Salaam aleykum waugwana. Nataka nifungue car wash business. Sasa naomba wazo la location ambayo ni nzuri waungwana ambapo baadae nitaweka na tyre fitting pia asanteni. Naombeni mawazo kidogo. Happy christmas and new year
Kwaniini niwe mbabe kaka. Asante kwa mawazoKama wewe ni mbabe/mtoto wa mjini basi nenda Mbezi mwisho a.k.a Mbezi luisi panapojengwa/kilipojengwa kituo kipya cha daladala, pata kipande pale upige kazi. Utaokota madafu hadi ukimbie.
Kwaniini niwe mbabe kaka. Asante kwa mawazo
Kama wewe ni mbabe/mtoto wa mjini basi nenda Mbezi mwisho a.k.a Mbezi luisi panapojengwa/kilipojengwa kituo kipya cha daladala, pata kipande pale upige kazi. Utaokota madafu hadi ukimbie.
Fuatilia thread tangu mwanzoJamani mwenye ujuzi na bei za mashine za carwash, aina na bei zake naomba msaada wa kunijuza hapa jamvini
Kuna wakati nilishakua na Idea ya kufanya hii biashara na nilizunguka kwa watu wanaoifanya hii kazi walinipa uzoefu wao na pia gharama ambazo utalizimika kuzitumia.
Kwa mfano kuna Tank la kuweka maji kuanzia Lita 5000 inategea na ukubwa wa carwash yako, ni muhimu kuweka tank kwa kuwa endapo utatumia maji direct kutoka kwenye mabomba ya dawasco wanadai bili itakuja kubwa kutokana na pump ile ya presha inavuta maji na hewa kwa wingi hii itafanya meter kuzunguka zaidi ya ilivyo kawaida.
Pia zile mashine za kuoshea uwe nazo at least 2 ambazo kwa bei ya wakati huo (2014) zilikua kuanzia 1.5mil inategemea na ukubwa na brand ya mashine zile za Japan zinauzwa bei juu kidogo na wanadai ni imara zaidi. Usisahau mashine ya kuflonza vumbi ndani ya gari,ndoo kama 5 hivi, mpira, sabuni, uniform za wafanyakazi wako, na mishahara.
Vitu hapo juu yakupasa ununue baada ya kuhakikisha yard yako imekamilika sio mbaya ukianza na inayoingiza gari 4 kwa wakati mmoja.
Vifaa vinavyohitajika kwa Kuanzia ni Pressure Washer Hii bei yake inategemeana na ukubwa wa Mashine yenyewe lakini niliwahi kuona moja Jengo la NHC posta Bei ikiwa ni laki Sita Kama miaka mitatu nyuma.
Kifaa kingine ni Vacuum hiki ni kwaajili ya kuvuta uchafu ndani nayo bei yake inategemea
Tatu MAJI unafikiria kazi au biashara hii basi ufikirie maji ya uhakika kama hakuna maji ya Dawasco basi kwa Dar kuna wale wanaouza kwenye Makenta
Eneo ambapo biashara hii utaifanya hapa bei inategemea na eneo na mwenye eneo
Lakini Pia Kingine ni Sabuni Maalumu za Kuoshea Magari hizi sifahamu wapo zinapatikana na bei zake sifahamu
Vijana wa Kufanya nao kazi ambao watakuwa wanaosha malipo mtakubaliana
Vitambaa vya kuoshea na kufutia magari
Polish na Airfresh
Baada ya hapo Bei nadhani zinajulikana japokuwa zinatofautiana sehemu na sehemu Lakini Bei nayofahamu mimi ni Shilingi Elfu 10 kwa gari ndogo hizi Sedan, SUV hatchback nk.
Mengi nadhani wapo wanaoweza kuongezea Kila La Heri katika Kulifanikisha Hili
MZA inaweza kulipa sana maana ongezeko la magari ni kubwa na pia MZA kuwa njia ya magari yaendayo Bukoba, Musoma, Uganda, Kenya, Burundi na Rwanda. Nachoweza kukusaidia ni site nzuri hapa MZA kwa kujenga carwash.
MZA inaweza kulipa sana maana ongezeko la magari ni kubwa na pia MZA kuwa njia ya magari yaendayo Bukoba, Musoma, Uganda, Kenya, Burundi na Rwanda. Nachoweza kukusaidia ni site nzuri hapa MZA kwa kujenga carwash.