Ushauri na Mbinu Mbalimbali Kuhusu Uendeshaji wa Biashara ya Kuosha Magari (Car Wash)

Salaam aleykum waugwana. Nataka nifungue car wash business. Sasa naomba wazo la location ambayo ni nzuri waungwana ambapo baadae nitaweka na tyre fitting pia asanteni. Naombeni mawazo kidogo. Happy christmas and new year.
 
Salaam aleykum waugwana. Nataka nifungue car wash business. Sasa naomba wazo la location ambayo ni nzuri waungwana ambapo baadae nitaweka na tyre fitting pia asanteni. Naombeni mawazo kidogo. Happy christmas and new year

Kama wewe ni mbabe/mtoto wa mjini basi nenda Mbezi mwisho a.k.a Mbezi luisi panapojengwa/kilipojengwa kituo kipya cha daladala, pata kipande pale upige kazi. Utaokota madafu hadi ukimbie.
 
Kapotea, nahisi ni mchina anatumia google translator into Kiswahili. Car wash inalipa maeneo yenye shughuli za bar, saloon, stand ya mabasi.
 
Mnamkumbuka member mwenye jina la TQ_4U, Kiswahili chake kilikuwa hivyo. Nilikuja kugundua jamaa yule ni Mmarekani aliwahi kusoma chuo fulani hapo Arusha. JF ni international bwana!
 
Kama wewe ni mbabe/mtoto wa mjini basi nenda Mbezi mwisho a.k.a Mbezi luisi panapojengwa/kilipojengwa kituo kipya cha daladala, pata kipande pale upige kazi. Utaokota madafu hadi ukimbie.
Kwaniini niwe mbabe kaka. Asante kwa mawazo
 
Kwaniini niwe mbabe kaka. Asante kwa mawazo

Plot kama zile pale mbezi Luisi hazipatikani kirahisi hata kama una pesa. Kama uko dar basi pale ni miongoni mwa maeneo hot kwa sasa. Njia ya kinyerezi inatokea pale,njia ya goba inatokea pale, njia ya mpigi Magohe inatokea pale, Vipanya vyote vitaishia pale, kwa hiyo muda mfupi sana kuanzia leo Mbezi Luisi itageuka Mwenge fulani hivi.
 
Alykum salam! Hongera sana, unaweza ongeza hair saloon, min supermarket na ka0grocery kama imani yako inaruhusu hivi pia vinaweza leta wateja.
 
Kama wewe ni mbabe/mtoto wa mjini basi nenda Mbezi mwisho a.k.a Mbezi luisi panapojengwa/kilipojengwa kituo kipya cha daladala, pata kipande pale upige kazi. Utaokota madafu hadi ukimbie.

I concur with you 100%
 
Car wash ni biashara ambayo imekuwa ikiimarika kili siku, jarii kuongeza kipato chako kwa kutumia machine a mvuke kuoshea magari kwa ajili ya biashara au kwa matumizi yako binafi tembelea link ifuatayo kwa maeleo na picha zianazoweza kuongeza uelewa wako katika hili ni biashara prifitable.
 
Jamani mwenye ujuzi na bei za mashine za carwash, aina na bei zake naomba msaada wa kunijuza hapa jamvini.
 
Jamani mwenye ujuzi na bei za mashine za carwash, aina na bei zake naomba msaada wa kunijuza hapa jamvini
 
Hints:

1. Find a location that needs a car wash. A high-profile location, such as a busy street with good visibility, is a necessity for a business such as this to succeed.

2. Contact the city department that handles business licenses and request an application.

3. Inquire as to what other requirements there are for opening a business. You may be required to provide insurance or follow certain restrictions for the area.

4. Contact the Franchise Tax Board to get a wholesale permit, if required. This will allow you to purchase goods without paying taxes if they are to be used in your business.

5. Research car washes. Decide whether you want a fully automated car wash or a partially automated one that requires workers to complete part of the washing and drying process.

6. Decide if you want to purchase a franchise or open an independent business.

7. Make a business plan. You'll need to have all of the aspects of opening and running the business worked out for the short and long term.

8. Get financing. Unless you have a lot of money lying around, you will need to borrow money to build the business.

9. Advertise your new business. Use creative marketing to draw customers, such as a coupon book or a frequent-washer program.

10. Hope for rain. Rain creates mud, mud makes cars dirty, and you'll make them clean.
 
Wadau naulizia gharama za kujenga car wash ya kisasa katika mikoa ya dodoma,tanga,morogoro ama mwanza inaweza kuwa kwenye kiasi gani? Na zile mashine za kuoshea huwa zinauzwa kiasi gani? Yani kwa ujumla hii biashara inahitaji mtaji wa kiasi ganai?


=============================

MAONI NA USHAURI
====================================


Kuna wakati nilishakua na Idea ya kufanya hii biashara na nilizunguka kwa watu wanaoifanya hii kazi walinipa uzoefu wao na pia gharama ambazo utalizimika kuzitumia.

Kwa mfano kuna Tank la kuweka maji kuanzia Lita 5000 inategea na ukubwa wa carwash yako, ni muhimu kuweka tank kwa kuwa endapo utatumia maji direct kutoka kwenye mabomba ya dawasco wanadai bili itakuja kubwa kutokana na pump ile ya presha inavuta maji na hewa kwa wingi hii itafanya meter kuzunguka zaidi ya ilivyo kawaida.

Pia zile mashine za kuoshea uwe nazo at least 2 ambazo kwa bei ya wakati huo (2014) zilikua kuanzia 1.5mil inategemea na ukubwa na brand ya mashine zile za Japan zinauzwa bei juu kidogo na wanadai ni imara zaidi. Usisahau mashine ya kuflonza vumbi ndani ya gari,ndoo kama 5 hivi, mpira, sabuni, uniform za wafanyakazi wako, na mishahara.

Vitu hapo juu yakupasa ununue baada ya kuhakikisha yard yako imekamilika sio mbaya ukianza na inayoingiza gari 4 kwa wakati mmoja.

Vifaa vinavyohitajika kwa Kuanzia ni Pressure Washer Hii bei yake inategemeana na ukubwa wa Mashine yenyewe lakini niliwahi kuona moja Jengo la NHC posta Bei ikiwa ni laki Sita Kama miaka mitatu nyuma.

Kifaa kingine ni Vacuum hiki ni kwaajili ya kuvuta uchafu ndani nayo bei yake inategemea
Tatu MAJI unafikiria kazi au biashara hii basi ufikirie maji ya uhakika kama hakuna maji ya Dawasco basi kwa Dar kuna wale wanaouza kwenye Makenta

Eneo ambapo biashara hii utaifanya hapa bei inategemea na eneo na mwenye eneo
Lakini Pia Kingine ni Sabuni Maalumu za Kuoshea Magari hizi sifahamu wapo zinapatikana na bei zake sifahamu

Vijana wa Kufanya nao kazi ambao watakuwa wanaosha malipo mtakubaliana
Vitambaa vya kuoshea na kufutia magari
Polish na Airfresh

Baada ya hapo Bei nadhani zinajulikana japokuwa zinatofautiana sehemu na sehemu Lakini Bei nayofahamu mimi ni Shilingi Elfu 10 kwa gari ndogo hizi Sedan, SUV hatchback nk.

Mengi nadhani wapo wanaoweza kuongezea Kila La Heri katika Kulifanikisha Hili
 
MZA inaweza kulipa sana maana ongezeko la magari ni kubwa na pia MZA kuwa njia ya magari yaendayo Bukoba, Musoma, Uganda, Kenya, Burundi na Rwanda. Nachoweza kukusaidia ni site nzuri hapa MZA kwa kujenga carwash.
 
MZA inaweza kulipa sana maana ongezeko la magari ni kubwa na pia MZA kuwa njia ya magari yaendayo Bukoba, Musoma, Uganda, Kenya, Burundi na Rwanda. Nachoweza kukusaidia ni site nzuri hapa MZA kwa kujenga carwash.

Hayo magari ya safari sidhani kama ni wateja wazuri wa car wash, ni wachache wanaoosha magari kabla hawajafika mwisho wa safari ni wachache. Wateja wa ukweli ni wakazi. Hiyo site ni mitaa gani Mkuu?
 
MZA inaweza kulipa sana maana ongezeko la magari ni kubwa na pia MZA kuwa njia ya magari yaendayo Bukoba, Musoma, Uganda, Kenya, Burundi na Rwanda. Nachoweza kukusaidia ni site nzuri hapa MZA kwa kujenga carwash.

Mkuu hebu nisaidie maeneo mazuri na pia gharama yake inaweza kuwa pesa ngapi kulipia kiwanja kwa kukodi
 
Kwa Mashine Nzuri na za Uhakika, Waone GMI Tanzania, au Bahdella Dar es Salaam, Tanzania, wanauza Brand ya Karcher, ask for Karcher HD 1025, ni mashine nzuri. GMI au General Motors wapo opposite na Pepsi. Wao ni Authorised Dealer.
 
Back
Top Bottom