Uchaguzi 2020 CASE STUDY - Jimbo la Hai - Walitumia teknolojia gani kupata matokeo sahihi ya kila kituo ndani ya saa 8?

Waulize maana watapewa tu.

Simply ni neno la kilatini, meaning; "a place to stand", yaani malalamiko yako mahakamani yana "base" kwenye nini.
Me Naelewaaa Mkuu... Mara nyingi kwenye kila kesi huwa tunaangalia je parties wana locus stand au wamedandia tu gari kwa mbele
 
Hatua nyingi Sanaa Mkuu.....
-Kwenda jumuiyaa za kimataifa..
-Maandamano ya Aman.. tena yangefanikiwa maan watu walikuwa na morale kubwa sanaa
-kufungua pingamizi mahakaman n.k
Maandamano ya amani katika kipindi kipi ?

Kwenda kwenye jumuiya za kimataifa kufanya nini ?
 
Hatua nyingi Sanaa Mkuu.....
-Kwenda jumuiyaa za kimataifa..
-Maandamano ya Aman.. tena yangefanikiwa maan watu walikuwa na morale kubwa sanaa
-kufungua pingamizi mahakaman n.k
Kufungua pingamizi mahakamani dhidi ya nini mkuu ?
 
Maandamano ya amani katika kipindi kipi ?

Kwenda kwenye jumuiya za kimataifa kufanya nini ?
Maandamano ya Aman kushinikiza tume huru kabla ya uchaguzi Mkuu.....
Kuomba jumuiya za kimataifa kushinikiza kuwepo kwa tume huru
 
kutokuwa na iman na tume....
Mahakamani huwa hatuendi kwa hisia tunaenda kwa facts.

Kukumbusha tu mahakamani tumepeleka kesi mbili moja ni kupinga wakurugenzi wa wilaya kuwa wasimamizi wa uchaguzi mahakama kuu ilikubali ombi letu ila mahakama ya rufaa ikaruhusu wakurugenzi kusimamia uchaguzi.

Mpaka hapo mlango wa mahakama tulishapita na tukagonga mwamba.
 
Maandamano ya Aman kushinikiza tume huru kabla ya uchaguzi Mkuu.....
Kuomba jumuiya za kimataifa kushinikiza kuwepo kwa tume huru
Mkuu maandamano huwezi kuyaamsha tu there must be a cause.

Platform ya uchaguzi huu imetupatia hiyo cause kwa uwazi kwa kila mtu.

Kuhusu jumuiya za kimataifa Uchaguzi ni internal affairs ndiyo maana mashinikizo yoyote hayawezi kutolewa zaidi ya matamko ya kibalozi tu.
 
Mahakamani huwa hatuendi kwa hisia tunaenda kwa facts.

Kukumbusha tu mahakamani tumepeleka kesi mbili moja ni kupinga wakurugenzi wa wilaya kuwa wasimamizi wa uchaguzi mahakama kuu ilikubali ombi letu ila mahakama ya rufaa ikaruhusu wakurugenzi kusimamia uchaguzi.

Mpaka hapo mlango wa mahakama tulishapita na tukagonga mwamba.
mkuu... ishu ni kwamba hakuna mahakama ya bongo ya kuiamin...
Hapa ni kama Rev mtikila case ya 2011 tunaenda African court tunapeleka pingamizi letu na facts mahakama ya africa itaamua...
Maamuzi yake sawaa sio binding kwa Tanzania ila yatabind karibia commission zote ambazo zitakuja kuangalia uchaguzi....
After Hizo commission za SADC,EAC na Au hawawez kusema uchaguzi ni wa huru na haki kama maamuzi ya african court hayajafatwa....
hii itakua ni hatua moja ya kuelekea demokrasia....
Tanzania italizimika ku domesticate yale maamuzi ili kulinda heshima yake kimataifa
 
Hayo matokeo ya vituoni hayakutumika kwenye majumuisho
Nilikuwa naongea na baba. Yeye alikuwa mwenyekiti wa TANU wa wilaya. Aliniambia mambo ya kutafakarisha sana. Alisema kuwa Magufuli alikuja na CCM mpya. Alipoingia nadarakani hakuwa anatambua Chama. Alikuwa anaita Serikali ya Magufuli badala ya Serikali ya CCM. Mbele kidogo pale tukaona Wazee wa CCM wanatiwa msukosuko. Mzee Yusufu Makamba, mzee Abd. Kinana, Nape, Januari na wengine waliokuwa nguzo za Chama wakatiwa msukosuko. Baadaye tukamsikia akisema kwa wazi kuwa Viongozi waliomtangulia yeye hakuna walichofanya. Tuliona Mzee Mkapa akilipinga hilo kwa nguvu na wazi. Hata mzee Kijwete amelipinga hilo wazi. Lakini jina hili la CCM MPYA limetumika marakwa mara.
Hii ni ccm ya akina Bashiru na kina Polepole. Ni ccm isiyo na maadili wala isiyozingatia itikadi yake ya awali. Si ya kijamaa wala ya kibepari. Ni ccm inayotumia nguvu badala ya hoja. Hata hekima ya kawaida tu ccm hii mpya haina. Magufuli anasema, "Wewe mkurugenzi, ukiwa msimamizi wa uchaguzi siwezi kuwa nakupa mshahara, gari , nyumba na narupurupu mengine alafu umtangaze mpinzani eti kashinda uchaguzi!" Maneno haya usingesikia yakitoka kwa Wazee wale wa namna ya Makamba wala Kinana. Walikuwa viongozi wa chama chenye hekima na maarifa. Bashiru alisema wazi kuwa ccm itatumia vyombo vya dola kubaki madarakani. Loh! Hiyo ndoyo hekima ya ccm hii mpya.
Mara tukaona utamaduni mpya wa ccm hii mpya kwenye uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa mwaka jana. Mzengwe ulifanywa na wagombea wa upinzani wakaenguliwa wote. Tulikuwa hatujui kwa kumbe huo ndio utamaduni wa ccm mpya. Imedhihirika kwenye uchaguzi mkuu huu kuwa ccm hii inataka kushinda kwa mabavu, hila, na unyanganyi. Tuliona watia nia wa upinzani wakitekwa na kunyanganywa fomu ili wasirudishe. Tuliona wengine wakitiwa ndani kwa kutumia polisi na hata takukuru ilitumika. Tuliona uenguaji wa kimkakati wa wagombea wa upinzani kwa kutumia NEC ambapo kila mwenye macho yanayoona aliona mkakati wa ccm mpya wa kushinda uchaguzi nje ya sanduku la kura. Kampeni zilidhihirisha nia hii ya ccm mpya. Hakuna kwa wapinzani kutumia vyombo vya habari vya umma wala vya binafsi. Hakuna wapinzani kubandika mabango ya wagombea uraisi popote. Wagombea wa upinzani walipewa adhabu ya kutokufanya kampeni kwa makosa ambayo wale wa ccm mpya walifanya na wao hawakuguswa.
Lakini uchaguzi kama huu haujaonekana miaka ya nyuma. Makaratasi ya kura zilizopigwa yalikamatwa kwa maelfu sehemu mbalimbali. Mwisho hata Kanuni ya majumuisho haikufuatwa. Ilikuwa ni kujaza idadi ya kufikirika na kutangaza mshindi kwa kuwa mawakala wa upinzani walifukuzwa.
Mwisho mzee yule alisema kuwa kama hali hii itaachwa kuendelea, yaani kama hakuna hatua yoyote itakayochukuliwa kwa heri ama kwa shari kukomesha utamaduni wa kundi hili wa kushinda kwa kupora kura, huu utakuwa mwanzo wa mwisho wa taifa zuri la Tanzania tuliyoipenda. Utakuwa mwisho wa demokrasia kwa nchi yetu.
 
Ndio tumesha mchinja kwa hooks na kelele zako hazita saidia
Jimbo la uchaguzi la HAI liko mkoa wa Kilimanjaro. Ni jimbo ambalo "the most wanted person" na watawala wa CCM, mwenyekiti wa taifa wa chama kikuu cha upinzani Tanzania - CHADEMA ndugu Freeman Aikael Mbowe aligombea ubunge kupitia chama chake hicho.

Ilikuwa kwa vyovyote vile asitangazwe mshindi either by HOOKS or by CROOKS. Hili lilikuwa apizo la Magufuli na wenzake na walilifanya kwa ushamba na ujinga wa viwango vyote vya ujinga duniani.

Kwa waliopoteza kumbukumbu, jimbo la HAI ndilo lilikuwa jimbo la kwanza kutoa matokeo ya uchaguzi takribani masaa yasiyozidi 8 baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa ile saa 10:00 jioni ya tarehe 28/10/2020.

Kwa teknolojia ya uhesabuji kura ktk vituo vya kupigia kura, kujaza fomu mbalimbali, compilation ya matokeo ngazi ya kata na jimbo ili kumpata mshindi wa udiwani na mbunge na kwa kuzingatia jiografia ya majimbo yetu ya uchaguzi yote Tanzania mtu anaweza kuona ugumu wa kuikamilisha kazi hiyo ktk interval ya masaa takribani 9 au 10 tu katika ngazi ya jimbo.

Bahati njema mimi nilikuwa mmoja wa maafisa wa uchaguzi huu nikiwa mwajiriwa ndani ya serikali, nikipewa jukumu hili pia.

Katika eneo nililosimamia mimi, kituo cha mwisho kuleta matokeo wilayani (jimboni) ili kufanya majumuisho kumpata mshindi wa ubunge ilikuwa ni saa 2asb kesho yake yani 29/10/2020!

Kwa kawaida, baada ya kituo cha kupigia kura kufungwa saa 10:00 jioni, uwezekano wa mtu wa mwisho kupiga kura inaweza kuwa kati ya saa 1 hadi 1.30 kutegemea na kituo na idadi ya wapiga waliokuwepo kabla ya saa 10 jioni. Hii maana yake mtu wa mwisho alipiga kura saa 11:30jioni kabla ya kuanza kuhesabu..

Kuna vituo vingine zoezi la kuhesabu kura, kubishana na mawakala na kutatua migogoro inayojitokeza na kujaza fomu mbalimbali ikiwemo ya taarifa ya kituo lilikwenda hadi saa 4usiku..

Baada ya hapo kwa kawaida msimamizi wa kituo cha kupigia kura hubeba masanduku ya kura na matokeo hadi makao makuu ya kata ili kufanya majumuisho ili kumpata mshindi wa udiwani na kumtangaza..

Baada ya hapo msimamizi wa kituo cha kupigia kura wakiambatana na msimamizi msaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata hubeba masanduku ya kura, matokeo ya kura za ubunge na urais hadi jimboni/wilayani kwenda kufanya majumuisho ya kura za ubunge na Urais..

Likifanyika hili, mshindi wa ubunge hutangazwa na kisha msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hutuma NEC matokeo ya kura za urais za jimbo...

Je, haya yalifanyika pale Hai katika interval ya masaa machache vile? How exactly?..

Na pengine tujaribu kujiuliza HAI, Kilimanjaro jiogarafia ya jimbo hilo ikoje? Walitumia teknolojia gani kiasi ambacho ndani ya masaa 8 tu baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa wakawa wamepata matokeo sahihi ya kila kituo na kuwatangaza wasindi wa udiwani na ubunge?

Mimi nasema, ni uongo. Haiwezekani abadani unless matokeo yawe yalikuwa yakitumwa kutoka vituo vya kupigia kura kwa njia ya mtandao wa computer!

Matokeo ya kawaida ya majimbo - ubunge japo na yenyewe ni wizi mtupu yalianza kutangazwa kesho yake ya tarehe 29/10/2020 kuanzia ingalau saa 6mch..

Ni wazi bila shaka kulikuwa na matokeo mengine "fake" tofauti na matokeo halisi yaliyotumika kutangaza washindi.
 
Mkuu maandamano huwezi kuyaamsha tu there must be a cause.

Platform ya uchaguzi huu imetupatia hiyo cause kwa uwazi kwa kila mtu.

Kuhusu jumuiya za kimataifa Uchaguzi ni internal affairs ndiyo maana mashinikizo yoyote hayawezi kutolewa zaidi ya matamko ya kibalozi tu.
Maoni yangu nazani umeyaona kuhusiana na hili swala la mahakama na jumuiya za kimataifa....
 
mkuu... ishu ni kwamba hakuna mahakama ya bongo ya kuiamin...
Hapa ni kama Rev mtikila case ya 2011 tunaenda African court tunapeleka pingamizi letu na facts mahakama ya africa itaamua...
Maamuzi yake sawaa sio binding kwa Tanzania ila yatabind karibia commission zote ambazo zitakuja kuangalia uchaguzi....
After Hizo commission za SADC,EAC na Au hawawez kusema uchaguzi ni wa huru na haki kama maamuzi ya african court hayajafatwa....
hii itakua ni hatua moja ya kuelekea demokrasia....
Tanzania italizimika ku domesticate yale maamuzi ili kulinda heshima yake kimataifa
Hivi unajua kuwa waangalizi wa uchaguzi EAC wamesema ulikuwa huru na wa haki ?

Hivi unajua SADC pia wamesema uchaguzi ulikuwa huru na wa haki ?

Hivi unajua Tanzania pamoja na kesi ya Mtikila kuamuriwa kuwa Tanzania iruhusu mgombea binafsi mpaka sasa Tanzania haijatekeleza uamuzi huo ?

Hivi unajua Tanzania mpaka imeshajitoa law taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja kupeleka kesi mahakama ya Africa ya haki za binadamu?

Hivi unajua sasa hivi Tanzania imetunga sheria inayozuia mtu kufungua shauri la katiba katika mahakama za ndani hapa nchini ?
 
Huyu hajui mkoa Kilimanjaro ni mkoa mdogo sana baada ya dar
Hai ni jimbo dogo sana ukiangalia maeneo ambayo kuna makazi ya watu, kijiografia vituo vipo karibu karibu, kuwahi kutangazwa kwa matokeo sio ushahidi.
 
Uchama pembeni, hapa nauliza wewe mtu mzima na akili zako timamu kabisa pengine ni Baba/Mama wa familia unaandika ujinga wa kiwango hiki? Ok ana Makengeza does that one makes u Happy?

Wewe hapo ulipo umejiona kasoro ulizanazo! Acheni mambo ya kukosoa uumbaji wa Mwenyezi Mungu,shindaneni kwa hoja na siyo huu ujinga ulioandika hapa. Kila la heri.
Wakikosaga hoja wanaanzaga vioja ndio maana wanaita wenzao misukule!
 
Back
Top Bottom