafanikio ya chama tawala kwa matendo. Mjumbe huyo ambaye alikuwa Makamu wa CCM Tanzania Bara amesema kuwa wapinzani kama CHADEMA hawatakuwa na la kusema ikiwa wananchi wataona mafanikio yaliyoletwa na CCM kwa macho yao wenyewe....

Binafsi nimeshangazwa sana na wazo hili. Najiuliza ni mafanikio yapi ambayo CCM inaweza kuyaonyesha kwa vitendo mpaka wananchi waelewe?

Hawa watu bana!

Tangu hapo wananchi wa nchi hii walichokuwa wanalilia ni ustawi wao na unafuu wa maisha! Kwani nini jipya hapo? Wananchi wanaomba nini kila siku? Ni yaleyale ya tangu miaka ya 60....Maji, matibabu, barabara, umeme na uthibiti wa bei!

Na tatizo limekuwa ni lipi? Lilelile....Serikali na chama fisadi. Mapato ya taifa kwa asilimia kubwa yanapotelea kwenye mifuko ya watendaji wa serikali binafsi, rushwa imekithiri kila kona , haki imepotea na uhuru unatoweka kwa kasi ya kutatanisha!

Sasa tuongelee kuonyesha mafanikio kwa vitendo!...

Kwamba CCM itaonyesha jinsi ilivyofaulu kuwaibia wananchi kwa kuongeza kodi na bei za mafuta, hivyo kuwasababishia ongezeko kubwa la gharama za maisha??!

au CCm ionyeshe wananchi jinsi inavyochukulia mzaha suala la maendeleo vijijini kiasi kwamba pembejeo hakuna, na zikipatikana zinakuwa kwa uchache na kwa kuchelewa...masoko hakuna na inafikia sehemu hata mazao hayana bei elekezi. Mafanikio yanaextend mpaka mpaka kwenye kuwazuia wananchi wasiuze mazao nje ya nchi ambako kuna maslahi kwao! Yaani masoko ya ndani ovyo bei kila mlanguzi awanyonye anavyojua na nje ya nchi Msiuze. Sawa na kusema wakulima ni haki yao kuwa maskini!

au CCM ionyeshe mafanikio ya kushindwa kusimamia rasilimali zetu mpaka wanyama wanatoroshwa nje ya nchi kupitia viwanja vya ndege vyenye ulinzi masaa yote...au mafanikio katika kuwapa misamaha ya kodi wawekezaji kwenye sekta za madini na utalii hii ikiendana na kuwaachia wamiliki wa makampuni hayo na mahoteli kubadilisha majina kila muda wa kulipa kodi unapofika, sawa na kusema CCM na serikali yake inazidi kufanikiwa katika kupokea rushwa!

au CCM na serikali iwaonyeshe wananchi jinsi ilivyoweza kuwabaini mafisadi, kutangaza vua gamba na hatimaye kufeli jumla katika hilo? kimevuliwa kipi ? mikwara yote nani kashughulikiwa? So mniwie radhi ntakaposema ni sera isiyo rasmi ndani ya CCm kuwalinda wahalifu na wahujumu uchumi nchini!

au labda CCM ionyeshe mafanikio ya serikali yake katika kujiteulia Makandarasi wa kujenga barabara ambazo zimetokea kuwa chini ya kiwango mpaka kufikia kutomaliza mwaka mmoja kabla hazijayeyuka na kubanduka na kisha kuwalipa kwa gharama za juu,..gharama zinazohusisha ukaguzi wa barabara zenyewe......Mafanikio?

au CCM na serikali yake ionyeshe mafanikio ya kutumia Vyombo vya dola kwa maslahi ya kisiasa kuwatishia wapinzani na kuwadhuru wanaoipinga? ni mafanikio ya kuacha watu wafundishwe namna ya kudhuru wenzao kwa mapanga, visu na tindi kali eti kwa sababu tu ni wapinzani au wanaoikosoa serikali? ...au kuwaua waandishi na kuwang'oa kucha na meno huku polisi wakilazimisha kujichunguza ili kupindisha haki na ukweli?

CCM na serikali vionyeshe nini kwa watanzania? Jinsi kulivyopatikana mendeleo ya kutisha kwenye sekta ya elimu huku wanaofeli ni sawa na wanaofaulu( kwamba ukifelei umefaulu na ukifaulu umefaulu)? kwamba ukifanya mtihani na usipofanya unafaulu tuu hata kama umeshindwa kuandika hata jina lako??! ..kwamba kuna shule kibao za kata,walimu, madawati na maabara hakuna? jinsi rushwa hasa za ngono zinavyoamua viwango vya ufaulu wa vyuo vikuu huku wahadhiri wake na wasaidizi wao wakiachiwa uhuru wakusema nani kafaulu na nani kafeli bila kujali ufaulu umepatikanaje?

Ni hivi, CCM haina sauti ya kuonyesha wala kusemea chochote ambacho kitaitwa mafanikio ndani ya nchi. Labda kitu pekee ambacho CCM inawezafanya ni kuwa wakweli kwa wananchi wa Tanzania....Kuwa imewadanganya kwa muda mrefu, imewasababishia adha na madhila kwa muda mrefu na imeshindwa kuongoza, hivyo inaomba radhi kwa wananchi wa Tanzania kwa yote hayo na iahidi kutorudia tena, pia iahidi kuachia nchi haraka sana na kwa amani ili wanaoweza waiendeshe mpaka wao watakapojifunza kuwajibishana bila kuangaliana sura, kuwa WAZALENDO NA WAKWELI, ndiyo warudi kuomba ridhaa ya wanachi wa Tanzania tena. Hapo tutakuwa tunaelekea kuelewana kidogo. Vinginevyo mimi naona "ARI ZAIDI, NGUVU ZAIDI NA KASI YA HATARI KUELEKEA KUZIMU YA HAPAHAPA DUNIANI, KAMA CCM HAITAONDOKA MADARAKANI!

Nisamehewe kama kuna asiyenielewa! Mimi naishi uswazi, wazazi wangu na washkaji wengine wako kijijini na nayaona kwa macho!
 
Mkuu ni kweli uliyoyasema...ila tatizo mods watatoa hii thread kwasababu ni mwiba mchungu sana kwa magamba.
 
Mbona CCM wameleta mafanikio makubwa sana Kama kuwapiga CHADEMA mabomu huko Arusha kwa kutumia vyombo vya usalama EPA Meremeta RICHMOND na mengineyo
 
Mbona ccm wameleta mafanikio makubwa sana Kama kuwapiga CDM mabomu huko Arusha kwa kutumia vyombo vya usalama EPA Meremeta RICHMOND na mengineyo

twiga kupanda ndege..madawa ya kulevya hadi ktk vi2o vya daladala....division 0 wanafunz 70 kati ya mia.....
 
Jamani hamkumwelewa huyo Mzee, alisema; ssm iache kuzidi kujipaka matope, ingekuwa ina kiongozi, wangekuwa wanafanya kitu wakioneshe wazi. Si kwamba alisema ssm yake imefanya chochote. Ahadi kedekede za 2010 hazitekelezeki!!!! Alijua, hakuna Mtanzania mwenye upeo wa kufikiri kuwa ule ni ulaghai tu wa kujipatia "Kula" kwa kura za wajinga. Watu walikuwa wanasombwa na malori kwenda kuunga foleni ya pilao na kofia ya kijani ili wapige kelele ssm Oyeeeee. Baada ya pilao wakasahau ahadi ya "Maisha bora kwa kila Mtanzania, yawezekana." 2010 Hawakukumbuka kuwa miaka 5 ililiwa na nzige. Hawakuuona tena ule umasikini wao kwa pilao ya siku moja walio nunuliwa na pesa yao ya EPA. Leo, Mzee anasema ana bado kadi moja mfukoni. CCm wakiitoa hiyo, hakuna wa kuipinga. Siijui ni ipi, watu wamesha amka, pilao haiwasumbui, mabomu hawayaogopi, za moto hawaziogopi, na hata vitu vizito vya Chagonja hawaviogopi. Wanataka tu haki yao. Ufisadi umefikia kikomo baada ya kujichukulia wenyewe mali za watu, mtazirudisha tuu.
Sii Sii Emm Oyee.
 
Elly B Kweli wewe huoni. Hizo barabara, na mambo mengine Mengi ya maendeleo tunayoyashuhudia umefanya wewe? Tuache ushabiki wa vyama usio endelevu na usio na tija kama huo wako. Siku njema.
 
Last edited by a moderator:
Kweli wewe huoni. Hizo barabara, na mambo mengine Mengi ya maendeleo tunayoyashuhudia umefanya wewe? Tuache ushabiki wa vyama usio endelevu na usio na tija kama huo wako. Siku njema.

Na huo ubovu ninaoeleza we huuoni? unaona yanapendeza hayo kweli? Labda lugha niliyotumia ni ndefu sana. Nilichosema kwa ufupi ni kuwa mpaka sasa hayo tunayosguhudia ni matumizi mabaya ya mdaraka, rasilimali na kodi za wananchi.

Sasa nadhani utaelewa.
 
Mbona ccm wameleta mafanikio makubwa sana Kama kuwapiga CDM mabomu huko Arusha kwa kutumia vyombo vya usalama EPA Meremeta RICHMOND na mengineyo

Yeah!!!!..na kwa kuwa hayo mafanikio ni aibu kuyaonyesha hadharani, thats why nikasema waje na ukweli na apologies kwa umma!
 
Kweli wewe huoni. Hizo barabara, na mambo mengine Mengi ya maendeleo tunayoyashuhudia umefanya wewe? Tuache ushabiki wa vyama usio endelevu na usio na tija kama huo wako. Siku njema.


Ambagae Ambagae Ambage!

Kwani ni lipi hasa halijaeleweka hapo? Kwamba nimewazushia hayo? Hawajafanya yote? au...mi ndo sikuelewi ndugu yangu. Are you proud na jinsi utawala bora wa nchi ulivyozingatia matumizi ya rasilimali zetu na kodi za Watanzania?
Nashangaa!
 
Wewe mwenywe bila ccm usingefika hapo ulipo jitazame upya usidanganye watu.
Uncle Deo,

Nisingefika hapa is not good enough! Tunataka serikali inayowajibika kwa wananchi wake 100%, no excuses. Serikali imewekwa ili ifanye kazi za wananchi na siyo kutumia fedha za kodi ya wananchi ovyo na kuwalinda wanaoiba. We unaonaje is that fair? Kwamba kodi zilipwe mpaka na vibibi huko vijijini halafu zitumike na majizi flani tu kwa kujineemesha na familia zao! is that what you are suggesting?

Kwamba ni dhambi kuhoji ni kwa nini barabara ni mbovu na wakati zimejengwa jana? kwamba ni kwa nini kodi za maliasili na madini zinasamehewa na wanakamuliwa maskini wa nchi hii?..au ni kwa nini CCM inatumia vyombo vya dola ovyo, kinyume na taratibu au ni kwa nini katiba haiheshimiwi na CCM?.. this is boring!

....kwamba kwa sababu ni mama amekuzaa tu basi usingefika hapa hata kama umetupwa chooni! you can't be serious! hivi huwa mnafikiria kinyumenyume?
 
Jamani hamkumwelewa huyo Mzee, alisema; ssm iache kuzidi kujipaka matope, ingekuwa ina kiongozi, wangekuwa wanafanya kitu wakioneshe wazi. Si kwamba alisema ssm yake imefanya chochote. Ahadi kedekede za 2010 hazitekelezeki!!!! Alijua, hakuna Mtanzania mwenye upeo wa kufikiri kuwa ule ni ulaghai tu wa kujipatia "Kula" kwa kura za wajinga. Watu walikuwa wanasombwa na malori kwenda kuunga foleni ya pilao na kofia ya kijani ili wapige kelele ssm Oyeeeee. Baada ya pilao wakasahau ahadi ya "Maisha bora kwa kila Mtanzania, yawezekana." 2010 Hawakukumbuka kuwa miaka 5 ililiwa na nzige. Hawakuuona tena ule umasikini wao kwa pilao ya siku moja walio nunuliwa na pesa yao ya EPA. Leo, Mzee anasema ana bado kadi moja mfukoni. CCm wakiitoa hiyo, hakuna wa kuipinga. Siijui ni ipi, watu wamesha amka, pilao haiwasumbui, mabomu hawayaogopi, za moto hawaziogopi, na hata vitu vizito vya Chagonja hawaviogopi. Wanataka tu haki yao. Ufisadi umefikia kikomo baada ya kujichukulia wenyewe mali za watu, mtazirudisha tuu.
Sii Sii Emm Oyee.

Exactly my dear!

na ndiyo nikasema sioni CCM wana ubavu wa kusimama na kuonyesha nini kwa wananchi ili waeleweke! sioni kama wana sauti bila haya kusimama na kongea mafanikio ndani ya Tanzania (labda wawe na akili za wendawazimu)
Hakuna karata wala kete. Hii nchi imewashinda na ni wazi wameshachoka. They should just apologise and go peacefully watuache siye tujitibu manundu yetu na tuangalie mustakabali wa taifa letu kesho kwa ajili ya watoto wetu na wajukuu. Though wakirudisha walivyoiba itakuwa ni ishara ya nia ya dhati ya kutubia wizi..., sisi (kama wananchi) utafurahi na kuwapongeza bila kusahau kuwawajibisha at the same time.
 
Baadhi ya mafanikio ya rerikali ya CCM
Mafanikio ya nchi yanapimwa kimataifa na hivi sasa kigezo kikubwa cha kupima maendeleo ya nchi ni malengo ya millennia.

Barabara: mwaka 1961 zilikuwa kilomita 1,300
- baada ya miaka 50 kilomita zilifikia takribani 6,000
- hivi sasa kilomita zimeshafikia 11,000
- mwaka 2015 inakadiliwa kufikia 18,000
- bilioni 450 za barabara ukilinganisha na bilioni 56 miaka 5 iliyopita
- kujenga miundombinu ya barabara.

Elimu: mwaka 1961 chuo kikuu kimoja
- hivi sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 32 tunaongoza wa idadi katika EAC
- miaka 10 iliyopita tulizidiwa idadi ya vyuo vikuu na Kenya na Uganda
- kabla ya utawala wa Kikwete alikuta idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu 40,000
- hivi sasa idadi ya wanafunzi ni 160,000 hii ni mara 4 zaidi
- bajeti ya %24 ya wizara ya elimu ni mikopo kwa wanafunzi hakuna nchi ya EAC iliyotoa kiwango kikubwa cha msaada kwa wananchi wake kama hivi.
- UDOM-Chuo kikuu cha serikali kikubwa zaidi katika EAC kinachukua wanafunzi 40,000 ni idadi ya uwezo wa vyuo vikuu vyote vilivyokuwepo kabla ya serikali ya Kikwete.
- kuna shule za msingi kwenye kila kata.
- Kuongezeka ajira kwenye sekta ya elimu.
- Kujenga miundombinu ya selimu
Haya ni baadhi ya mafanikio machache nimechagua sekta mbili kama mfano lakini mafaniko ni mengi sana.
 
Elly B pole sana. Tatizo lako hauna data, unategemea taarifa za vijiweni. Ccm imefanya kazi kubwa sana, ila kama hutaki kuona sitakulazimisha
 
Wape hao mapimbi waelewe. Kazi yao kusema mambo wasiojua. Watolee na data za miradi inayotekeleza kupanua bandari mbalimbali, ununuzi wa meli kwenye maziwa, ujenzi wa viwanja vya ndege, fast ferri dar, na miradi ya umeme.
 
something, does not mean nothing, but something is likenothing once the possible capability is not proportional to something. Sasa, kuseama c c m haijafanya kitu. Tatizo ni hali ya maisha ya watanzania. Chukulia mkulima wa tanzania, ukizingatia takwimu sahihi za tz, zaidi ya asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima na wanaishi vijijini, wengine ni wafugaji na wafuvi. Kimsingi hali halisi ya maisha ni swala la kuangalia sana. Na ile hoja ya maisha bora kwa kila Mtanzania sijui. Pia swala la kilimo kwanza, ni nini cha pekee ambacho ni tofauti na ile ya Mwalimu, kuwa uti wa Mgongo ni kilomo, kuna jipya gani. We need to be realistic.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom