Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,116
CHAMA Cha Jamii (CCJ), jana kilishindwa kuwasilisha kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, maombi ya usajili wa kudumu na kitendo hicho sasa kitafanyika mapema wiki ijayo.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi, taratibu zote kuhusu maombi hayo zimekamilika.
Alisema taratibu hizo ni pamoja na chama kufanikiwa kupata zaidi ya wanachama 10,000 idadi ambayo alisema imevuka ile iliyotakiwa na msajili, ya wanachama 200.
Muabhi alisema walikuwa wamepanga kuwasilisha maombi hayo jana, lakini yeye alikuwa safarini kwenda mkoani Dodoma na mwenyekiti wake alikuwa anakwenda Zanzibar.
Msajili Msaidizi wa vyama vya Saisa, Ibrahim Kiyabo, alisema hadi jana kufikia saa 5:00 asubuhi, alikuwa hajapokea maombi hayo kutoka katika chama hicho chenye usajili wa muda.
Ilidaiwa kuwa CCJ ilichukua fomu ya usajili wa kudumu, wiki iliyopita na kutangaza kuwa jana kingewasilisha rasmi maombi yake ya usajili wa kudumu, ambao hadi sasa umeingia wa mashaka.
Hali hiyo inatokana na Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, kutangaza mpango wa kuanza uchunguzi ili kuona kama kilianza shughuli za kisiasa miaka miwili iliyopita au la.
Tendwa aliipa CCJ usajili wa muda Machi 2 mwaka huu na kuitaka ihakikishe kuwa ndani ya miezi sita kiwe imepata wanachama 200 kutoka mikoa kumi ya bara na kisiwani.
Hata hivyo, CCJ imetumia muda wa takribani miezi miwili kukamilisha kazi hiyo, jambo ambalo linajenga shaka kuwa huenda ilianza kupata wanachama kabla ya kupata usajili wa muda, hatua ambayo Tendwa alisema ni kinyume na sheria na kwa kufanya hivyo kinaweza kufutwa kabisa.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/5-habari-za-siasa/1433-ccj-yakwama-kuwasilisha-maombi
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi, taratibu zote kuhusu maombi hayo zimekamilika.
Alisema taratibu hizo ni pamoja na chama kufanikiwa kupata zaidi ya wanachama 10,000 idadi ambayo alisema imevuka ile iliyotakiwa na msajili, ya wanachama 200.
Muabhi alisema walikuwa wamepanga kuwasilisha maombi hayo jana, lakini yeye alikuwa safarini kwenda mkoani Dodoma na mwenyekiti wake alikuwa anakwenda Zanzibar.
Msajili Msaidizi wa vyama vya Saisa, Ibrahim Kiyabo, alisema hadi jana kufikia saa 5:00 asubuhi, alikuwa hajapokea maombi hayo kutoka katika chama hicho chenye usajili wa muda.
Ilidaiwa kuwa CCJ ilichukua fomu ya usajili wa kudumu, wiki iliyopita na kutangaza kuwa jana kingewasilisha rasmi maombi yake ya usajili wa kudumu, ambao hadi sasa umeingia wa mashaka.
Hali hiyo inatokana na Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, kutangaza mpango wa kuanza uchunguzi ili kuona kama kilianza shughuli za kisiasa miaka miwili iliyopita au la.
Tendwa aliipa CCJ usajili wa muda Machi 2 mwaka huu na kuitaka ihakikishe kuwa ndani ya miezi sita kiwe imepata wanachama 200 kutoka mikoa kumi ya bara na kisiwani.
Hata hivyo, CCJ imetumia muda wa takribani miezi miwili kukamilisha kazi hiyo, jambo ambalo linajenga shaka kuwa huenda ilianza kupata wanachama kabla ya kupata usajili wa muda, hatua ambayo Tendwa alisema ni kinyume na sheria na kwa kufanya hivyo kinaweza kufutwa kabisa.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/5-habari-za-siasa/1433-ccj-yakwama-kuwasilisha-maombi