CCM 2020 itaangushwa na Hali ngumu ya maisha tuliyonayo wananchi wa kawaida Chadema itakuwa ni Sabab

Lancashire

JF-Expert Member
Sep 20, 2014
14,045
10,329
Habari za Jumapili mabibi na mabwana.
Kwanza kabla ya yote ningependa Ku declare interest kwamba Mimi bado ni muumini wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na changamoto nyingi ninazopitia kutokana na baadhi ya matendo yasiyo yakuridhishwa yanayofanywa na Chama Changu.

Kama heading inavyojieleza nauona mwaka 2020 kama kaburi la chama changu huku nikizingatia wanachama wengi tunaoipitisha CCM huku mashinani ndio sisi tunaoisoma namba kwa sasa kutokana na hali ngumu sana ya kimaisha tunayoipitia.

Ni kweli kabisa serikali inatekeleza miradi mbali mbali kama ujenzi wa Kiwanja cha kimataifa cha Chato, ununuzi wa Boeing na bombardier na sasa tunaanza ujenzi wa reli ya kisasa.bila kusahau kuhamia Dodoma.
Lakini nikitafakari kwa undani haya yote hayamsaidii mwananchi wa kawaida huku kijijini ambako kwa sasa kilo ya sukari ni 2800 mpaka 3000 kunywa chai ni anasa. Kilo ya unga wa sembe ni 2000 hadi 2200, bei za bidhaa sokoni zimepanda kuliko wakati wowote ule.
Biashara ndogo ndogo ambazo wengi hutegemea kwa kipato na kujiendesha kimaisha zimekwama hakuna wateja, TRA wanadai kodi tumeishia kufunga. Sasa natafakari kwa kina mwisho utakuwaje. Jibu ni rahisi sana Wengi tutatafuta mbadala wa kutusaidia na hakutakua na mwingine zaidi ya Chadema chama kikuu cha Upinzani.
Nisingependa iwe hivyo lakini hakutakuwa na namna. Hapo mengi sana sijayaongelea ila kwa kifupi haya ndio nilitaka kukitahadharisha chama change ili hatua za dharura zichukuliwe mapema kuokoa uchumi wa nchi hii ambao unaelekea shimoni.

Wasalaam.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
 
Subiri wenzako waje mjadili.
Ungetaja kijiji ulichotembelea na kuweka bei ya mjini pia unapoisi tuone.

Wengine na mie ni tunaopenda viongozi wawili watatu kizaidi awamu hii....napita kimya kimya.
 
Kuna kitu ambacho haukijui mleta uzi,
Kwanza ni kweli unga na sukari vimepanda bei, hali hii imesababiswa na nini? Elezea angalau kwa kifupi ili tupate cha kujadiri
Kuzuia importation ya sukari toka nje ,so maamuzi ya Mzee Wa chato ndo tatizo
 
Uko sahihi mkuu, wanadhani ni utani na wanadhani TISSS, polisi na tume vitawasaidia lakini ushindi unaweza kua wa kishindo kwa hasira za wananchi mpaka watashindwa kuiba wataona aibu.
 
Uko sahihi mkuu, wanadhani ni utani na wanadhani TISSS, polisi na tume vitawasaidia lakini ushindi unaweza kua wa kishindo kwa hasira za wananchi mpaka watashindwa kuiba wataona aibu.
 
Uko sahihi mkuu, wanadhani ni utani na wanadhani TISSS, polisi na tume vitawasaidia lakini ushindi unaweza kua wa kishindo kwa hasira za wananchi mpaka watashindwa kuiba wataona aibu.
 
Ukawa anzisheni mfuko wa uchaguzi mapema..wasimamizi uchaguzi walipwe stahiki zao mapema..CCM 2020 ndembendembe kifo cha mende
 
Subiri wenzako waje mjadili.
Ungetaja kijiji ulichotembelea na kuweka bei ya mjini pia unapoisi tuone.

Wengine na mie ni tunaopenda viongozi wawili watatu kizaidi awamu hii....napita kimya kimya.
Imepenya hiyo.jamaa kalenga mulemule
 
Kuna kitu ambacho haukijui mleta uzi,
Kwanza ni kweli unga na sukari vimepanda bei, hali hii imesababiswa na nini? Elezea angalau kwa kifupi ili tupate cha kujadiri
Siyo kila kitu utafuniwe mleta mada ameeleza kwa ufupi.mshauri aandike makala kwenye gazeti usome vizuri.
 
Habari za Jumapili mabibi na mabwana.
Kwanza kabla ya yote ningependa Ku declare interest kwamba Mimi bado ni muumini wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na changamoto nyingi ninazopitia kutokana na baadhi ya matendo yasiyo yakuridhishwa yanayofanywa na Chama Changu.

Kama heading inavyojieleza nauona mwaka 2020 kama kaburi la chama changu huku nikizingatia wanachama wengi tunaoipitisha CCM huku mashinani ndio sisi tunaoisoma namba kwa sasa kutokana na hali ngumu sana ya kimaisha tunayoipitia.

Ni kweli kabisa serikali inatekeleza miradi mbali mbali kama ujenzi wa Kiwanja cha kimataifa cha Chato, ununuzi wa Boeing na bombardier na sasa tunaanza ujenzi wa reli ya kisasa.bila kusahau kuhamia Dodoma.
Lakini nikitafakari kwa undani haya yote hayamsaidii mwananchi wa kawaida huku kijijini ambako kwa sasa kilo ya sukari ni 2800 mpaka 3000 kunywa chai ni anasa. Kilo ya unga wa sembe ni 2000 hadi 2200, bei za bidhaa sokoni zimepanda kuliko wakati wowote ule.
Biashara ndogo ndogo ambazo wengi hutegemea kwa kipato na kujiendesha kimaisha zimekwama hakuna wateja, TRA wanadai kodi tumeishia kufunga. Sasa natafakari kwa kina mwisho utakuwaje. Jibu ni rahisi sana Wengi tutatafuta mbadala wa kutusaidia na hakutakua na mwingine zaidi ya Chadema chama kikuu cha Upinzani.
Nisingependa iwe hivyo lakini hakutakuwa na namna. Hapo mengi sana sijayaongelea ila kwa kifupi haya ndio nilitaka kukitahadharisha chama change ili hatua za dharura zichukuliwe mapema kuokoa uchumi wa nchi hii ambao unaelekea shimoni.

Wasalaam.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Nimenunua Kiroba cha sukari kg 25 kwa 65000/=
 
Magufonga ameshatuharibia chama alianza vzr tukaamin atafanya vzr kuliko watanguliz wake lkn matokeo yake yy ndio kaharibu kuliko wenzie woote ndan ya miaka miwili amepoteza mvuto kisiasa sio wafanyakaz wakulima wala wafanyabiashara wakubwa\wadogo woote ameshatuvuruga yaan huyu mtu 2020 kaz anayo
 
Back
Top Bottom