amba.nkya
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 446
- 131
WanaJF, ningependa kubainisha wazi kuwa nimekuwa mwanachama wa CCM lakini nimeamua kwa hiari yangu kabisa kutumia haki yangu ya kikatiba kumpigia kura Dr Slaa (Urais) na Bw Mnyika (Ubunge). Nimeamua hivyo kwasababu za makusudi kutokana na ukweli kwamba CHADEMA kwa ujumla wameonyesha nia ya dhati kuleta maendeleo na kujali maslahi ya mnyonge. Ingawa kura ni siri yangu lakini ukweli na msimamo wangu ndio huo na Mungu atanihukumu kama nitafanya tofauti siku ya 31/10/10. MUNGU ibariki Tanzania.