Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Chama cha Jamii kikiendelea kuonesha dhamiri yake ya kutokukubali kusukumwa pembeni kimetangaza jana baadhi tu ya ajenda zake ambazo ndio kiini cha kuwekewa mizengwe ya kupata usajili wa kudumu. Pamoja na ajenda hizo za siku 100 za kwanza na mwaka mmoja wa kwanza wa wabunge wake CCJ vile vile inandaa maandamano ya wanachama wake na pamoja na hayo imeandika barua kali kwenda kwa mabalozi kuelezea jinsi serikali ya CCM imekuwa ikiunyanyasa mchakato wa demokrasia tangu kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini mwaka 1992.
Ajenda hiyo kali ambayo imegawanywa katika mafungu mbalimbali ikiwemo ya kisheria (legislative) na ya kiutendaji (executive) ina lengo la kuanzisha mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala na utendaji nchini. Kuvuja kwa taarifa za ajenda hiyo tangu kuanza kwa CCJ ndiko kunakotajwa kulisababisha CCM na vyombo vyake kuapa kamwe CCJ isipate usajili wa kudumu kwani ajenda hiyo haiwezi kukubaliwa na CCM kwani ndiyo ajenda pekee itakayoweza kukingoa Chama cha Mapinduzi madarakani.
Pamoja na hayo, CCJ inapanga kuhoji uwezo wa msajili kuuliza kadi za uanachama kwani hakuna mahali popote katika sheria ya vyama vya siasa ambapo panataka mwanachama wa chama cha siasa kuwa na kadi ili ajitambulishe kuwa ni mwanachama. Masharti ya kupewa usajili wa kudumu kwa mujibu wa sheria hiyo hayahitaji wanachama wawe na kadi ya vyama ili kutambulisha uanachama wao kwani wanatakiwa kutimiza tu masharti ya kuweza kupiga kura - na katika hayo hakuna lenye kutaka wapiga kura wawe na kadi.
Hii ndiyo sababu mwanzoni tulisema kuwa uanachama wa CCJ ni wa itikadi na wa kadi! Kama ilivyo katika nchi nyingi za kidemokrasia kukubaliana na imani, malengo na mtazamo wa chama fulani cha kisiasa kunamfanya mtu kujitambua kuwa ni mwanachama wa chama hicho na ana haki ya kukitetea na kushiriki shughuli zake. Hii haimlazimishi kuwa na kadi.
Matakwa ya kuwa na kadi ili kumridhisha msajili ni kinyume na katiba ambayo inatakataza kulazimisha watu kujiunga na vyama - kwa kutaka wawe na kadi msajili analazimisha watu wawe kwenye vyama! Alichotakiwa kufanya ni kukubali orodha aliyopewa na kukubali wananchi wenyewe wanapojitambulisha kuwa ni wanachama wa CCJ na kuwa majina yao yako kwenye orodha hiyo.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo hoja hii ya mwisho ina lengo la kupindua kabisa nafasi na majukumu ya msajili wa vyama kwani amejipa uwezo asiokuwa nao na yaweza kuwa msingi wa kesi ya kikatiba huko mbeleni.
AGENDA ZA SIKU 100 ZA KWANZA NA MWAKA MMOJA WA KWANZA:
Kisheria:
- Kuleta mswada wa mabadiliko ya sheria mbalimbali nchini ambazo zimekuwa kikwazo cha mabadiliko ya kweli. Baadhi tu ya sheria ambazo CCJ italeta Bungeni ili kuzifuta au kuzifanyia mabadiliko makubwa ni pamoja na
- Kuanzisha mazungumzo ya utaratibu wa kuanza mchakato wa uandishi mpya wa Katiba yetu ili hatimaye kuondoa kero za Muungano, kuimarisha taifa letu, na hatimaye kutengeneza utaratibu bora, wa wazi na uwajibakaji na kusimamiana katika utawala wa taifa letu. Katika hili CCJ inakusudia kupunguza idadi ya wabunge ikiwemo kufuta ubunge wa kuteuliwa au wa kupewa na Rais na kuanzisha chemba ya juu ya Bunge ili Bunge letu liwe na sehemu mbili bicameral. Kuandika Katiba yetu upya ni ajenda kuu zaidi kwa CCJ na itaanza utaratibu ndani ya mwaka mmoja na kuhakikisha inakamilika ili uchaguzi mkuu mpya unafanyika chini ya Katiba Mpya.
-
Kiutendaji:
Serikali ya CCJ itachukua hatua kadhaa za kiutendaji ili kurudisha uwazi, uwajibikaji na uadilifu serikali bila kumuonea mtu, upendeleo, woga au jambo lolote lenye kuonesha uonevu. Baadhi TU ya hatua hizo ni pamoja na:
- Kuanzisha Mahakama Maalum ya Wahujumu Uchumi kwa mujibu wa sheria ya Mitandao ya Uhalifu na Wahujumu Uchumi ya 1984. Katika hili CCJ haitamwogopa mtu yeyote awe ni kiongozi wa wakati huu au wa huko nyuma ambaye amehusika kwenye vitendo vya kulihujumu taifa hili. Wale wote ambao wameshiriki katika kudhulumu utajiri na jasho la Watanzania watasimamishwa kujibu mashtaka dhidi yao bila uonevu, katika uwazo na haki yote. Tuko tayari kushirikiana na taasisi za kimataifa kuwafikisha wahusika wote kizimbani.
- Pamoja na hilo hapo juu CCJ itaanzisha uchunguzi wa viongozi na watendaji mbalimbali wa serikali ambao wanatuhumiwa au kuna sababu ya kuamini wanahusika katika kutumia madaraka yao vibaya kujitajirisha au kuficha mabilioni ya fedha ya nchi. Katika hili kila senti iliyochukuliwa pasipo uhalali kutoka kwa walipa kodi wa nchi yetu tuipendayo itarudishwa nchini bila kujali ni nani ameificha na wapi imefichwa. Tayari tuna uhusiano na watu mbalimbali ambao wanazo taarifa za viongozi na watendaji hao.
- Kuvunja Bodi ya Mikopo ya Elimu (pamoja na kufanyia mabadiliko ya sheria yao) ili hatimaye tuunde chombo kilicho huru, cha haki na cha uwezo ambacho kitasimamia mikopo ya wanafunzi nchini ili kuhakikisha hakuna kijana wa Kitanzania ambaye hapati elimu kwa sababu tu hana fedha. Katika hili tutawafanyia uchunguzi watumishi wote wa bodi hiyo ili kuhakikisha hawajatumia nafasi zao kujinufaisha wao nje ya taratibu za kisheria. Katika hili hatuna mapatano.
- Kufanya mabadiliko makubwa katika jeshi la Polisi kwa kubadili mfumo na muundo wake ili kulifanya liwe jeshi jepesi, la haraka, makini, la kisasa na lenye uwezo wa kushughulia uhalifu wa aina zote kwa utaalamu na weledi wa juu na kulibadilisha ndani ya miaka mitano kuwa Jeshi bora zaidi la Polisi katika Afrika nzima. Tunao wataalamu wenye kutushauri juu ya jambo hili.
na mengine kadhaa ambayo hakuna chama kingine cha upinzani kinaweza kuyapigania bila kujiuma meno.
Ajenda hiyo kali ambayo imegawanywa katika mafungu mbalimbali ikiwemo ya kisheria (legislative) na ya kiutendaji (executive) ina lengo la kuanzisha mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala na utendaji nchini. Kuvuja kwa taarifa za ajenda hiyo tangu kuanza kwa CCJ ndiko kunakotajwa kulisababisha CCM na vyombo vyake kuapa kamwe CCJ isipate usajili wa kudumu kwani ajenda hiyo haiwezi kukubaliwa na CCM kwani ndiyo ajenda pekee itakayoweza kukingoa Chama cha Mapinduzi madarakani.
Pamoja na hayo, CCJ inapanga kuhoji uwezo wa msajili kuuliza kadi za uanachama kwani hakuna mahali popote katika sheria ya vyama vya siasa ambapo panataka mwanachama wa chama cha siasa kuwa na kadi ili ajitambulishe kuwa ni mwanachama. Masharti ya kupewa usajili wa kudumu kwa mujibu wa sheria hiyo hayahitaji wanachama wawe na kadi ya vyama ili kutambulisha uanachama wao kwani wanatakiwa kutimiza tu masharti ya kuweza kupiga kura - na katika hayo hakuna lenye kutaka wapiga kura wawe na kadi.
Hii ndiyo sababu mwanzoni tulisema kuwa uanachama wa CCJ ni wa itikadi na wa kadi! Kama ilivyo katika nchi nyingi za kidemokrasia kukubaliana na imani, malengo na mtazamo wa chama fulani cha kisiasa kunamfanya mtu kujitambua kuwa ni mwanachama wa chama hicho na ana haki ya kukitetea na kushiriki shughuli zake. Hii haimlazimishi kuwa na kadi.
Matakwa ya kuwa na kadi ili kumridhisha msajili ni kinyume na katiba ambayo inatakataza kulazimisha watu kujiunga na vyama - kwa kutaka wawe na kadi msajili analazimisha watu wawe kwenye vyama! Alichotakiwa kufanya ni kukubali orodha aliyopewa na kukubali wananchi wenyewe wanapojitambulisha kuwa ni wanachama wa CCJ na kuwa majina yao yako kwenye orodha hiyo.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo hoja hii ya mwisho ina lengo la kupindua kabisa nafasi na majukumu ya msajili wa vyama kwani amejipa uwezo asiokuwa nao na yaweza kuwa msingi wa kesi ya kikatiba huko mbeleni.
AGENDA ZA SIKU 100 ZA KWANZA NA MWAKA MMOJA WA KWANZA:
Kisheria:
- Kuleta mswada wa mabadiliko ya sheria mbalimbali nchini ambazo zimekuwa kikwazo cha mabadiliko ya kweli. Baadhi tu ya sheria ambazo CCJ italeta Bungeni ili kuzifuta au kuzifanyia mabadiliko makubwa ni pamoja na
- Sheria ya Magazeti ya 1976
- Sheria ya Madaraka ya Rais wakati wa Dharura ya 1986
- Sheria ya vyama vya siasa ili kuweka tume huru ya uchaguzi na hatimaye kuruhusu wagombea binafsi
- Sheria ya Usalama wa Taifa ili kujenga idara mpya ya usalama wa taifa isiyofanya kazi kisiasa.
- Kuanzisha mazungumzo ya utaratibu wa kuanza mchakato wa uandishi mpya wa Katiba yetu ili hatimaye kuondoa kero za Muungano, kuimarisha taifa letu, na hatimaye kutengeneza utaratibu bora, wa wazi na uwajibakaji na kusimamiana katika utawala wa taifa letu. Katika hili CCJ inakusudia kupunguza idadi ya wabunge ikiwemo kufuta ubunge wa kuteuliwa au wa kupewa na Rais na kuanzisha chemba ya juu ya Bunge ili Bunge letu liwe na sehemu mbili bicameral. Kuandika Katiba yetu upya ni ajenda kuu zaidi kwa CCJ na itaanza utaratibu ndani ya mwaka mmoja na kuhakikisha inakamilika ili uchaguzi mkuu mpya unafanyika chini ya Katiba Mpya.
-
Kiutendaji:
Serikali ya CCJ itachukua hatua kadhaa za kiutendaji ili kurudisha uwazi, uwajibikaji na uadilifu serikali bila kumuonea mtu, upendeleo, woga au jambo lolote lenye kuonesha uonevu. Baadhi TU ya hatua hizo ni pamoja na:
- Kuanzisha Mahakama Maalum ya Wahujumu Uchumi kwa mujibu wa sheria ya Mitandao ya Uhalifu na Wahujumu Uchumi ya 1984. Katika hili CCJ haitamwogopa mtu yeyote awe ni kiongozi wa wakati huu au wa huko nyuma ambaye amehusika kwenye vitendo vya kulihujumu taifa hili. Wale wote ambao wameshiriki katika kudhulumu utajiri na jasho la Watanzania watasimamishwa kujibu mashtaka dhidi yao bila uonevu, katika uwazo na haki yote. Tuko tayari kushirikiana na taasisi za kimataifa kuwafikisha wahusika wote kizimbani.
- Pamoja na hilo hapo juu CCJ itaanzisha uchunguzi wa viongozi na watendaji mbalimbali wa serikali ambao wanatuhumiwa au kuna sababu ya kuamini wanahusika katika kutumia madaraka yao vibaya kujitajirisha au kuficha mabilioni ya fedha ya nchi. Katika hili kila senti iliyochukuliwa pasipo uhalali kutoka kwa walipa kodi wa nchi yetu tuipendayo itarudishwa nchini bila kujali ni nani ameificha na wapi imefichwa. Tayari tuna uhusiano na watu mbalimbali ambao wanazo taarifa za viongozi na watendaji hao.
- Kuvunja Bodi ya Mikopo ya Elimu (pamoja na kufanyia mabadiliko ya sheria yao) ili hatimaye tuunde chombo kilicho huru, cha haki na cha uwezo ambacho kitasimamia mikopo ya wanafunzi nchini ili kuhakikisha hakuna kijana wa Kitanzania ambaye hapati elimu kwa sababu tu hana fedha. Katika hili tutawafanyia uchunguzi watumishi wote wa bodi hiyo ili kuhakikisha hawajatumia nafasi zao kujinufaisha wao nje ya taratibu za kisheria. Katika hili hatuna mapatano.
- Kufanya mabadiliko makubwa katika jeshi la Polisi kwa kubadili mfumo na muundo wake ili kulifanya liwe jeshi jepesi, la haraka, makini, la kisasa na lenye uwezo wa kushughulia uhalifu wa aina zote kwa utaalamu na weledi wa juu na kulibadilisha ndani ya miaka mitano kuwa Jeshi bora zaidi la Polisi katika Afrika nzima. Tunao wataalamu wenye kutushauri juu ya jambo hili.
na mengine kadhaa ambayo hakuna chama kingine cha upinzani kinaweza kuyapigania bila kujiuma meno.