CCM kwa kiasi kikubwa ni chama kilichobobea katika mikakati ovu na chenye ufanisi uliopitiliza katika utekelezaji.
Chama hiki kwa kadiri ya miaka inavyozidi, na aina ya viongozi inaowapata kinazidi kujiimarisha katika uharamia, uovu, ulaghai na mbinu chafu, na katika utekelezaji wa hayo, hufanya kwa ufanisi wa kiwango kilichopitiliza. Kinapotekeleza uharamia wake kinakuwa kimesoma kwa umakini mazingira na aina ya watu kinaowafanyia uharamia, na kutambua wazi matokeo, na madhara yake na jinsi kitakavyokabiliana nayo:
1. Mwaka 2020, kwa namna ya kiwango cha hali ya juu kabisa, kiliweza kujitangazia ushindi wa pekee kwa kuwatumia makada wake waaminifu, Tume ya uchaguzi, wakurugenzi wa Wilaya na jeshi la polisi. Na katika kutekeleza uharamia uliopangwa, hakikuwa na swalia Mtume, aliyeonekana kisiki alikamatwa, aliteswa, wengine wakapoteza hata maisha, na wengine bado wapo ndani. Kwa kutumia Tume ya Uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi, kuna maeneno kilizuia mawakala wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi kutoingia vyumba vya kupigia kura, kuwachelewesha na hata kuwazuia kushuhudia ujumlishaji wa kura. Kwa kutumia Tume ya uchaguzi, kilijitengenezea kura fake, zilizobebwa kwenye mifuko, nyingine zilikamatwa, lakini nyingine zilifanikiwa kuingizwa na kuhesabiwa. Kikajitangazia ushindi ulipitiliza zaidi hata ilivyopangwa.
Siyo kwamba CCM ilikuwa haijui kuwa wapiga kura watachukia, lakini kilikwishaujua uwoga wa wapiga kura na kuutumia uwoga huo kukamilisha uovu bila ya hofu yoyote. Walipojifanya kutaka kuandamana, kwa kuutambua uoga wa wapiga kura, kiliitumia vyema hiyo karata. Ikayazima kwa urahisi kabisa.
2) Kutumia mali za Serikali. CCM wakati wote imekuwa ikizitumia rasilimali za serikali kwa manufaa yake bila hofu yoyote. Imeyafanya hayo kwa kuwatambua Watanzania walivyo waoga, wasomi walivyo wanafiki, na wengi wa Watanzania wanavyopenda kusimamia zaidi manufaa ya tumbo kuliko mstakabali wa Taifa lao. Safari wamevuka mipaka, kuna taarifa za uhakika zisizothibitishwa kuwa pesa ya covid 19 na vitambulisho vya mchinga, nayo ilipelekwa kwenye chama kitukufu
3) Mwaka 2015, CCM kwa kumtumia mwenyekiti wake, kinyume kabisa na katiba, ilipiga kabisa marufuku ya mikutano ya vyama vya upinzani, huku Polepole na Bashiru wakipuyanga nchi nzima kufanya mikutano ya CCM kwa kadiri wapendavyo. Kwa msaada wa Jeshi lake la Polisi, hakuna mwananchi wala chama kilichonyanyua pua kupinga kwa namna yoyote ile ya kuitikisa CCM na vyombo vyake
4) Kwa kutumia Polisi waie, iliwakamata na kuwasweka ndani viongozi na wapenzi wa upinzani waliojifanya kukosa sifa ya uoga, nchi nzima. Wote wakaufyata. Iliwatoa ndani kwa namna ilivyotaka.
5) Kwa kutumia wasiojulikana, baadhi walipotezwa, akina Lisu walimimininiwa risasi, wengine kucharangwa mapanga na kupoteza maisha. Hakuna mtuhumiwa wala mshtakiwa. Wote kwa uwoga na unafiki, tukaufyata
6) Kiliamua kuwanyima huduma muhimu wananchi waliochagua upinzani, tena kwa kumtumia mwenyekiti wake, kikatamba waziwazi na kuwaambia wananchi kuwa waliochagua upinzani watakula jeuri yao. Wote kimya. Nani atanyanyuka asiye na sifa ya uoga wa kupoteza maisha au kyozea jela au kufilisiwa kama alivyofanyiwa Mbowe?
7) Sahizi kinaamua kujinyofolea yeyote na kumpa ubunge, na kumbatiza kuwa ni mbunge wa upinzani. CHADEMA wamewafuta uwanachama wale waliotii maelekezo ya CCM ya kutengeneza upinzani bandia bungeni. Lakini mnadhani kutabafilisha chochote? Halima na wenzake wataendelea kuwa wabunge, CCM ikitaka inaweza kuwapa hata uwaziri wa mambo ya ndani ili wakawadhibiti waliowafukuza uwanachama. Nani atanyanyuka na kusema hapana?
8) CCM kwa kutumia serikali na bunge lake, imetengeneza sheria nyingi za kidikteta zinazozuia uhuru wa maoni, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kupata habari. Kwa kutumia serikali yake, inazisimamia hasa. Wote wanajua ni sheria za hovyo, lakini nani wa kunyanyuka. Wanaonyanyuka kidogo, wananlachwa pekee yao waozee mahabusu kama nyumbu wanavyofanya mmojawapo akikamatwa na simba. Yaani wanasema aheri amekamatwa mwenzangu, labda akimla yule atashiba, hatanila tena mimi. Asichojua ni kuwa njaa haiishii kwa kumla nyumbu mmoja leo.
Duniani kuna wanadamu magaidi, kuna vyama magaidi, kuna Serikali magaidi, kuna Polisi magaidi, n.k. Ugaidi msingi wake mkuu ni kumtendea uovu wa kutisha kila anayeenda kinyume nawe ili kumjengea uwoga anayetendewa au kundi linalotendewa.
Leo Tanzania imekuwa nchi ya wananchi waoga, vyama vioga, viongozi wa dini waoga, vyombo vya habari vioga, viongozi wastaafu waoga. CCM sasa imefanikiwa kuwatisha watu na taasisi zote kwa kutumia vyombo vyake.
Kimsingi, CCM ni terrorist party.
Sent using Jamii Forums mobile app
Chama hiki kwa kadiri ya miaka inavyozidi, na aina ya viongozi inaowapata kinazidi kujiimarisha katika uharamia, uovu, ulaghai na mbinu chafu, na katika utekelezaji wa hayo, hufanya kwa ufanisi wa kiwango kilichopitiliza. Kinapotekeleza uharamia wake kinakuwa kimesoma kwa umakini mazingira na aina ya watu kinaowafanyia uharamia, na kutambua wazi matokeo, na madhara yake na jinsi kitakavyokabiliana nayo:
1. Mwaka 2020, kwa namna ya kiwango cha hali ya juu kabisa, kiliweza kujitangazia ushindi wa pekee kwa kuwatumia makada wake waaminifu, Tume ya uchaguzi, wakurugenzi wa Wilaya na jeshi la polisi. Na katika kutekeleza uharamia uliopangwa, hakikuwa na swalia Mtume, aliyeonekana kisiki alikamatwa, aliteswa, wengine wakapoteza hata maisha, na wengine bado wapo ndani. Kwa kutumia Tume ya Uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi, kuna maeneno kilizuia mawakala wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi kutoingia vyumba vya kupigia kura, kuwachelewesha na hata kuwazuia kushuhudia ujumlishaji wa kura. Kwa kutumia Tume ya uchaguzi, kilijitengenezea kura fake, zilizobebwa kwenye mifuko, nyingine zilikamatwa, lakini nyingine zilifanikiwa kuingizwa na kuhesabiwa. Kikajitangazia ushindi ulipitiliza zaidi hata ilivyopangwa.
Siyo kwamba CCM ilikuwa haijui kuwa wapiga kura watachukia, lakini kilikwishaujua uwoga wa wapiga kura na kuutumia uwoga huo kukamilisha uovu bila ya hofu yoyote. Walipojifanya kutaka kuandamana, kwa kuutambua uoga wa wapiga kura, kiliitumia vyema hiyo karata. Ikayazima kwa urahisi kabisa.
2) Kutumia mali za Serikali. CCM wakati wote imekuwa ikizitumia rasilimali za serikali kwa manufaa yake bila hofu yoyote. Imeyafanya hayo kwa kuwatambua Watanzania walivyo waoga, wasomi walivyo wanafiki, na wengi wa Watanzania wanavyopenda kusimamia zaidi manufaa ya tumbo kuliko mstakabali wa Taifa lao. Safari wamevuka mipaka, kuna taarifa za uhakika zisizothibitishwa kuwa pesa ya covid 19 na vitambulisho vya mchinga, nayo ilipelekwa kwenye chama kitukufu
3) Mwaka 2015, CCM kwa kumtumia mwenyekiti wake, kinyume kabisa na katiba, ilipiga kabisa marufuku ya mikutano ya vyama vya upinzani, huku Polepole na Bashiru wakipuyanga nchi nzima kufanya mikutano ya CCM kwa kadiri wapendavyo. Kwa msaada wa Jeshi lake la Polisi, hakuna mwananchi wala chama kilichonyanyua pua kupinga kwa namna yoyote ile ya kuitikisa CCM na vyombo vyake
4) Kwa kutumia Polisi waie, iliwakamata na kuwasweka ndani viongozi na wapenzi wa upinzani waliojifanya kukosa sifa ya uoga, nchi nzima. Wote wakaufyata. Iliwatoa ndani kwa namna ilivyotaka.
5) Kwa kutumia wasiojulikana, baadhi walipotezwa, akina Lisu walimimininiwa risasi, wengine kucharangwa mapanga na kupoteza maisha. Hakuna mtuhumiwa wala mshtakiwa. Wote kwa uwoga na unafiki, tukaufyata
6) Kiliamua kuwanyima huduma muhimu wananchi waliochagua upinzani, tena kwa kumtumia mwenyekiti wake, kikatamba waziwazi na kuwaambia wananchi kuwa waliochagua upinzani watakula jeuri yao. Wote kimya. Nani atanyanyuka asiye na sifa ya uoga wa kupoteza maisha au kyozea jela au kufilisiwa kama alivyofanyiwa Mbowe?
7) Sahizi kinaamua kujinyofolea yeyote na kumpa ubunge, na kumbatiza kuwa ni mbunge wa upinzani. CHADEMA wamewafuta uwanachama wale waliotii maelekezo ya CCM ya kutengeneza upinzani bandia bungeni. Lakini mnadhani kutabafilisha chochote? Halima na wenzake wataendelea kuwa wabunge, CCM ikitaka inaweza kuwapa hata uwaziri wa mambo ya ndani ili wakawadhibiti waliowafukuza uwanachama. Nani atanyanyuka na kusema hapana?
8) CCM kwa kutumia serikali na bunge lake, imetengeneza sheria nyingi za kidikteta zinazozuia uhuru wa maoni, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kupata habari. Kwa kutumia serikali yake, inazisimamia hasa. Wote wanajua ni sheria za hovyo, lakini nani wa kunyanyuka. Wanaonyanyuka kidogo, wananlachwa pekee yao waozee mahabusu kama nyumbu wanavyofanya mmojawapo akikamatwa na simba. Yaani wanasema aheri amekamatwa mwenzangu, labda akimla yule atashiba, hatanila tena mimi. Asichojua ni kuwa njaa haiishii kwa kumla nyumbu mmoja leo.
Duniani kuna wanadamu magaidi, kuna vyama magaidi, kuna Serikali magaidi, kuna Polisi magaidi, n.k. Ugaidi msingi wake mkuu ni kumtendea uovu wa kutisha kila anayeenda kinyume nawe ili kumjengea uwoga anayetendewa au kundi linalotendewa.
Leo Tanzania imekuwa nchi ya wananchi waoga, vyama vioga, viongozi wa dini waoga, vyombo vya habari vioga, viongozi wastaafu waoga. CCM sasa imefanikiwa kuwatisha watu na taasisi zote kwa kutumia vyombo vyake.
Kimsingi, CCM ni terrorist party.
Sent using Jamii Forums mobile app