CCM, Angelina Mabula na Stanslaus Mabula, hizo nyumba zilizouzwa na Jiji la Mwanza zinaenda kuwa ajenda ya kwanza ya wapinzani. Mtatikiswa!

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
11,983
20,634
Rais Samia amefungulia mikutano ya hadhara, na katika majiji ambayo Chadema wanajiwinda kuyadhibiti ni Mwanza, Arusha, Mbeya na Dar es salaam. Wanatafuta ajenda nzito za kutikisa na kuwashika wananchi.

Arusha walifanya tukio, Sasa hivi wote wananyea debe, angalau wanaarusha wanaelewa hatua zimechukuliwa.

Kwa Jiji la Mwanza, Mkurugenzi wa Jiji na maafisa ardhi nao hawajachelewa kuwapa wapinzani ajenda.

Kuna habari kwamba Jiji la mwanza limeuza nyumba zake katikati ya Jiji kwa bei ya kutupa, bila kufuata taratibu.

Maeneo hayo yameuzwa wakati machinga mjini hawana maeneo ya biashara, wameenda kutupwa igoma nyamongolo huko ambako hakuna wateja, na kiloleli, na bila kuzingatia maelekezo ya Rais ya ubia kati ya sekta binafsi na Serikali, kiasi kwamba wangeongea na taasisi yoyote ile au mtu binafsi, akawekeza, wakawa wanakula faida, na eneo likabali lao.

Ni kwamba, wanamwanza wameibiwa.

Stanslaus Mabula, wewe ndio mbunge wa Nyamagana, bila shaka unalijua Jimbo linakuwaga la moto, hasa ukizingatia "sponsor kafa".

Angelina Mabula, wewe ndio Waziri wa hiyo ardhi ya serikali iliyouzwa, na uhamishaji miliki usingefanyika bila kupitia Ofisi za ardhi. Na sijui kwa nini kama mamlaka ya serikali inapotaka kuuza ardhi isitakiwe kupata Kibali Cha Waziri wa Ardhi au Waziri Mkuu! Au Rais! Uwepo udhibiti.

Mna kazi moja tu, kuirudisha ardhi hiyo, hatutaki Rais aanze kupata shida kupata kura za Mwanza wakati alishanyoosha mapito yake kwa miradi mikubwa ya maendeleo.

Ni hapohapo mwanza machinga aliyekuwa anauza ndizi, Jiji lilimwaga ndizi zake na kumpiga, Leo Jiji Lina ardhi hapohapo katikati ya mji linaiuza!

Njia moja tu, kurejesha hizo nyumba, na Kila Afisa aliyehusika apelekwe mahakamani, wanamwanza wataridhika wakiwaona wahusika wanapanda kizimbani, na kupelekwa gereza la Butimba.
 
Rais Samia amefungulia mikutano ya hadhara, na katika majiji ambayo Chadema wanajiwinda kuyadhibiti ni Mwanza, Arusha, Mbeya na Dar es salaam. Wanatafuta ajenda nzito za kutikisa na kuwashika wananchi.

Arusha walifanya tukio, Sasa hivi wote wananyea debe, angalau wanaarusha wanaelewa hatua zimechukuliwa.

Kwa Jiji la Mwanza, Mkurugenzi wa Jiji na maafisa ardhi nao hawajachelewa kuwapa wapinzani ajenda.

Kuna habari kwamba Jiji la mwanza limeuza nyumba zake katikati ya Jiji kwa bei ya kutupa, bila kufuata taratibu.

Maeneo hayo yameuzwa wakati machinga mjini hawana maeneo ya biashara, na bila kuzingatia maelekezo ya Rais ya ubia kati ya sekta binafsi na Serikali, kiasi kwamba wangeongea na taasisi yoyote ile au mtu binafsi, akawekeza, wakawa wanakula faida, na eneo likabali lao.

Ni kwamba, wanamwanza wameibiwa.

Stanslaus Mabula, wewe ndio mbunge wa Nyamagana, bila shaka unalijua Jimbo linakuwaga la moto, hasa ukizingatia "sponsor kafa".

Angelina Mabula, wewe ndio Waziri wa hiyo ardhi ya serikali iliyouzwa, na uhamishaji miliki usingefanyika bila kupitia Ofisi za ardhi. Na sijui kwa nini kama mamlaka ya serikali inapotaka kuuza ardhi isitakiwe kupata Kibali Cha Waziri wa Ardhi au Waziri Mkuu! Au Rais! Uwepo udhibiti.

Mna kazi moja tu, kuirudisha ardhi hiyo, hatutaki Rais aanze kupata shida kupata kura za Mwanza wakati alishanyoosha mapito yake kwa miradi mikubwa ya maendeleo.

Ni hapohapo mwanza machinga aliyekuwa anauza ndizi, Jiji lilimwaga ndizi zake na kumpiga, Leo Jiji Lina ardhi hapohapo katikati ya mji linaiuza!

Njia moja tu, kurejesha hizo nyumba, na Kila Afisa aliyehusika apelekwe mahakamani, wanamwanza wataridhika wakiwaona wahusika wanapanda kizimbani, na kupelekwa gereza la Butimba.
Acha propaganda, hizo nyumba za matope zilizouzwa katikati ya mji ziliuzwa kufuata taratibu zote na order ilitoka ofisi ya rais, wewe kama umelipwa na hilo zee liswahili maneno mengi(adamu malima), na kama hawakumpa fungu la kutosha mwambie kamnofu kalikuwa ni kadogo.
 
Acha propaganda, hizo nyumba za matope zilizouzwa katikati ya mji ziliuzwa kufuata taratibu zote na order ilitoka ofisi ya rais, wewe kama umelipwa na hilo zee liswahili maneno mengi(adamu malima), na kama hawakumpa fungu la kutosha mwambie kamnofu kalikuwa ni kadogo.
Maji mtaita "mma" ajenda ni moja tu, hizo nyumba zirudi, na lazima mkanyee ndoo.

Sheria ya ardhi inatambua kiwanja, sio nyumba ya tope, kilichouzwa ni kiwanja, na kina thamani ya mabilioni kadhaaa
 
Acha propaganda, hizo nyumba za matope zilizouzwa katikati ya mji ziliuzwa kufuata taratibu zote na order ilitoka ofisi ya rais, wewe kama umelipwa na hilo zee liswahili maneno mengi(adamu malima), na kama hawakumpa fungu la kutosha mwambie kamnofu kalikuwa ni kadogo.
Kwahiyo wanashitakiana kwa lipi?
 
Maji mtaita "mma" ajenda ni moja tu, hizo nyumba zirudi, na lazima mkanyee ndoo.

Sheria ya ardhi inatambua kiwanja, sio nyumba ya tope, kilichouzwa ni kiwanja, na kina thamani ya mabilioni kadhaaa
Pale kulikuwa na nyumba au kichuguu, mbona hii ishu umeikomalia sana wewe na RC wako, tunaomba muwasilishe hati miliki ya hiyo ardhi tuliyoiuza.
 
Pale kulikuwa na nyumba au kichuguu, mbona hii ishu umeikomalia sana wewe na RC wako, tunaomba muwasilishe hati miliki ya hiyo ardhi tuliyoiuza.
Sheria ya Ardhi inatambua kiwanja, pale kariakoo Kuna nyumba za tope, tena za miti, lakini waliuza wanauza kiwanja sio nyumba, kiwanja kina-appreciate in value, nyumba Ina depreciate, mtatuambia kama mliuza nyumba au kiwanja.
 
Kwahiyo wanashitakiana kwa lipi?
Ishu ni mgao mkurugenzi alimpa mkuu wa mkoa gawio kidogo, sasa mkuu wa mkoa akakataa kuchukua akijua viwanja hivyo viwili vimeuzwa kwa bei kubwa zaidi kumbe ni bilion moja tu, sasa mkuu wa mkoa ndio akatata kumwaga mboga, na mkurugenzi akasema na yeye atamwaga ugali tena na kuufukia kwa kueleza uozo wote wa hili zee linaloitwa adamu malima
 
Ishu ni mgao mkurugenzi alimpa mkuu wa mkoa gawio kidogo, sasa mkuu wa mkoa akakataa kuchukua akijua viwanja hivyo viwili vimeuzwa kwa bei kubwa zaidi kumbe ni bilion moja tu, sasa mkuu wa mkoa ndio akatata kumwaga mboga, na mkurugenzi akasema na yeye atamwaga ugali tena na kuufukia kwa kueleza uozo wote wa hili zee linaloitwa adamu malima
Kwa hiyo uozo upo au haupo?
 
Sheria ya Ardhi inatambua kiwanja, pale kariakoo Kuna nyumba za tope, tena za miti, lakini waliuza wanauza kiwanja sio nyumba, kiwanja kina-appreciate in value, nyumba Ina depreciate, mtatuambia kama mliuza nyumba au kiwanja.
Tyr tulishauza na sasa kuna project inaendelea, na ukitaka kubishana nenda ofisi ya rais huko ndio tulipata baraka zote.
 
Ishu ni mgao mkurugenzi alimpa mkuu wa mkoa gawio kidogo, sasa mkuu wa mkoa akakataa kuchukua akijua viwanja hivyo viwili vimeuzwa kwa bei kubwa zaidi kumbe ni bilion moja tu, sasa mkuu wa mkoa ndio akatata kumwaga mboga, na mkurugenzi akasema na yeye atamwaga ugali tena na kuufukia kwa kueleza uozo wote wa hili zee linaloitwa adamu malima
Aliyekamatwa na ngozi ndio mwizi, aliyekabidhiwa hizo nyumba ni mkurugenzi, na Saini yake ndio inaonekana katika makaratasi.

Yaani hawa nyuki tumeenda na kiroba katika mzinga, tukawapakia ndani ya kiroba, tukawatumbukizia pilipili kichaa, tunakitikisa kiroba nyuki wapandishe hasira, halafu tunakuja kukifungua kiroba Ofisi za Jiji wawadunge misumari vilivyo
.
Kwa mujibu wa sheria ya serikali za mitaa(The Local Government-Urban Authorities) Act, kifungu Cha 16 nadhani, mkurugenzi alikabidhialwa kiwanja hicho akitunze, yeye kauza na bila kufuata taratibu
 
Hilo ni zee la porojo kila siku linaitisha mkutano kuhusu ujenzi wa airport Mwanza na hakuna kinachofanyika, kazi kuwasagia kunguni wenzio kama vile yeye ni perfect.
Airport hiyo muda si mrefu inafumuliwa, mnajenga airport ndani mnaweka choo Cha shimo, aliyechora airport hajawahi kuchora airport yoyote zaidi ya ramani za vyoo vya manispaa, haijui hata Heathrow Airport anayosema aliigizia ramani, eti anadanlodi ramani ya jengo la airport, nyanoko
 
Aliyekamatwa na ngozi ndio mwizi, aliyekabidhiwa hizo nyumba ni mkurugenzi, na Saini yake ndio inaonekana katika makaratasi.

Yaani hawa nyuki tumeenda na kiroba katika mzinga, tukawapakia ndani ya kiroba, tukawatumbukizia pilipili kichaa, tunakitikisa kiroba nyuki wapandishe hasira, halafu tunakuja kukifungua kiroba Ofisi za Jiji wawadunge misumari vilivyo
.
Kwa mujibu wa sheria ya serikali za mitaa(The Local Government-Urban Authorities) Act, kifungu Cha 23 nadhani, mkurugenzi alikabidhialwa kiwanja hicho akitunze, yeye kauza na bila kufuata taratibu
Nenda kaangalie master plan ya jiji eneo hilo linapaswa pawepo na nini? Na pia hiyo sehemu kawauzia wawekezaji ili wafiate hiyo master plan.... Nashangaa unakuja na hoja eti ilo eneo mara machinga hawana eneo, shenxy type.. Unataka kila sehemu hiwe na machinga?
 
Back
Top Bottom