CCM difinisheni gani utaipa?

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Nimesikia na kusikiliza mengi ila hili jina la CCM naona limebeba urefu wa maneno mengi kila mmoja na tafsiri yake ukilinganisha na vyama vingine vya siasa.
Je wewe kama mfuatiliaji wa siasa za Tanzania na vyama vyake kutokana na hali ilivyo tokea unapokumbuka mpaka hii leo conclushen yako ni nini juu ya kirefu cha CCM zaidi ya msemo maarufu wa " CHAMA CHA MAPINDUZI "
Kwa upande wangu nimeona kirefu na mabacho kinabeba uzito ulio na maana ya kina kabisa ni CHAMA CHA MATAPELI.
Chama cha matapeli CCM kinautapeli tokea kwenye uchaguzi mpaka kwenye majukwaa,Raisi Mkapa ni tapeli mawaziri wake matapeli haya madili makubwa makubwa yote wamefanyiana utapeli wenyewe kwa wenyewe.
Kikwete amewatapeli wananchi kwa kuwaahidi maisha bora kwa kila Mtanzania wananchi walio wengi wakainunua sera ya kasi mpya nguvu mpya na ari mpya ,leo jamaa anapanda paipu akielekea maulaya utazani anaenda kulala zamu (ameoa wake zaidi ya mmoja)
Sijui nyie wengine mtaiona vipi maana ya CCM ,hebu elezeni vile muionavyo CCM ,dah chama hakina dira wala lengo ni wizi tu !!Kila unapopagusa basi wameshapita na kumega !!!
 
Chama cha Mafisadi ambao kinafanya kila njia kuhakikisha mafisadi hao hawaguswi na mkono wa sheria pamoja na ufisadi mkubwa walioufanya dhidi ya Watanzania. Umeshasikia fisadi yeyote ndani ya CCM kafukuzwa chama? Umeshasikia CCM wanawafukuza wabunge mafisadi ili ufanyike uchaguzi mpya wa wabunge waliofukuzwa?
 
Nimesikia na kusikiliza mengi ila hili jina la CCM naona limebeba urefu wa maneno mengi kila mmoja na tafsiri yake ukilinganisha na vyama vingine vya siasa.
Je wewe kama mfuatiliaji wa siasa za Tanzania na vyama vyake kutokana na hali ilivyo tokea unapokumbuka mpaka hii leo conclushen yako ni nini juu ya kirefu cha CCM zaidi ya msemo maarufu wa " CHAMA CHA MAPINDUZI "
Kwa upande wangu nimeona kirefu na mabacho kinabeba uzito ulio na maana ya kina kabisa ni CHAMA CHA MATAPELI.
Chama cha matapeli CCM kinautapeli tokea kwenye uchaguzi mpaka kwenye majukwaa,Raisi Mkapa ni tapeli mawaziri wake matapeli haya madili makubwa makubwa yote wamefanyiana utapeli wenyewe kwa wenyewe.
Kikwete amewatapeli wananchi kwa kuwaahidi maisha bora kwa kila Mtanzania wananchi walio wengi wakainunua sera ya kasi mpya nguvu mpya na ari mpya ,leo jamaa anapanda paipu akielekea maulaya utazani anaenda kulala zamu (ameoa wake zaidi ya mmoja)
Sijui nyie wengine mtaiona vipi maana ya CCM ,hebu elezeni vile muionavyo CCM ,dah chama hakina dira wala lengo ni wizi tu !!Kila unapopagusa basi wameshapita na kumega !!!

Nikisoma siasa miaka ya shuleni, kulikuwa na maneno kama ujamaa kama wa Tanzania usingafanikiwa kwasababu ili ujamaa uje, ilitakiwa ubepari ufikie hatua ya juu kabisa. Sisi Watanzania tuliingia kwenye ujamaa bila kupitia hatua ile mbaya kabisa ya ubepari.

Nafikiri hatua ambayo CCM imefikia sasa, pamoja na ubaya wake wote, huenda ikafungua milango kwa mfumo au viongozi wengine wajao ambao watawajibika na kuwa waadilifu zaidi.

Nafikiri CCM wamefikia kile kiwango cha juu kabisa cha kushindwa maadili ya uongozi. Wananchi wote tumejua matatizo na huenda sasa tutakuwa waangalifu zaidi tunapochagua viongozi wetu.

Changamoto tu kwasasa ni je sisi wengine wote tuko tofauti na hao viongozi wa CCM? Huenda tofauti yetu ni ya mmoja kuwa na madaraka wakati mwingine akivizia na yeye afike juu aanza kukwapua.

Ikiwa hivyo basi tutegemee viongozi wa ajabu mno kabla ya neema kuja.
 
CCM haiwezi kusurvive bila dola.
hii ni kwa sababu ikipatikana dola yahaki isiyopendelea upande wowote basi viongozi woote wa CCM wataozea kwenye magereza kwa jinsi walivyofanya maovu pindi walipokuwa madarakani...
na wahenga wanasema "shina likitikiswa matawi hufuata mkumbo" so hata wnachama wa CCM nao watakumbwa na kashfa tu.
 
CCM ni chama cha maskini ni chama pekee tanzania kilichopenya hata kwa maskini wengi vijijini na mijini


CCM ni chama cha miundo mbinu chama ambacho kinaendelea kujitahidi kuweka miundo mbinu itayosaidia kukuza maendeleo


CCM ni chama cha maelewano inajitahidi kuboresha maelewano mema kati ya jamii vyama visivyo vya kiserikali vyama vya upinzni na wengine ili kuendeleza siasa safi.

CCM chama cha maadili ni chama ambacho kimesimamia kidete maadili ya jamii na maadili ya viongozi wake na wanachama wake, yeyote anaenda kinyume na maadili CCM hamuonei haya hata awe ana cheo gani

CCM ni chama Mafanikio ni chama pekee chenye sera ya kuwanufaisha wananchi wa ngazi zote kuanzia wanafunzi wafanyakazi na wafanya biashara na wengineo


CCM ni chama cha msimamo, CCM haiyumbi wala haiyumbishwi na wanaopenda kuiona ikiyumba


haya machache mengi nnaweka ili kuendeleza hoja
 
Nafikili Kashfa zote hizi zinazotokea ni tatizo la kiongozi mmoja mmoja tu, (Individual Ethical Issues), and have nothing to do with Chama (CCM).
Kwa hiyo si zani kama ni busara kukichafua chama kwa kukipa maneno machafu machafu.Chamuhimu ambocho tunatakiwa kukifanya ni kuwaweka wazi na kuwakemea hawa viongozi mpaka wakiache chama, kama wakikataa kuhama chama then next time you know what do when you cast your vote.Hima tuwakataeni hawa watu kama tulivyomkataa Mkoloni.
 
kwani hao mafisadi na wala rushwa wakubwa wa nchi hii baada ya uozo walioufanya CCM imechukua hatua gani kama chama?

hao kina karamagi, chenge, lowasa, msabaha na hata mkapa wamechukuliwa hatua gani na CCM?

Msije mkazani kujiuzulu ni shinikizo la chama...wale wamejiuzuru serikalini lakini kwenye chama hakuna bado wapo na wanaendeleza gurudumu la ufisadi kama kawaida. so CCM ni uozo
 
kwani hao mafisadi na wala rushwa wakubwa wa nchi hii baada ya uozo walioufanya CCM imechukua hatua gani kama chama?

hao kina karamagi, chenge, lowasa, msabaha na hata mkapa wamechukuliwa hatua gani na CCM?

Msije mkazani kujiuzulu ni shinikizo la chama...wale wamejiuzuru serikalini lakini kwenye chama bado wapo na wanaendeleza gurudumu la ufisadi kama kawaida. so CCM ni uozo
 
kwani hao mafisadi na wala rushwa wakubwa wa nchi hii baada ya uozo walioufanya CCM imechukua hatua gani kama chama?

hao kina karamagi, chenge, lowasa, msabaha na hata mkapa wamechukuliwa hatua gani na CCM?

Msije mkazani kujiuzulu ni shinikizo la chama...wale wamejiuzuru serikalini lakini kwenye chama hakuna bado wapo na wanaendeleza gurudumu la ufisadi kama kawaida. so CCM ni uozo
Mkuu chomba heshima natanguliza utashangaa hawa watu hawana utashi wala aibu eti naye Masha anazungumzia swala la uwanja wa nyamagana wakati WAKATI IMMA ADVOCATES ILISAJILI KAMPUNI YA KITAPELI YA DEEP GREEN FINANCE LIMITED HAJASEMA KITU YUKO KIMYA,SASA KAJIFANYA ANAUCHUNGU NA NYAMAGANA KWANINI? WILSON KABWE MKULUGENZI WA JIJI LA MWANZA HAKUMSHILIKISHA MULUNGULA, SASA KAWA KAUZIBE KWA WILSON,HAWA MKUU WANAJUANA KICHAMA WOTE WACHAFU WELL DONE MKUU FOR NICE DIFINITION.
 
Kuhusu Slaa Mkuu Wataendelea Kukenua Meno Tu,pale Sasa Hivi Hakuana Watu Wenye Uwezo Wa Ku Deal Na Slaa Kila Mtu Anangalia Jinsi Ya Kuficha Visenti Vyake
 
Hata Wadudu Wamewashutukia Jana Mugwana Ilbidi Ajifiche Ndani Ya Gari Singida, NYUKI WALIPROTEST KWAMBA MR HUWEZI KAZI,nyuki Walikataa jk ilibidi asomewe risala ndani ya gari, nyuki walizuia ufunguzi wa shule, Kwani kazi hiyo Halimuhusu Si Kazi Yake anatakiwa amvue kinga mkapi na afunguliwe mashitaka, kushika mikasi si kazi yake ni kazi Mzee Wa Mikasi Dr Shein,
 
CCM ina wanachama Milioni 3 nchi nzima ina maana wote hao ni mafisadi?Kuna wana CCM wazalendo kabisa wanaokerwa na Ufisadi,rushwa na hila zote za kuvuruga Chama!Kama kuna Mwana Chadema mla rushwa ina maana chadema yote haifai?
 
Mtu wa Pwani unaweza kujibu maswali haya machache??

Chama cha CCM kinaleta maendeleo gani ya miundo mbinu ingali zaidi ya asilimia 70 ya barabara zxa nchi yetu ni mbovu kabisa, hakuna usafiri wa kueleweka ndani ta Tanzania hii??

Chama caha pekee kilichopenya hata kwa maskini vijijini kivipi?
kwani swala ni kupenya kwa wananchi au ni kuwaondolea hao wananchi umaskini?? na unajua ni kwanini kimepenya mpaka vijijini? kwa kukueleza tu ni matumizi ya pesa za walipa kodi zinazotumika na chama cha mafisadi. e.g uchaguzi 2005

Maelewano yani kinachoimarisha hiki chama?
Ni hivi karibuni kimevuruga maelewano kati yake na CUF, pili unakumbuka uchaguzi mdogo wa jimbo la kiteto, wajumbe wakuu wa CCM kitaifa walifanya kitu gani? ndio amani hiyo

Je unakumbuka mauaji ya Manzese na kule zanzibar?? na hiyo ni ndogo tu, angalia nguvu inayotumika na polisi wa nchi iliyoko chini ya CCM jinsi wanavyokabiliana na matukio na kusababisha vifi vya watu, e.g UDSM, katalamba, Viongozi wakuu wanauwa wananchi.

Maadili yapi hayo unayoyazungumzia wewe?
Tuliona Fisadi mkapa akifanya biashara ikulu, na wana ccm walikuwa wakijua ila walikaa kimya, tumneona mwenendo wa hali halisi ya sasa jinsi ccm wanavyoingoza nchi yetu na madhambi kibao yanayoendelea, jee haya ndio maadili kwa mtazamo wa CCM sio?? wako wapi akina mkapa, lowassa hawa si mnawaonea haya na ndio maana wanaendelea kufanya watakavo

Hiki sio chama tena bali ni matatizo matupu, labda ingekuwa vizuri ukijibu hayo maswali machache na kutoa mifano halisi unaweza kufanya tukuelewe kidogo

TUPE CHAMA MBADALA!!!
 
CCM ina wanachama Milioni 3 nchi nzima ina maana wote hao ni mafisadi?Kuna wana CCM wazalendo kabisa wanaokerwa na Ufisadi,rushwa na hila zote za kuvuruga Chama!Kama kuna Mwana Chadema mla rushwa ina maana chadema yote haifai?
Hapo napata difinisho nyengine CCM-Chama Cha Mazuzu .nikikupa mifano hai ni baadhi ya wanachama wake kutoelimika na utaona CCM vigogo wanafurahia kuwa na wanachama wajinga wasiokuwa na uelewa wowote na ukiangalia Lowasa amekumbwa na lawama za kifisadi na yeye mwenyewe amejiuzulu kutokana na kukubaliana na hoja zilizotolewa kwamba mbali ya kushiriki katika dili ambako anapinga lakini amehusika katika kulisababishia Taifa hasara kubwa hasara ambayo bado inaendelea ,ila CCM wanachama wamemtandikia zulia jekundu na kumkaribisha kama shujaa sasa wananchi wa aina hiyo ambao ni wanachama wa CCM utawaweka kundi gani,CCM kama Chama kinawatenga watu wa dizaini za kina Lowasa ila wanachama ambao ni wananchi wanaolalamika kuwa hawajawahi kuona barabara ya lami ,wanaolalama kuwa hakuna dawa mahospitali,wanaolalamika na kuchangishwa michango ya nguvu katika kujenga shule za msingi na sekondari ndio hao wanaonekana kuwa na mhusika mkuu wa hasara kwa Taifa ,yaani hatujakaa vizuri nao wakazi wa bariadi wameanza kulalamika na hivyo wanamsubiri shujaa wao ili wampokee kwa shangwe na vigelegele ,wanachama hawa wa CCM utawaitaje kama bado wako katika ujinga na hawaelewi au hawana uwelewa wa vyama vingi ,jambo ambalo CCM hawataki wananchi waeleweshwe na kufahamishwa uwepo na faida ya vyama vingi wanaloliona na kulitaka CCM ni wananchi wawepo CCM tu na kuendelea kuwazuga.
Kusema kuna waCCM wazalendo hilo halina Ukweli kwani kama hao ni wana siasa na wameona namna CCM inavyovuruga bila ya kuona aibu ,wangelitoka kwenye Chama na kurudi kwa wananchi wale waliowapigia kura na kutoa kila lililo rohoni mwake na hapo hapo uwanjani akarudisha kadi ya CCM ,ninavyoamini Chama chochote atakachojiunga basi Ubunge wake upo maana amewaeleza wapiga kura wake kuwa ..haiwezekani kuendelea na CCM kwa sababu hizi na zile huku akimwaga razi basi 100% atahama chama na wapiga kura wake bila ya tatizo lolote .Baada ya muda mchache hata wananchi wataelewa ila hao wazalendo ndio wanaosababisha ujinga kwa wengine.Wapinzani Kenya walipata nguvu kutokana na wabunge na Mawaziri wa Chama Tawala KANU wakati huo kukihama chama na kwa kweli waliondoka na wapiga kura wao na kuwafanya wakenya kupiga hatua moja mbele katika kuchagua ni Chama kipi waweke kura yao.
Kibaki ni kutoka upinzani ambae aliiangusha KANU lakini uchaguzi wa juzi ameangushwa na sababu kuu wananchi wake kupata uelewa wa faida ya kuwepo kwa vyama vingi vya siasa ,sasa WaKenya wapo katika mambo madogo madogo ya mpito ambayo wanasiasa wanatakiwa wayafahamu kuwa ule wakati wa kumteka mwananchi kwa kuwa ni wa chama changu umo ukingoni ,ifahamike raia mwananchi wa kawaida anaweza kabisa kubakia katika Chama chake lakini linapokuja suala la maisha bora kwa kila Mwananchi basi hapo anatakiwa atazame ni wapi kwenye ukweli na ni wapi alipopata hasara ,kwa Tanzania mwananchi amepata hasara kwa kuwaweka CCM Vigogo madarakani nini kifanyike Uchauzi unaokuja inatakiwa abadilishe upande na kuchaguwa vigogo wa Chama kingine.
 
bravo gang chomba.. chama ni watu si majengo au bendera tu kama ni suala la matatizo ya mtu binafsi naamini chama makini kisichokumbatia ufisadi na mafisadi wenyewe lazima wangewafanyia kweli hao mafisadi. Ukiangalia mafisadi wote waliopamba vichwa vya habari ni wana-CCM wamejiuzuru nyadhifa zao serikalini lakini ukifika wakati wa vikao vya CCM wamo ndani ya gree & yellow na wanakaa front seat karibu na brother kaka sasa hapo utasema kuna chama??? Siku hizi wengine wanaita CCM - Chukua Chako Mapema sijui kuna siri gani wameigundua hawa wenzetu mpaka wanafanya kufuru ya aina hii??? Kulindana ndio kulikoshika hatamu sana ndani ya CCM....ukibofoa mashariki unahamishiwa mashariki maana wa kusini hawezi kukufata ni mbali mno. Kama kweli CCM chama makini haya wapigeni chini hao mafisadi wana-CCM wenzenu tuone kweli mnajuwa wajibu wenu. Kulonga mbali kutenda mbali.Hovyooo!!!
 
Hata Wadudu Wamewashutukia Jana Mugwana Ilbidi Ajifiche Ndani Ya Gari Singida, NYUKI WALIPROTEST KWAMBA MR HUWEZI KAZI,nyuki Walikataa jk ilibidi asomewe risala ndani ya gari, nyuki walizuia ufunguzi wa shule, Kwani kazi hiyo Halimuhusu Si Kazi Yake anatakiwa amvue kinga mkapi na afunguliwe mashitaka, kushika mikasi si kazi yake ni kazi Mzee Wa Mikasi Dr Shein,

Nalaila Kiula mugosha wa nyumba hakutaarifiwa ujio huo nini?
 
Kwa mtazamo wangu naona CCM ni CHAMA CHA MAJAMBAZI/CHAMA CHA MATAPELI/CHAMA CHA MAFISADI.
Kama wanachama hao wanao jitetea eti ni wachache kwa nn wamewakumbatia kama sio kulindana ni nn??wawatimue kabisa kundini.Ndo maana tunadanganywa kila kukicha mm NITAUA MTU nina machungu balaa.
 
Kwa mtazamo wangu naona CCM ni CHAMA CHA MAJAMBAZI/CHAMA CHA MATAPELI/CHAMA CHA MAFISADI.
Kama wanachama hao wanao jitetea eti ni wachache kwa nn wamewakumbatia kama sio kulindana ni nn??wawatimue kabisa kundini.Ndo maana tunadanganywa kila kukicha mm NITAUA MTU nina machungu balaa.

Chama Cha Matapeli, Chama cha Mabeberu,Chama cha MAFISADI, Chama Cha MAJAMBAZI na pia kwa sasa kinaendeleza utapeli kwa hari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Ambao hawataki inabidi watoe hoja. Hivi unaweza je kukaa kwenye chama ambacho kila muharifu anajificha humo.

Ukiona gari lolote lina bendera ya CCM nyuma au mbele ujue kuna madhambi limeficha.Fanya tafiti utagundua. Mafisadi wote wakati wanafanya ufisadi lazima watangulize chama.

Mwaka juzi kule airport waliua majambazi na majambazi hayo yalikuwa yametinga na nguo za CCM. Halafu kifuani zikiwa na picha kubwa ya Mzee wa kasi.

Kwa hiyo hali halisi ya definition unaweza kuona inavyojieleza yenyewe. na unaweza kuona ina sura nyingi, Kuna Matapeli, Mabeberu, Mafisadi na Majambazi, mwanzo ongeza tu CHama CHa......


Wale wazuri itabidi watafute kichaka kingine maana CCM ina wenyewe na wenyewe ni wale wale wanaoendeleza UFISADI, UTapeli, Ubeberu, UJambazi na UFISADI kwa kasi mpya, nguvu mpya na hali mpya.
 
Back
Top Bottom