RockCarnegie
JF-Expert Member
- Jan 17, 2019
- 963
- 1,927
Habari wana JF!
Chama cha siasa ni itikadi ya ushawishi kwa wananchi ili kiweze kuungwa mkono na kupewa uongozi wa nchi kwa njia za kidemokrasia!
Chama cha Mapinduzi kilitarajiwa kuwa kisima cha maarifa, fikra na hoja za kujenga taifa la watu wamoja na waliostaarabika!
Badala yake CCM imegeuka kuwa genge la watu wa kulindwa kwa mtutu wa bunduki kama ilivyonukuliwa ƙwa mwenyekiti wake akijinadi kuwa majeshi yapo kwa maslahi mapana ya CCM!
Maneno ya RPC Arusha kuwa wana CCM hawana sababu ya kulialia kwa kuwa wao ni dola yalikuwa si ƴa bahati mbaya, ndiyo maana walisikika na kuonekana wakishangilia kauli ile, wakisahau kuwa kutegemea majeshi ni kujinyima fursa ya kujielimisha ili uwe na maarifa ya kushawishi watu kwa hoja na si kwa mabavu!
Chama kinapobakiza wapiga kelele kama Musiba, Lusinde na Musukuma, wakijinadi kuwa ni watetezi wa mwenyekiti wa chama chao, ujue chama hicho kimeshakufa! Kwani mwenyekiti wao amegeuka kinɗa la ndege linaloogopa kunƴakuliwa na mwewe!?
CCM ya JPM imejaa hofu, haina sera wala itikadi. Haina maarifa wala fikra! Inaona maadui kila mahali! Vitisho na uƙatili ndiyo mbinu pekee iliyobaki kulazimisha watu wakiunge mkono!
CCM ya JPM, Musiba, Lusinde na Musukuma si salama tena! Iachwe ife ili Watanzania wapone!
Chama cha siasa ni itikadi ya ushawishi kwa wananchi ili kiweze kuungwa mkono na kupewa uongozi wa nchi kwa njia za kidemokrasia!
Chama cha Mapinduzi kilitarajiwa kuwa kisima cha maarifa, fikra na hoja za kujenga taifa la watu wamoja na waliostaarabika!
Badala yake CCM imegeuka kuwa genge la watu wa kulindwa kwa mtutu wa bunduki kama ilivyonukuliwa ƙwa mwenyekiti wake akijinadi kuwa majeshi yapo kwa maslahi mapana ya CCM!
Maneno ya RPC Arusha kuwa wana CCM hawana sababu ya kulialia kwa kuwa wao ni dola yalikuwa si ƴa bahati mbaya, ndiyo maana walisikika na kuonekana wakishangilia kauli ile, wakisahau kuwa kutegemea majeshi ni kujinyima fursa ya kujielimisha ili uwe na maarifa ya kushawishi watu kwa hoja na si kwa mabavu!
Chama kinapobakiza wapiga kelele kama Musiba, Lusinde na Musukuma, wakijinadi kuwa ni watetezi wa mwenyekiti wa chama chao, ujue chama hicho kimeshakufa! Kwani mwenyekiti wao amegeuka kinɗa la ndege linaloogopa kunƴakuliwa na mwewe!?
CCM ya JPM imejaa hofu, haina sera wala itikadi. Haina maarifa wala fikra! Inaona maadui kila mahali! Vitisho na uƙatili ndiyo mbinu pekee iliyobaki kulazimisha watu wakiunge mkono!
CCM ya JPM, Musiba, Lusinde na Musukuma si salama tena! Iachwe ife ili Watanzania wapone!